Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Wataalamu wa upasuaji wamegundua kuwa kuondoa nywele kwenye eneo la mwili kabla ya kufanya upasuaji, kunaongeza hatari ya athari na maambukizi katika ngozi.
Imeelezwa kuwa unaponyoa nywele zote ktika maeneo ya sehemu za siri, unaongeza hatari ya maambukizi na huchoche bakteria kuingia ndani ya mwili kupitia vitundu vidogo vinayoachwa baada ya nywele hizo kuwa zimenyolewa.
Vile vile, kunyoa nywele zote za maeneo ya siri huongeza hatari ya maambukizi ya magonjwa ya ngono kutokana na majimaji yanayokuwepo wakati wa ufanyaji wa mapenzi kupenya katika vitundu vidogo vilivyobakia baada ya nwele hizo kunyolewa.
Kunyoa nywele za sehemu za siri kunaweza kukusababishia muwasho na kukuletea kero hata unapokuwa mbele za watu. Hebu fikiria umenyoa nywele za sehemu za siri halafu uko mbele ya mkutano kazini, mara ghafla unapatwa muwasho katika maeneo ya siri na makwapa. Unadhani unapatwa na hali gani? mfadhaiko unaoupata unaweza kukuletea fedheha kubwa.
Nywele za sehemu za siri huwa na kazi ya kuizuia ngozi dhidi ya michubuko, pamoja na bakteria mbalimbali ambao wanaweza kushambulia maeneo nyeti. Vile vile nywele kama za makwapa hudanya kazi ya kufyonza jasho linalotoka ili lisitiririke katika maeneo mengie ya mwili wako.
Uamuzi ni wako. Ikiwa utaamua kunyoa nywele za sehemu za siri ama la, hiyo ni juu yako. Lakini kumbuka kujiweka safi musa wote na kuhakikisha kuwa mwili wako unakuwa nadhivu na wenye afya.
zotekali blog
Imeelezwa kuwa unaponyoa nywele zote ktika maeneo ya sehemu za siri, unaongeza hatari ya maambukizi na huchoche bakteria kuingia ndani ya mwili kupitia vitundu vidogo vinayoachwa baada ya nywele hizo kuwa zimenyolewa.
Vile vile, kunyoa nywele zote za maeneo ya siri huongeza hatari ya maambukizi ya magonjwa ya ngono kutokana na majimaji yanayokuwepo wakati wa ufanyaji wa mapenzi kupenya katika vitundu vidogo vilivyobakia baada ya nwele hizo kunyolewa.
Kunyoa nywele za sehemu za siri kunaweza kukusababishia muwasho na kukuletea kero hata unapokuwa mbele za watu. Hebu fikiria umenyoa nywele za sehemu za siri halafu uko mbele ya mkutano kazini, mara ghafla unapatwa muwasho katika maeneo ya siri na makwapa. Unadhani unapatwa na hali gani? mfadhaiko unaoupata unaweza kukuletea fedheha kubwa.
Nywele za sehemu za siri huwa na kazi ya kuizuia ngozi dhidi ya michubuko, pamoja na bakteria mbalimbali ambao wanaweza kushambulia maeneo nyeti. Vile vile nywele kama za makwapa hudanya kazi ya kufyonza jasho linalotoka ili lisitiririke katika maeneo mengie ya mwili wako.
Uamuzi ni wako. Ikiwa utaamua kunyoa nywele za sehemu za siri ama la, hiyo ni juu yako. Lakini kumbuka kujiweka safi musa wote na kuhakikisha kuwa mwili wako unakuwa nadhivu na wenye afya.
zotekali blog