Usikubali kusaini nyaraka hii unapopekuliwa na Polisi

Kama kweli huyu ni wakili basi ni bogas kabisa.. Upekuzi wowote unafanyika kwa kufuata utaratibu, utàratibu huo ni kuwa upekuzi lazma ufanyike mbele kiongozi Wa serikali ya mtaa, au hata mbele ya wakili wako au mashahidi wengne kama ndugu zako.

Pia anayepekuliwa lazma aelezwe kwamba ni kitu gani kinatakiwa katka upekuzi huo.. Sasa huyu kanjanja sijui anaongea nini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi naona ameelezea vizuri. Kuna upekuzi mwingine unafanyika ili kupandikiza ushahidi wa uongo. Fikiria askari ana kusearch na katika kufanya hivyo anaonesha ulikuwa na bangi ilhali sio kweli! Utakubali kusign?
Usisign upigwe virungu ufe uache familia
 
Kazi ya wakili ni kukataa kosa hata kama umetenda kweli
Kazi ya Wakili siyo kukataa kosa bali ni kumtetea mtuhumiwa au mteja wake mkuu. Kama una wakili wa hivyo basi hakufai kabisa.

Mfano kesi ya kuua mtu ambaye umemfumania mtu anafanya mapenzi na mke wako. Huwezi ukasema sikuua. Bali lazima Wakili akuongoze vyema ili uileze mahakama ni kwa namna gani au mazingira gani hicho kifo kilitokea.

Mfano
Wakiki: Shahidi/mtuhumiwa ieleze mahakama ni nini kilitokea tarehe 5/6/2020.

Shahidi/mtuhumiwa: manamo tarehe hiyo nilitoka kazini mida ya saa mbili usiku. Nilipofika nyumbani chumbani nilimkuta marehemu anafanya mapenzi na mke wangu.

Mfano mwingine ni kifo kilichotokea wakati wa kujitetea( self defense). Hapa Wakili inabidi wakati wa utetezi akuongoze wewe uoneshe mazingira ambayo hicho kifo kilitokea.
 
Unaweza ukasaini au kutosaini na bado certificate of seizure ikawa haina maana so inategemea aina ya kesi ya jinai mfano unakutwa na mali zinatiliwa shaka kwamba ni za wizi. Polisi akasaini na wewe ukasaini pamoja na shahidi huru. Lakini kule mahakamani yule Shahidi(mtu aliyelalamika kuibiwa) akashindwa kufanya utambuzi/ kutambua hizo mali anazosema zimeibiwa pale mahakamani. Do you think mpaka hapo certificate of seizure itasaidia?
 
asante
 
Kuna mashahidi kadhaa wanakuwepo wanaotakiwa kujiridhisha kinachofanyika kina uhalali labda nao hao washawishiwe kukuruka
Suala la kupandikiza ushahidi unaliangalia kwa wepesi mno!!

Evidence Planting sio lazima ifanywe na polisi!! Nimeshakupa njia mbili za namna gani ushahidi unaweza kupandikizwa! Polisi wanaweza kupandikiza ushahidi au wakati mwingine watu wake wale wale unaowaamini wanaweza kununuliwa na kupandikiza ushahidi!

Wakati wewe unaamini nyumba ipo safe, kumbe watu wameshafanya yao, na baada ya hapo architect wa mchezo anaihalifu polisi kwamba, kwa mfano nyumba x wanajihusisha na mihadarati!
 
Wakili:

Ukikataa kusaini inakuwaje?

Ni poa tu? Kwa nini watu husaini na vitu hawañutwa navyo kama ni poa kukataa kusaini? Changamoto huwa ni nini?

Usiposaini na kuna baadhi ni kweli wamechukua unavipata pataje mwisho wa kesi kama ulikataa kusaini na hakuna rekodi ?

Hiyo kesi ya Mahakama Kuu what was the case or controversy before the court ? Wachina walisema tumesaini gizani au tuliwekewa pisto utosini au hatuelewi maandishi ya Kiswahili au saini sio zetu, zimeghushiwa???

Na mahakama ikasema screw you all China men, ukisaini umesaini ?????

Umesema na umerudia rudia kwamba hati hii hujazwa endapo kuna chochote kinachotakiwa kuchukuliwa. Kinachotakiwa na nani ? Unashutumiwa kutumia matusi na uchochezi kwenye mkutano wa hadhara, ushahidi video. Wanakunyang'anya simu. Hiyo simu inatakiwa kuchukuliwa, inatakiwa na nani ??? Sheria ipi ? Au utuambie ni kitu ambacho wao wanataka kukichukua?

Na unasema hati hii hujazwa hasa pale ambapo kuna chochote kinachotakiwa kuchukuliwa kama ushahidi. Ni mazingira gani mengine ambapo hakuna kinachochukuliwa lakini bado wanakutaka ujaze ? Kama hakuna, kwa nini umetumia maelezo ya "hasa pale ambapo" ? Uliteleza, au ???????
 
hiyo sio rahisi kutokea labda kama shahidi ameamua kuturn hostile. kwa kawaida, kabla ya kuja mahakamani shahidi huwa anaandaliwa na prosecutor, anaonyeshwa hadi exhibits zote za mahakamani au kama zipo tayari kule anafafanuliwa zilivyo, kiufupi ni kwamba anafundishwa.period. sasa huko kufika mahakamani na kushindwa kutambua itaanzia wapi?
 
kama unakubaliana na mimi kuwa hata asiposaini haitamsaidia sasa huyu mwanasheria ametoa ushauri kuwa wasisaini kwa faida gani sasa? kama umemwelewa yeye lengo lake kuleta hapa hiyo hoja alikuwa anaamini usiposaini hiyo certificate itakuwa worthless/valueless, na anaamini mshitakiwa anaweza kutokea hapo, kitu ambacho sio always! alijielekeza vibaya na kwa watu waelewa, hata yeye mwenyewe tu, ninaamini ameshatambua mapungufu yake na amekubaliana nayo tayari. ninyi tu wengine ndio mnahangaika ila mtu mwelewa anayeamini siku zote tunaishi kwa kujifunza na kukosolewa huwa anakubali kurekebishwa.
 
Unaweza kusaini ktk listi unayoiona.... Bila tatizo.... Alafu jamaa wakaongeza pembe ya ndovu katika listi wakati wewe haupo... Mchakato ukaanzia hapa....

Inatia shaka....
kwa taarifa yako, hizo risiti/certificate nyingi zinakuwa sio tu na saini ya kawaida, bali na dole gumba. sasa kama watafoji na dole gumba lako basi utakuwa uliweka dolegumba la aina nyingine unayoijua wewe. ukiona certificate hauiamini, unaweza kuibishia na kuomba ichunguzwe dole gumba kama saini unaona imefojiwa. kwa kawaida kabla haijatolewa mahakamani si lazima upewe uichunguze na useme cha kusema?
 
the sameway unaposema sio sawa kumzaba mtu, na mimi ningesema sio sawa kutoa mitego kwa wahalifu ili wakwepe mkono wa sheria wakati wanakuwa wameleta madhara aidha kwa watu binafsi au kwa serikali. unajua kabisa kuwa mtu amekutwa navyo na yeye anajua, halafu anakataa kusaini, utamwachaje kumzaba kwa mfano? na ninawashaurini, ukikutwa na kitu usilete ubishi utakuja upigwe na fimbo isiyo ya kawaida na hutaamini macho yako kwa kitu kidogo tu. we saini mengine mtapambana mahakamani. kuna maeneo utapigwa kwa mfano kwenye tigo huko na hautajulikana kama ulipigwa. huyo mwanasheria anawapotosha mtajuta. akili za mbayuwayu changanya na za kwako. nimekuwa PP kwa miaka mingi sana najua ninachoongea.
 
Huyu ni Wakili kweli? Nina mashaka na uwakili wake!! Upekuzi umefanyika kwa kufuata taratibu na sheria halafu mtu akatae kusaini.
umemuelewa lakini??? kweli umepekuliwa.....na wewe wajua huna bangi kwako ...wakakuchezea cheusi chekundu banga ikkawepo ghafla..lakini katika ile fomu BANGE imeorodheshwa....utasaini??
 
Namaanisha Hivi..... Unaweza kusaini ukatia na dole gumba.... Jamaa wakaenda kuongeza item kwenye list ile uliyosaini awali....
 
Sawa hebu tuletee tena kihusu huyu aliyepigwa na akalazimishwa kusaini mahakama inasemaje hapa
 
Kumbuka tu kuna muda watachukua mali yako halali kwa kuishuku tu sasa ukikataa kusaini maana yake hawakuchukua.Hivyo Mkumbushe mwananchi kuwa siyo kila kilichochukuliwa wakati wa upekuzi siyo cha kukataa kusaini maana kuna muda unaikana Mali yako halali maana upelelezi ukikamilika na ikabainika hiyo mali haihusiki utarudishiwa.
 
Namaanisha Hivi..... Unaweza kusaini ukatia na dole gumba.... Jamaa wakaenda kuongeza item kwenye list ile uliyosaini awali....
wakiongeza item, siku inapokuja kutolewa mahakamani wewe utajua waliongeza item na itakuwa mojawapo ya sababu ya objection, pia kutakuwa na independent witness ambaye atakusapoti kwa hilo. cha msingi ni kwamba, hata ukigoma kusain iwe kwa dole gumba au pen inaweza kupokelewa tu, though kila kesi huamuliwa kulingana na mazingira yake.
 
Mkuu inawezekana hukumuelewa vizuri wakili. Hakumaanisha kuwa nyaraka haitapokelewa, alichomaanisha ni uzito wa hiyo nyaraka katika kesi, itakuwa imepokelewa lakini bila kuwa na uzito wa kumuweka hatiani mtuhumiwa tofauti na ingekuwa na saini yake. Hicho ndio msingi wa uzi. Msisitizo, amesema ikiwa unaona umebambikiwa vitu halisia au karatasi limeandikwa vitu visivyopo kihalisia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…