Utafiti: Ndoa nyingi zimeshakufa ingawa watu bado wanaishi kama mke na Mume

Utafiti: Ndoa nyingi zimeshakufa ingawa watu bado wanaishi kama mke na Mume

Ndoa nyingi zinaanza kwa kuunganishwa na mapenzi kati ya mke na mume, lakini baadae mapenzi kati ya wawili hao hufa na ndoa kubaki inaunganishwa na uwepo wa watoto kati ya mume na mke.

Wazungu sijui huwa wanawaandaa vipi watoto wao kisaikolojia kuishi pale ambapo baba na mama zao huachana, huku kwetu watoto mara nyingi hupitia kipindi kigumu sana kisaikolojia pale ambapo wazazi wao hutengana.

Naamini kwa kutambua hili, ndio maana wazazi huamua kuishi pamoja kwa shingo upande ilimradi watoto wabaki na amani yao, na kufanya hivi kwangu sio unafiki, ni uamuzi wa kijasiri kati ya wana ndoa.
Tatizo letu huku ni umaskini na roho mbaya
 
Mkuu kumbuka hao wadada wa kazi watakuwa ni wamama wa nyumbani tu, hawawasaidii kutafuta pesa wala kuhudumia familia, watakuwa wanawategemea waume zao kiuchumi

Mimi nazungumzia wale wanawake ambao, mnataka wawasaidie kutafuta pesa na kuhudumia familia, na bado mnataka wafanye majukumu ya nyumbani kama wadada wa kazi hilo ni gumu sana

Hoja yangu ni kwamba lazima mchague kimoja mpoteze kimoja hamuwezi kupata vyote, ni either uoe mama wa nyumbani ambaye atafanya majukumu ya nyumbani ila atakuwa tegemezi kwako kiuchumi, au uoe mfanyakazi au mfanyabiashara ambaye hatafanya majukumu ya nyumbani lakini atakusaidia kuhudumia familia na hatakuwa tegemezi kwako kiuchumi
Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;
1 kor 13:4-8.
Nina mashaka na tunda la upendo kuwepo Kwa wanandoa wengi.
Nonabyofahamu Mimi, palipo na upendo kila mmoja hujitahidi kujitoa kufanya jambo Kwa ajili ya kumpendeza mwenzie, kadhalika hujizuia kutofanya lolote ajualo kwamba litamchukiza mwenzie.
Ndoa nyingi zimevunjika na nyingine zimekufa kivitendo sababu mwanandoa mmoja au wote waliacha kujali Wala kuthamini hisia za wenza.
 
Mkuu bila shaka unafahamu kuwa wanaume hawahitaji uwape sababu ya kuchepuka, wao wanajiona kwamba wameumbwa hivyo tu kuwa hawatosheki na mwanamke mmoja hata wakioa mke mmoja ila wakichepuka lazima wasingizie kwamba sababu ni wake zao hata kama si kweli, na kwanini unaona kama mwanamke tu ndiye anayetakiwa ayachukulie na ayapotezee madhaifu ya mume wake au unashauri na mwanaume naye afanye vivyo hivyo kwa mke wake

Nimegundua ninyi ndio mnaodanganya wanaume kwamba inawezekana mwanamke kufanya majukumu yake huku akisaidia na ya mwanaume, mwisho wa siku wakiingia kwenye ndoa wakakutana na hali tofauti wanaanza kuwalaumu wanawake, wakati kumbe ni wao ndio walikuwa na expectations nyingi zisizo na uhalisia

Hivi kwa karne hii unadhani ni wanawake wangapi wanaweza kubalance hayo yote bila kutetereka mahali, ukizingatia wanaume wenyewe ndio hawa wasio na shukurani hivyo wanawake nao wanaona ya nini kujichosha, wewe mwenyewe umesema ulianza kubalance hayo yote pale watoto wako walipokuwa wakubwa na kuanza kuenda boarding unaona sasa hapo

Sasa vipi katika ile miaka yote ambayo watoto ni wadogo na wanasoma day schools unadhani mtu anajibalance vipi hapo, mimi hoja yangu ni kwamba kwanini mwanamke atwishwe majukumu mengi kuliko mwanaume, ilihali wote wana uwezo wa kusaidiana sawa kwa sawa au kuweka wasaidizi na maisha yakaenda vizuri tu
Upendo Hauna balance.
Kila mmoja ana jitahidi Kwa kadri awezavyo kutokana na fursa na vipawa alivyojaliwa na mwenyezi Mungu, kumfurahisha mwenzie.
 
Inatakiwa kushika vyote. Kazi ufanye uchangie kwenye uchumi wa familia na majukumu yako ya nyumbani utimize.

Kwani mwanaume kuwa na kazi na kuleta kipato kunamfanya asitengeneze mda Kwa ajili ya mkewe na watoto au shughuli fulani za nyumbani?
Mkuu,
Ndo maana twawakwepa wanawake wa namna hii.
Akiwa na kazi basi anajiona na yeye ni mwanaume.
Wanaume wawili ndani wa kazi Gani!!
 
Mm niliivaaan na mwanamke fulan back in time na ndoa tukafunga
Alinisumbua Bado nusu nijinyonge
But nkajikaza nkapiga moyo konde nkaamua kutalikiana nae
Wengine wapo
Akampata mwanamke mwingine anae adabu balaa nashukur mung now na kitambi kinatoka

Yes,I made a mistakes just because life comes without instructions
 
Na kwanini na ninyi wanaume msifanye vyote kama mnaona ni rahisi
Tukifanya vyote , mwanamke hata kuwa Tena na thamani kwetu.
Wanawake, msitafute ulinganifu.
Kiasili sisi ni watawala wenu.
Tunaweza kufanya chochote Kwa kujisikia. Hii haituongezei Wala kutupunguzia nafasi kwenye utawala wetu, kama ambavyo mfanyakazi hawezi kijaji kumuwajibisha bosi wake.
Halafu mwatafuta ulinganifu ili iweje!!
Mahali nani kalipa?
 
Mm niliivaaan na mwanamke fulan back in time na ndoa tukafunga
Alinisumbua Bado nusu nijinyonge
But nkajikaza nkapiga moyo konde nkaamua kutalikiana nae
Wengine wapo
Akampata mwanamke mwingine anae adabu balaa nashukur mung now na kitambi kinatoka

Yes,I made a mistakes just because life comes without instructions
😊😊 adi kujinyonga mzee ilikuwa hatari alikuwa anachepuka nn?
 
Na kwanini na ninyi wanaume msifanye vyote kama mnaona ni rahisi
Kwani huwa hatufanyi vyote tulete chakula, tulipe ada za watoto, tutume matumizi kwa wazazi wa wake zetu, tuwavishe mke na watoto. Mda huo wewe kama unafanya kazi ela yako ni ya kwako. Tuweke mtu wa kufanya kazi za nyumbani mwanaume ndio amlipe.

Nguvu inayotumika kutafuta hiki kipato kutimiza haya yote kwako ni sawa na wewe unaekaa nyumbani kudeki na kupika na pengine kuna mfanyakazi unamuelekeza tu anafanya.

Basi mi mwanaume uniwekee mfanyakazi nikae nyumbani au kama nafanya kazi ela yangu iwe yangu halafu tuone kama ntashindwa kufanya vyote

Au vyote vipi unaviongelea?
 
Hilo mbona wanawake hawana shida nimegundua wanaume ndio mna shida, haki sawa haihusu majukumu ya kiuchumi tu, bali inahusu hata majukumu ya nyumbani nayo inabidi mfanye wote 50 50

Na pia haki sawa haina cha mwanaume kumtawala mwanamke, wala mwanamke kumtii mwanaume inatakiwa kila mmoja ajitawale mwenyewe, na kila mmoja amheshimu na amsikilize mwenzake

Sasa wanaume wengi mkiambiwa hivyo hamtaki yani kwa kifupi ninyi hamtaki haki sawa ila mnataka majukumu sawa tena ikibidi mwanamke ndio afanye zaidi, huko kuendelea kung'ang'ania kwenu mfumo dume ndiko kunafanya wanawake nao washindwe kuwasaidia kuhudumia familia, na waendelee kutaka muwahudumie hata kama wana uwezo wa kuwasaidia
Ndoa asili yake sio usawa.
Itakapofikia hapo kwenye usawa,
Ni pale ambapo mahali litaondolewa kuwa takwa la kufunga ndoa.
 
Tukifanya vyote , mwanamke hata kuwa Tena na thamani kwetu.
Wanawake, msitafute ulinganifu.
Kiasili sisi ni watawala wenu.
Tunaweza kufanya chochote Kwa kujisikia. Hii haituongezei Wala kutupunguzia nafasi kwenye utawala wetu, kama ambavyo mfanyakazi hawezi kijaji kumuwajibisha bosi wake.
Halafu mwatafuta ulinganifu ili iweje!!
Mahali nani kalipa?
Jidaaaanganyeeeee🤣🤣🤣🤣
 
Kuna majirani zangu familia moja ni wazazi wa Producer mkubwa tu apa nchini na familia ingine ni wananchi wa kawaida tu, yan hawa ndoa zao zilishavunjika kitambo kila mmoja analala kwenye chumba chake kwenye nyumba moja ila nje wanaonekana kama wanandoa
 
Kuna majirani zangu familia moja ni wazazi wa Producer mkubwa tu apa nchini na familia ingine ni wananchi wa kawaida tu, yan hawa ndoa zao zilishavunjika kitambo kila mmoja analala kwenye chumba chake kwenye nyumba moja ila nje wanaonekana kama wanandoa
Kiburi cha uzima huko, siku mmoja akipatwa na maradhi utawaona wanajifanya kupendana na kujaliana .... Waswahili "wanasema nyoko nyoko kuonana".....Yani mnagombana sababu mnaonana, mna afya, siku mwenzio akifariki, au akiwa katika deathbed ndo utajua umuhimu WA kuishi kwa maelewano.
 
Back
Top Bottom