Utajiri ni Siri, na Siri ndio Utajiri wenyewe

Utajiri ni Siri, na Siri ndio Utajiri wenyewe

fedha na dhahabu ni Mali ya Bwana Mungu umpa ampendae . sio siri. utajiri wa siri ni washetani hata shetani ni tajiri sana . je? wewe unaongelea utajiri gani? kweli utajiri wa shetani ni siri kubwa uwa mama au mtoto au watoto , kuvunja na kupora na kuua. wizi wa mali mbali mbali na ujambazi kisha ukawa tajiri ndio Maana matajiri wengi na utajiri ni siri kubwa wakikueleza unaweza kuzimia au kufa kabisa.

Hata shetani humpa amtakaye, kwani wangapi wanaamini uchawi na uganga na bado ni masikini

Utajiri ni Siri, Ukiwa kiropo ropo hata usali mara elfu kwa Mungu hawezi kukupa utajiri kwa ukiropo ropo wako.

Mungu huwapa watu wenye siri, sio utajiri tuu hata akili, maarifa, ubunifu n.k
 
Ungesoma kidogo kidogo uambulieamo

Nimemuambia hata shuleni kuna walioishia darasa la pili, wala asijali, kila mmoja anakula urefu wa kamba yake.

Yeye asitake kwa vile kaishia la pili basi akadhani watu wote wanataka waishie la pili kama yeye
 
wewe umefikiria siri za kupata utajiri ni siri . ila hujafikiria njia wanazopita Matajiri zikoje na kwanini ? ni siri kubwa nadhani mtoa Mada ni kijana bado mimi ni mzee miaka 64 sasa nyani mzee amekwepa Mishale Mingi. Pia nina Maisha Mazuri sana ila si tajiri . achana na siri ya Mtu tajiri . kwa Mungu hakuna siri . Mungu anampa ampendae utajiri sio kwa siri . hata wewe unae soma ujumbe huu Mungu akupe utajiri kwa Mapenzi yake . siri kwa siri Anae toa kwa siri ni shetani kwa sababu njia zake si halali
 
Mkuu hapa duniani Kuna mambo mengi Sanaa tumelishwa na mpaka leo yamekua kizungumkuti kwa fact hyo hiyo ya kusema "we amini hivo"...

Sasa na ww naomba usipite humo humo katika kuweka njia panda...unless ungeamua tu huu Uzi kubaki nao kichwani....lakini as long as umeamua kuleta elimu ya kututoa kwenye giza kutuleta kwnye mwanga then you must be at list a lillte bit open.......

Funguka hata kwa uchache tu au kwa juu juu tu.......tell us ni watu gani hao and how do they know our tomorrow's
Amesema ni siri unataka atoe siri so atakua maskini.
 
wewe umefikiria siri za kupata utajiri ni siri . ila hujafikiria njia wanazopita Matajiri zikoje na kwanini ? ni siri kubwa nadhani mtoa Mada ni kijana bado mimi ni mzee miaka 64 sasa nyani mzee amekwepa Mishale Mingi. Pia nina Maisha Mazuri sana ila si tajiri . achana na siri ya Mtu tajiri . kwa Mungu hakuna siri . Mungu anampa ampendae utajiri sio kwa siri . hata wewe unae soma ujumbe huu Mungu akupe utajiri kwa Mapenzi yake . siri kwa siri Anae toa kwa siri ni shetani kwa sababu njia zake si halali

Kwa Mungu hakuna Siri? Mzee wangu unajua hata maana ya Mungu?
Unapoambiwa Mungu aliyesirini unaelewa nini/

Unasema hakuna siri kwa Mungu,
Unajua kwa nini mpaka sasa hakuna aliyewahi kumuona Mungu?
Unasema hakuna Siri kwa Mungu, mzee acha hizo bhana.

Unajua siku yako ya kufa?
Unajua siku ya mtu kufanikiwa au kuanguka?

Unajua kwa nini Mungu ameficha mawazo ya mtu na mtu, yaani wewe ukifikiria mimi sijui, nami nikifikiria nawe hujui? Unajua maana yake hivyo?

Unasema hakuna siri kwa Mungu kana kwamba kesho unaijua,

Kesho ni muhimu kwa sababu hatuijui, kesho ni siri na walio nayo ni wale wenye siri hiyo.

Kwa Mungu kuna siri nyingi kuliko kwa shetani,
Mungu bila siri hawezi kuwa Mungu,
Kusema kwa Mungu hakuna siri tafsiri yake ni kuwa Mungu hana thamani tena
 
kuna watu hawana siri ni wawazi na wakweli na uwazi wao uliwapatia utajiri Mkubwa . kuna vitu vitatu ukitaka kufanikiwa maishani Uwe Mwaminifu sana, uwe kweli, uwe Msikivu na Mnyenyekevu. uwe na bidii na juhudi na Maarifa. Mtangulize Mungu kwa kila kitu .
 
vijana wa hizi wao wanajua kila kitu , sisi wanaona tumechelewa wao wamewahi , mnakopita tulipita long time mi nasaidia tu kutoa maoni yangu ukiona yanafaa yachukue ila ukiona ni hayafai ya tupe kapuni.[emoji120]
 
Ndio haya maswali ya masikini yanavyokuwaga,

Wewe hata nikiwa tajiri unafikiri itakusaidia?

Nashukuru mfano bora umejitokeza, na wewe utakuwa Case Study humu Jamvini
Matjiri wala hawaongei sana kam wewe.
Vilevile sio kweli kuwa matajiri hawana marafiki wengi,akina Ginimbi si uliwaona wewe!
 
Bandiko bora kabisa kwa huu mwaka, mimi niko tofauti sana na viropo ropo..

Hapa kuna ndugu yangu tayari nimemuweka kando, nilimpa mchongo matokeo yake akaanza kutangaza kwa kila mtu mpka watu ambao kwa vyovyote hawawezi fanya hiyo issue, nikaona hapa hamna mtu saiz namchukulia kama jamaa tu!
 
Kisa kingine,
Miaka ya nyuma, nlipata mchongo na wazungu flani.
Ilkua biashara ya kununua magogo Aina flani ya miti kutoka kusini

yanakusanywa, kontena likijaa nawataarifu

Wanakuja na mashine yao, wanayasaga saga mogogo yote yakua unga.

Kisha wanapaki kwenye viroba na KISHA WANANILIPA CHANGU kwa Kila kilo ya unga iliyopatikana Na kuyasafirisha kwenye ndege.

Nikaja nikamdokeza iyo fursa Binamu yangu mmoja Alkua anaishi maisha ya tabu sana.
Lengo lilikua tuunganishe Nguvu, niweze kukusanya mzigo wa kutosha FAIDA iwe kubwa.

Na nkajitolea siku moja naenda kuchukua mzigo nkaenda nae kabisa,
Siku nakabidhiwa malipo yangu, mchakato mzima anauonana KABISA.

Alichokifanya,
Akaanza kuhangaika kuomba omba mitaji kwa ndugu na watu wengine.

Nkashangaa kwny grup la familia,
Katibu wetu kaanzisha Uzi na anaomba wanafamilia wote wamchangie ndugu yetu afanikishe iyo project yake.

Siku sio nyingi nkaanza kuona watu wananifatilia,

Mara niamshwe usiku usiku, polisi wamekuja kunikagua nyumbani.

Nkiendesha usiku, Mara polisi wenye pikipiki wanisimamishe kunikagua.

Mara niitwe na

Nikakamatwa nikihisiwa kufanya biashara ya madawa ya kulevya.

Polisi, ananihoji eti Kuna miti huwa nasaga nasafirisha unga unga.
Nimweleze uwo unga unakazi gani.

Nikakana Kila kitu,
Walinishikilia siku 3.

Yaani ilkua Ni usumbuf JUU usumbufu.

Baadae,
Kule nlikokua nanunua mzigo, wakaanza kunitilia mashaka Kila nkija kununua mzigo.

Mara waanze kunihoji hoji maswali hayana kichwa Wala miguu.

Siku sio nyingi,
Wale wazungu wakaja kuchukua mzigo Kama kawaida,

Baadae nkaja kuskia wamedakwa na polisi usiku airport wakipakia mzigo kwny ndege.

Taarifa zikaenea kua ule unga ulkua inachanganywa na vitu vingine kutengeneza Aina flani ya dawa za kulevya.

Nkaona isiwe tabu,
Nkahama ule mkoa haraka sana na NAMBA ya SIMU nkabadilisha kabisa.

Nkafunga mawasiliano na ndugu na wanafamilia wote.

Almost 2yrs,
Ule upepo ulipopoa ndo nkarejea kwny maisha ya kawaida.

NAJUTA KABISA.
Mkuu mbona unanitisha sana na hawa ndugu
 
Back
Top Bottom