Usijaribu kufanya biashara za ahadi na wabongo utaumia (Promissory Notes)

Usijaribu kufanya biashara za ahadi na wabongo utaumia (Promissory Notes)

Wabongo hatuna nidhamu ya pesa na wala hatujali mara baada ya kutatuliwa shida zetu. Akina na shida anatoa huruma anaweza piga hata magoti.
Yaani uswahili haufai kabisa kwenye hela za watu.
 
Yaani chalii angu hata akiwa ni nani akishakaa pande hizi tu ana adopt tabia chap chap anakua nae ni mzawa fasta tu.

Mimi huyo aliyenizingua nilimchukulia brakedown tukavuta ki rav-4 chake mpk home nikakiwekea na turubai fresh kabisa,jamaa wa brakedown nilimlipa 120,000 tu mchezo ukawa umeisha na uzuri case yangu ilikua inajulikana sehemu nyingi so asingeweza kusema nimemuibua ndinga yake.

Alirudisha mpunga wangu+gharama ya brakedown baada ya siku 3 tu.
Duu
 
Nilitaka kuandika kitu hiki hiki,pole sana mkuu kuna mbwa na mimi walishanilostisha kwa kujifanya wao warushi sana ila na mimi nilichukua mali zao zenye thamani ya niachowadai,ila ndio kujifunza kwenyewe huko.

Na kama chalii angu uko kaskazini(Arusha, Kilimanjaro-na ndio home kwetu) kurushana/kudhulumu watu kuko kwny damu kabisa na ni sifa kabisa.

Niiliwahi kufanya baishara na wasukuma/kanda ya ziwa ki ukweli sio kwamba nawasifia wala nini ila atleast ni waoga wa mali ya mtu yaani hata akichelewesha malipo unamuona ana kauoga flani na atakulipa lkn wale ndg zangu wengine aisee cha mtu hawakiogopi wala nini.

Hii ni experience yangu ya biashara.


Juzi nilikua mpakani mwa Kenya huko.kuna biashara nilikua nafanya moyo tu ukaniambia niseme ukwel natokea moro ...wakaniambia ungesema unatokea Dar tungekataa kufanya mishe na ww watu wa Dar mikoani wanaogopwa mnoo! Inasemekana ni matapeli konky! Kitu mbaya sana
 
Back
Top Bottom