Usilogwe ukaondoka nyumbani na kwenda usipopajua kwa kigezo cha kutafuta maisha

Usilogwe ukaondoka nyumbani na kwenda usipopajua kwa kigezo cha kutafuta maisha

Kak uwe makini Kuna lijamaa la twita huko linajita buyobe atakuaja kuiba hii story na kwenda kuuza huko telegrams. Kama alivyo iba story ya yoga huku wew ukiwa ujapata lolote story Ni nzuri Sana Bora ukaiuze tu kuliko kuleta huku bure

Fany kitu hi story uiuze upige pesa mambo ya bure bure ishapitwa na wakt

Ni hayo tu
Kuna uhusiano kati ya Buyobe na account ya yoga ,so take it easy broh
 
SEHEMU YA KUMI NA TATU

Ilipoishia,,,,,,,,,,,,,

Basi chuma ikaamsha taratibu, Sity akawa analikimbiza gari paka likatoka nje ya kituo, Basi gari ikakamata morogoro road, Sity tukamuacha kasimama tu pale kaduwaa gari inaondoka, Basi chuma ikaamsha Arusha moja hiyo

Endelea,,,,,,,,,,,,,,,,

Chuma ikawa inatambaa balaa, safari imeshika kasi, watu naona wana mzuka kinoma na safari, naona kama wana enjoy, tofauti kabisa na mimi, sina raha, mawazo kibao, pembeni nimekaa na mtoto mzuri wa kichaga lakini sina hata time nae ( Nilijua ni mchaga baada ya kusikia akiongea na simu kichaga),

Nipo zangu kimya sina story na mtu mara simu ikaita, kucheki nikakuta ni Sity anapiga, nikapokea, Akauliza tumefika wapi, Nikamwambia tupo mbali sana, maana hata maeneo mi siyajui huko njiani, Basi akasema yeye kalala anahisi kama anaumwa vile, nikamwambia aende basi akachek maleria, akasema wala si maleria , ni mawazo tu anawaza ataishi vipi bila mimi, Ana feel upweke hadi anaumwa, Nikamwambia tuombe Mungu tu mambo yakikaa fresh tutaonana soon, basi tukaingia porini porini huko hakuna network simu ikakata,

Basi safari ikaendelea, mara nikapitiwa na usingizi nikalala sana, Kuja kushtuka nakuta gari imesimama watu wanashuka, nikamuuliza yule dada wa kichaga, dada hapa wapi, Akasema Mombo watu wanashuka kwenda kula, kucheki saa ni saa saba, kwenye simu kuna miscall za Sity kama zote, Nikampigia, Akasema mmefika wapi, nikamwambia ndo tupo mombo sehemu ya kula panaitwa Liverpool, Akauliza, we umekula, nikamwambia mi hata hamu ya kula sina, akanibembeleza na kunisihi sana, kwamba nikienda kula hata yeye atapata faraja,

Basi nikaona isiwe shida, nisije nikamuudhi mtoto mzuri bure, nikashuka nikaenda toilet, nikatoka nikaenda kununua sambusa mbili za nyama na soda nikarudi kwenye gari nikatulia,

Basi watu wakarudi gari ikaamsha, tukafika moshi mjini kama saa kumi hivi, Basi likaingia stendi, wenye kushukia moshi wakashuka, Wakapanda wengine wanaoenda Arusha, Basi likakaa pale kama nusu saa hivi hatimae likaondoka, safari ya kuelekea Arusha ikaanza,

Tukafika Arusha kama saa moja hivi usiku, Nikashuka pale kama mtu anaejua anapoenda vile, ili machalii ya r yasije niona wakuja yakanidandia maana stori zao nnazo,

Basi nikazunguka zunguka pale stand mwisho nikaamua nikae kwenye vile vibanda vya abiria, Pembeni kuna mama mmoja kaweka vitu vyake pale anauza chakula, Nikamsalimia yule mama, nikamuuliza eti kiwanda cha nguo kipo maeneo gani, akasema kipo kisongo kinaitwa a to z, nikamuuliza ni mbali kutoka hapa, akasema ndio, ni nje ya mji, unapanda kihiace ( daladala) nauli mia tano, Nikamuuliza hivyo vihiace vipo hapa, akasema inabidi uende standi ndogo inaitwa kilombero, huko ndo kuna vihiace vinavyoenda nje ya mji, basi akanielekeza ilipo hiyo stand, ila nikaona hata nikienda saivi ni usiku ntapata shida tu huko, ni bora nitulie tu pale stand paka kesho asubuhi ndo nianze hizo mishe,

Basi nikatoa simu nikampigia Sity nimjulishe nimefika salama, tukapiga stori pale kidogo basi tukamaliza,

Pale stand abiria wanaolala pale ni wengi tu, wanaotoka maeneo ya mbali ambao wanasubiri magari ya alfajiri sana, basi nikawa sina wasiwasi,

Muda ulivyoenda nikaweka begi langu kama mto, nikatia mbonji pale kwenye benchi, ila nikawa nalala kwa machale, kila saa nashtuka shtuka wasije machalii ya r wakapita na mimi,

Basi asubuhi ikafika, nikaenda kwenye kamgahawa flani hivi nikaomba maji nikanawa uso, nikapiga chai pale fresh, Nikatoka nikashika njia kuelekea stand ya kilombero huku naulizia maana ni mbali kidogo,

Kufika pale daladala kama zote, basi nikaskia kisongo kiwandani!!, Kisongo kiwandani!!, Basi nikajua ndo hii na hicho kiwanda itakiwa ndo hicho cha nguo, basi nikazama ndani, badae kikajaa hicho kikaamsha,

Basi tukatembea weeee tukatoka nje ya mji kabisa, tukafika sehemu tukakata kushoto tukatembea kiasi hivi mara nikaskia wale wa kiwandani!!, wale wa kiwandani!!, basi tukashuka, abiria wengine wakabaki gari hiyo ikageuza tulipotoka,

Basi pale ndo kiwandani, kuna geti kubwa na walinzi hapo nje, sema geti ni la nondo kwaiyo ndani unapaona, ila ndani tena kuna geti jingine huko ndo huwezi kuona maana geti si la nondo,

Basi pale nje kuna maduka na vibanda vingi tu, Nikajivuta kwenye kibanda kimoja nikanunua soda nikakaa nakunywa huku nasoma mazingira, nikajaribu kumuulizia jamaa pale kuhusu chance za kazi pale kiwandani, akasema pale kila ijumaa wnakujaga hapo getini wanachukua watu, nikapiga hesabu siku hiyo ilikuwa jumatano,kwaiyo inabidi nisubiri paka ijumaa ndo nije,

Basi nikajaribu kumuulizia kuhusu wale jamaa zangu kama anawafahamu lakini wapi, basi nikakaa sana pale paka jioni wafanyakazi wakaanza kutoka, aisee!! ni wengi kichizi, basi nikawa nawaulizia kama wanawajua wale jamaa zangu ila hakuna hata mmoja anaewajua, Nikasema sasa hapa kazi ipo.,

Basi kigiza kikaanza kuingia, hapa sasa nitafute pa kulala, mfukoni nna kama elf 60 hivi na machenji, nikaulizia gest maeneo yale nikaambiwa gest paka kisongo,

Basi nikachkua boda pale buku paka kisongo, nikaulizia gest pale nikaelekezwa gest moja maeneo yale, nikafika nikaulizia chumba nikaambiwa single elf 5 nikasema fresh, basi nikapewa chumba nikaeka begi langu nikaenda kuoga, nikatoka nikaenda kucheki msosi huko road,nikala nikarudi zangu room, nikajilaza kitandani nikampigia Sity tukaanza kupiga story,

Itaendelea
Machalii wa r tungekusanukia, tungekusororesha moko moko by ngondi, una bahati arifu
 
SEHEMU YA KUMI NA TATU

Ilipoishia,,,,,,,,,,,,,

Basi chuma ikaamsha taratibu, Sity akawa analikimbiza gari paka likatoka nje ya kituo, Basi gari ikakamata morogoro road, Sity tukamuacha kasimama tu pale kaduwaa gari inaondoka, Basi chuma ikaamsha Arusha moja hiyo

Endelea,,,,,,,,,,,,,,,,

Chuma ikawa inatambaa balaa, safari imeshika kasi, watu naona wana mzuka kinoma na safari, naona kama wana enjoy, tofauti kabisa na mimi, sina raha, mawazo kibao, pembeni nimekaa na mtoto mzuri wa kichaga lakini sina hata time nae ( Nilijua ni mchaga baada ya kusikia akiongea na simu kichaga),

Nipo zangu kimya sina story na mtu mara simu ikaita, kucheki nikakuta ni Sity anapiga, nikapokea, Akauliza tumefika wapi, Nikamwambia tupo mbali sana, maana hata maeneo mi siyajui huko njiani, Basi akasema yeye kalala anahisi kama anaumwa vile, nikamwambia aende basi akachek maleria, akasema wala si maleria , ni mawazo tu anawaza ataishi vipi bila mimi, Ana feel upweke hadi anaumwa, Nikamwambia tuombe Mungu tu mambo yakikaa fresh tutaonana soon, basi tukaingia porini porini huko hakuna network simu ikakata,

Basi safari ikaendelea, mara nikapitiwa na usingizi nikalala sana, Kuja kushtuka nakuta gari imesimama watu wanashuka, nikamuuliza yule dada wa kichaga, dada hapa wapi, Akasema Mombo watu wanashuka kwenda kula, kucheki saa ni saa saba, kwenye simu kuna miscall za Sity kama zote, Nikampigia, Akasema mmefika wapi, nikamwambia ndo tupo mombo sehemu ya kula panaitwa Liverpool, Akauliza, we umekula, nikamwambia mi hata hamu ya kula sina, akanibembeleza na kunisihi sana, kwamba nikienda kula hata yeye atapata faraja,

Basi nikaona isiwe shida, nisije nikamuudhi mtoto mzuri bure, nikashuka nikaenda toilet, nikatoka nikaenda kununua sambusa mbili za nyama na soda nikarudi kwenye gari nikatulia,

Basi watu wakarudi gari ikaamsha, tukafika moshi mjini kama saa kumi hivi, Basi likaingia stendi, wenye kushukia moshi wakashuka, Wakapanda wengine wanaoenda Arusha, Basi likakaa pale kama nusu saa hivi hatimae likaondoka, safari ya kuelekea Arusha ikaanza,

Tukafika Arusha kama saa moja hivi usiku, Nikashuka pale kama mtu anaejua anapoenda vile, ili machalii ya r yasije niona wakuja yakanidandia maana stori zao nnazo,

Basi nikazunguka zunguka pale stand mwisho nikaamua nikae kwenye vile vibanda vya abiria, Pembeni kuna mama mmoja kaweka vitu vyake pale anauza chakula, Nikamsalimia yule mama, nikamuuliza eti kiwanda cha nguo kipo maeneo gani, akasema kipo kisongo kinaitwa a to z, nikamuuliza ni mbali kutoka hapa, akasema ndio, ni nje ya mji, unapanda kihiace ( daladala) nauli mia tano, Nikamuuliza hivyo vihiace vipo hapa, akasema inabidi uende standi ndogo inaitwa kilombero, huko ndo kuna vihiace vinavyoenda nje ya mji, basi akanielekeza ilipo hiyo stand, ila nikaona hata nikienda saivi ni usiku ntapata shida tu huko, ni bora nitulie tu pale stand paka kesho asubuhi ndo nianze hizo mishe,

Basi nikatoa simu nikampigia Sity nimjulishe nimefika salama, tukapiga stori pale kidogo basi tukamaliza,

Pale stand abiria wanaolala pale ni wengi tu, wanaotoka maeneo ya mbali ambao wanasubiri magari ya alfajiri sana, basi nikawa sina wasiwasi,

Muda ulivyoenda nikaweka begi langu kama mto, nikatia mbonji pale kwenye benchi, ila nikawa nalala kwa machale, kila saa nashtuka shtuka wasije machalii ya r wakapita na mimi,

Basi asubuhi ikafika, nikaenda kwenye kamgahawa flani hivi nikaomba maji nikanawa uso, nikapiga chai pale fresh, Nikatoka nikashika njia kuelekea stand ya kilombero huku naulizia maana ni mbali kidogo,

Kufika pale daladala kama zote, basi nikaskia kisongo kiwandani!!, Kisongo kiwandani!!, Basi nikajua ndo hii na hicho kiwanda itakiwa ndo hicho cha nguo, basi nikazama ndani, badae kikajaa hicho kikaamsha,

Basi tukatembea weeee tukatoka nje ya mji kabisa, tukafika sehemu tukakata kushoto tukatembea kiasi hivi mara nikaskia wale wa kiwandani!!, wale wa kiwandani!!, basi tukashuka, abiria wengine wakabaki gari hiyo ikageuza tulipotoka,

Basi pale ndo kiwandani, kuna geti kubwa na walinzi hapo nje, sema geti ni la nondo kwaiyo ndani unapaona, ila ndani tena kuna geti jingine huko ndo huwezi kuona maana geti si la nondo,

Basi pale nje kuna maduka na vibanda vingi tu, Nikajivuta kwenye kibanda kimoja nikanunua soda nikakaa nakunywa huku nasoma mazingira, nikajaribu kumuulizia jamaa pale kuhusu chance za kazi pale kiwandani, akasema pale kila ijumaa wnakujaga hapo getini wanachukua watu, nikapiga hesabu siku hiyo ilikuwa jumatano,kwaiyo inabidi nisubiri paka ijumaa ndo nije,

Basi nikajaribu kumuulizia kuhusu wale jamaa zangu kama anawafahamu lakini wapi, basi nikakaa sana pale paka jioni wafanyakazi wakaanza kutoka, aisee!! ni wengi kichizi, basi nikawa nawaulizia kama wanawajua wale jamaa zangu ila hakuna hata mmoja anaewajua, Nikasema sasa hapa kazi ipo.,

Basi kigiza kikaanza kuingia, hapa sasa nitafute pa kulala, mfukoni nna kama elf 60 hivi na machenji, nikaulizia gest maeneo yale nikaambiwa gest paka kisongo,

Basi nikachkua boda pale buku paka kisongo, nikaulizia gest pale nikaelekezwa gest moja maeneo yale, nikafika nikaulizia chumba nikaambiwa single elf 5 nikasema fresh, basi nikapewa chumba nikaeka begi langu nikaenda kuoga, nikatoka nikaenda kucheki msosi huko road,nikala nikarudi zangu room, nikajilaza kitandani nikampigia Sity tukaanza kupiga story,

Itaendelea
Machalii wa r tungekusanukia, tungekusororesha moko moko by ngondi, una bahati arifu
 
SEHEMU YA KUMI NA TANO

ilipoishia,,,,,,,,,,,,,

Kweli kesho ikafika, Daah ni siku ambayo sitakaa niisahau maishani mwangu, yani yaliyonipata siku ile ni Mungu tu aliingilia kati, daah!! We acha tu, Basi bana siku ilianza fresh tu yaani,kulipambazuka vizuri nikajiandaa pale niende zangu moshi,

Endelea,,,,,,,,,,,,

Nikachomoka kiwandani nikapanda daladala pale nje huyoo paka town, Nikashuka pale nikadandia kosta ya moshi nauli buku mbili fresh,

Nikafanikiwa kufika moshi town pale, basi nikaona hieace za majengo, nikamuuliza konda zinafika majengo secondary akasema eeeh!! panda twende, Nikapanda pale ngoma ikajiachia hiyoo,

Basi tukafika sehemu konda akasema we wa sekondary sogea mbele, basi nikajivuta mbele, mara gari ikasimama nikashuka, Kumbe shule ipo njiani kabisa haina hata haja ya kuulizia, Maana nliposhuka tu nikaona wanafunzi, nikaona na kibao Majengo Secondary school nikasema yes mambo si ndo hayo, maana mi nlijua kuna mambo ya kuchukua bodaboda,

Basi nikasogea pale getini nikakuta mlinzi pale, nikamwelezea shida yangu, basi mlinzi akaniambia, bwana hata nikikuruhusu kuingia hutofanikiwa sababu mwalimu mkuu wiki ya pili sasa hayupo, Kaenda dodoma kwenye vikao vyao, na yeye ndo muhusika mkuu, Nikushauri tu uende alafu urudi siku nyingine, Basi nikasema sawa,

Basi nikaondoka zangu sijui hata nielekee wapi, Wakati nawaza au nirudi zangu nikapande gari nirudi Arusha basi nikaona upande wa pili zile fremu za maduka zilivyojipanga lazima zitakuwa zimezunguka uwanja wa mpira,

Basi wazo likanijia niingie huko ndani uwanjani, Basi kuna kageti hivi nikaingia kweli bana ni uwanja mkubwa sana wa mpira, Basi nikawa natembea tembea huko uwanjani na begi langu mgongoni,

Sa wakati natembea nikahisi kama kuna watu nyuma yangu, ile kugeuka hivi kweli bana kuna majamaa mawili yananifata, Nikipinda kushoto nao wana pinda, nikienda kulia nao wanaenda nikasema hawa ni vibaka, sasa hapa cha msingi ni kufunga mota tu, Basi kwa mbele kule kulikuwa kuna dada mmoja na yeye anapita pale uwanjani, Nikasema nikimbilie alipo yule dada,

Basi nikatoka nduki hiyo, jamaa wakaanza kunikimbiza, sasa wakawa wanapiga makelele kamata mwizi huyo!!, kamata mwizi huyoo!! , Basi yule dada alipogeuka akaniona nakimbilia ule upande wake akajua mi ndo mwizi, acha aachie yowe hilo, mwiziiii!!! Mwizi!!! huku anakimbia, heeeh! , Mara naona watu hao wanatoka pande tofauti tofauti wananikimbiza, basi nikasema nisimame, wale vibaka wakanikamata wakaanza kunipiga, wakachukua lile begi langu,
wananipiga wanasema mi mwizi,

Basi watu wakajaa nikaanza kupigwa, Najitetea jamani mimi si mwizi, wezi ni wale wamechukua begi langu, hakuna mtu ananisikiliza, Nikapigwa mtama huo,Nikaanguka chini, nikapigwa, Nikakatwa katwa, najaribu kujitetea hakuna mtu ananisikiliza, mwenye jiwe, mwenyet fimbo, mwenye rungu, mapanga ndo usiseme, nilipoona nimezidiwa nikainama chini wapige tu sehemu zote lakini si usoni,

Basi nikapigwa sana, yaani namaanisha sana yani, Mwili wote umetapakaa damu, basi mi nimejiinamia nalia tu, Nalia paka makamasi yanatoka yanachnganyikana na damu, Nasema jamani mnaniua mimi nimewakosea nini, msiniue jamani mimi si mwizi,

Basi nilipigwa na kitu hicho mgongoni nahisi ni tofali lile, nikasikia kama uti wa mgongo umevunjika yaani, nikajinyoosha nikalala na tumbo, hapo sa ndo naona nakufa sasa, maana nalia hata sauti haitooki, Watu hawajui mzee, waoo wanapiga tu, basi sasa nikawa siskii tena hata maumivu, wanapiga mi hata siskii,

Mara macho yakaingia nuru flani hivi kama miale ya jua la jioni, Basi nikawa naona kama naelea angani vile, Mara nikamwona Sity anakuja kunikumbatia anatabasamu na vidimpo vyake vile, Mara namwona Da J kama ananipa mikono hivi anipokee, Mara anatokea mama kama ananiita vile, namwona baba na yeye, Mara nikaona watu kama malaika hivi wanakuja kunichukua, mara wakapotea, nahisi fahamu zikawa zimenirudi nikawa naskia kelele za watu, kumbe bado wanajipigia tu mi sijui,

Basi nikaona kama nimekalishwa hivi, nikahisi kitu kama tairi nimevalishwa huku nikekaa, Mara namwagiwa kama maji hivi kumbe ni mafuta taa, nikajaribu kufungua macho kwa mbali nikaona watu wamenizunguka, mmoja ana kibiriti anahangaika kukiwasha, Basi nataka nimwambie nisamehe usifanye hivyo ila mdomo haufunguki, nataka ninyooshe mkono nimzuie ila siwezi, Mara nikapigwa na kitu sjui ni nini, kuanzia hapo ndo sikujua nini kiliendea tena, nikawa nimefloot,

Itaendelea
😔
 
Dawa ya bibi bagamoyo inafanya kazi bibi yupo vizuri alisema aliyeiba arudishe laptop akifunga hafungui
 
Dah hii sehemu ya mwisho imenisononesha Sana.

Wengi wanauwawa bila kuwa na hatia yoyote. Wezi wanaosingiziwa wanakufa vifio vby Sana. Nahisi na vyeti vilipotelea hapo naama nakumbuka nilisafiri nchi za mbali na vyeti vyangu, ilikuwa kama MTU akichukua begi bas ndio amechukua kila kitu changu..

nashukuru ilikuwa vyeti na nilifanikiwa kuvitumia kuapply abroad.

Ndg stori yako imetulia ila tuambie ni true story au ni chai??
 
Back
Top Bottom