Aaliyyah
JF-Expert Member
- Mar 20, 2022
- 19,041
- 46,239
Nimekumbuka vitu kadhaa leo ngoja nijitahidi kuandika japo sio mwandishi mzuri sana.
Kunawakati tunapitia vitu vingi na tunakutana na watu wengi tofauti tofauti kwenye maisha wenye kutufurahisha na kutukwaza lakini tujitahidi kujifunza ustaarabu na unyenyekevu hasa tunapokwazika inawezekana ukatulipa vizuri bila kujua ni wakatigani na katika mazingira gani.
Tujitahidi Kuishi kwa wema hata kama unaona ni watu wa chini sana kukuzidi, tusidharauliane.
Nimekumbuka tukio lililonifundisha kuwa ustaarabu unalipa;
Nilikuwa nasafiri mkoa fulani, kipindi hiki stendi ni Ubungo Terminal sikukata tiketi na nilichelewa sana. Nikafika Dar saa nne usiku, hadi nafika Ubungo ni saa tano. Nikashuka kwenye daladala lengo nielekee ndani kukata tiketi.
Sikuwa mwenyeji maeneo yale wale, wabeba mizigo wakaanza kunigombaniia huku mmoja akivuta begi langu nikafanikiwa kumnyang'anya lakini bahati mbaya likakatika mkono. Nilichukia sana aisee, nikimuangalia kwa hasira lakini nikaishia kumwambia aache, sikumtusi wala sikumtolea kauli chafu.
Wakat natoka kuna kaka akanifata kunielekeza kuwa kuna njia ya shortcut, akanionesha upande wa kupita, Ilikuwa usiku nikiwa sielewi nipite wapi. Nikiangalia upande wa pili wa barabara nikamuona yule kaka aliyeniharibia begi akinitazama sana nikawa namuangalia kiwizi wizi.
Akanionyesha ishara nisipite na yule kaka bali ninyooshe barabara kubwa. Kwakweli nilikuwa nishakubali kupita kule kwenye giza nilikoambiwa kuwa ni shortcut, nikafata maelekezo mwingine nikanyoosha nikakuta geti nikaingia nikiwa salama.
Sijui ingekuwaje ningepita kule kichochoroni, aliniokoa sana pengine lingenikuta jambo baya. Nikajiuliza ingekuwaje ningemjibu vibaya au kumtukana kwa makosa yake ya kunikatia mkanda wa begi?!
Nafikiri sote hatujakamilika lakini huenda haya madogo madogo yakatubeba. Unayemdharau leo huenda ndio akakusaidia kesho na kuwa mnyenyekevu na mstaarabu siyo kukosa akili bali ni jambo la kiungwana sana 🙏🙏🙏.
Sio lazima ukitukanwa ujibu au ukichukizwa ulipize, tuishi humo wapendwa.
Kunawakati tunapitia vitu vingi na tunakutana na watu wengi tofauti tofauti kwenye maisha wenye kutufurahisha na kutukwaza lakini tujitahidi kujifunza ustaarabu na unyenyekevu hasa tunapokwazika inawezekana ukatulipa vizuri bila kujua ni wakatigani na katika mazingira gani.
Tujitahidi Kuishi kwa wema hata kama unaona ni watu wa chini sana kukuzidi, tusidharauliane.
Nimekumbuka tukio lililonifundisha kuwa ustaarabu unalipa;
Nilikuwa nasafiri mkoa fulani, kipindi hiki stendi ni Ubungo Terminal sikukata tiketi na nilichelewa sana. Nikafika Dar saa nne usiku, hadi nafika Ubungo ni saa tano. Nikashuka kwenye daladala lengo nielekee ndani kukata tiketi.
Sikuwa mwenyeji maeneo yale wale, wabeba mizigo wakaanza kunigombaniia huku mmoja akivuta begi langu nikafanikiwa kumnyang'anya lakini bahati mbaya likakatika mkono. Nilichukia sana aisee, nikimuangalia kwa hasira lakini nikaishia kumwambia aache, sikumtusi wala sikumtolea kauli chafu.
Wakat natoka kuna kaka akanifata kunielekeza kuwa kuna njia ya shortcut, akanionesha upande wa kupita, Ilikuwa usiku nikiwa sielewi nipite wapi. Nikiangalia upande wa pili wa barabara nikamuona yule kaka aliyeniharibia begi akinitazama sana nikawa namuangalia kiwizi wizi.
Akanionyesha ishara nisipite na yule kaka bali ninyooshe barabara kubwa. Kwakweli nilikuwa nishakubali kupita kule kwenye giza nilikoambiwa kuwa ni shortcut, nikafata maelekezo mwingine nikanyoosha nikakuta geti nikaingia nikiwa salama.
Sijui ingekuwaje ningepita kule kichochoroni, aliniokoa sana pengine lingenikuta jambo baya. Nikajiuliza ingekuwaje ningemjibu vibaya au kumtukana kwa makosa yake ya kunikatia mkanda wa begi?!
Nafikiri sote hatujakamilika lakini huenda haya madogo madogo yakatubeba. Unayemdharau leo huenda ndio akakusaidia kesho na kuwa mnyenyekevu na mstaarabu siyo kukosa akili bali ni jambo la kiungwana sana 🙏🙏🙏.
Sio lazima ukitukanwa ujibu au ukichukizwa ulipize, tuishi humo wapendwa.