Usiyoyajua kuhusu Biashara ya Simu za Kariakoo, ukijua haya utakuwa mjanja…

Mr_mkisi

Member
Joined
Sep 24, 2024
Posts
15
Reaction score
47
Ugomvi kati ya wateja na wauzaji wa simu, hasa hizi used za Dubai au refurbished, ni jambo linalotokea mara nyingi. Mara nyingi, chanzo kikuu ni pale simu inapoharibika, na mteja anataka kuirejesha ili abadilishiwe. Kuna wakati muuzaji anakuwa sahihi, na kuna wakati mteja anakuwa sahihi. Je, ni katika mazingira gani hali hizi hutokea?


Naitwa Mkisi

Nauza simu na laptop hapa Kariakoo kwa muda wa miaka 7 sasa. Natoa maarifa na makala kama hizi kila siku. Pia nina group WhatsApp na Telegram kwa updates za bei za jumla za simu na laptop.


Kesi za Ugomvi wa Wateja na Wauzaji wa Simu

Nina uzoefu mkubwa wa kushughulikia kesi kama hizi, hasa kwenye simu kuliko laptop. Kesi hizi hutokea pale ambapo:

  1. Mteja amenunua simu, kisha ikaharibika kwa bahati mbaya au makusudi, na anataka kuirejesha dukani ili abadilishiwe nyingine.

Mazingira Ambayo Muuzaji Anaweza Kukusaidia

  1. Simu yako ikiharibika kwa tatizo la software, kama vile:
    • Haishiki mtandao
    • Ime-corrupt
    • Inastack
    • Haipandishi mtandao
  2. Simu iliyo zima yenyewe tu bila sababu. Hii ni baada ya fundi kuthibitisha kuwa simu imezima bila sababu ya msingi.

Mazingira Ambayo Muuzaji Hataweza Kukusaidia

  1. Ukiharibu simu kwa kuidumbukiza kwenye maji.
  2. Simu ikiharibika kwa kupiga shoti kwenye motherboard.
  3. Simu ikiharibika kioo, iwe kwa bahati mbaya au makusudi (imeanguka, kugongwa, n.k.).
  4. Ukiamua kubandua sticker inayounganisha kioo na body ya simu, ambayo huonyesha kama simu imefunguliwa au la.

Shida Haswa Huwa Wapi?

Tatizo kubwa ni kwamba:

  • Wateja wengi hawasomi terms & conditions zilizowekwa kwenye warranty card.
  • Kuna dhana potofu kwamba wauzaji wote wa simu, hasa mtandaoni, ni matapeli au wanauza simu mbovu.

Mfano wa Terms & Conditions za Warranty

Kama mteja, unatakiwa kuelewa kwamba warranty haitaweza kusaidia katika hali zifuatazo:

  1. Ukiharibu kioo cha simu kwa bahati mbaya au makusudi.
  2. Ukiingiza simu kwenye maji.
  3. Simu ikiwa na tatizo lingine lakini ukairudisha ikiwa na crack kwenye kioo.
  4. Simu ikipiga shoti.

Ushauri Wangu

  1. Ili kuepusha ugomvi, ukiona ni ngumu au hatarishi, bora usinunue bidhaa hiyo, tafuta mbadala.
  2. Tafuta store nzuri ya simu ambayo inauza bidhaa zenye ubora wa hali ya juu.

 
Ugomvi kati ya wateja na wauzaji wa simu, hasa hizi used za Dubai au refurbished, ni jambo linalotokea mara nyingi. Mara nyingi, chanzo kikuu ni pale simu inapoharibika, na mteja anataka kuirejesha ili abadilishiwe. Kuna wakati muuzaji anakuwa sahihi, na kuna wakati mteja anakuwa sahihi. Je, ni katika mazingira gani hali hizi hutokea?


Naitwa Mkisi

Nauza simu na laptop hapa Kariakoo kwa muda wa miaka 7 sasa. Natoa maarifa na makala kama hizi kila siku. Pia nina group WhatsApp na Telegram kwa updates za bei za jumla za simu na laptop.


Kesi za Ugomvi wa Wateja na Wauzaji wa Simu

Nina uzoefu mkubwa wa kushughulikia kesi kama hizi, hasa kwenye simu kuliko laptop. Kesi hizi hutokea pale ambapo:

  1. Mteja amenunua simu, kisha ikaharibika kwa bahati mbaya au makusudi, na anataka kuirejesha dukani ili abadilishiwe nyingine.

Mazingira Ambayo Muuzaji Anaweza Kukusaidia

  1. Simu yako ikiharibika kwa tatizo la software, kama vile:
    • Haishiki mtandao
    • Ime-corrupt
    • Inastack
    • Haipandishi mtandao
  2. Simu iliyo zima yenyewe tu bila sababu. Hii ni baada ya fundi kuthibitisha kuwa simu imezima bila sababu ya msingi.

Mazingira Ambayo Muuzaji Hataweza Kukusaidia

  1. Ukiharibu simu kwa kuidumbukiza kwenye maji.
  2. Simu ikiharibika kwa kupiga shoti kwenye motherboard.
  3. Simu ikiharibika kioo, iwe kwa bahati mbaya au makusudi (imeanguka, kugongwa, n.k.).
  4. Ukiamua kubandua sticker inayounganisha kioo na body ya simu, ambayo huonyesha kama simu imefunguliwa au la.

Shida Haswa Huwa Wapi?

Tatizo kubwa ni kwamba:

  • Wateja wengi hawasomi terms & conditions zilizowekwa kwenye warranty card.
  • Kuna dhana potofu kwamba wauzaji wote wa simu, hasa mtandaoni, ni matapeli au wanauza simu mbovu.

Mfano wa Terms & Conditions za Warranty

Kama mteja, unatakiwa kuelewa kwamba warranty haitaweza kusaidia katika hali zifuatazo:

  1. Ukiharibu kioo cha simu kwa bahati mbaya au makusudi.
  2. Ukiingiza simu kwenye maji.
  3. Simu ikiwa na tatizo lingine lakini ukairudisha ikiwa na crack kwenye kioo.
  4. Simu ikipiga shoti.

Ushauri Wangu

  1. Ili kuepusha ugomvi, ukiona ni ngumu au hatarishi, bora usinunue bidhaa hiyo, tafuta mbadala.
  2. Tafuta store nzuri ya simu ambayo inauza bidhaa zenye ubora wa hali ya juu.

Wewe unatoa warranty ya mda gani.. maana nyie sim zenu tatizo linaanzia kwenye warranty ya mwezi mmoja au wiki mbili.. sasa ni warranty ya aina gani hiyo maana inaonyesha hata wewe muuzaji una mashaka na kifaa unachouza kuhusu ubora wake au unajua kina ubovu flan ambapo unaona ni gharama kurekebishika au haurekebishiki ..

Mfano pengine curcuit ya cm ilishaguswa guswa au upande wa sauti au uoande wa kunasa mtandao ulishaguswa sasa unajua kuwa kuna uwezekano tatizo likajirudia ndani ya siku au wiki kadhaa au simu ikaooteza ufanisi kitu ambacho c chankukiona kwa mara moja au siku kadhaa ndo maana mnatoa warranty za ajabu ajabu
 
Back
Top Bottom