Kabla haujaogopa saaaaaana, bwana
DeMostAdmired tazama faida zote hizi anazopata mtu kwa kuwa na upungufu wa kinga mwilini.....
Yas! Ni faida za
UKIMWI mwilini. Tena kuna makosa ya kiuandishi ningeandika tu faida za UKIMWI. Au basi faida za UKI mwilini. Nadhani tumeelewana kuwa ninazungumzia Upungufu wa Kinga MWILINI. Nafanya hivi nikiamini kwamba kuhusu suala la hasara mtakuwa mpo vizuri. Hasara za kinga mwilini kama huzijui unaweza kutafuta mtandaoni kuna majarida mengi tu kuhusiana na hilo suala.
So zifuatazo ndo faida za ukimwi kama ulikuwa hujui;
1. Humsaidia mama mjamzito kuishi na mtoto tumboni kwa amani; mtoto tumboni kwa mjamzito huwa ni kiumbe kingine hivyo mama alipaswa kutumia kinga yake kukishambulia hicho kiparasite. Lakini ataishusha ili akilee maana anakipenda. Asanteni sana mama zetu kwa upendo. Japo mnapata madhara kama vi UTI, fangasi na malaria lakini hamjali – asee nani kama mama?
Hii ndiyo sababu ni muhimu kwa mama mjamzito kupata kinga na tiba na kingatiba dhidi ya magonjwa mbalimbali kama maralia na pepopunda ili kujilinda yeye pamoja na mtoto wake. Afanye hivi badala ya kutegemea kinga yake maana ipo inapunguzwa kimakusudi kabisa.
2. Humsaidia binti kushika ujauzito kwa kuwezesha shahawa ziishi; Mambo mengi yanahusika na kushusha kinga ya mwili kwenye via vya uzazi ili visishambuliwe bali viogelee hadi vikatungishe mimba. Baadhi ya kemikali zipo kwenye shahawa zenyewe ikiwamo vikinza-asidi na vishusha kinga humohumo. Mwanamke pia anayo nafasi ya kuruhusu hayo yatokee ndio maana akiwa hajampenda sana mwanaume kuna uwezekano wa kuviua vyote asishike mimba, au kuviua vya kiume akabakiza vya kike. Hata uasidi katika njia ya kike hutofautiana kulingana na ‘amsha’ aliyonayo mwanamke. Na katika hali ya uasidi mbegu nyingi zinazokufa ni za kiume kuliko za kike au zote kwa pamoja.
Nadhani hii ni moja ya sababu kwa nini ubakaji mwingi haupelekei mimba, na vikizaliwa vingi vinakuwa vitoto vya kike. Usichukue mojakwamoja maneno yangu lakini, chunguza na wewe.
3. Humsaidia mwenye wapenzi wengi kuvumilia aina mbalimbali za bakteria za wapenzi wake; Wapenzi wanapaswa kushare wadudu walionao au at least kutopambana na wadudu waliopo katika biological profile ya wapenzi wao. Ukiwa huna mpenzi kinga yako inabakia yako huruhusu mdudu mwingine inavumilia wadudu ulionao tu. Ukiwa na mpenzi mmoja utavumilia wako na wa huyo mpenzi wako. Ukikataa unakuwa na aleji nae ohoo!! Wakiwa wengi labda saba unawavumilia wooote hao kiasi ambacho kinga yako inabidi iwe chini sana kuliko kawaida……. Ndiyo unaitwa upungufu wa kinga mwilini.
Sasa kutokana na tafiti zinazoendelea inaonesha kwamba kila mwanadamu anazo aina tofauti tofauti za wadudu/bakteria mwilini mwake. Inaitwa microbiome. Kwa hiyo kila mpenzi anayo mamilioni ya bacteria ambao wengine unao na wengine ni wapya kabisa kwako. Na ili muishi pamoja basi inawapasa kuvumiliana na zaidi kushirikishana kila mmoja akimgawia mwenzake na kupokea asichonacho.
Pata hii hint: ‘As many as 80 million bacteria are transferred during a 10 second kiss, according to research published in the open access journal Microbiome. The study also found that partners who kiss each other at least nine times a day share similar communities of oral bacteria.’
4. Humsaidia teja maskini kupata high ya dharula bila kujiua; Kuna mtindo wa mateja wenye arosto bila hela kunyonya damu ya mwenzake na kujidunga na yeye ili apate raha. Sasa kama kundi la damu ni tofauti kinga ya mwili ingepambana na angepata kitu kinaitwa kuganda-kwa-damu-kulikosambaa-mwili-mzima na kufa! Lakini ikiwa kinga yake ya mwili ni ndogo ataivumilia hiyo damu nyingine hivyo ataishi.
Lazima utambue kuwa madawa ya kulevya na pombe ni moja kati ya vitu vinavyoweza kuoelekea upungufu wa kinga mwilini hasa madawa ya kulevya. Mtumiaji wa madawa ya kulevya anaweza kusumbuliwa na magonjwa ya watoto kama vile pneumonia kwa sababu ya kuwa na kinga pungufu. Jitahidi usiingie katika mtego huu ndugu.
5. Humsaidia mwenye kifua kikuu au maambukizi sehemu nyingine nyeti kuishi badala ya kupageuza uwanja wa vita halafu afe; Tunafahamu kwamba moja ya chanzo cha kifo kwa wagonjwa wa corona ni kupigana vita sehemu nyeti. Mpambano katika mapafu husababisha mapafu kuvimba na kujaa maji na kifo. Mpambano katika damu husababisha damu kuganda mwili mzima. So ukiwa na kinga kubwa ni hatari kama mdudu kakaa sehemu mbaya. Hili linazingatiwa sana haswa kwa wagonjwa wa kifua kikuu hutibiwa kifua kikuu kwanza kabla ya kuanza kupandisha kinga ya mwili la si hivyo watapata kuzidiwa kutokana na kuamka ghafla kwa kinga ya mwili. So kinga ndogo hapa ni faida.
Utafiti ungefanyika kuona kiwango cha minyoo na vitu vingine vinavyopunguza kinga ya mwili na madhara ya ugonjwa kama uviko. Ili siku nyingine tujiandae vizuri zaidi.
6. Husaidia kupunguza usumbufu na kutibutibu vimagonjwa vidogo na visivyo na maana mfano aleji; Mtu mwenye kinga ndogo ya mwili hapati vialejialeji kwa vitu visivyo hatari. Na hata kwa magonjwa hatari hatapata dalili zozote hadi ugonjwa uwe siriazi kidogo. Mfano maralia itakaa, ikipiganwa chinikwa chini ikiwa zembe itapigwa ikiwa siriazi ndio jamaa atajua atameza vidonge. Hali ni tofauti kwa mwenye kinga kubwa maana yeye kidogo tu mara kajiskia vibaya, mara kichwa kinauma halafu mara kimepona. Si bora asingejua tu kila mtu akafanya kazi yake bhana aah!.
Tafiti zinaendelea namna ya kupunguza kinga za mwili kwa baadhi ya watu mfano kuwapa minyoo au dawa ili kinga ipungue. IBS, Crohns disease ni magonjwa yanayosumbua mfumo wa mmengenyo wa chakula.
7.
Humsaidia aliyepandikizwa kiungo aishi nacho kwa amani bila kukiua. Kama nilivyozungumza kwa mama mjamzito kitu cha nje kisichokuwa wewe huwa kinapaswa kupigwa. Lakini kama kinakusaidia ni busara zaidi ukikivumilia na kujifunza kuishi nacho. Ndio maana mtu akipandikizwa figo hupewa dawa za kushusha kinga ya mwili kwa muda.
8.
Humsaidia mtu binafsi kuishi na aina nyingi zaidi za wadudu mwilini; Na huu ndiyo unaitwa utajiri wa bioanuwai mwilini. Unakuta mtu anao bakteria wa kuzuia UTI, bakteria wa kumen’genya maziwa na wa kuvunja sumu mbalimbali hivyo anakuwa na ujamaa wa kujitegemea/self sufficiency/self reliance. Mfano ngombe anao bakteria wa kumen’genya majani tumboni ndo maana ukimpa antibiotic mdomoni anaweza kufa!
9.
Husaidia mtu kuwa mpole na amani itawale mwilini; I mean seriously mwili unakuwa unajisamehe kwa urahisi zaidi badala ya kujishambulia [autoimmunity]. Maana autoimmunity mda mwingine inatokea kwa labda sehemu ya mwili inaenda sehemu ambako siko [uzururaji wa seli] kinachotakiwa pale ni kuvipa adhabu hivyo viseli vinavyozurula tu basi. Sio unavipiga vyenyewe unawapiga na wazazi wake[kwamba wao ndo wamemfundisha ujinga] unaenda unaanza kuwapiga na wajomba zake na rafiki zake jamanii!? Hasira mbaya mwilini. Mfano mtu akipigwa ngumi ya jicho baadhi ya viprotini vikasambalia kwenye damu, vidhibitiwe hivyo tu. Sio kupitiliza hadi kushambulia jicho lote na mbaya zaidi kwenda kushambulia jicho lingine ambalo hata halikuhusika.
Ni hayo machache kwa leo. Labda nimalizie na baadhi ya njia zinazoweza kusaidia kurekebisha kinga mwilini
1. Homoni, 2. Madawa, 3. Vinasaba, 4. Virusi, 5. Vilevi, 6. Minyoo, 7.Lishe, 8. Mawazo, 9. Experience/umri
May 16,
Madaktare mtusaidie kucrarify kidogo hapo
mbarika Lukonge DR Mambo Jambo @dr*
Herbalist Dr MziziMkavu
Na
mshamba_hachekwi