Usiombe uumwe USA

Usiombe uumwe USA

Sisi huku tuna afya tele tunavimbiwa, hospitali kibao unaandikiwa dawa pharmacy kila kona. Daladala tuna mpaka treni sikuizi, bado ya ndege kwenda moshi mbeya mwanza kila mahali magufuli yupo bwana na mwakyembe wataleta kwanini mnapata shida huko si mrudi huku simu sio lazima uweke hela unaweza kuwa una beep tuu unapigiwa nyie mpaka mlipe! Kila mahali hapa ukibanwa mkojo unakojoa njooni huku waachieni mashida yao!
Maboga, mihogo, mahindi. Maharage mabichi weee njooni. Kuna ng'ombe wa kupeleka kwa dume kule home njooni tusaidiane
Njooni bwn msitesekee kwa watu kwani huko mnafanya nini. Wazee wete majukumu yamewazidi huku magogoni mje kuwasaidia.

Hivi hotuba za kila mwisho wa mwezi huwa bado zinafanyika .... Hii inafanania!!
 
kweli nakubali ukiumwa na ukienda kunakohusika hata kama huna karatasi utapatiwa matibabu
 
Kuna mdada mmoja mkenya aliumwa 2 weeks saa hizi nyumba hajalipa gari umeme na maji an simu .na kazi Hana Leo kuna kikao cha kumchangia.maisha gani hayo siheri Arudi Kenya tu .unaumwa week 2 tu unakutwa na drama lote hilo.kuishi paycheck to paycheck no heri urudi bongo
nDIO MAANA mAREKANI NI nCHI TAJIRI KUPITA ZOTE DUNIANI. nA sISI NI MASIKINI KUPITA NCHI ZOTE ZILIZOFUATA UKOMUNISTI. Kulipa nyumba na bili za simu, maji, umeme ni lazima kwa kila mpangaji. Tena hakuna excuse. Ila ukiwa na matatizo ya kuachishwa kazi na unakabiliwa na matatizo mengi kimaisha , kuna mahali kwingi sana sana kwenda kupata misaada. Hapa New York city,, kuna sehemu inaitwa workforce, hapo unapewa food stamp na kucollect unemployment wages kwa siku kadhaa. Hakuna shida kabisaa wala Njaa hapa marekani. labda huyo dada alikuwa kazini wiki moja tuu na hakumaliza three months probabation.

wewe usiombe kuishi marekani. Mwarabu wa saudi, Iraq, Bahrain, UAE na Libya, anafanya bahati nasibu ya Gree card masaa 24 ili aje aishi marekani ingawa nchi zao huzalisha pesa utafikiria wanatungua na makota mtini.

Hakuna mtu asiyependa kurudi tanzania. Ila upatikanaji wa kazi ni finyu na madawa ya kujitibu ni fake sana, je hili linavutia kweli kuja tanzania?huku kama umejikata, kutoa jino, operation ndogo, kukamuliwa jipu, kuna dawa za pain killer, ambazo unapewa kufuta maumivu. Utamu wa dawa hizo na raha yake, ni mara tano ya kulala na msichana. Je bongo dawa hizo zipo kweli ? na kama zipo si zitakuwa fake. mimi nemishi dar, sasa nataka nikirudi, nikaishi Sumbawanga au katavi, je ni raisi kupata kazi huko au ndo nilazimike kuja ishi dar tena?
 
Shida ya huyo dada ni kutokuwa na makaratasi kwa hiyo haki zake zote anapoteza..

Lakini hauwezi kulinganisha huduma za afya zinatolewa US.ukalinganisha na India,ndiyo maana mafisadi wetu wote wanakimbilia India.Wambie waende US kama wanajeuri..
 
Health insurance inalipwa kazini automatically
40 million Americans have no health insurance, don't they have jobs to cover their insurance?

Vitu vingi ambavyo masikini wa US wanaaford, msomi ofisa wa bongo ni kama luxury, like a show off thang.
Vitu vingi vitu gani, taja kimoja ambacho ofisa wa Bongo anashindwa ku afford halafu illiterate wa USA anaweza. Naanza mimi kutaja, ofisa wa Bongo anajenga nyumba, masikini wa US anaweza kujenga au kununua nyumba cash?
 
nakubaliana na kila mtanzania kuwa nchi yetu inajengeka vizuri na communication net work zinavutia. Lakini uingizaji wa bidhaa feki CHina, Malaysia, Taiwan na Indonesia, umekomeshwa? Halafu unakuta kiongozi anachekiwa afya India na kurudi bongo. Kwa nini asiagize vile vifaa toka india na aje avitumie hapa bongo ili wengi wanufaike? Mambo kama hayo hutukatisha sana tamaa kuja ishi Bongo ila piga pigiika, radha ya vyakula vya bongo inavutia sana na kweli tunaimiss.
vyakula kama kisamvu cha sombe, samaki wa kavu kutoka kigoma, sanbusa, vitumbua,kalmati, bagia,matembele,wali kwa nyama za ngombe/kuku wa bongo radha yake ni nzuri sana. halafu nyama za ngombe wa bongo unaweza kutafuna mara sita kabla ya kumeza. Ila nyama za hapa ni raini sana(tender) hula kama keki. Ukitafuna mara moja ishasagika jinoni!
 
Bongo ukikomaa unatoka ile mbaya uvivu wenu tu ndo unawatangisha tangisha. bongn una uwezo wa kuwa na shamba nyumba na miradi hata kama unalipwa kima cha chini ni kukomaa tu.
 
Kuna mdada mmoja mkenya aliumwa 2 weeks saa hizi nyumba hajalipa gari umeme na maji an simu .na kazi Hana Leo kuna kikao cha kumchangia.maisha gani hayo siheri Arudi Kenya tu .unaumwa week 2 tu unakutwa na drama lote hilo.kuishi paycheck to paycheck no heri urudi bongo
Hana insurance?
 
40 million Americans have no health insurance, don't they have jobs to cover their insurance?

Vitu vingi vitu gani, taja kimoja ambacho ofisa wa Bongo anashindwa ku afford halafu illiterate wa USA anaweza. Naanza mimi kutaja, ofisa wa Bongo anajenga nyumba, masikini wa US anaweza kujenga au kununua nyumba cash?
mmarekani kwa sababu ya kupenda raia zake haibi ili kujenga nyumba. yeyey hukopa benki na kulipa kwa miaka kama kumi au ishirini taratibu. Lakini huyo ofisa wa bongo lazima adhurumu haki za raia milioni arobaini, akafiche pesa zao uswiss halafu ajenge nyumba. Unakataa ukweli huu mkuu mwenzangu?

Wizi uliotokea benki kuu, mikatataba feki ya madini gharama zake unaweza kununua ndege za F16 ishirini na sita na misiles zake.

Tazama daraja la kigamboni tulivyotapeliwa. Huwezi kujenga daraja kama hili ili yapishane magari mawili. hapo ni lazima yawe yanapisha magari manne. Halafu daraja hili ni jembamba sana haliwezi kukidhi haja ya wingi wa magari tanzania. hapa New York city, kuna daraja la brocklyn linalounganisha manhatan na broklyn. lilijengwa mwaka 1958 likiruhusu magari nane kupisha. Yaani maane upande mmoja na manne upande mwenginewe. Halijawahi kuwa kero tangia mwaka 1958. sasa wewe angalia hilo la kigamboni.

Limeanza kuwa kero kabla ya hata kumalizika. halafu sijaona njia za wapita kwa miguu zikiwa pana au pengine hazipo. unaona hatari yetu sisi wabongo. Upo tayari kuiba pesa bila kujali madhara yatakayotokana na wizi wako. Hapo magari yakigongana basi abilia wote watazama kirahisi kwa wembamba wa barabara.
 
mmarekani... hukopa benki na kulipa kwa miaka kama kumi au ishirini taratibu. Lakini huyo ofisa wa bongo lazima adhurumu haki za raia milioni arobaini, akafiche pesa zao uswiss halafu ajenge nyumba. Unakataa ukweli huu mkuu mwenzangu?
Nyumba gani hiyo Marekani inalipwa deni ndani ya miaka kumi? Si kila mtu na shangazi yake angekuwa na nyumba. Nambie uliweka down kiasi gani na interest ni kiasi gani na bei ya nyumba ni ngapi na uliinunua Marekani ya wapi hiyo nyumba? Unless ni trailer park la kuvuta na lori.

Wastani wa miaka ya kulipa deni la nyumba Marekani ni miaka thelathini na ushee, sio kumi ishirini, tuambiane ukweli jamani.

Na sio kila mjenzi Tanzania ana akaunti ya wizi Uswizi. Ukisema kujenga Tanzania lazima uibe basi huijui Tanzania.

hapa New York city, kuna daraja la brocklyn linalounganisha manhatan na broklyn.
Brocklyn na Broklyn ndio nchi gani hizo mkubwa?
 
Naomba msinitishe mwenzenu hapa nina tiketi ya kuelekea huko.............!!! Ohooooooo tusiharibiane image jamani.
 
Health insurance inalipwa kazini automatically .......

Ingelikuwa rahisi hivyo kusingekuwa na watu wasiokuwa na heath insurance.

Kwanza sio kila mtu mwenye kazi, na sio kila mwenye kwenda kazini anakatiwa health insurance huko.
 
Mwenzako akinyolewa na wewe unatia maji, je na nyie wachangiaji hamuishi ki-'paycheck to paycheck'? Yaweza kuwakuteni hayo hayo, manake maradhi hayana mwenyewe...
 
Hakuna shida kabisaa wala Njaa hapa marekani......
Na wale homeless?

huku kama umejikata, kutoa jino, operation ndogo, kukamuliwa jipu, kuna dawa za pain killer, ambazo unapewa kufuta maumivu. Utamu wa dawa hizo na raha yake, ni mara tano ya kulala na msichana. Je bongo dawa hizo zipo kweli ? na kama zipo si zitakuwa fake.

Seriously?! Duh!

Are you sure you are not an addict?
 
JAMANI KUMBUKENI HATA NYIMBO ZA WASANII WENU... MF. NARUDI NYUMBANI By REMMY ONGALA. Ukiusikiliza lazima urudi bongo bana. Bongo heshima wakuu huko chumeni then mrudi mfurahie life nyumbani kwa raha.
 
40 million Americans have no health insurance, don't they have jobs to cover their insurance?

Vitu vingi vitu gani, taja kimoja ambacho ofisa wa Bongo anashindwa ku afford halafu illiterate wa USA anaweza. Naanza mimi kutaja, ofisa wa Bongo anajenga nyumba, masikini wa US anaweza kujenga au kununua nyumba cash?
Mkuu watu wengi wako brain washed.. hawajijui wala kujitambua tena kwa Ugonjwa wa nchi zilizoendelea ndio maana saa zingine huleta ndoto hapa!!! Wanasahau kiwango cha watu wasio na makazi na kuishi kwenye mazingira magumu ni USA!! Wanasahau kuwa bongo ni salama zaidi kuishi kuliko USA!!
 
nichangien nini miye marekani c hijui zaidi ya kwenye movie, hata ndege tu sijawai panda zaidi ya lift ya helcopter ya maafa niliyoombewa msaada na mpwa mpaka mwanza. ha ha aha

-ila nasikiaga ni BORA kuzaliwa MBWA ulaya kuliko kuzaliwa mtu AFRICA
 
Back
Top Bottom