Utafiti mpya wa kisayansi wa Covid19 – Msaada mkubwa wa kujikinga na kuzuia maambukizi kwa wengine

Utafiti mpya wa kisayansi wa Covid19 – Msaada mkubwa wa kujikinga na kuzuia maambukizi kwa wengine

MM Togolani,
IMG-20200320-WA0001.jpg
 
mkuuu mimi nataka kujua structure halisi ya kibilogia ya hichi kirusi kimeumbwa je umbwaje..!? ....na pia kinawezaje kupenye membrane zilizope kwe mwili na kuingia kwenye celll na kusababisha ugonjwa... !!!?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanasayansi wa Australia wamegundua ndani ya ndizi Kuna maji maji ambayo yana uwezo wa kuuwa virusi vya Corona..

Wingi wa vitamin b6 kwenye ndizi ndio inazifanya ndizi ziwe na uwezo huo

hivi Sasa wanasayansi wa Australia tayari wamesha tegengeza chanjo ya kuzuia Corona kutokana na ndizi

Wanasayansi wetu wa Tanzania wako wapi?
 
chabuso,
Ndugu chabuso, nadhani huku ni kuwaonea wanasansi wetu. Sio lazima kila nchi wagundue dawa au kinga. Jumuia ya wanasayansi duniani ni moja na solutions za kisayansi hazibaki ndani ya mipaka ya nchi moja. Kwani wa nchi nyingine zaidi ya 190 duniani wako wapi kwenye hili?

Ila la muhim zaidi kutambua, ukiona au kusikia nchi fulani wameanza kudungua dawa au kinga ya Covid19, usidhani hizo tafiti zilianza Covid19 ilipolipuka. Mara nyingi gunduzi hizo ni mwendelezo wa tafiti ambazo nyingine wamezifanya kwa miaka kadhaa. Wana maaabara zenye vifaa vya kisasa; wana fedhaza kufanya tafiti; wana wataalamu; na nchi zao zinaheshimu tafiti na sayansi.

Hivyo tusianzie na kuuliza dawa au kinga ya Covid19 toka kwa wanasayansi wetu. Tuanze na kuuliza sisi kama taifa tumewekeza kiasi gani kujenga mazingira wezeshi ya tafiti na gunduzi za kisayansi? Bajeti yetu kwa mwaka ya tafiti ni kiasi gani? Maabara zetu zikoje? Wanasayansi wetu wanawezeshwa na wanalipwa kiasi gani? Tunaheshimu tafiti na sayansi kwa kiasi gani tunapofanya maamuzi? Ni mara ngapi tunawatumia wanasayansi wetu kutoa solutions na tukaziheshimu?

Tukipata majibu ya haya, basi turudi kuwauliza kuhusu kinga na dawa za Covid19.
 
MM Togolani,
Unakataa mtu mwenye afya kujikinga kwa mask na wakati huo huo unataja matabibu kutumia hizo maski kujikinga na wagonjwa! Kwa mujibu wa mantiki yako ni kwamba mtu wa kawaida hatakiwi kujikinga ila wanaostahili ni wahudumu wa afya tu eti kwavile raia hawatumii vifaa vya kukinga macho.

Swali liko pale pale; kama unajua kuwa SARS-CoV-2 (siyo COVID-19) ana kiherehere cha kumuingia mtu kupitia macho, kwanini hujashauri raia watumie vyote mask na goggles kama wafanyavyo wahudumu? Kuna ubaya gani endapo raia wa kawaida wakivaa gloves, mask na goggles? Au unatetea pointi ya yule mama kwamba mtu ambaye hajaambukizwa atembee wazizi kwenye "hot spots?

Lakini ripoti inayotajwa hapa inataja kitu "infectious dose" (ID50); je unajua maana yake? Je, nikisema kuvaa mask kunapunguza "infectious dose" ukilinganisha na kutokuvaa kabisa nitakosea?
 
mkuuu mimi nataka kujua structure halisi ya kibilogia ya hichi kirusi kimeumbwa je umbwaje..!? ....napia kinawezaje kupenye membrane zilizope kwe mwili na kuingia kwenye celll na kusababisha ugonjwa... !!!?

Sent using Jamii Forums mobile app

Ndugu victor moshi nadhani watu wa Molecular Biology na Madaktari wanaweza kujibu swali lako vizuri zaidi kuliko mimi. Ila nataka kuamini kwamba iwapo umesoma Biology, basi utakua unaelewa Viruses ni viumbe wa aina gani na structure/anatomy yao ikoje. Viruses wako wa aina nyingi sana na wana complex structures based on either RNA or DNA sequences (the genetic materials). Ila itoshe tu kusema Covid19 ana sifa za msingi za virusi wengine unaowafahamu.

Tofauti ya Covid2 na wengine ni upya wake kwenye familia au ukoo wa virusi wa Coronavirus. Hadi alipolipuka hakua amefahamika. Ila ukoo wa Coronaviruses unafahamika siku nyingi na wengi wao wanashambulia mfumo wa upumuaji (upper respiratory track). Covid19 ana binamu zake wa karibu wanasababisha mafua ya kawaida; ana pacha (twin sister) anayeitwa SARS-Coronavirus ambaye naye alilipuka China mwaka 2002/2004 lakini hakufanikiwa kusambaa kwa kiwango hiki. SARS-Covid1 alidhibitiwa kwa haraka na hajaibuka tena. Pia, ana dada yake mwingine anaitwa Middle East Respiratory Syndrome (MERS) Coronavirus aliyelipuka 2012 lakini hakusambaa njie ya Mashariki ya kati.

Sifa kubwa ya viruses ni viumbe ambao hawana uhai wao wenyewe hivyo wanakua inactive na kutozaliana bila kuwa ndani ya kiumbe mwingine (inaweza kuwa ndani ya bacteria, mmea au mnyama). Wanapoingia kwenye mwili au cell ya kiumbe mwingine, kazi ya kwanza na ya haraka wanayofanya ni kuzielekeza cells za kiumbe hicho kuzalisha virusi wengine (duplicating themselves). Ugonjwa wanaosababisha ni matokeo ya uwepo wao kwa wingi ndani ya mwili kama wavamizi; nini hasa wanashambulia ndani ya mwili; na ni cells au kungo gani la mwili.

Covid19 akiingia kwenye mwili anakimbilia kwenye nyuma ya matundu ya pua yako (nasal passage) na kwenye utando wa koo (mucus membrane at the back of your throat). Tazama picha yake hapa chini utaona vitu vinaitwa "spikes" (vyekundu) ambavyo ndivyo anavipenyeza kwenye membranes za cells na kuanza kumimina genetic material zake (tuite mbegu zake). Genetic material zake zinaanza kuingilia utendaji kazi wa kawaida wa cells za mwili na kuziamrisha zianze kufanya kazi ya kuzalisha virusi wengine.

1584742708810.png

Wanapoanza kuzalishwa wanaendelea kutoka kwa wingi na kuvamia cells zingine kwa haraka na ndio mana dalili za kwanza mtu anapoambukizwa ni mafua, kikohozi kikavu na koo kukereketa (sore throght). Kwa haraka sana wanaendelea kuzaliana na kushuka kwenye koo chini kueleka kwenye mapafu na kuingia kwenye cells za mapafu zinazohusika na kazi ya kuchuja hewa (kutoa hewa ukaa-CO2 na kuingiza Oksijeni O2). Hapa mapambano kati ya Covid19 na cells huwa makali zikijilinda ili kuendelea na majukumu yake. Cells za mapafu nyingi zinaanza kuvimba, kutoa usaha na hata kufa kwenye vita hiyo. Ndio mana dalili nyingine inayofuata kwa haraka ni kubanwa kifua na kushindwa kupumua maana oksijeni inashindwa kupita kama kawaida.

Sasa mtu mwenye afya njema, mwili wake unaweza kupambana na Covid19 na kuwashinda na ndio mana anakua na dalili zisizo kali na anapona ndani ya siku kuanzia 5 hadi 14. Kwa mtu ambaye tayari mwili wake uko busy kupambana na magonjwa mengine kama ya TB (kifua kikuu), diabetic (kisukari), cancer (kiharusi), magonjwa ya moyo, figo, nk; Covid19 wakiingia wanapelekea hali yake kuwa mbaya zaidi (cells zake zinalemewa na kushindwa kutimiza majukumu yake). Zikishindwa kabisa ndio kifo kinakuja. Ndio mana utaelewa ni kwa nini zaidi ya 95% ya vifo vyote vya Covid2 duniani ni wazee na watu wengine ambao tayari wana chronic diseases kama niliyotaja hapo juu. Asilimia ndogo sana ya watoto na vijana wenye afya njema ndio wameathika.

Na hii ndio sababu nilikosoa uharaka wa serikali ya Kenya, yetu na zingine za Afrika kufunga shule na vyuo haraka kama hatua ya kwanza ya kudhibiti ugonjwa (nimejadili kwingine). Kundi hili sio hatarishi kwa Covid19. Evidence from emprical data worldwide inaonesha hatari ya ugonjwa huu unategemea umri (age dependent). Kwa mfano, kwa wagonjwa chini ya miaka 20 ni mtu 1 kati ya 10,000 (0.01%) anakua na hali mbaya na kuhitaji intensive care wakati kwa watu wazima ni mtu 1 kati ya 12 (8.3%). Walifariki Italy, karibu 99% ni watu wazee na waliokua na magonjwa mengine. Kati wagonjwa zaidi ya 160 UK, mgonjwa mdogo kabisa kufariki ana miaka 45 na alikua na ugonjwa hatiri wa motor neurone disease hivyo Covid19 ikamalizia.

Sina hakika kama nimejibu vema swali lako. Kama nilivyosema, watu wa Microbilogy na Madktari wanaweza kukusaidia zaidi maana nami bado nina ujinga mwingi kwenye eneo hili. Mimi nimejikita zaidi kwenye mifumo ya namna ya kufuatilia na kuzuia magonjwa (disease surveillance and response systems) hivyo ndio eneo ambalo naweza kuliongelea kwa mamlaka zaidi.

MM Togolani
 
X-bar,

Ndugu,

Uliyemtaja kama SARS-CoV-2 (Severe Acute Respiratory Syndrome Coronavirus 2) ndio huyo Coronavirus Novel au New Coronavirus anayesabisha Coronavirus Disease 2019 kwa kifupi kama Covid19 au Covid-19. Nadhani hili la semantic sio issue maana tunajua tunayemwongelea ni nani.

Tuelewane kwamba hakuna aliyekuzuia kuvaa gloves, masks, na miwani za wanaochomelea vyuma iwapo unashawishika vitakusaidia. Pia waweza kuvaa zile suti za makaratasi wanazovaa wanaohudumia wagonjwa wenye virusi hatari kama ebola, na ukiwa na vyote hivyo ukaenda ofisini na kwingine unapokuwepo siku nzima. Unaweza kuongelea logic yake upendavyo na ikakupa maana unayotaka.

Ila mimi ninaongelea sayansi. Kwamba masks sio kinga maana haizuii wewe kujishika macho wala droplets kuuingia machoni. Pili, sayansi inahitaji masks kuvaliwa ndani ya masaa machache na kubadilishwa maana ina hatari ya kuwa chanzo cha magonjwa mengine. Hili ni gumu kufanyika iwapo mtu analazimika kuzivaa muda wote. Tatu, kuvaa mask pekee hakukikingi maana una mikono na meneo mengine yanayoweza kukutana na kirusi. Mask unayovaa inaweza kurukiwa na droplet na saa unaibadilisha au kuitoa bado ukakutana na kirusi kwa jishika au kujigusa na mask hiyohiyo.

Wanaotutibu wanavaa maana wao wanahudumia watu waliokuja tayari kama wagonjwa. Pia, wanavaa kuzuia wao wasiambukize magonjwa kwa watu wanaowahudumia (maana nao ni binadamu wana magonjwa na wanaweza kupata Covid19 pia. Umeona Italy makumi ya wahudumu wamepata na wengine wamefariki).

Mwisho, kwa kua sayansi inatoa ushauri kwa kutumia evidence za kitafiti, hakuna ushahidi wa kitafiti ulionesha uvaaji wa mask ni kinga. Kama unafuatilia vema, utagundua kwamba uvaaji wa masks kule China ni moja ya tamaduni zao kutokana na uchafunzi mkubwa wa hali ya hewa hivyo huzivaa kupunguza uvutaji wa hewa chafu. Walikua wanafanya hivyo hata kama ya Covid19. Na walipopata Covid19 hakuna aliyekua anajua ugonjwa unasambaa kwa njia gani hivyo uvaaji wa masks ukaendelea kwa kasi. Shida watu wameunganisha walichokiona China wakidhani ni kinga ya Covid19 bila kutafuta kuelewa muktadha wake.

Haya mambo ya kisayansi yanahitaji kupata uelewa na muktadha sahihi badala ya kujikita tu kwenye kinachoitwa "logic" kama njia ya kukuelekeza kufanya maamuzi yenye TIJA.

MM Togolani
 
X-bar,
Kuhusu titer concentration infection dose TCID50/L inayotajwa kwenye huu utafiti, hiki ni kipimo cha kutazama concentration ya virusi inavyopungua kadiri muda unavyoongezeka based on half-life decay concept.

Ni wazi kwamba kiwango cha virusi watakaokuwepo mwanzoni aerosol inapotolewa na mwathirika, ni kubwa kulinganisha na watakaokuwepo mwishinoni maana wanakua kuna wanaokua inviable and not infectious.

Measurement hii inahusikaje na uvaaji wa mask?
 
MM Togolani,
Lengo langu halikuwa kubishana na wewe au kukukosoa. Lengo ni kukukumbusha katika ushauri wako kwa jamii kuhusu namna ya kujikinga na maambukizi haya. Nimeona umeshauri kunaawa mikono kwa sababuni na kukausha kwa kitambaa au tishu. Logic ya kunawa mikono ni kuua vijidudu ambavyo unaweza kuvipata kwa kugusa vitu vilivyoambukizwa (cross-contamination). Upo sahihi kabisa.

Hata hivyo nimeshangazwa pale ulipobainisha kuwa "njia kuu ya kusambaa" maambukizi ya ugonjwa huu ni hewa (aerosols) na bado ukasahau kupendekeza matumizi ya "vikingapua" (mask/respirator) kwa ajili ya kuzuia au kupunguza aerosols (infectious dose). Nimeshangaa sana siyo siri! Kama kuvaa mask hakusaidii eti kwavile hatuvai mawani ya kukinga macho, sasa kunawa mikono peke yake kuna maana gani wakati pua na mdomo viko wazi?

Lakini unanishangaza zaidi kuona unaendelea kupuuza matumizi ya mask tena bila ushahidi wa kitaalamu. Yaani umeshindwa kushauri nanmna ya ku-intervene njia kuu ya kusambaa kwa maambukizi (aerosols) na badala yake unatoa ushauri tujikite katika kupapambana na "njia ndogo" (cross-contamination) kwa kunawa mikono! Hii ni ajabu sana kwa mtu mwenye akili!

Mbali na hayo, umepotosha sana kuhusu Infectious Dose (ID50) na pia kuhusisha concept yako ya half-life (Ct50) na ile iliyotumika kwenye utafiti huu. Sitaki kutoa maelezo ya huo upotofu kwa maana nisije kuharibu baadhi ya points muhimu ulizotoa kwa jamii kwenye "darsa" lako. Ila nitafanya hivyo nikiona kuna haja.
Asante sana.
 
Back
Top Bottom