Nikisema hamna kitu unajua hapa duniani utasema nimekudharau lakini ndiyo ukweli wenyeweUganga ama uchawi haupo, ni watu wenye akili fupi tu wanaweza kuamini kitu kinaitwa uganga, uchawi, ulozi ama ushirikina, ni watu wenye akili ndogo tu wanaamini hayo mambo.
Brother umekuwa mwokovu?OK sawa lakini maslahi yangu niliyotangaza bado yanajieleza wazi kwamba mimi sio mganga na sijawahi kuwa mganga wa kienyeji.. Ushirikina niliofanya mimi ni Fantasy witchcraft.. Huu hauna maagano wala hauna madhara kwa wengine na ndio maana niliweza kuuacha na kuokoka
Duh! ..Mchawi anaroga na kuagua, mwanga sana sana ni michezo ya usiku ya kuchezea watu wakiwa wamelala ni kama hatua za mwanzo za uchawi, mlozi ni mtu anayependapenda mambo yote ya kishirikina na kufanya baadhi...
Jini ni kiumbe roho kisichotokana na binadamu, pepo ni kiumbe roho kinachotoka na wafu na viumbe roho wengine nje ya majini
The end.Natangaza maslahi yangu! Mimi sio mganga na sifanyi ushirikina tena!
Kati ya waganga wote wa kienyeji ni asililia kumi hivi kati ya mia moja ndio wakweli na kati ya hao wakweli ni asilimia 5 tu ndio wenye masharti nafuu na wanaoweza kukusaidia moja kwa moja..! Ishu ya kuwajua feki na wakweli tutaona huko mbele
Kwanza lazima tukubaliane kuwa ushirikina ni utumwa, na ushirikina ni masharti na vigezo..Na ushirikina ni kitu chenye kuhitaji update kila wakati.. Na waganga wengi ni wapigaji!
Pamoja na shida zako zote usijaribu kwenda huko kwenye ushirikina kutafuta 'assist' huko unaenda kufanya registration kwenye data base yao na hatimaye kuwa kwenye himaya yao. MAKINIKA!
Chochote kinachohusika na ajira ama biashara ukiachana na visomo vya kidini lazima kitahusisha damu. Automatically itakuwa damu ya mnyama hasa mbuzi na ng'ombe ama kuku.. Kwa uchache kabisa na kwa siri kubwa damu ya mtu itahusika.
Mnyama anayechinjwa kwa shughuli za ushirikina ni wazi analazimishwa kufa kabla ya muda wake wa kufa kutimia. Vita yake yoyote ya kiroho baada ya hapo utaibeba wewe.. Kwahiyo utakuwa na vita mbili ama zaidi ya kupigana.. Vita yako, vita ya kuku, vita ya mbuzi nknk.. Na hapa ndio siri ya side effect asiyokwambia mganga, Lakini lingjne ni hili... Yule mnyama aliyetumika kukutengenezea mambo yako ana ukomo wake wa kuwa, hivyo wakati wake wa kufa ukifika, kafara ulilotengenezewa nalo hufa rasmi..! Hapo ndio utaona mambo yako yanavyoanza kuyumba na hatimaye kuharibika kabisa
Lingine ni kwamba kuna wakati katika maisha mambo huenda mrama bila sababu yoyote ile..ni asili tu inafanya kazi, wewe kwa kuhofia kuwa tayari umeshapigwa na kitu kizito tena, utakimbilia kwa mtaalam wako tena, na yeye hata kama hakuna tatizo atalitengeneza na kukutisha sana. Juu ya yote kwakuwa tayari uko kwenye database zao kuna wakati huamua kukorofisha mambo ili tu umuendee ajione bingwa ama kuna kitu umtimizie
Mwishowe unakosa kabisa ladha ya maisha unafanya biashara lakini hutulii ni makafara kwa kwenda mbele, una kazi yako nzuri Lakini masharti ni kama yote unapata pesa Lakini huna furaha nazo.
Mganga naye ni binadamu akiamua kula bata hutengeneza tatizo kwakuwa kila mganga ni mchawi.. Pesa ya kutengeneza tatizo ndio huwa pesa ya starehe kwakuwa haimpi masharti kama ile pesa ya kilinge inayotokana na tatizo genuine!
Mwanzoni mwa biashara, ajira na hata mahusiano na miradi mingine epuka sana kuyanajisi na ishu za giza yasije yakaja kukutesa mbeleni, kwa kuwa kuingia huko ni rahisi sana lakini kutoka ni habari nyingine. Na ni shughuli pevu
Asante sana brother, kayahubirie mataifa yapate kumjua bwana.Ndio mkuu nakikaribisha nawe uje nuruni
Nimeshaandika sana hapa na nadhani 90% ya mada zangu zinahusu ulimwengu wa giza ila haikuwa rahisi maana upinzani niluokutana nao si wa kitoto.. Lakini nilisonga mbele bila hofu kwakuwa nilikuwa nafahamu nafanya niniAsante sana brother, kayahubirie mataifa yapate kumjua bwana.
Lakini kama itakupendeza na unahisi haiwezi kuwa tatizo kwako ningendekeza uweke thread mpya utufungue akili wengine maana tunasikia tu kwenye masimulizi kwamba most of world famous people wanaongozwa na msukumo wa nguvu kubwa ya ziada kufika pale walipo sasa, natamani nami siku niwe entertainer au influencer mkubwa ulimwenguni lakini nikifikiria issue ya supernatural power na hayo MA-voodoo, witchcraft nk najikuta narudi nyuma hatua kadhaa.
Sawa mkuu, wacha sasa nianze kuzipitia nyuzi zako moja baada ya mojaNimeshaandika sana hapa na nadhani 90% ya mada zangu zinahusu ulimwengu wa giza ila haikuwa rahisi maana upinzani niluokutana nao si wa kitoto.. Lakini nilisonga mbele bila hofu kwakuwa nilikuwa nafahamu nafanya nini
Kuna ID mpya (multiple) ziliibuka kila nilipoweka uzi mpya![emoji23] lakini tayari nilikuwa nimeshatengeneza mfumo na mtandao wa siri kuzing'amua
Nakupa moyo utimize ndoto zako lakini ni lazima uji equip na maarifa ya kutosha, hekima uvumilivu na staha maana utakutana na upinzani mkubwa mno
Jifunze zaidi kupitia mikasa ya waliokuwa huko then wakaacha hayana faida.Wew Mkuu barikiwa sna leo nakupa credit Mimi nimfatiliaji Mzuri WA mada zako Ila sio mchangiaji
Nimejifunza Mengi sna kupitia wew hasa haya Mambo ya uchawi, maji ya Baraka ect
God bless you.
Hapo kafara kubwa zitahusika Lakini itabidi ufanye renewal kila wakati au updateIla ukitaka utoboe mpaka watu washangae tumia waganga. Ila kuuwa iwe sumu kwako!
Sent using Jamii Forums mobile app
Hapakuna kitu umeongea hususani hapo kwenye mateka Nisha prove kwa mtu aliepandisha mashetaniViumbe roho wanyama na binadamu wanaingiliana bila shida...tofauti yao ni yale majumba mwili wanayofaa yanayowatofautisha kwenye uhayawani na ufahamu wa kibinadamu
Nitaendelea nikitulia....
Matendo mema hukuandalia pepo na kukupa kinga na ulinzi madhubuti wa kiroho..
Dhana ya pepo na jehanum huanzia hapa.. Pepo yako haiko mbunguni iko pale kaburini, roho yako ikitulia pale inakuwa iko peponi, ILA ikikengeuka na kukutoroka hujeuka kuwa lipepo na mzimu wenye kutaabika na kunaswa na washirikina kupitia shetani.. Kuna baadhi ya mapepo ni mateka wa hawa watu