USIWE KONDOO MWENYE KIBURI: Kukomoana Huzaa Msiba

USIWE KONDOO MWENYE KIBURI: Kukomoana Huzaa Msiba

Joined
Apr 4, 2016
Posts
60
Reaction score
69
images (33).jpeg

Kondoo wawili walikuwa wakitokea tofauti za mto. Mmoja akitokea mashariki na mwingine magharibi.

Walipoufikia ule mto, kila mmoja kwa upande wake alihitaji kuvuka. Kwa bahati mbaya, mto ule haukuwa na daraja pana zaidi ya gogo lililokuwa limelazwa kwa kuvukia.
images (36).jpeg


Basi, walipolifikia lile gogo wote walilazimisha kuvuka kwa pamoja.😳 Hakuna hata mmoja aliyekuwa tayari kusimama ili mwenzake apite kwanza.🫢 Hatimaye walipokutana katikati ya lile gogo, walilazimisha kupishana.
images (39).jpeg


Kwa bahati nzuri, kama si mbaya,🤣 gogo like halikuwa na nafasi ya kutosha wao kupishana. Hivyo, walijikuta wamegongana uso kwa uso na wote kuangukia mtoni wakasombwa na maji.🤦🏽‍♂️

FUNZO: Tunaposhindana kukomoana, tusisahau kujiuliza kitakachotukumba ikiwa tutashindwa. Hata kama tukishinda, bado tusisahau, kukomoana huzaa uhasama, visasi na mwishowe huzua msiba.
 
Kwa hiyo umeona Bora utumie mfano wa kondoo kutufikishia ujumbe?

Ila kondoo wangu sio wajinga kiasi hicho
 
Kwa hiyo umeona Bora utumie mfano wa kondoo kutufikishia ujumbe?

Ila kondoo wangu sio wajinga kiasi hicho
Hahaha ni uchaguaji tu ili kufikisha kinachokusudiwa. Ni mfano tu, hakuna kiumbe mkamilifu zaidi ya mwingine.🤗🤗🤭🤭
 
Back
Top Bottom