Usimkopeshe mtu kuanzia leo 1-6-2024 mpaka Disemba 31, halafu utaona amani itavyorudi moyoni

Usimkopeshe mtu kuanzia leo 1-6-2024 mpaka Disemba 31, halafu utaona amani itavyorudi moyoni

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
15,835
Reaction score
23,776


xxxxxxxxxx.jpeg


Ndugu Mtanganyika , usimkope ndugu yako hela kwa sababu kuna hatari ya kuharibu uhusiano wenu. Kukopa hela kwa ndugu kunaweza kusababisha migogoro na mvutano, hasa kama kuna tatizo la kulipa deni kwa wakati au kama kutakuwa na hali ya kutokuelewana juu ya masharti ya mkopo.

Ndugu huyo utakuwa mtumwa kwake, ukimpihgia simu hata kwa jambo lisilojusu deni hatopokea simu , atakwambia yupo busy na mmambo kama hayo.

Lakini atakusema vibaya kwa mke wake au mume, kwa jamii na kukufanya adui zake.

Badala ya kukopa hela, jaribu njia nyingine za kutatua matatizo yako ya kifedha, kama vile:

Kuanzisha Bajeti: Angalia mapato na matumizi yako na uone kama kuna maeneo unaweza kupunguza gharama.​
  1. Kazi za Ziada: Tafuta kazi za muda au njia za ziada za kuongeza kipato chako.​
  2. Kuomba Mikopo Benki: Angalia uwezekano wa kupata mkopo kutoka benki au taasisi nyingine za kifedha.​
  3. Misaada ya Kijamii: Tafuta mipango ya serikali au mashirika yasiyo ya kiserikali ambayo inaweza kusaidia katika hali yako ya kifedha.​
 
Kukopesha mtu hela ni mbaya,hela yako itakutesa kuipata wakati wa kuidai
Unajengewe chuki, unasimangwa, anakufanya mpaka usinhizie una msiba ama wazazi wahgonjwa ili tu ulipwe haki yako.
 
Ahahaha 😭😭😭
Yaani pesa yako unakuwa mnyonge na kupanga gear ya kumfuata madeni wako
 
Mjomba ,rafiki wa karibu na Mimi hatuko kama zamani baada ya kulia shida sana ,nikafungua moyo nikamkopesha huu ni mwaka hata story hatupigi ,nikimpigia haishiwi ubize ,mwisho kaniachia huzuni kuu
 
Back
Top Bottom