"Usiwe na Haki kupita kiasi" Ina maana gani?

"Usiwe na Haki kupita kiasi" Ina maana gani?

Hapo kuna hatari! Acha kabisa usiguse maana huwezi jua labda majambazi walipora vitu vingine ukaja kuunganishwa navyo
Kama ni hivyo hata pesa ulizookota zaweza kuwa ziliibwa mahali zikafichwa au kuangushwa na mzigo ukakuangukia wewe kwahio ni bora umtafute au ukisikia mtu akitangaza kaangusha pesa na uhahisi ndizo ulizookota bora urudishe
 
Kama ni hivyo hata pesa ulizookota zaweza kuwa ziliibwa mahali zikafichwa au kuangushwa na mzigo ukakuangukia wewe kwahio ni bora umtafute au ukisikia mtu akitangaza kaangusha pesa na uhahisi ndizo ulizookota bora urudishe
Huko ndiko kuwa na haki kupita kiasi sasa....
 
Penda kutenda haki, ila usizidishe kiwango (kiasi). Kila kitu kina kiwango chake, siyo wema wala haki pekee.

Maana haki ikitendwa kupitiliza huleta maovu.
 
Penda kutenda haki, ila usizidishe kiwango (kiasi). Kila kitu kina kiwango chake, siyo wema wala haki pekee.

Maana haki ikitendwa kupitiliza huleta maovu.
Hapo kwenye kuzidisha kiwango ndipo tatizo lilipo,utajuaje kiwango kimezidi,mtu anadai chake mpe,amedhulumiwa chake arudishiwe,yaani anachostahili kwa mujibu wa sheria au makubalino apewe

Sasa ni kwa kipimo gani utajua hapa umezidisha?
 
Maana fupi ya neno haki ni "Taratibu au mwongozo unaotakiwa".

Haki inayosemwa katika dini inaendana na mwongozo na taratibu za dini husika na haina uhusiano na haki inayojulikana kiserikali au mahali pengine. Unavyosema kudai haki unatumia mwongozo upi?

Mfano katika biblia utaratibu ni kwamba muumini atapata furaha ya milele in the next life endapo atafuata taratibu in this life, Na hii ni haki ya kila muumini anaefuata taratibu. Je muumini anaweza kusema (with certainity) kwamba ni haki yake kwenda mbinguni?

Maneno "Usiwe na haki" ni sawa na maneno "usijihesabie haki", ikimaanisha kwamba anaekupa hiyo haki pengine anatumia vigezo ambavyo anaepewa haki hua anavipuuza.

Anaejiongezea hekima ni yule jamaa anaejua anajua kumbe hajui[emoji28][emoji28]. By the way haya ni maoni yangu tu, naweza nisiwe sahihi[emoji23][emoji23]
 
Jibu la swali lako linapatikana katika Mhubiri 7:15-21 kwamba:-
Mtu mwadilifu hufa ingawa ni mwadilifu, ambapo mtu mwovu huendelea kuishi maisha marefu ingawa ni mwovu.

16 Basii, usiwe mwadilifu sana, wala usiwe mwenye hekima mno! Ya nini kujiangamiza wewe mwenyewe?

17 Lakinii pia, usiwe mwovu sana wala usiwe mpumbavu! Ya nini kufa kabla ya wakati wako?

18 Inakupasa ushike la kwanza na la pili pia; maana anayemtii Mungu atajengwa kwayo.

19 Hekima humfanya mwenye busara kuwa na nguvu zaidi kuliko watawala kumi mjini.

20 Hakika, hakuna mtu mwadilifu duniani atendaye mema daima bila kutenda dhambi.

21 Usitie maanani maneno yote wasemayo wanadamu, usije ukamsikia mtumishi wako akikutukana. 22Wewe mwenyewe wajua moyoni kwamba umeapiza wengine mara nyingi.
Ni fundisho
Too much of anything is harmful
 
Maana fupi ya neno haki ni "Taratibu au mwongozo unaotakiwa".

Haki inayosemwa katika dini inaendana na mwongozo na taratibu za dini husika na haina uhusiano na haki inayojulikana kiserikali au mahali pengine. Unavyosema kudai haki unatumia mwongozo upi?

Mfano katika biblia utaratibu ni kwamba muumini atapata furaha ya milele in the next life endapo atafuata taratibu in this life, Na hii ni haki ya kila muumini anaefuata taratibu. Je muumini anaweza kusema (with certainity) kwamba ni haki yake kwenda mbinguni?

Maneno "Usiwe na haki" ni sawa na maneno "usijihesabie haki", ikimaanisha kwamba anaekupa hiyo haki pengine anatumia vigezo ambavyo anaepewa haki hua anavipuuza.

Anaejiongezea hekima ni yule jamaa anaejua anajua kumbe hajui[emoji28][emoji28]. By the way haya ni maoni yangu tu, naweza nisiwe sahihi[emoji23][emoji23]
Aisee,naona tafsiri ni nyingi,asante
 
Tatizo waliondoa Jukwaa la dini sasa hakuna namna tusubiri majibu mchanganyiko tu
Jukwaa la dini mbona lipo?
Labda huna access nalo, au wakati lilipoondolewa awali, liliporudishwa tena hukupewa access....lipo mpwa
 
-Ukiwa na haki kupita kiasi utatumika kwa manufaa na wengine, pia itakufanya ujiumize kwa ajili ya haki..

-Ukijiongezea maarifa utajiongezea ukiwa; Kwa sababu ukiwa na maarifa mengi/hekima unaweza kugundua vitu ambavyo havisemwi, sio lazima mtu aongee ili kukufanya umuelewe, matendo yake tu yanakupa jibu la nini anamaanisha ( MHUBIRI 2:14
macho yake mwenye hekima yamo kichwani mwake) ukizingatia hakuna mkamilifu duniani! kwahiyo unakuta mda mwingi matendo ya watu yanakukwaza rohoni tofauti na ungekua huna maarifa na hekima ungekua unaona kawaida tu (Na ndio maana mazezeta wananenepaga)
 
Jukwaa la dini mbona lipo?
Labda huna access nalo, au wakati lilipoondolewa awali, liliporudishwa tena hukupewa access....lipo mpwa
Sikujua aise,kwahio ili nipate access inabidi niwaombe waniunge?maana mwanzo lilikuwa open tu
 
-Ukiwa na haki kupita kiasi utatumika kwa manufaa na wengine, pia itakufanya ujiumize kwa ajili ya haki..

-Ukijiongezea maarifa utajiongezea ukiwa; Kwa sababu ukiwa na maarifa mengi/hekima unaweza kugundua vitu ambavyo havisemwi, sio lazima mtu aongee ili kukufanya umuelewe, matendo yake tu yanakupa jibu la nini anamaanisha ( MHUBIRI 2:14
macho yake mwenye hekima yamo kichwani mwake) ukizingatia hakuna mkamilifu duniani! kwahiyo unakuta mda mwingi matendo ya watu yanakukwaza rohoni tofauti na ungekua huna maarifa na hekima ungekua unaona kawaida tu (Na ndio maana mazezeta wananenepaga)
[emoji3][emoji3] eti mazezeta wengi wananenepaga tu,kwakuwa hawana mawazo sio,

Nashukuru kwa mchango wako ila swali utajuaje hio haki imepita kiasi?
 
Mhu 7:16 SUV
Usiwe na haki kupita kiasi; Wala usijiongezee hekima mno; Kwani kujiangamiza mwenyewe?
Hili andiko naona limetumia maneno vibaya au walio walio tuwekea kwa Kiswahili,hawakumakinika na maana ya maneno haya.
 
Back
Top Bottom