Usitake kumfunika boss wako, kilichomuondoa Makamba Wizara ya Mambo ya Nje

Usitake kumfunika boss wako, kilichomuondoa Makamba Wizara ya Mambo ya Nje

Steven Joel Ntamusano

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2023
Posts
5,203
Reaction score
3,913
Kwenye masuala ya uongozi kuna kanuni moja muhimu sana isemayo ' usitake kumfunika boss wako'.

Kwa kingereza wanasema 'never outshine your master', anayekuapisha daima ni mkubwa wako wa kazi hata kama nafsi yako inakuambia kwamba wewe unamzidi maarifa na kila kitu. Siku zote jifanye mjinga kwa mtu anayekupa mshahara na kukufanya ukaonekana na kuthaminika.

Hiyo kanuni imekuwa ngumu kwa Mheshimiwa January Makamba, ni mtu mwenye kujitutumua kila anapopata nafasi kiasi cha kusahau matendo yake yanaonekana vipi kwa wakubwa waliomuapisha pale ikulu.

Kuna lile suala la kutokuelewena kati ya mamlaka ya anga ya Tanzania TCAA na mamlaka ya Anga ya Kenya. Na mkurugenzi wa mamlaka ya Tanzania akawaandikia wale wa Kenya kuhusu umuhimu wa kufungua anga lao kwa biashara zetu kwa mujibu wa taratibu za anga za kimataifa.

Ni suala ambalo kwa namna yoyote ile barua iliyotoka upande wa Tanzania ilikuwa imetosha kuwakumbusha majirani juu ya kupunguza kiburi na dharau katika sekta zao, na kwa namna yoyote ile lisingeweza kuvuka siku tatu bila ya ufumbuzi kuwa umepatikana.

Na ilikwishatokea hivyo hivyo wakati wa awamu ya tano na mawaziri wa mambo ya nje wa Kenya na Tanzania wakaliachia limalizwe katika ngazi za wakurugenzi bila ya wao kulazimika kuingilia kati.

Safari hii katika awamu ya sita Mheshimiwa Makamba akaona ni sehemu ya 'kutokea', akaona ni nafasi ya kuchukulia ujiko kwa bosi wake. Akaamua kuingilia kati akimhusisha waziri wa mambo ya nje wa Kenya. Hakujua kwamba ameikera ofisi iliyomteua na kumwapisha kiasi cha mwenye ofisi kuwapigia simu wahusika akimshangaa waziri wa mambo ya nje kwa namna alivyoingilia suala lenye kutakiwa kumalizwa katika ngazi za chini.

Kingine kilichomkera SSH ni kuona kwamba hilo ni suala la wizara ya uchukuzi na mawasiliano na hapakuwa na haja ya wizara ya mambo ya nje kutumia nguvu kubwa kwenye utatuzi.

Tatizo la mheshimiwa ni kujiweka katika haiba ya urais akidhani anasubiri tu muda ufike aapishwe pale ikulu. Anaishi na tatizo hili akilini mwake na hajijui kuwa analo.

Wazungu wanasema ' never outshine your master'.
 
Kuna watu walikuwa wanasema kuwa Bwana January kapelekwa mambo ya nje kwa ajili ya kuandaliwa kuwa Rais! Hiki tuliwaambia ni kichekesho.

Aliyesema ukiwa waziri wa mambo ya nje unakuwa Rais ni nani? Tuliwauliza je? Mama Mulamula alipokuwa waziri wa mambo ya nje alikuwa anaandaliwa kuwa Rais? Ambacho hamkujua ni kuwa alipelekwa mambo ya nje ili akae kwenye mwanga mkali zaidi ili madudu yake yaonekane na sasa yamekuwa wazi sana na amebakia kuwa historia ya waziri wa mambo ya nje aliyekaa muda mfupi sana ofisini.

Britanicca
 
Kuna watu walikuwa wanasema kuwa Bwana January kapelekwa mambo ya nje kwa ajili ya kuandaliwa kuwa Rais! Hiki tuliwaambia ni kichekesho.

Aliyesema ukiwa waziri wa mambo ya nje unakuwa Rais ni nani? Tuliwauliza je? Mama Mulamula alipokuwa waziri wa mambo ya nje alikuwa anaandaliwa kuwa Rais? Ambacho hamkujua ni kuwa alipelekwa mambo ya nje ili akae kwenye mwanga mkali zaidi ili madudu yake yaonekane na sasa yamekuwa wazi sana na amebakia kuwa historia ya waziri wa mambo ya nje aliyekaa muda mfupi sana ofisini.

Britanicca
Jamaa sijui ana nini na kenya,eti achukue pesa za wastaafu akajenge ghorofa la kupangisha nairobi!
 
..Maza uwezo wake ni mdogo.

..sasa itabadilisha wangapi kwasababu wamemfunika?
Makamba NI zero kabisa hata mi ningemtimua, weka pembeni ishu ya kupanga jambo Hatari ambalo imebaki Siri tuje la kawaida yaani unawezaje kuwa waziri wa mambo ya nje halafu unazurura manchi mengine huko unajitutumua kama wewe ndiyo Rais wa nchi?

Yaani unasafiri kama waziri wa mambo ya nje na uko na Rais kwenye ziara unakuwa na timu yako ya waandishi wa habari mbali na waandishi wa habari wa Rais wanaku brand wewe kuliko Rais wako? Yaani unashindana na Rais au?

Yaani unawezaje kuwa kwenye ziara nje ya nchi unataka wewe kama waziri uambatane na mawaziri wengine yaani wewe ni Rais?

Huu ni ulimbukeni na ujinga wa hali ya juu sana. Tunaposemaga January hana akili hiii ndiyo ilikuwa maana yake lakini wengi sana hawakuwa wanataka kuelewa lakini sasa nadhani mmeelewa kwa kuwa mmerahisishiwa kuelewa kwa kufukuzwa kwake.

Britanicca
 
Makamba NI zero kabisa hata mi ningemtimua, weka pembeni ishu ya kupanga jambo Hatari ambalo imebaki Siri tuje la kawaida yaani unawezaje kuwa waziri wa mambo ya nje halafu unazurura manchi mengine huko unajitutumua kama wewe ndiyo Rais wa nchi? Yaani unasafiri kama waziri wa mambo ya nje na uko na Rais kwenye ziara unakuwa na timu yako ya waandishi wa habari mbali na waandishi wa habari wa Rais wanaku brand wewe kuliko Rais wako? Yaani unashindana na Rais au? Yaani unawezaje kuwa kwenye ziara nje ya nchi unataka wewe kama waziri uambatane na mawaziri wengine yaani wewe ni Rais? Huu ni ulimbukeni na ujinga wa hali ya juu sana. Tunaposemaga January hana akili hiii ndiyo ilikuwa maana yake lakini wengi sana hawakuwa wanataka kuelewa lakini sasa nadhani mmeelewa kwa kuwa mmerahisishiwa kuelewa kwa kufukuzwa kwake.

Britanicca

..mimi siikubali Ccm yote, lakini nadhani kuna watu huko mnamuona Makamba ni tishio ndio maana mnampiga vita.
 
..Maza uwezo wake ni mdogo.

..hajui nchi ilikotoka, na inatakiwa kwenda wapi.

..kwa kifupi yeye ndio anaharibu kuliko hata hao anaowabadilisha.

..yeye na chama chake wanatakiwa kuondolewa kupitia sanduku la kura.
Jenga hoja zenye kueleweka za huo udogo wa uwezo wake kuliko kuja na maneno ya kulazimisha kwamba hana uwezo.
 
Back
Top Bottom