.......uso kwa uso na mwana JF mwenzangu

.......uso kwa uso na mwana JF mwenzangu

Kwi kwi kwi kwi kwi lol!!!! Hahahaha mie mwenyewe karibu nibambwe mara mbili mara ya kwanza jamaa zangu wakanialika kwao. Nikakaa huko for four days kila mara wakati niko kwao nikawa naingia JF kutumia PC yao basi kuna wakati wakaja wote kwenye nilipokuwa mimi nikifuatilia majadiliano ya hapa ikabidi nicheze kama pele ili wasiione ID yangu. Baada ya miezi michache wakaja kwangu nikawa niko humu nao wanaangalia TV basi nikawajoin wote tukawa tunaangalia TV mmoja akadai nionyeshe PC ilipo nataka kutumia nilikuwa sijalog off JF ikabidi nicheze kama pele tena ili ID yangu isijulikane. Baadaye katika mazungumzo mmoja kaanza kuisagia JF kwamba siku hizi wazushi wamekuwa wengi sana haingii sana kama zamani na hata akiingia ni kuchungulia mara moja tu haandiki chochote.

Juzi juzi nikawa kwenye mnuso mmoja watu wakawa wanaongelea ile case ya uforoo wengine wakadai hawaijui lolote kuhusu hiyo kesi. Mdada mmoja akawauliza nyie mnapata wapi habari zenu? Mmoja akajibu magazetini mdada akajibu ukitaka latest habari nenda JF. Mie kimya, mdada akaendelea sasa hivi hapa niko JF (mkononi yuko busy na simu yake) na mkaka mwingine naye hata mimi nasoma yanayojiri kule JF (naye busy na simu yake mkononi) mie natamani nikae upande wao lol!!! Ili nizijue ID zao maana tulikuwa tunaangaliana.

Mwiko kutumia pc za watu kuingia JF simu yangu inatosha kabisa na kama nina wageni simu pia itatumika kuingia huku lol!! Mpaka wageni waondoke.
 
Mamboz wana cc.........

mmh ngoja niwaambie yalonikuta maana nimejikuta nakutana Live na member mwenzangu bila kutarajia

mie ni mtu wa JF sana hata ofisini huwa wananiita mama wa JF sasa jana niko ofisin
kuna kaka mmoja tunafanya nae kazi..akawa ananiambia hebu nitajie jina lako la JF
nikamkatalia...kumbe na yeye ni member tena active tu

YEYE;akasema wewe utakuwa King'asti
H.O.E; hapana bana sio mimi ila ID yangu hata sikutajii.....
YEYE; King'asti nae mtata yule.....Ila huwa napenda kusoma comments zake
H.OE nikamwambia kumbe wawafaham watu enhe

Nikajua yameisha akaendelea

YEYE:au wewe ni Heaven on Earth
H.O.E:wala sio mimi...ndio nani huyo kwanza maana mi siwajui watu wengi JF
YEYE:Kadada fulani hivi kana majibu ya mkato hako...ila kanaonekana kako charming
H.O.E nikacheka tu nikasema sio mimi......(Sijui kwanini alikuwa anasema "KA")

akaendelea tu

YEYE: au wewe utakuwa amu
H.O.E nikamwambia bana hapana huyo nae ni nani...wote siwajui na mie sio active kihivo
YEYE:Mhh sio active wewe......Unanidanganya Live LIVE
H.OE:Ndio na wote ulionitajia sio mimi..na ID yangu sikutajii

maongezi yakaisha baadae alikuja kwenye desk langu sa mie nishajisahau akaona ID yangu
kachekaje huyo kumbe wewe ndio H.O.E lol...

na mie sijakubali ka umejua yangu na wewe hadi nijue ID yake kuja kunitajia Lahaula kumbe wakati
tunapishana kona za JF na huku Ofisini tunapishana pia....nimecheka sana alivyonitajia ID yake........
na huku tunatanianaga sana.....ni mtu wa karibu pia ...Nilifurahi sana tu

basi siku hizi ananiita H.OE akinitext ndio anasema Heaven on earth......
Ila nilicheka sana tu

Long Live JF

please dont use H.O.E coz it rhymes with W.H.O.R.E.....
 
natamani namie nimjue huyo uliyekutana nae. lol. hebu ajitaje basi tupate uhondo kamili
 
Back
Top Bottom