Usianzishe biashara wala kutafuta kazi kupitia waganga wa kienyeji

Usianzishe biashara wala kutafuta kazi kupitia waganga wa kienyeji

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Natangaza maslahi yangu! Mimi sio mganga na sifanyi ushirikina tena!

Kati ya waganga wote wa kienyeji ni asililia kumi hivi kati ya mia moja ndio wakweli na kati ya hao wakweli ni asilimia 5 tu ndio wenye masharti nafuu na wanaoweza kukusaidia moja kwa moja..! Ishu ya kuwajua feki na wakweli tutaona huko mbele

Kwanza lazima tukubaliane kuwa ushirikina ni utumwa, na ushirikina ni masharti na vigezo..Na ushirikina ni kitu chenye kuhitaji update kila wakati.. Na waganga wengi ni wapigaji!

Pamoja na shida zako zote usijaribu kwenda huko kwenye ushirikina kutafuta 'assist' huko unaenda kufanya registration kwenye data base yao na hatimaye kuwa kwenye himaya yao. MAKINIKA!

Chochote kinachohusika na ajira ama biashara ukiachana na visomo vya kidini lazima kitahusisha damu. Automatically itakuwa damu ya mnyama hasa mbuzi na ng'ombe ama kuku.. Kwa uchache kabisa na kwa siri kubwa damu ya mtu itahusika.

Mnyama anayechinjwa kwa shughuli za ushirikina ni wazi analazimishwa kufa kabla ya muda wake wa kufa kutimia. Vita yake yoyote ya kiroho baada ya hapo utaibeba wewe.. Kwahiyo utakuwa na vita mbili ama zaidi ya kupigana.. Vita yako, vita ya kuku, vita ya mbuzi nknk.. Na hapa ndio siri ya side effect asiyokwambia mganga, Lakini lingjne ni hili... Yule mnyama aliyetumika kukutengenezea mambo yako ana ukomo wake wa kuwa, hivyo wakati wake wa kufa ukifika, kafara ulilotengenezewa nalo hufa rasmi..! Hapo ndio utaona mambo yako yanavyoanza kuyumba na hatimaye kuharibika kabisa

Lingine ni kwamba kuna wakati katika maisha mambo huenda mrama bila sababu yoyote ile..ni asili tu inafanya kazi, wewe kwa kuhofia kuwa tayari umeshapigwa na kitu kizito tena, utakimbilia kwa mtaalam wako tena, na yeye hata kama hakuna tatizo atalitengeneza na kukutisha sana. Juu ya yote kwakuwa tayari uko kwenye database zao kuna wakati huamua kukorofisha mambo ili tu umuendee ajione bingwa ama kuna kitu umtimizie

Mwishowe unakosa kabisa ladha ya maisha unafanya biashara lakini hutulii ni makafara kwa kwenda mbele, una kazi yako nzuri Lakini masharti ni kama yote unapata pesa Lakini huna furaha nazo.

Mganga naye ni binadamu akiamua kula bata hutengeneza tatizo kwakuwa kila mganga ni mchawi.. Pesa ya kutengeneza tatizo ndio huwa pesa ya starehe kwakuwa haimpi masharti kama ile pesa ya kilinge inayotokana na tatizo genuine!

Mwanzoni mwa biashara, ajira na hata mahusiano na miradi mingine epuka sana kuyanajisi na ishu za giza yasije yakaja kukutesa mbeleni, kwa kuwa kuingia huko ni rahisi sana lakini kutoka ni habari nyingine. Na ni shughuli pevu
 
"Ushirikina ni masharti na vigezo, na ushirikina huitaji update kila wakati"

"Yule mnyama uliyemtumia kutengenezea kafara nae ana muda wake wa kuishi, hivyo muda wake ukifika kikomo na kafara lako pia huisha"

Hizo nukuu zako hapo juu nimezielewa haswa.
 
Sasa Mashana hebu tuambie wewe katika hao 100 ulikuwa kundi gani. Kwenye hao 10 au 90? Na kama ulikuwa katika hao kumi je ulikuwa kwenye wale 5 wasio na masharti magumu au kundi jingine.

Na kama ulikuwa kwa wale 90 ni kwanini.
Natangaza maslahi yangu! Mimi sio mganga na sifanyi ushirikina tena..!
 
Uganga ama uchawi haupo, ni watu wenye akili fupi tu wanaweza kuamini kitu kinaitwa uganga, uchawi, ulozi ama ushirikina, ni watu wenye akili ndogo tu wanaamini hayo mambo.
Dah, zamani nilikuwa na akili za kijinga kama zako, ila sina haja ya kukuhakikishia kama wachawi na waganga wapo au hawapo ila nakushauri funguwa kitabu cha dini unayoabudu ukikuta hakuna wachawi na waganga basi upo sahihi.

Na kinyume chake ukikuta verse kwenye kitabu cha dini yako kinatambuwa uwepo wa wachawi na waganga basi ujuwe wewe ndio mjinga zaidi au dini yako ndio ya kijinga zaidi.
 
Vipi kuhusu wanyama tunaowachinja Kama kitoweo Cha kawaida je siku zao pia huwa zimefika au tunawalazimisha kufa?
Kila mnyama ana ibada yake wakati wa kuchinjwa.. Na hii ibada ni kuzuia mabaya yote yatokanayo na huko kuchinjwa kwake kwa mchinjaji na kwa mlaji .. Waislam wanajua sana hiki kitu
Huko vilingeni na kwenye madhabahu za giza mnyama anakatwa shingo na kuachwa arukeruke hadi kifo..huo ukatili hauna msamaha
 
Uganga ama uchawi haupo, ni watu wenye akili fupi tu wanaweza kuamini kitu kinaitwa uganga, uchawi, ulozi ama ushirikina, ni watu wenye akili ndogo tu wanaamini hayo mambo.
Baadhi yenu huogopa kukiri uchawi upo mkidhani kukubali kwenu uwepo wake utawafanya muonekane nanyi mnashiriki hayo mambo, kumbe unaweza kukiri uwepo wake kama uhalisia ulivyo, lakini ukaishi kwa imani kwamba hauwezi kukupata, just be brave.
 
Back
Top Bottom