Ndenji five
JF-Expert Member
- Nov 1, 2021
- 1,985
- 3,109
Uzur wake nimepata nilichokuwa nakitakaww kma ni Muislamu nakuita muislamu jina mna huna sifa za kua Muislamu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Uzur wake nimepata nilichokuwa nakitakaww kma ni Muislamu nakuita muislamu jina mna huna sifa za kua Muislamu
Na uzuri wake ni kua utakufa na utaviacha hivo ulivovitakaUzur wake nimepata nilichokuwa nakitaka
Na uzur wake umenistua nitauza vyote niende mm kama mmNa uzuri wake ni kua utakufa na utaviacha hivo ulivovitaka
mkuu nawezaje kuzifut hizo signature?Chale ni signature ya kuwa connected kuzimu,kuzimu inakutambua
hivi ukichoma mninga au mti wowote ukawa jivu hilo jivu ukajichanjia hapo utakuwa umefanya maagano na nani?mkuu nawezaje kuzifut hizo signature?
Paka ndimu na chumvi.Pili kataa kabisa kuamini kwamba msaada wako unatoka huko.mkuu nawezaje kuzifut hizo signature?
Amina [emoji1545][emoji1545][emoji1545]Wew Mkuu barikiwa sna leo nakupa credit Mimi nimfatiliaji Mzuri WA mada zako Ila sio mchangiaji
Nimejifunza Mengi sna kupitia wew hasa haya Mambo ya uchawi, maji ya Baraka ect
God bless you.
Kwani umeshaona mambo yote duniani.naamini hujawa na kama hujawai kuona yote ya dunia sema wewe hujawai kuona ila usiseme kua jambo flani halipo kabisa duniani.Dunia ni zaidi ya uijuavyo wewe na binadamu wana mengi yakushangaza.Uganga ama uchawi haupo, ni watu wenye akili fupi tu wanaweza kuamini kitu kinaitwa uganga, uchawi, ulozi ama ushirikina, ni watu wenye akili ndogo tu wanaamini hayo mambo.
Ushauri wanguKaka Mshana Jr nisaidie katika hili please
Nimeona andiko lako kuhusu Biashara na ushirikina...naomba nisaidie jambo moja mimi ni mfanyabiashara kwa hapa mtaani ndo mfanyabiashara kinara wa shughuli za huduma za kifedha(Mpesa,Airtel,Bank etc) na kuuza Simu,,ofisi yangu mimi ndo msimamizi mkuu zaidi kuna kijana mmoja kama fundi ambae yeye kaweka meza yake kwa nje na mara chache sana wadogo zangu wakiwa likizo huwa wananisaidia japo watu huwa wananihisi ni mshirikina ila sijawahi kanyanga kwa mganga yeyote yule ila nawazaga sana kwenda siku moja kutafuta kinga ya biashara kwani kuna michezo kama ya chuma ulete huwa naona mwaka jana mwanzoni ilitokea sana unashangaa hesabu inapungua laki mbili ukicheki sms zotee za miamala ziko sawa ila hela hamna ukawa ni mchezo kila mwezi tar za 15-20 napoteza laki mbili hadi tatu,,nikawaza kwenda kwa mganga ila katika pitapita kuna jamaa nikasikia huwa ana michezo ya chuma ulete sana na mwanzoni hakuwa mteja wangu ila mwaka jana alinizoea sana kuwa anakuja na nilivopima siku nayoona hasara lazima alikuja kutuma pesa nikaona isiwe kesi kazi si yangu nikamtumia ujumbe wa kumuomba katika maisha yake yote asikanyage katika eneo langu la biashara wala kuisogelea wala kutuma mtu yeyote,,akataka kujua sababu nikamwambia nimeamua iwe hivyo,,alituma baadhi ya watu kunihoji nikawaambia hakuna sababu nimeamua sitaki kumuona,,tokea nimpige marufuku mambo yakaenda vizuri sana nashukuru Mungu kwa kweli kama miezi minne mfululizo(wa nane hadi 12) sijawahi pata loss yeyote ila juzi nahisi tena ule mchezo umerudi sijui ni nani tena kanisababishia ya laki mbili...
Kaka hebu naomba ushauri au maelekezo wapi naweza kwenda au nini nifanye kuidhibiti biashara yangu isichezewe kabisaa
Asante
Asante kaka nitatafuta leo leo ndimu,,Ushauri wangu
1. Ulipoteza na ukajizuia kwenda kwenye ushirikina...Ilikuwa ni test kwako baada ya kufaulu ukaongozwa kumjua aliyekuwa anakuchezea.. Sasa inarudi tena huoni kuwa huo ni mtihani mwingine unajaribiwa?
2. Sikushauri uende huko yaani ni sawa na kuruka mkojo ukanyage kinyesi... Huko utatishwa sana ili uwekwe sawa..
Kwenye biashara za fedha kuna ushirikina mwingi sana hivyo nakushauri kwenye droo yako ya pesa usikose kipande cha ndimu na cha chumvi ya mabonge
Bila shaka 90% ya waliokupa Likes hapa wameshafanya sana Shirki na 10% iliyobaki ndiyo Sisi ambao hatujaufanya na kamwe hatutoufanya pia.Natangaza maslahi yangu! Mimi sio mganga na sifanyi ushirikina tena!
Kati ya waganga wote wa kienyeji ni asililia kumi hivi kati ya mia moja ndio wakweli na kati ya hao wakweli ni asilimia 5 tu ndio wenye masharti nafuu na wanaoweza kukusaidia moja kwa moja..! Ishu ya kuwajua feki na wakweli tutaona huko mbele
Kwanza lazima tukubaliane kuwa ushirikina ni utumwa, na ushirikina ni masharti na vigezo..Na ushirikina ni kitu chenye kuhitaji update kila wakati.. Na waganga wengi ni wapigaji!
Pamoja na shida zako zote usijaribu kwenda huko kwenye ushirikina kutafuta 'assist' huko unaenda kufanya registration kwenye data base yao na hatimaye kuwa kwenye himaya yao. MAKINIKA!
Chochote kinachohusika na ajira ama biashara ukiachana na visomo vya kidini lazima kitahusisha damu. Automatically itakuwa damu ya mnyama hasa mbuzi na ng'ombe ama kuku.. Kwa uchache kabisa na kwa siri kubwa damu ya mtu itahusika.
Mnyama anayechinjwa kwa shughuli za ushirikina ni wazi analazimishwa kufa kabla ya muda wake wa kufa kutimia. Vita yake yoyote ya kiroho baada ya hapo utaibeba wewe.. Kwahiyo utakuwa na vita mbili ama zaidi ya kupigana.. Vita yako, vita ya kuku, vita ya mbuzi nknk.. Na hapa ndio siri ya side effect asiyokwambia mganga, Lakini lingjne ni hili... Yule mnyama aliyetumika kukutengenezea mambo yako ana ukomo wake wa kuwa, hivyo wakati wake wa kufa ukifika, kafara ulilotengenezewa nalo hufa rasmi..! Hapo ndio utaona mambo yako yanavyoanza kuyumba na hatimaye kuharibika kabisa
Lingine ni kwamba kuna wakati katika maisha mambo huenda mrama bila sababu yoyote ile..ni asili tu inafanya kazi, wewe kwa kuhofia kuwa tayari umeshapigwa na kitu kizito tena, utakimbilia kwa mtaalam wako tena, na yeye hata kama hakuna tatizo atalitengeneza na kukutisha sana. Juu ya yote kwakuwa tayari uko kwenye database zao kuna wakati huamua kukorofisha mambo ili tu umuendee ajione bingwa ama kuna kitu umtimizie
Mwishowe unakosa kabisa ladha ya maisha unafanya biashara lakini hutulii ni makafara kwa kwenda mbele, una kazi yako nzuri Lakini masharti ni kama yote unapata pesa Lakini huna furaha nazo.
Mganga naye ni binadamu akiamua kula bata hutengeneza tatizo kwakuwa kila mganga ni mchawi.. Pesa ya kutengeneza tatizo ndio huwa pesa ya starehe kwakuwa haimpi masharti kama ile pesa ya kilinge inayotokana na tatizo genuine!
Mwanzoni mwa biashara, ajira na hata mahusiano na miradi mingine epuka sana kuyanajisi na ishu za giza yasije yakaja kukutesa mbeleni, kwa kuwa kuingia huko ni rahisi sana lakini kutoka ni habari nyingine. Na ni shughuli pevu
Hahahaha kwamba wewe una akili kubwa kuliko manabii walio utambua upo?Uganga ama uchawi haupo, ni watu wenye akili fupi tu wanaweza kuamini kitu kinaitwa uganga, uchawi, ulozi ama ushirikina, ni watu wenye akili ndogo tu wanaamini hayo mambo.
Na uzuri wake ni kua wewe una mkataba na Mungu kwamba unajua lini utakufaNa uzur wake umenistua nitauza vyote niende mm kama mm
Waliumbwa na Nani?Kiasili mapepo yanatokana na wafu na roho zinazohamanika.. Majini ni viumbe walioumbwa kwa moto na wasiotokana na wafu