Usomaji wa magazeti redioni kurasa ndani ufunguliwe. Wananchi wa vijijini nao wana haki ya kupata habari

Usomaji wa magazeti redioni kurasa ndani ufunguliwe. Wananchi wa vijijini nao wana haki ya kupata habari

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Uhuru wa kupata Habari ni chakula muhimu ambacho kila mtu huiitaji kushiba, awamu iliyopita usomaji wa magazeti redioni katika kurasa za ndani ulifungiwa bila maelezo ya msingi.

Kufungiwa habari za ndani za magazeti kupitia redio wengi wa walioathirika ni wananchi wa vijijini ambao ni ngumu kupata nakala ya gazeti kutokana na kuwa magazeti mengi huuzwa mjini na sio vijijini. Hivyo kusomewa tu vichwa vya habari pekee redioni humwacha njia panda.

Wakati huo huo magazeti hayo hayo husambazwa mitandaoni ambao mtumiaji wa mtandaoni huwa na uwezo wa kusoma habari zote za gazeti husika, lakini kwa Wasikilizaji wa redio na watazamaji wa television ambao idadi yao ni kubwa hukosa kabisa haki ya kupata habari za kila siku kupitia magazeti.
 
KWA HIYO WAKISOMEWA NA HABARI ZA NDANI UNADHANI WATANUNUA HAYO MAGAZETI YENYEWE!!!???
Afu kumbekuna watu bado wanasoma magazeti???
 
Gazeti gani linafika kijiji cha lupembe lwa senga au makadupa huko kusini iringa?
Wewe na babaako nwakyembe mligoma kabisa kutumia akili.
Kwa hivyo hapo ndipo akili yako imefika mwisho wa kuchakata hili jambo?
 
Tunanyamvua na kunyumburisha
 
Ukisoma kila kitu ni pigo kwa kampuni husika ya magazeti kumbuka nao wanahitaji kuuza
 
Ukisoma kila kitu ni pigo kwa kampuni husika ya magazeti kumbuka nao wanahitaji kuuza
Umesahau kwamba mitandaoni ukiingia unasoma kurasa zote mkuu. Wananchi walio vijijini huko wanakosa habari za kwenye magazeti
 
Umesahau kwamba mitandaoni ukiingia unasoma kurasa zote mkuu. Wananchi walio vijijini huko wanakosa habari za kwenye magazeti
Hata mtandaoni husomi kurasa zote labda uwe unelipia.
 
Back
Top Bottom