joto la jiwe
JF-Expert Member
- Sep 4, 2017
- 26,117
- 46,617
Aisee, ikifikia mtu anaona bora kufa kuliko kuishi nchini mwake, basi jua hali imefikia kiasi cha kutovumilika. Hali hii ilijitokeza sana hapa Tanzania mwanzoni mwa miaka ya 80s, vijana wengi walikua wanajificha katika meli ili waende Ulaya, wengi walitupwa na kufa baharini.Ngoja waje, waseme ya kuwa wao ndiyo happiest nation in the bloc if not on earth.
Mmoja alitaka kukimbilia ulaya kama wanavyofanya inzi au mbu.
Aisee, ikifikia mtu anaona bora kufa kuliko kuishi nchini mwake, basi jua hali imefikia kiasi cha kutovumilika. Hali hii ilijitokeza sana hapa Tanzania mwanzoni mwa miaka ya 80s, vijana wengi walikua wanajificha katika meli ili waende Ulaya, wengi walitupwa na kufa baharini.
Ni vizuri ukaelewa "Mukhtadha", yaani " context" ya mazungumzo. Hakuna nchi hata moja duniani ambako raia wake hawapendi kutoka nje ya nchi yao, ila kinachotofautiana ni kwa kiwango gani na sababu zipi.Ni ukweli gharama ya maisha imepanda sana Kenya lakini mnatudanganya mkisema hakuna watz ambao wanataka kuenda ngambo wajaribu kupata maisha bora. Stop being negative majamaa si ungwana.
Nimekuskiza na hatakama sijakubaliana naNi vizuri ukaelewa "Mukhtadha", yaani " context" ya mazungumzo. Hakuna nchi hata moja duniani ambako raia wake hawapendi kutoka nje ya nchi yao, ila kinachotofautiana ni kwa kiwango gani na sababu zipi.
Wajapan wengi wanapenda kuishi Marekani, sawa na wakenya au watanzania wanavyopenda kuishi Marekani, lakini sababu kubwa ya wajapani kupenda kwenda USA ni "Social", wakati sisi huku ni " Economical".
Kwa sasa hivi uchumi wa Kenya umeyumba sana ukilinganisha na Tanzania, kwahiyo ni wazi kwamba wakenya wengi wanapenda kwenda USA kuliko watanzania.
Wewe inaonekana ni mgeni, lakini inaonekana bado hujachafuliwa na malumbano ya hapa JF, bado unatumia busara kujadili hoja kuliko sisi wenyeji ambao wengi tunatumia ushabiki zaidi.Nimekuskiza na hatakama sijakubaliana na
mengi uliyosema, umesema vitu vya maana.
Saa zingine huwa nafurahi nikiona mandugu zangu watz mitandaoni mkiongea vibaya kutuhusu sisi wakenya. Hizi nguvu mnazoziweka kutuharibia jina haitafanya Tanzania ingare wala ifanikiwe na ninawaomba mtoke online mwende mkajenge nchi yenu vile.
Hilo ni swali nzuri.Wewe inaonekana ni mgeni, lakini inaonekana bado hujachafuliwa na malumbano ya hapa JF, bado unatumia busara kujadili hoja kuliko sisi wenyeji ambao wengi tunatumia ushabiki zaidi.
Ningependa kukuuliza maswali machache unijibu.
1)Hivi kwanini wakenya mumeambizana na kuamini kwamba kitendo cha Tanzania kuchoma vifaranga pale Namanga ni kosa, na lengo ni kuhujumu Kenya?
Twaendelea kuijenga. Hiyo ilikuwa typo lakini shukran.kwani nchi yenu imejengeka?
na sio ingare bali ni ing'are
Huo mtazamo ulionao dhidi ya Tanzania, ndio sababu kubwa inayotufanya tukorofishane na Kenya, tatizo ninyi wakenya muda mwingi hamfikirii sana, huwa mnatumia mihemuko badala ya kutumia busara.Hilo ni swali nzuri.
Sisi kama wakenya hatukuelewa huo msimamo wa serikali yenu kuchoma vifaranga vyetu kwa sababu ya “virusi” nyinyi mngeturudishia vifaranga sisi tuendelee na shughuli zetu sasa kutuchomea ilisababisha wafanyibiashara waone hii serikali ya JPM iko na kasoro na hiyo kasoro ni hamaapendi wakenya na hamtaki afrika mashariki iendelee kusonga mbele. na wakumbuka ile time mlichukua ngombe wetu mkawashika wakenya wamasai na mkawatia rumande? Wakenya hatukuridhishwa na jambo hilo na namwelewa JPM ywafaa kulimda maslahi ya watu wake lakini zile vitu anazozifanya are in bade faith.
Na wacha nikuulize swali, katika afrika mashariki mbona watanzania hamtaki sisi sote tufanye trade, biashara na kazi pamoja? Kila masaa unaskia waganda na wakenya mara warwanda na waburundi wamefurushwa kwa sababu ya reasons zisizojulikana. Na je kama marehemu Nyerere angekuwa hai wadhani angeridhishwa na vile mnavyowafanyia wenzenu na vile tanzania haijihusishi sana na maswala ya EAC kama zamani?
Lengo la maswali yangu ni kutaka tutafute tatizo lipo wapi Kati ya Kenya na Tanzania katika uchomaji wa vifaranga, na wale Ng'ombe.Nchi ni yenu na mwaruhusiwa kufanya chochote mnachotaka joto la jiwe
Kenya on the wrong path? |The Big Story
Get the latest news,entertainment and sports news from Kenyawww.standardmedia.co.ke
Wakenya wengi wamekata tamaa ya maisha kutokatana na gharama za maisha kuwa juu nchini mwao, rushwa na ukosefu wa ajira. Matokeo ya utafiti huu yanaendana na utafiti mwingine ulioonyesha kwamba, wakenya wengi hawapendi kuishi nchini mwao na wanapenda kutoroka na kuishi nchi za nje.
Hali hii ya wakenya kukata tamaa ya maisha na kuwaza kutoroka, imesababisha mkenya mmoja Jana kujificha katika eneo la gurudumu la ndege ya KQ ili aweze kutoroka Kenya, bahati mbaya amefariki kabla ya kutimiza lengo lake.
Hivi unajua tofauti kati ya utafiti na maoni ya mtu?Jamani mbona vitu vimepanda ghafla
Wakuu habari zenu poleni na majukum ya kitaifa Kuna jambo limenishangaza sana mbona maisha yanazidi kupanda sana toka tarehe moja nimeenda dukani kununua sukari kilo moja kwetu huku ilikuwa tsh 2600 sasa hivi imefika 2800 Bati pia hivyo hivyo bando moja hizi za rangi nimekuta bei imepanda toka...www.jamiiforums.com
Unafanya watu wazima waonekane watoto...Hivi unajua tofauti kati ya utafiti na maoni ya mtu?