Usikubali kusaini nyaraka hii unapopekuliwa na Polisi

Usikubali kusaini nyaraka hii unapopekuliwa na Polisi

wewe ni mwanasheria mchanga, bado una safari ndefu. kwa taarifa yako, hata usiposaini, lakini wamesaini independent witnesses, haimaanishi certificate of seizure haitapokelewa mahakamani, na haimaanishi haitakuwa na mashiko. usipoteze wenzako maboya. halafu, hivi kwa akili yako huwa kuna mtu anayesaini kwa kupenda au ameshavurugwa kwa kichapo na vitisho? ati usikubali,wanasheria huwa mnapotosha sana watu kwa vitu vya wazi. chukulia mfano hao kina song lei, wanakutwa na pembe za ndovu sijui faru live kwenye gari yao au kwenye begi, au mtu anakutwa na kichwa cha mtu kwenye mfuko, auu mtu anakutwa na unga tumboni au kwenye begi, unaanzaje kukataa kwa mfano, hata wakikuzaba kibao watakuwa wamekuonea kweli? na hakuna ushahidi kama ulichapwa wala nini....hujawahi kamatwa ndio maana unaongea hivyo, ukija kufanya kosa la maana ukakamatwa ukawa peke yako chumbani kule polisi utajua kama mtu anaweza kusaini au akawa na uhuru kukataa. unaweza kukataa kama wanakubambika, n a wao ni binadamu wanaweza kukuacha wasikuchape, ila umekutwa navyo na unakataa utajikuta wewe mwenyewe unaomba peni usaini. pia, uwepo wa independent witnesses huwa una cure hiyo hoja yako and still certificate of seizure can be admissible in court without the signature of the accused on it.
Mkuu, kama cheti hicho kinaweza kuwa admissible na kuwa na mashiko bila hata ya saini ya mtuhumiwa kuna umuhimu gani wa kumlazimisha asaini?? Maana unasema kabisa watu huwa hawasaini kwa kupenda bali kwa lazima.

Na unaona ni sawa kwa mtuhumiwa kuzabwa vibao sababu amekutwa redhanded ilhali yeye hakubali kuwa amekutwa redhanded? Unaona ni sawa kwa sababu tu hakutakuwa na ushahidi wa kuonesha kuwa alipigwa? Hao independent witness wanakuwa wapo kwa ajili ya kushuhudia kila kinachotokea au wapo kwa ajili ya kuhakikisha mtuhumiwa anasaini?

Sio vyema kabisa kufurahia matumizi ya nguvu kwenye upekuzi au ukamataji. Hapa bado tunahitaji sana maaskari wetu wapewe body cams ili kuepusha mambo kama haya. Kesi inajengwa kwa ushahidi imara na sio wa kulazimishana
 
Mtabishana wao watasema sahihi ni yako na wewe utasema sahihi sio yako, hapo itafunguliwa kesi ndogo na ile ya msingi itaachwa, kwenye kesi ndogo wataitwa waataalamu wa maandishi ikibainika ulidanganya utapewa adhabu ndipo inaanza kusikilizwa kesi ya msingi tena

Inakuwa hasara kwako maana kesi ndogo nayo haiishi haraka inachukua muda, plus adhabu ya kuidanganya mahakama unapewa adhabu ambayo hata ukishinda utatumikia adhabu ya kesi ndogo sasa kwanini usiokoe muda kwa kwenda straight aidha ushindwe utumikie adhabu moja au ushinde kabisa

Unafikiri mambo ni mepesi hivyo?
Wataalamu wa mwandiko watafanya nini kugundua ni mimi nimeandika?..ikiwa nimebadilisha uumbaji wa herufi na nimebadilisha sign?..mfano mwandiko ulioandika kwa mkono wa kushoto ambao siutumii kuandika.
 
Umeniwahi mkuu, mwenyewe nimemshangaa sana, sasa kama umekutwa na hizo mali unaanzaje kukataa?, na je wasipokuja na hiyo form wakaenda kujaza wanavyojua wao utamlaumu nani,? Hapa wambie watu kwamba ile form isome vizuri na hakikisha kilichoandikwa ndicho ulichokutwa nacho ndio utie sahihi sio kusema asisaini.
Wakili Yakubu ameeleza hivi;

Aidha, ni muhimu kujua kuwa ikiwa unapinga kuhusu kile kinachochukuliwa kuwa hukukutwa nacho ama hakikukutwa kwako basi usikubali kusaini fomu hiyo.

Hii ni kwasababu kukubali kwako kusaini fomu hiyo tafsiri yake kisherria ni kuwa umekubali kuwa umekutwa na hicho kitu.

Na endapo utafikishwa mahakamani basi fomu hiyo itawasilishwa kama ushahidi na kwasababu ulisaini basi ulikubali kuwa ulikutwa na kitu hicho.

Vinginevyo uwe unakubali kuwa ni kweli hicho kitu umekutwa nacho, basi hapo waweza kusaini. Lakini kama hukubali basi usisaini.
 
Huyu ni Wakili kweli? Nina mashaka na uwakili wake!! Upekuzi umefanyika kwa kufuata taratibu na sheria halafu mtu akatae kusaini.
Hata mimi imenishangaza hasa ukizingatia mfano alioutoa wa Wachina kukutwa kwenye gari na nyara za serikali!
 
Wataalamu wa mwandiko watafanya nini kugundua ni mimi nimeandika?..ikiwa nimebadilisha uumbaji wa herufi na nimebadilisha sign?..mfano mwandiko ulioandika kwa mkono wa kushoto ambao siutumii kuandika.
Utaandikaje wakati huo mkono hautumii? Labda uanze kufanya mazoezi leo hii.
 
Huyu ni Wakili kweli? Nina mashaka na uwakili wake!! Upekuzi umefanyika kwa kufuata taratibu na sheria halafu mtu akatae kusaini.
Umesoma na kuelewa?
Amesema Kama unauhakika umekutwa nacho sawa, lakini hujakutwa na kitu usisaini.

Kufuatwa kwa taratibu za upekuzi hakufanyi ukutwe na kinachohisiwa.
Be serious
 
Unaweza kusaini ktk listi unayoiona.... Bila tatizo.... Alafu jamaa wakaongeza pembe ya ndovu katika listi wakati wewe haupo... Mchakato ukaanzia hapa....

Inatia shaka....
 
Wakili hajatoa elimu amefanya uchochezi ambao watu wasipoelewa vizuri watajikuta matatizoni.

Alitakiwa kusema iwapo hukukutwa nacho kataa lakini kama umekutwa nacho saini.

Huwezi kukutwa na bangi (nazungumzia kukutwa nayo sio zile za kuwekewa) halafu ukaamua tu kukataa.

Kwahiyo watu waelewe ni kile usichokutwa nacho tu.
Soma kwa uangalifu na umakini utaona hayo uyasemayo yamo
 
  • Thanks
Reactions: T11
Mkuu, kama cheti hicho kinaweza kuwa admissible na kuwa na mashiko bila hata ya saini ya mtuhumiwa kuna umuhimu gani wa kumlazimisha asaini?? Maana unasema kabisa watu huwa hawasaini kwa kupenda bali kwa lazima.

Na unaona ni sawa kwa mtuhumiwa kuzabwa vibao sababu amekutwa redhanded ilhali yeye hakubali kuwa amekutwa redhanded? Unaona ni sawa kwa sababu tu hakutakuwa na ushahidi wa kuonesha kuwa alipigwa? Hao independent witness wanakuwa wapo kwa ajili ya kushuhudia kila kinachotokea au wapo kwa ajili ya kuhakikisha mtuhumiwa anasaini?

Sio vyema kabisa kufurahia matumizi ya nguvu kwenye upekuzi au ukamataji. Hapa bado tunahitaji sana maaskari wetu wapewe body cams ili kuepusha mambo kama haya. Kesi inajengwa kwa ushahidi imara na sio wa kulazimishana
hapa tunaongelea admissibility of a certificate of seizure which the accused did not sign for whatever reason. kama kuna independent witness plus the searching officers, ni admissible. utazunguruka koote lakini utarudi tu kwenye point hii. msidanganye watu.
 
hapa kuna vitu viwili, iwe ni risiti au certificate of seizure,kama kuna ushahidi kwamba ulitakiwa kusaini ukagoma, na wapo mashahidi waliosaini kwenye certificate na wakaongea hivyo mahakamani, hiyo risiti itakubana tu hata ufanyeje. labda PP awe boya.
Wakili Yakubu ameeleza hivi;

Aidha, ni muhimu kujua kuwa ikiwa unapinga kuhusu kile kinachochukuliwa kuwa hukukutwa nacho ama hakikukutwa kwako basi usikubali kusaini fomu hiyo.

Hii ni kwasababu kukubali kwako kusaini fomu hiyo tafsiri yake kisherria ni kuwa umekubali kuwa umekutwa na hicho kitu.

Na endapo utafikishwa mahakamani basi fomu hiyo itawasilishwa kama ushahidi na kwasababu ulisaini basi ulikubali kuwa ulikutwa na kitu hicho.

Vinginevyo uwe unakubali kuwa ni kweli hicho kitu umekutwa nacho, basi hapo waweza kusaini. Lakini kama hukubali basi usisaini.
kama
 
hapa tunaongelea admissibility of a certificate of seizure which the accused did not sign for whatever reason. kama kuna independent witness plus the searching officers, ni admissible. utazunguruka koote lakini utarudi tu kwenye point hii. msidanganye
Alichosema wakili ni kuwa usisaini kama hukubali kukutwa na hivyo vitu au hukubali kuwa ni vyako. Wewe ulichojibu ni kuwa hata bila kusaini bado cheti kina maana, lakini wakati huohuo ukalazimisha mtu asaini kwa sababu hata asiposaini bado haitamsaidia.

Sasa kama hata asiposaini haimsaidii, kwa nini alazimishwe kusaini?? Sio kwamba saini yake itarahisisha kazi kwa upande wa huyo PP kuliko ambavyo asiposaini. Hakuna kinachodangwanywa hapa, kutosaini kunamsaidia mtuhumiwa kuliko ambavyo angesaini, ndicho anachosema wakili
 
Tatizo virungu aisee, acha kabisa, ukipigwa kimoja cha ugoko unaasaini tu lasivyo utapewa kilema cha kudumu
 
Wakili Yakubu ameeleza hivi;

Aidha, ni muhimu kujua kuwa ikiwa unapinga kuhusu kile kinachochukuliwa kuwa hukukutwa nacho ama hakikukutwa kwako basi usikubali kusaini fomu hiyo.

Hii ni kwasababu kukubali kwako kusaini fomu hiyo tafsiri yake kisherria ni kuwa umekubali kuwa umekutwa na hicho kitu.

Na endapo utafikishwa mahakamani basi fomu hiyo itawasilishwa kama ushahidi na kwasababu ulisaini basi ulikubali kuwa ulikutwa na kitu hicho.

Vinginevyo uwe unakubali kuwa ni kweli hicho kitu umekutwa nacho, basi hapo waweza kusaini. Lakini kama hukubali basi usisaini.
Wakili Yakubu ameeleza hivi;

Aidha, ni muhimu kujua kuwa ikiwa unapinga kuhusu kile kinachochukuliwa kuwa hukukutwa nacho ama hakikukutwa kwako basi usikubali kusaini fomu hiyo.

Hii ni kwasababu kukubali kwako kusaini fomu hiyo tafsiri yake kisherria ni kuwa umekubali kuwa umekutwa na hicho kitu.

Na endapo utafikishwa mahakamani basi fomu hiyo itawasilishwa kama ushahidi na kwasababu ulisaini basi ulikubali kuwa ulikutwa na kitu hicho.

Vinginevyo uwe unakubali kuwa ni kweli hicho kitu umekutwa nacho, basi hapo waweza kusaini. Lakini kama hukubali basi usisaini.
Nashukuru mkuu lakini heading yake haijakaa kimkakati.
 
Wataalamu wa mwandiko watafanya nini kugundua ni mimi nimeandika?..ikiwa nimebadilisha uumbaji wa herufi na nimebadilisha sign?..mfano mwandiko ulioandika kwa mkono wa kushoto ambao siutumii kuandika.
Unafikiri unachofikiri watu hawakufikiri?
 
Hivi una habari polisi wana kawaida ya ku-plant evidence?! Au sometimes mtu mwenye visasi na wewe anaweza ku-plant evidence halafu akakuripoti polisi!!

Anachosema ni kwamba, with your knowledge una uhakika kabisa kwamba, kwa mfano ndani kwako hakuna heroin, lakini ghafla wanakuonesha paketo ya heroin !

Hapo ndo unaambiwa goma kusaini kwa sababu ukishasaini, inakuwa umeshakubali kwamba hiyo bhangi ni wewe ndie uliweka!

Hakusema hivyo kwa sababu, hali hiyo inatokea katika mazingira ya kupandikiziwa evidence!! Kwa mfano, polisi anakuta kabisa pistol ikiwa chini ya godoro huku wewe ukiwa hujui imefikaje fikaje hapo... kumbe kuna mtu kakuchezea mchezo! Kwahiyo sio kwamba hujakutwa na hicho kitu, bali unakutwa nacho kabisa lakini hujui kimefikaje fikaje hapo!
Kuna mashahidi kadhaa wanakuwepo wanaotakiwa kujiridhisha kinachofanyika kina uhalali labda nao hao washawishiwe kukuruka
 
Hivi una habari polisi wana kawaida ya ku-plant evidence?! Au sometimes mtu mwenye visasi na wewe anaweza ku-plant evidence halafu akakuripoti polisi!!

Anachosema ni kwamba, with your knowledge una uhakika kabisa kwamba, kwa mfano ndani kwako hakuna heroin, lakini ghafla wanakuonesha paketo ya heroin !

Hapo ndo unaambiwa goma kusaini kwa sababu ukishasaini, inakuwa umeshakubali kwamba hiyo bhangi ni wewe ndie uliweka!

Hakusema hivyo kwa sababu, hali hiyo inatokea katika mazingira ya kupandikiziwa evidence!! Kwa mfano, polisi anakuta kabisa pistol ikiwa chini ya godoro huku wewe ukiwa hujui imefikaje fikaje hapo... kumbe kuna mtu kakuchezea mchezo! Kwahiyo sio kwamba hujakutwa na hicho kitu, bali unakutwa nacho kabisa lakini hujui kimefikaje fikaje hapo!
Unatakiwa kuwa makini sasa wewe mwenye nyumba na inashauriwa hata kuingia ndani utangulie wewe, hata chumbani tangulia wewe wengine wafuate hiyo bastola wataweka saa ngapi?

Polisi hawawezi kuhadaa ujumbe mzima wa watu zaidi ya watano wakugeuke utakuwa ulichokwa tu na mtaa wako
 
Unawajua Polisi wa Tz? Hujakaa sawa una mbata moja inakukalisha chini, ile unataka kujua ni yupi kakupiga unapigwa katafunua moja halafu unapewa pen usaini.
Hapo utajipima mwenyewe.


Labda wanawafanyia hayo wajinga wajinga wasojielewa!

Lakini nawashauri polisi hata wajinga wasiwatende kwa hiyana bali kwa haki na kanuni .
Msitumie ujinga wa mtu kama fimbo ya kumchapa nayo.

Zingatieni miiko yenu ya kazi.

Polisi haruhusuwi kumpiga au kumdhuru mtu kwa namna yoyote ile isipokuwa pale tu inapobidi kwa kujihami au kujilinda.

Anaweza ku apply minimum force pale mtuhumiwa anapokataa kutii amri bila kumdhuru au kumsababishia maumivu.

Hiyo ni kwa mujibu wa mkataba wa Haki za Binadamu ambao nchi yetu imeridhia na kuingia mikataba ya kimataifa kama mwanachama wa jumuia ya Madola.

WaTZ mnapaswa kujua hayo.

Polisi ni watu tu kama nyie wanalipwa kodi zetu watutumikie kwa kutulinda sisi na mali zetu.

Msiwaogope!

Kuwa Polisi ni mgawanyo wa majukumu na tunategemeana.

Kila binadamu anastahili heshima na Utu bila kujali chochote.
 
Una sign signature ambayo si yako ukifika mahakamani unawakata kiulaini,hakuna haja ya kubishana nao hawa jamaa ni wajinga kweli kweli wakiwa katika anga zao wanaweza kukuumiza vibaya kisa ubishi wa kijinga ambao mwisho wa siku ukitumia akili unawaacha kwenye mataa.

Je wakitaka Dole Gumba ?
 
Back
Top Bottom