Usidanganyike, vita kuu ya tatu ya dunia haitakuja kwa mfumo huu, bali mfumo wa kidini

Usidanganyike, vita kuu ya tatu ya dunia haitakuja kwa mfumo huu, bali mfumo wa kidini

Sio inakuja.....ilishaanza........kule Ukraine sababu ya yale mapigano yapo kiroho zaidi......,moyo wa kanisa la orthodox la urusi upo Ukraine......ndo maana papa anakomaa sana upande wa Ukraine na Zelensky hadi alitaka kuhamisha tarehe ya xmas ya kanisa la orthodox Ukraine ihamie tarehe 25 dec badala ya January kama ilivyozoeleka orthodox..............mrusi kaibuka tena baada ya kulifufua kanisa lake na kuliunganisha kwenye utawala, Putin kuna makosa ya enzi za ukomunisti wa USSR kaamua kurekebisha maana enzi hizo serikali na kanisa walikua kama chui na paka
Umenena vyema,

Uelekeo ni vita kuu ya Dunia ktk mfumo wa kiimani, Si Uchumi Wala siasa,

Ujio wa Trump utaleta mapumziko ya harakati hizi ktk uongozi wake.
 
Umenena vyema,

Uelekeo ni vita kuu ya Dunia ktk mfumo wa kiimani, Si Uchumi Wala siasa,

Ujio wa Trump utaleta mapumziko ya harakati hizi ktk uongozi wake.
Ndo maana babu Biden sahivi anahangaika ili kuchochea moto zaidi kabla hajaingia Trump maana jamaa akishaingia ikulu anafuta mipango yao yote na wao walitegemea rais angekua Kamala ili mipango iendelee kuelekea Ww3 na NWO
 
Ndo maana babu Biden sahivi anahangaika ili kuchochea moto zaidi kabla hajaingia Trump maana jamaa akishaingia ikulu anafuta mipango yao yote na wao walitegemea rais angekua Kamala ili mipango iendelee kuelekea Ww3 na NWO
Tumuombee maana wanampangia mabaya.

Ile neema ya Daudi kuokoka katika mipango ovu ya kukatisha uhai wake Toka Kwa mahasimu wake, neema hiyo ikafuatane na Donald Trump.
 
Nina wasiwasi utabiri wako hautakuja kutokea kwa kuzingatia mambo yafuatayo:
1. Ukristo unazidi kutokomea ulaya na Marekani na kuna uwezekano mkubwa karne ijayo hata Kanisa Katoliki waumini wengi watakuwa Afrika na Asia kuliko ulaya yenyewe (tegemeeni kupata Papa aidha mwafrika au mhindi); hivyo sioni kama kuna misingi ya kupigana vita ya dunia kwa misingi ya kidini wakati wenye silaha zote nzito ni wapagani

2. Hamna nchi ya kiarabu inayoweza kupigana vita ya dunia (ni ndoto za alinacha)
 
Nina wasiwasi utabiri wako hautakuja kutokea kwa kuzingatia mambo yafuatayo:
1. Ukristo unazidi kutokomea ulaya na Marekani na kuna uwezekano mkubwa karne ijayo hata Kanisa Katoliki waumini wengi watakuwa Afrika na Asia kuliko ulaya yenyewe (tegemeeni kupata Papa aidha mwafrika au mhindi); hivyo sioni kama kuna misingi ya kupigana vita ya dunia kwa misingi ya kidini wakati wenye silaha zote nzito ni wapagani

2. Hamna nchi ya kiarabu inayoweza kupigana vita ya dunia (ni ndoto za alinacha)
Mbingu na Nchi zitapita, lakini neno la Mungu litasimama milele.

Mungu hajawahi Sema uongo, alilosema litatimia.
 
Anabeba kusudi la Mungu katika KITI Cha Urais wake.

Anaisikia sauti ya Mungu na kufuata maelekezo yake, ndio maana Yuko mstari wa mbele kukataa UOVU wa USHOGA, utoaji mimba nk nk
Wakati mwingine ni vizuri ukakubali kufundishwa na ukafundishika. Wamarekani wenyewe wakikusikia, watakupa hela hadi uzikimbie! Ahahahahaha!!!
 
Nina wasiwasi utabiri wako hautakuja kutokea kwa kuzingatia mambo yafuatayo:
1. Ukristo unazidi kutokomea ulaya na Marekani na kuna uwezekano mkubwa karne ijayo hata Kanisa Katoliki waumini wengi watakuwa Afrika na Asia kuliko ulaya yenyewe (tegemeeni kupata Papa aidha mwafrika au mhindi); hivyo sioni kama kuna misingi ya kupigana vita ya dunia kwa misingi ya kidini wakati wenye silaha zote nzito ni wapagani

2. Hamna nchi ya kiarabu inayoweza kupigana vita ya dunia (ni ndoto za alinacha)
Pia weka hili akilini,

Wakatoliki Si wakristo, pia Islam hawatambuliki Mbinguni.

Dini hizo mbili ndizo zitaungana Kupambana na wamwaminio Yesu( Waliookoka) ambao hawatakubali kuabudu sanamu ya shetani.

Utakubaliana nami kuwa dini hizo kubwa mbili zinaabudu sanamu, Moja Muungu jua, dini ingine wanaabudu muungu jua na mwezi, hao kamwe hawezi kataa kuabudu sanamu maana wameshazoea Ibada hizo.
 
Salaam, Shalom!!

Mikwara ni mingi duniani Kwa sasa, mashariki, magharibi, kaskazini na kusini,

Silaha nzito za maangamizi Kila Taifa kubwa linazo, ni kutishana tu, haitakuwepo vita kuu ya tatu ya Dunia Kwa mfumo huu kama wengi wanavyodhani.

Kinac.hoendelea hivi sasa ni tetesi tu za vita sawa sawa na Mathew chapter 24, ni Taifa na Taifa litapingana, kundi na kundi, lakini vita ya Dunia nzima haitakuwepo.

Vita itakayokuja Dunia nzima ni ya mfumo wa kiimani, ni vita ya wamwaminio Yesu vs Wasiomwamini hii vita kuu ijayo itaitwa Armageddon war. Vita hii itakuja baada ya kunyakuliwa Kanisa.

Shika sana ulichonacho, mtu asikudanganye na kuitwaa taji Yako.

Mungu awabariki.

Ameen.
Dini gani maana wazungu washaachana na mambo ya dini
 
Dini gani maana wazungu washaachana na mambo ya dini
Si dini,

Bali mfumo wa Wamwaminio Yesu vs Wamwaminio mpinga Kristo.

Dini zote kubwa uzijuazo Islam na katolica na wapagani ni waabudu sanamu hivyo kamwe hawezi kumpinga mpinga Kristo.

Wamwaminio Yesu ,Wana wa Mungu ni waliookoka, wanenao Kwa lugha, walionunuliwa Kwa Damu ya msalaba, waongozwao na Roho mtakatifu, hao ndio watakaopifwa vita.
 
Pia weka hili akilini,

Wakatoliki Si wakristo, pia Islam hawatambuliki Mbinguni.

Dini hizo mbili ndizo zitaungana Kupambana na wamwaminio Yesu( Waliookoka) ambao hawatakubali kuabudu sanamu ya shetani.

Utakubaliana nami kuwa dini hizo kubwa mbili zinaabudu sanamu, Moja Muungu jua, dini ingine wanaabudu muungu jua na mwezi, hao kamwe hawezi kataa kuabudu sanamu maana wameshazoea Ibada hizo.
Islam hawatambuliki mbinguni lini wewe umekwenda na ukapewa hizo taarifa uje utuambie hapa, unaposema Roman Catholic si wakristo umetumia vigezo gani?

Labda nikuulize kitu kimoja nipe ushahidi kwa kutumia maandiko ya biblia ni wapi Yesu Kristo alianzisha dhehebu? Au kwanini hasa Yesu ilibidi kuja duniani?
 
Unyakuo imeandikwa ndani ya BIBLIA,

Tapeli ni wewe unayepunguza maandiko na kukataa kitu kilichoandikwa ndani ya BIBLIA.
Biblia ipi hiyo?

Mnapotosha maandiko ndio maana kina mwamposa wanawauzieni maji na mafuta,andazi na keki kwa 10,000 eti yana upako


Huu utapeli eti Kwamba kutakuwa na unyakuo wa siri, watu wa Mungu wataondoshwa duniani pasipo watu wengine kuona na hivyo kuwaepusha watakatifu wa Mungu na ile tabu inayoujia ulimwengu kama ilivyotabiriwa katika maandiko matakatifu.

kwa mujibu wa fundisho hili watakatifu wa Mungu hawatapitia mateso.
Inafundishwa kwamba mpinga Kristo (mnyama aliyetabiriwa katika Ufunuo 13) ataibuka katika siku za mwisho na atatawala kwa miaka 7. Kutakuwa na miaka mitatu na nusu ya mateso kwa wakazi wa dunia, ambapo Israeli watapewa nafasi nyingine ya kumkubali Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yao. Warumi 11:26. Wakati hayo yakitokea kanisa la Mungu litakuwa limetoweshwa duniani na hvyo mateso hayo ni kwa ajili ya kuwafanya Israeli wamkubali Yesu na kuokolewa.

Matapeli wanatumia andiko hili katika kufundisha hayo ni Mathayo 24: 40-41. “Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa; wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa.”

Mambo mengi yaliyopo katika fundisho hili hayana ushahidi katika maandiko matakatifu;

1. Hakuna mahali katika Biblia inaelezwa kuwa mpinga Kristo atatawala kwa muda wa miaka 7, bali tunaona akitawala kwa muda wa miezi 42 au miaka 1260. Danieli 7:25, Ufunuo 11:3, 12:6.

2. Taabu inayozungumzwa katika Biblia, Mathayo 24:22, Marko 13:20. Tena ni kwa sababu ya wateule wa Mungu ndiyo maana hata siku za taabu zitafupishwa. Sasa ikiwa kanisa la Mungu litakuwa limenyakuliwa, kwa maana kwamba halipo duniani, ni akina nani hao ambao kwa ajili yao siku za taabu zitafupishwa, kwamba pasipo hivyo asingaliokolewa mtu hata mmoja?

3. Israeli walipomkataa Mungu hadhi yao ya kuwa taifa teule la Mungu ilikoma. Na kuanzia hapo sisi wote tunahesabika kuwa watoto wa Ibrahimu kwa Imani. Warumi 4:16. Maangamizi ya mji wa Yerusalemu mwaka 70 BK kupitia majeshi ya Rumi ilikuwa ni ishara kuwa Israeli siyo tena taifa teule la Mungu. Baada ya kumpiga mawe Stefano, wanafunzi walitawanyika na milango ikawa wazi kwa mataifa kupata habari njema za wokovu ambazo Israeli walizikataa na kuwaua wajumbe wake. Lakini hii haimaanishi kuwa wamefungiwa kumwamini Kristo, la. Ni kwamba ile nafasi maalumu kama taifa teule haipo tena na hakuna tofauti kati ya myahudi na mtu wa mataifa.

4. Biblia inasema kuwa walio hai hawatawatangulia waliokufa katika kumwona Kristo, na kuja kwa kristo kutakuwa mara moja na ataonekana kila mahali kama ambavyo radi huonekana pande zote. Maelezo Zaidi juu ya mtiririko wa matukio ya kurudi kwa Yesu mara ya pili yatakuwa katika somo maalumu.

Kanuni moja ya kweli ni kwamba neno la Mungu halijipingi, kwa maana limevuviwa na Roho mtakatifu. 2 Timotheo 3:16. Biblia ni mkusanyiko wa vitabu vilivyoandikwa na watu mbalimbali lakini wote waliongozwa na Roho mmoja hivyo sharti kuwe na kukubaliana miongoni mwao. Ikiwa utaona kwamba Biblia inajipinga basi fahamu Dhahiri kuwa hujaelewa vizuri nini hasa Biblia inasema juu ya hilo jambo.
Kanuni nyingine ambayo ni nyongeza juu ya hiyo ni kwamba andiko lazima litafsiriwe katika nuru ya maandiko mengine. “Kwa sababu hiyo neno la Bwana kwao litakuwa hivi, amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo; ili waende na kuanguka nyuma, na kuvunjwa, na kunaswa, na kuchukuliwa.” Isaya 28:13. Japo fungu moja peke yake laweza kuwa msingi wa fundisho na kujitosheleza, lakini ni vema kuchukua huku kidogo na huku kidogo, kanuni juu ya kanuni na amri juu ya amri, na kwa kupitia hivyo tutaweza kuwa na msingi imara wa nini hasa Biblia inafundisha pasipo kuyumbishwa na kila upepo wa mafundisho. Waebrania 13:9.
Katika sura ya 24 ya kitabu cha Mathayo kuanzia fungu la 36 hadi 44, “Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.
37 Kwa maana kama vile ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.
38 Kwa kuwa kama vile siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika watu walivyokuwa wakila, na kunywa, wakioa na kuolewa, hata siku ile aliyoingia Nuhu katika safina,
39 wasitambue, hata Gharika ikaja, ikawachukua wote, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.
40 Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa;
41 wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa.
42 Kesheni basi; kwa maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu.
43 Lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.
44 Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.” Yesu alikuwa akielezea hali ya dunia itakavyokuwa wakati wa kuja kwa mwana wa Adamu. Alielezea hili kwa kutumia uzoefu wa kipindi cha Nuhu. Tuangalie mambo kadhaa katika haya mafungu ambayo yatatusaidia kuelewa kile ambacho Biblia inafundisha;

1. Wakati wa Nuhu watu waliochukuliwa na gharika ndiyo waliopotea au kuangamia. Wakati Nuhu anaingia katika safina watu walikuwa katika pilika pilika za maisha ya kila siku wasijue hatari iliyo mbele yao na gharika ilivyokuja ikawachukua (ikawatwaa) wote asipone hata mmoja. Hivyo wale waliosalia, yaani Nuhu pamoja na familia yake ndiyo waliookolewa.

2. Biblia haisemi kuwa wanaotwaliwa wanaenda mbinguni kama wengi wanavyodai. Na hata tukisema kwamba waliotwaliwa wanaenda mbinguni na tukalichukuwa fungu kama lilivyo (literal meaning) basi inaonyesha kwamba nusu ya ulimwengu itaenda mbinguni na nusu nyingine itaangamia jambo ambalo siyo kweli. Ni Dhahiri kuwa katika hayo mafungu Yesu hakuzungumzia habari ya kuchukuliwa kwenda mbinguni.

3. Katika hayo mafungu ni wazi kuwa Yesu alikuwa anazungumzia habari ya hukumu ya Mungu juu ya wanadamu. “Nikatazama hata viti vya enzi vikawekwa, na mmoja aliye mzee wa siku ameketi; mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji, na nywele za kichwa chake kama sufu safi; kiti chake cha enzi kilikuwa miali ya moto, na gurudumu zake moto uwakao. Mto kama wa moto ukatoka ukapita mbele zake; maelfu elfu wakamtumikia, na elfu kumi mara elfu kumi wakasimama mbele zake; hukumu ikawekwa, na vitabu vikafunuliwa.” Danieli 7:9-10. Danieli alionyeshwa hukumu iliyokuwa ikiendelea mbinguni wakati Yesu hajaja duniani. Hivi sasa tunavyoishi kuna hukumu inaendelea mbinguni, kila jambo tunalolifanya, liwe jema au baya, linawekwa katika vitabu na kuletwa hukumuni. Yesu atakapokuja duniani atakuja kuwalipa watu ujira wao kulingana na matendo yao. Mathayo 16:27.
4. Tukidumu katika kielelezo cha Nuhu, kwamba waliochukuliwa na gharika ndiyo walioangamia, basi ni wazi kuwa waliotwaliwa pia ndiyo walioangamia. Neno kutwaliwa hapa linaonyesha kuchukua kwa nguvu. Hivyo wakati watu wakiwa katika mambo yao wakistarehe, wakinywa na kula, wakioa na kuolewa, wasijue kuwa kuna hukumu inaendelea ndipo mwisho wao unaamuliwa aidha kwa uzima wa milele au kwa uangamivu wa milele. Hivyo tunaweza kusema hukumu ya Mungu iliwachukua (iliwatwaa).

5. Yesu alitumia kielelezo cha watu wawili ili kuonyesha pande mbili zitakazokuwepo kama matokeo ya hukumu ambazo ni uzima wa milele au mauti ya milele, hakuna upande utakaokuwa katikati. Watu wawili hawakuwakilisha idadi wala uwiano kati ya watakaookolewa na watakaoangamizwa.

Tumekwisha kuona muktadha wa kile Yesu alichokuwa anazungumzia katika hayo mafungu. Jambo la msingi ambalo tunapaswa kushikilia ni kwamba; tunaishi wakati wa hukumu kama ambavyo tumeona katika kitabu cha Danieli, hukumu ya upelelezi. Vitabu vinafunuliwa na kumbukumbu zinaletwa. Jambo la msingi ambalo tunaweza kulifanya wakati huu ni kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yetu na kudumu katika kufanya yaliyo mapenzi ya Mungu
 
Tambueni Siri hii,

Donald Trump ni mtumishi wa Mungu,

Donald Trump ni Nabii wa Mungu.

Ukidhani Nabii ni Hadi asimame madhabahuni unakosea, Daudi alikuwa Mfalme na Nabii wa Mungu wakati huo huo.
Trump nabii tena ?....
 
Tambueni Siri hii,

Donald Trump ni mtumishi wa Mungu,

Donald Trump ni Nabii wa Mungu.

Ukidhani Nabii ni Hadi asimame madhabahuni unakosea, Daudi alikuwa Mfalme na Nabii wa Mungu wakati huo huo.
Trump ni tapeli kama matapeli wengine

Trump na waliomuweka pale lao moja ,tatizo unakurupuka sana



Waarabu wote pale Saudia wamefurahi sana kurudi kwa dady yao. Wametoa salamu za kimahaba na kuahidi kufanya kazi naye. Wakati wa ziara ya Trump Israeli akiwa rais wa 45 wa Marekani, Wayahudi walimpokea kwa majani ya mitende na kumwita Koreshi kwa kuitambua Yerusalemu kuwa mji mkuu wa Israeli mnamo october 17, 2017. Wakaunda shekeli yenye picha ya Trump na kumwita Koreshi wa kizazi cha leo. Marabi wakamkaribisha mbele ya ukuta wa kulia machozi, wakasali pamoja naye kwa furaha.

Kumbuka pia wakati wa ziara ya Trump huko Saudia akiwa rais, baada ya kutoka Israeli mfalme na mwanawe walimfanyia sherehe kubwa sana mbele ya wafalme wa Ghuba na wakacheza naye muziki wa kiarabu kwa madaha. Na wote akawapatanisha na Israeli na kufungua mahusiano upya ya kitaifa. Netanyahu na Salman wakapatana dhidi ya Iran, adui yao wa jadi. Trump akasaini mikataba ya biashara na silaha kwa wote Saudia na Israeli.

Trump alimtetea Prince Mohamed bin Salman na Saudia dhidi ya kashfa ya kumuua Kashanog huko Uturuki alipoenda kumwaga siri chafu za ufalme. UN, chama cha demokratiki na vyombo vya wanaharakati wa habari na demokrasia walipiga kelele dhidi ya tukio hilo lakini Trump akaweka kifua kwa mwanawe na yakapita. Hii ilidhihirisha kuwa wana mapenzi ya baba na mwanawe; na Trump alisema kwa umuhimu wa Saudia, kamwe USA haiwezi kuitupa sababu ya Kashanog.

Sasa Trump amerejea na tumeona ameungwa na jopo la masheikh na Waislamu kwa ujumla huko Marekani. Je yeye na watoto wake wataupyaisha uhusiano wao wa jadi dhidi ya Iran ambayo Trump ameahidi kuinyamazisha? Tusubiri.

Iran wao wamesema hawaoni tofauti ya Biden na Trump, wapo tayari kukabiliana na ujio mpya wa Trump aliyewaongezea vikwazo vizito sana ambavyo Biden alikuja kuviregeza na zaidi akamuua Qasim Seleman, jenerali mkuu wa Iran katika jeshi la Quds.

Wakati Marekani ikiwa bize na uchaguzi wa kumchagua rais wa 47 leo naam na leo tena huko Iran sarafu yao imeporomoka kwa kiasi kikubwa sana ambacho hakijawahi tokea katika historia yake. Na Trump ameahidi sio mazuri kwa Iran bali mabaya atakapokalia kiti cha white house.
 

Attachments

  • FB_IMG_1732959356458.jpg
    FB_IMG_1732959356458.jpg
    51.5 KB · Views: 1
Back
Top Bottom