Usikubali kila mtu akufute machozi wengine wana leso zenye pili pilipili

Usikubali kila mtu akufute machozi wengine wana leso zenye pili pilipili

Mwanasayansi Kalivubha

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2024
Posts
344
Reaction score
926
USIKUBALI KILA MTU AKUFUTE MACHOZI WENGINE WANA LESO ZENYE PILI PILIPILI

Kilio chako kikisikika na kila mtu tegemea kutonyamanza kwa sababu kuna watu watatumia kama fursa ya kukuliza zaidi kwa sura ya kukufuta machozi kwa kutumia vitambaa vyenye pili pili.

Kwa haraka utaona wanakuja kukusaidia kumbe ndio wanakuja kuongeza ukubwa wa tatizo.

Matatizo yako yanahitaji suluhisho ila usifanye matangazo kwa sababu kuna adui wanatafuta namna ya kukudhuru kwa njia ya kupitia madhaifu yako.

Kipindi ambacho unatakiwa kuwa makini sana ni pale unapokuwa na changamoto hapo ndipo unatakiwa utumie busara kubwa ya kuruhusu nani ajue na nani aendelee kukuona upo sawa .

#Mwanasayansi Saul kalivubha
#Mitandaoni Fikia Ndoto Zako.
 
Back
Top Bottom