Utaifa wa EAC unachelewesha maendeleo

Kwani historia inahusu mambo ya sasa hivi?

..Historia ni jambo zuri.

..Na historia inatakiwa itusaidie kufanya maamuzi mazuri zaidi.

..Historia haitakiwi itukwamishe ktk kufanya maamuzi, au iwe kikwazo cha maendeleo ktk EAC.
 
big up sana Omera nakuunga mkojo. Kuna vizee vijinga sana pande hizi mbili eac ilikuwa moja tu.

mzungu kawagawa ikawa hivo mpaka leo naona km walituroga hivi. Eti anakata nchi km andazi na inakuwa hivo hadi leo!

Jitu kubwa lina nywere nyeupe kila mahali linaogopa kuungana. Eti mara huyu hivi mara hivile yaani ijinga mtupu.

hapa ni kuzichapa tuondoe wajinga wote tubaki damu mupya!
 
Tunapoandika humu tujaribu kuandika mambo ya ukweli na kuacha upotoshaji wa kijinga.

Baada ya uhuru wa Tanganyika, nchi hii ikiwa chini ya utawala wa Mwl Nyerere iliamua kufuata mfumo wa ujamaa na kujitegemea na ndipo mwaka 1967 Nyerere alipoamua kutaifisha mali zote za mabepari baada ya kutangaza azimio la Arusha.

Na kimsingi matatizo ya Tanzania yalianzia hapo rasmi, vita ilikuja kuongezea tu balaa ambalo tayari liliisha kuwepo.

Tanzania baada ya kuwadhulumu matajiri mali zao haikuweza kupata tena wawekezaji na eti serikali ndio ikageuka kuwa mwekezaji mambo anayotaka kutuletea tena Magufuli leo.

Nchi ikabaki bila viwanda na kilimo kikabaki kwa watu maskini ambao hawakusoma na wale waliokata tamaa ya maisha. Nchi ikawa inanyemelewa na njaa hadi Nyerere kwenda nje kutembeza bakuli.

Itakumbukwa kwamba jumuiya ilivunjika mwaka 1977 na vita vya Tanzania na Uganda vikaja kuanza Novemba 1978 hadi Aprili 1979.

Itakumbukwa kwamba Kenya ilikuwa ni koloni kamili la Uingereza na hivyo waliwekeza sana huko tofauti na walivyofanya Uganda na Tanzania.

Hivyo sera ya Nyerere ya ujamaa ndio ilikuwa msingi wa Tanzania kuwa na uchumi dhaifu toka mwanzo na hiyo fikra aliyowarithisha watu walio kwenye mamlaka ktk nchi hii hadi leo ndio imekuwa chanzo cha nchi hii kutokupiga hatua yoyote ya maana katika maendeleo pamoja na kuwa na rasilimali nyingi kuliko nchi kama Kenya na Uganda.

Tanzania haina nafasi yoyote ya kuipiku Kenya kiuchumi kwani kufuatia yanayoendelea katika nchi hii kwa sasa tukinyimwa tu haki ya kukopa.....tumeisha ndani ya wiki moja tu, sasa uchumi tegemezi hivyo una kipi cha kutambia, absolute nothing.
 
Tumezoea kukaa kwenye jumuia za kupiga domo. Wakisema tufanye vitendo mambo yaende tunaanza visingizio.
Mi mwenyewe huwa najiuliza, hivi hatuna jambo ambalo tukilipeleka huko EAC litatufaidisha sana sisi? Kwanini kila mara wenzetu wanaleta miswada tunagoma eti haitatufaidisha lakini sijasikia sisi tukipeleka!. Tupo defensive muda wote. Mfano, sisi tuna advantage kwenye uzalishaji wa mazao ya chakula, tumewahi peleka mswada kuwe na soko huru la chakula EAC? Ni kama hatutaki huu muungano ila tunaogopa kuwaambia wenzetu.
Kwa deadline waliyojiwekea nafikiri mwaka huu tulikuwa tuwe na sarafu ya EA.
Mi naona bora nchi zingine zitutoe kwenye jumuia. Uganda, Kenya, Rwanda na SS waunde jumuia yao. Sisi wazembewazembe tubaki hivyohivyo.
 
Mleta mada nakuunga mkono asilimia Mia!

Diversity is the real future! Na ndicho kinawabeba sana wamarekani mpaka sasa! Considering the fact of technology being the world’s current state, ujanja ni kuungana na sio kutengana!

Ipo siku kama sio watoto wetu basi wajukuu zetu wataifanya Africa Taifa moja, United Nations of Africa (UNfA the f will be silent). Ipo siku!

Hata wahenga wa kabla ya Uhuru walisema “umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu “ (bahati mbaya wengine tukatafsiri in terms of vijiji vya ujamaa)
 
mngekuwa mnafikiri sawa sawa mngejua engene ya huu muungano ni TZ,ndio maana inaposua sua hakuna kinachoendelea.TZ yenyewe binafsi imeshajua ndio maana hamuoni ikiunga mkono wa hili swala.

EA inaihitaji TZ kuliko TZ inavyoihitaji EA.
kuna Kenya,UG na Ethiopia wanaweza wakiamua,waache uoga.
 
Diversity is the real future! Na ndicho kinawabeba sana wamarekani mpaka sasa!
Mbona hujazungumzia waChina, Wajapan, n.k.; wao hawakujibeba?

Hujawahi kumsikia Trump akilalamika kuhusu NAFTA, ushirikiano kati ya Mexico, Canada na USA?

Hiyo 'diversity' unayozungumzia ni kitu tofauti kabisa na haya yanayojadiliwa hapa.

Hakuna anayekataa kushirikiana na wengine, lakini ushirikiano hauwezi kulazimishwa.

Kushirikiana sio swala la kushirikiana tu, ni lazima nchi washirika wawe ni nchi zinazopenda kushirikiana kwa dhati, huwezi kutaka ushirikiano kwa nchi moja kudhani itafaidika zaidi ya washirika wenzake kwa hira au mbinu chafu..
 


Chief, ni mjadala huru hence mawazo huru! Huo ndio mtazamo wangu!

Lakini ipo siku East Africa na Africa itasimama pamoja kama kitu kimoja chenye kauli moja! Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu!

Ipo siku!
 
Kwani wanaokwamisha shirikisho la EAC ni nani kama sio wabongo?
Swali ni: Kwanini iwe lazima kuwa na "shirikisho la EAC"?

Kwani hatuwezi kuwa na 'Mashirikisho' mengine, mbona tunao majirani wengi tu wa kuunda shirikisho nao?
 

..ninavyoelewa mimi engine inarahisha kazi, badala ya kufanya kazi ziwe ngumu zaidi.

..sasa kama Tz ni engine ya eac basi tulitakiwa tuonyeshe njia kwa wenzetu, tuwe chachu na siyo kikwazo ktk jumuiya.

..yako mambo mengi ambayo yanatokea ktk jumuiya na reaction ya serikali na wananchi wetu ni kama vile tumeshtukizwa.

..serikali yetu inajua nini kinachokuja mbeleni ktk masuala ya integration lakini wananchi hawaandaliwi ku-take advantage au kukabiliana na hali hiyo.

..Labda nikupe mfano mdogo...Tanzania tuna population kubwa kuliko majirani zetu, kwa hiyo sisi ndio wenye labour force kubwa zaidi. Je, tumefanya marekebisho na maboresho yoyote ktk mfumo wetu wa elimu ili vijana wa Tz wawe in high demand kujaza soko la ajira la Afrika Mashariki?

..Unaposema EA inaihitaji Tz kuliko Tz inavyoihitaji EA una maana gani? Nchi za EA zinahitaji waalimu toka Tz? Zinahitaji Engineers toka Tz? Zinahitaji bidhaa za viwandani toka Tz?

..Wenzetu wanatuhitaji "Watanzania", au wanaihitaji "Tanzania"? Na kwanini?
 
Chief, ni mjadala huru hence mawazo huru! Huo ndio mtazamo wangu!

Lakini ipo siku East Africa na Africa itasimama pamoja kama kitu kimoja chenye kauli moja! Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu!

Ipo siku!
Ni wapi nilipokukataza kuwa na "mawazo yako"; kwani mimi hutaki niwe na mawazo yangu kama hayo niliyoyatoa?

Tatizo liko wapi?
 
Ni wapi nilipokukataza kuwa na "mawazo yako"; kwani mimi hutaki niwe na mawazo yangu kama hayo niliyoyatoa?

Tatizo liko wapi?

Mtazamo wangu; kuungana EAC ni bora na Faida zaidi kuliko hasara!

Mtazamo wako; sio bora wala sio lazima, miungano ipo mingi!

Kila mmoja abaki na wake. Ahsante
 
Mtazamo wangu; kuungana EAC ni bora na Faida zaidi kuliko hasara!

Mtazamo wako; sio bora wala sio lazima, miungano ipo mingi!

Kila mmoja abaki na wake. Ahsante
Sasa nikitaka kukueleza kuwa "EAC" sio bora na haina "Faida zaidi" utaona nimeingilia mawazo yako?
Ingekuwa hivyo basi ungekaa nayo mawazo yako hayo na usiyaweke hapa.
Ukishaweka hapa ukumbini, maana yake ni kwamba unakaribisha mawazo mbali mbali, ikiwa ni pamoja na yale yanayopingana na yako.
 

sijui kama umenielewa au mawazo unachojua ndicho nilitaka ukielewe ila tayari unakijua ila kwa namna tofauti kidogo.

niliposema ni engene sio kwa maana ya kwamba tayari tunaendesha EAC,hapana.ni kwamba sisi ndio hot cace ya muunganiko huo.ndio maana tunaposita kutia miguu yote,muungano wote unakosa mashiko.rejea UK na EURO.

hiyo pop ndio backup no 2 ukiondoa ardhi,sisi tunayoitegemea kiuchumi,rejea china na uchumi wake.ina jitoshereza kwa soko la ndani kibiashara na viwanda.kuhusu kujiandaa kuwa na workforce hilo lisikutishe,ndio sababu vyuo na shule zinajengwa kila siku,ukiacha miaundombinu.

ninaposema EA inaihitaji TZ namaanisha hapo juu,kwa maana kujibu swali lako TZ haihitaji eng kutoka nchi nyingine hapa tz,wala dr,wala mtaalamu yeyote.

wenzetu wanahitaji TZ sio watz,ndipo kigugumizi cha tz kilipo.so for now wacha kila mtu ashinde mechi zake tu.
 
wenzetu wanahitaji TZ sio watz,ndipo kigugumizi cha tz kilipo.so for now wacha kila mtu ashinde mechi zake tu.

..asante.

..mimi nadhani na sisi inabidi tujiongeze ili wenzetu watuhitaji "watanzania."

..Ni kweli tuna ardhi kubwa kuliko wenzetu, na ninaunga mkono kuilinda kwa ajili ya waTz.

..lakini hali itaendelea hivyo kwa muda gani kabla hatujaanza kubanana wenyewe kwa wenyewe?

..Tukumbuke kwamba ardhi haiongezeki, kwa hiyo tujiandae kwa EA ambapo ardhi ni ndogo hata kwa Watanzania wenyewe.
 
Kenya sio kama tunawaogopa ishu ni ndumi la kuwili hatuhitaji ushirikiano nao
 
Kenya sio kama tunawaogopa ishu ni ndumi la kuwili hatuhitaji ushirikiano nao

Watanzania tuna utamaduni wa kujidanganya na kujiaminisha uongo. Mfano sio wazo baya kuammua kwamba kama nchi hatutafanya lock down ya Corona kwa sababu za kiuchumi lakini hiwezi kuwa na akili zako ukafikiri corona haipo kabisa au inaishia kwenye mipaka Lakini kwasababu tunapenda kujidanganya tunatumika kwa faida binafsi. Hivyo ni ngumu kujadili mambo kama watu wameamua kuamini uongo. Mengi tunayo amini kuhusu jirani zetu ni uongo.
 

Chief mimi na wewe wote wachangiaji na kwenye kuchangia mada kila mmoja ako na opinions zake!

Narudia tena maoni yangu muungano wa nchi za Africa mashariki na Africa kwa ujumla unafaida nyingi zaidi ya utengano, na kile ukionacho kibovu kwako kwa wengine kina thamani na kinyume chake!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…