Utabiri: Siku chache zijazo itatokea ajali ya Ndege ya abiria

Utabiri: Siku chache zijazo itatokea ajali ya Ndege ya abiria

Hebu shuka hapo chini​

Mit 26:4-12 SUV​

Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake; Usije ukafanana naye. Umjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake; Asije akawa mwenye hekima machoni pake. Apelekaye ujumbe kwa mkono wa mpumbavu Hujikata miguu, na kunywa hasara. Miguu yake achechemeaye huwa dhaifu; Kadhalika mithali katika kinywa cha mpumbavu. Kama mfuko wa vito katika chungu ya mawe; Kadhalika mtu amheshimuye mpumbavu. Kama mwiba uingiao katika mkono wa mlevi; Kadhalika mithali katika kinywa cha mpumbavu. Fundi stadi hufanyiza vitu vyote; Bali amwajiriye mpumbavu ni kama awaajiriye watu wapitao. Kama vile mbwa arudiavyo matapiko yake; Kadhalika mpumbavu afanya upumbavu tena. Je! Wamwona mtu mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.
Sawa. Kwa sasa unasemaje? Au umepotea kwa ndege?
 
Nilifanikiwa kwa asilimia kubwa
*ndege nyekundu no
*vifo na majeruhi no
*ndege kukatika katikati no
Taarifa kamili hakuna vifo wala majeruhi na ndege haijakatika katikati
Ushindwe mwenyewe na hizo keywords hapo juu
Aiseee?
 
Wewe ni mpumbavu hakuna ajali itakayotokea IN JESUS NAME
Navunja roho zote chafu
Na kulifunika anga lote kwa damu takatifu ya YESU! Amen
Je wewe ni mpumbavu?
 
Hajaenda mbali sana kukosea, tuseme alitabiri karibu na ukweli.

Hiyo logo ndotoni yaweza kutafsirika ama onekana kama ni nyekundu kweli.

Haijalishi hata kama kuokolewa walitangulia watu wazima, lakini na watoto walikuwepo!

Kikubwa tunaangalia kuwa ndoto ya maono juu ya: "ajali ya ndege ya hivi karibuni" imetimia kwa usahihi takribani %100.
Aiyetangulia kuokolewa ni mtoto , then mchina , baadae mchina akapewa mtoto amshike ,akafuatiwa na mama mjamzito. Hii ni accorsing to yule mwokozi Majaliwa
 
Basi tunakupa wewe...kenge kabisa ww
Msimpe credit mtoa mada mana ni muongo km waongo wengine

Angekuwa anajua mambo ya mbele angesema direct kwamba ndege fulani, inatokea mkoa flan kwenda mkoa fulani,watakufa abiria kadhaaa,wapona kadhaa
 
Halafu ili kuutukanisha UISLAM unaanza na kutoa salam ya kiislam ili watu wajue mtoa mada kuwa ni muislam, na hayo ndio yanayo waaminisha watu kuwa waislam ni wapiga ramli,
Katika mafundisho ya kiislam hakuna mtu mwenye elimu ya jambo linalotarajiwa kutokea, huo ni USHIRIKINA, na nikinyume kabisa na uislam, km mnakuwa na mada zenu za kishirikina acheni kujinasibisha na uislam toeni tu salam zenu za kawaida, endeleeni na mambo yenu, inafahamika hili ni jukwa huru, ila msitutukanishie dini yetu.
Hiyo siyo salamu ya Kiislamu ni salamu inayotumika na wanaozungumza lugha ya kiarabu.
 
Back
Top Bottom