Usipende kununua magari yaliyotumika Tanzania

BIG THINKER

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2018
Posts
680
Reaction score
1,436
Hii nakupa tu ushauri wewe unayetaka kumiliki gari lako na lisikupe mawazo ya kuonana na mafundi Kila siku.

Asilimia 85 ya magari used Tanzania mmliki huuza kwa Sababu gari linamsumbua, asilimia.

Asilimia 10 tu huuza gari kwa Sababu ya changamoto za kimaisha.

Asilimia 5 tu ndiyo huuza gari Ili wanunue gari lingine.

Mbaya zaidi mbongo kusema ukwel ni dhambi kubwa kwake atakwambia hii gari ni kuwasha na kuondoka kumbe yeye anajua shida Iko wap hakwambii.

Ukifika huko unashangaa gar inamatatizo kibao

Nashauri ingiza gar Toka nje kidogo zinakuwa nzima japo ni used, usiogope ushuru kwa Sasa unalipika siyo kuhangaika na gari lililomshinda mwenzako.

Madalali watakuja hapa kupinga huu utafiti wangu lakini mimi Big thinker nimetimiza jukumu langu usije sema sikukwambia
 
Gari gani nitaagiza Kwa million 2? hebu nisaidie hapo bwashee.
 
HAPO HAPO UKISHAAGIZA UKIITAJI KUBADILI UTATAKA APATIKANE MTEJA KUTOKA KUNDI HILO HILO ULILOLISHAURI LISINUNUE USED FROM TZ.

Kwa uchumi wa kila mtanzania haiwezekani wote kuagiza nje. Wachache watanunua 0km. Wengi kama wewe watanunua used from Japan na kwingineko halafu wanaobaki watanunua mikononi mwa walioagiza na kununua 0km.

BORA USHAURI KUWA, BAADA YA KUTUMIKA YAUZWE KWA BEI YENYE UHALISIA WA UCHAKAVU. SIO GARI IMETUMIKA MIAKA 8 NCHINI INAUZWA PUNGUFU MILIONI TATU NA UKIAGIZA.
 
Hii ndiyo comment Bora kwenye mada yako
 

Upuuzi, sema wanaitaji kuwa makini na sio vinginevyo, nimeagiza magari 7 maishani mwangu, yote nimeuza na niliowauzia wanashukuru mpaka leo.

Nimenunua magari yaliyotumila ma 4 katika maisha yangu na sijajuta,

Cha muhimu:

  • Body zuri.
  • Spare zipo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…