Utajiri wa Magofu ya Rapta

Utajiri wa Magofu ya Rapta

Mugabonihela, hii Hadithi ndivyo ilivyo isha, ? 😀😀😀Au umepatwa na changamoto huku sisi hatujui maana ishakuwa ni the long wait...
 
TUNAENDELEA WAKUU MAMBO YALIKUA MENGI KUNA DHARULA NYINGINE HAZIELEZEKI

Ebu tuiangalie hii methylphenidate ina fanana na cocaine katika namna ipi,

Kwanza kabisa hii methylphenidate na cocaine mfanano wake unaanzia kwenye chemical properties.

Ukiacha ufanano huo wa kikemikali, methylphenidate na cocaine zote huchochea uzalishwaji wa homoni zinazojulikana kama dopamine.

Kazi ya hii homoni ya dopamine ni kumfanya mtu ajisikie raha, kwaiyo ukiona ukifanya jambo au ukila kitu Fulani unahisi raha basi jua tu kama ukiwa kwenye jambo hilo kuna uzalishwaji mwingi wa dopamine ndio maana unakupelekea au unasikia raha.

Mara nyingi dopamine huzalishwa kwenye mambo kadhaa kama vile sex (wakati wa kufanya mapenzi), chakula apa ukiwa unakula chakula kizuri unachokipenda. Lakini pia wakati wa kusikiliza Muziki mzuri unaoupenda au hata kamali pia,

Apa kwenye kamali kwa wale wazee wa kuweka mikeka kama siku hujabeti unakosa amani kabisa lakini ukiweka mkeka nafsi inapoa inatakata broh!!!! hiyo ni kazi ya dopamine na ndio maana wataalamu wanasema kamali ni ulevi pia kama ulevi mwingine.

Kuhusu kiasi cha dopamine inayozalishwa wakati wa kushiriki ngono (sex) inasemekana haifikii kile kiasi cha dopamine kinachozalishwa baada ya kutumia unga (madawa ya kulevya). Kwa mantiki hii raha ya kuvuta madawa ni zaidi ya mbili au mara tatu ya raha ya kufanya ngono, hivyo teja au mtumiaji wa madawa anapata raha zaidi kuliko mtu anaefanya ngono.

Hhhhhmmm ni ukweli ugumu sana kuukubali lakini trust me, ndio maana mtumiaji wa dawa za kulevya si rahisi kuacha ata mkipambana vipi kwani kwa raha anayopata kule hakuna sehemu anaweza akafidia starehe ile.

Kazi kwako sasa ifikirie raha ya kula tunda alafu unaambiwa haifikii raha ya kuvuta unga, usione baadhi ya watu maarufu wameshindwa kutoka kwenye kifungo cha madawa ni kwasababu hakuna kitu kingine kinachoweza kumpa raha itakayofanana na unga.

Wakati we unakaa vijiweni unabishana tu kuwa hakuna kitu kitamu kama asali na pussy, watoto mjini wala ngada wanakuchora wanakuona mshamba hujui kitu.
Tusitoke sana nje ya mada nilikua najaribu kuelezea mfanano uliopo kati ya methylphenidate na cocaine tuendelee na upande mwengine.

Utofauti uliopo kati ya methylphenidate na cocaine au madawa mengine ya kulevya kama heroin hizi ni kwamba zenyewe hutengeneza kitu kimoja maarufu kama arosto.

Mara nyingi tunawasikia mateja wakilalamika kuhusu arosto, je! Hii arosto ni nini na mtu hujisikiaje akiwa kwenye arosto na afanye nini kuiondoa arosto.

Sasa ni hivi kadili mtumiaji anavyoendelea kutumia cocaine zaidi ndivyo hivyohivyo pia mwili huitaji cocaine zaidi ili kuendelea kuzalisha dopamine ya level ile ile ambayo humfanya ajiskie raha isiyo kifani.

Na ikitokea mwili umekosa cocaine hapo ndipo unakutana na neno arosto, mtumiaji hupitia wakati mgumu sana kwani mwili na akili kwa pamoja vinapambana kwa kutumia energy nyingi ili kujirudisha kwenye hali ile ya raha.

Kuna mfano mmoja niliwahi kupewa tatizo una lugha mbaya,

Imagine umemuandaa mtu kwenye kula tunda na umeanza tu zile in and out, alafu unatoa mashine unavaa unaondoka, asee apo binti atakupiga ata na stuli kama ipo karibu.

Hiki anacho feel binti wakati huo yaani alikua kwenye raha ya ajabu alafu from no where raha zinapotea lazima ata ghazibika sana. Sasa kwa mateja ile graph ya levels ya dopamine huwa juu akishatumia unga lakini ndani ya muda mfupi sana graph inashuka.

Sasa basi arosto ni ule mchakato wa ndani ya mwili wa kupambana kurudisha graph juu bila ya kuwa na cocaine, apa mwili hutumia energy kubwa na mwili ukifeli kurudisha graph juu kinachofata ni maumivu.

Mtumiaji hupatwa na shida nyingi zikiwemo maumivu ya viungo, kichwa kusikia baridi kali mapigo ya moyo na presha kuwa juu na wengine hupatwa na maumivu makali ya tumbo kukosa hamu ya kula na ata kutapika pia.

Katika point hii sasa ndio teja ata pambana kwa namna yoyote kupata tena unga ili ahakikishe anarudi kwenye zile raha na akifikia hatua hii tayari amekua mtumwa na hana future tena kwani kila atakachokua ana fanya ni kwa ajili ya kupata unga.

Usione kuna baadhi ya watu maarufu wamezama huko na hawawezi kutoka ukawaona wajinga na hawana akili hapana kosa lao la kwanza ilikua ni kujaribu. Jinsi ya kutoka huko sio rahisi inahitajika nguvu kubwa ya kimatibabu na nguvu ya kiroho pia ili uweze kutoka kwenye utumwa huo wa madawa ya kulevya.



Kuna siku nitagusia vita inayoendelea kati ya mabepali wa duniani na monopolization ya biashara ya cocaine na heroin, kuna namna ata vile vita vinavyoendelea huko Afghanistan ni miongoni mwa mipango ya mabepali katika interest za biashara zao.

Zile shida anazopitia mtumiaji wa cocaine wakati wa arosto mara nyingi japo sio kwa watu wote hupitia changamoto hiyohiyo baada ya matumizi ya methylphenidate.

Yaani ukitoka kutumia methylphenidate probably utapitia mambo yafuatayo kama sio yote basi Baadhi,
  • kichefuchefu au ata kutapika
  • usingizi kukosa hamu ya kula
  • maumivu ya kichwa n.k

Unatakiwa kujua kuwa methylphenidate ni dawa halali na imehalalishwa na mamlaka zote za dawa na chakula duniani, lakini tukiwa kwa upande mwingine yaani huku kwenye unga nadhani kila mtu anajua balaa lake ikitokewa umakutwa ata na gram moja nini kinakupata.

Turudi kwenye simulizi tusichoke,

Baada ya kuijua dawa hii ya methylphenidate nilijiuliza ina maana fatemeh ni mgonjwa na ndio maana anatumia methylphenidate, kama ni kweli mgonjwa mbona sijawahi kuona dalili yoyote ya ugonjwa huo kwake.

Kuna muda maisha ya fatemeh yalikua yananiumiza kichwa kiasi kwamba siutaka ata kuyafikiria, nilimuuliza shahzad vipi kuhusu future ya mjukuu wake yaani baada ya hapo akiwa anaendelea na dawa hizo haiwezi kuleta shida ukubwani akishakua mtu mzima.
Shahzad alijibu hakuna tabu yoyote tena kwakua ameanza tiba tokea akiwa na miaka sita na ukilinganisha tatizo lenyewe sio la kimaumbile na saikolojia ataweza kuishi vizuri na kufanya kazi vizuri bila kuleta changamoto zozote.

Kibongobongo sidhani kama watoto wenye shida hizi hujulikana mapema na kupewa tiba, kama hawajulikani na hawapewi tiba basi makazini mwetu tuna wafanya kazi wenzetu ambao nao pia ni wahanga wa ADHD lakini bila wao kujua.

MIMI: hhhmmm sasa mzee shahzad mjukuu wako anaweza kufanya shughuli zipi za kitaaluma ambazo hazita leta shida kwenye changamoto aliyonayo.

Shahzad alicheka sana akauliza kwani mimi mpaka muda huo nimeona changamoto gani kwa mjukuu wake huyo.

Kiukweli sikua nimeona changamoto yoyote ile zaidi ya kumuona yupo kawaida, ila shahzad aliongezea kitu kutokana na swali langu nililouliza kuhusu shughuli anazoweza kufanya mjukuu wake apo baadae.

Shahzad alisema wengi wa watu wenye changamoto hiyo ya ADHD hujishughulisha na ujasilia mali, wengine wengi akiwa na mfano wa nchi hiyo ya Iran na kwingineko hutumika kama computer programmers huku waliobaki unudumu kwenye viwanda au sector zinazohitaji creativity.

Kwa nchi ya Iran kulingana na tafiti zilizofanywa na taasisi iliyojulikana kama psychosocial health Research institute, waliwahi kuchapisha au kutoa makala iliyo toa taarifa za tatizo hilo la ADHD ( attention deficit hyperactivity disorder) kwa nch hiyo.


Makala hii ilitaja kuwa kuanzia mwaka 1990 mpaka kufikia mwaka 2014 idadi ya watoto na watu wazima waliozaliwa na tatizo la ADHD walikadiliwa kufikia 33,000 ( therathini na tatu elfu).

Unaweza kuona ni idadi kubwa kiasi gani kwa nchi kama Iran kuwa na watu wenye shida hiyo hivyo ADHD haikuwa changamoto mpya miongoni mwa raia wa Iran.

Tukirudi kwa fatemeh sasa, niliona ni busara kwenda kumuuliza yeye mwenyewe kuhusu matumizi ya dawa hizo kwani mpaka wakati huo alishakuwa muwazi kwenye baadhi ya mambo yanayohusu maisha yake.

Lakini pia wakati huo huo nilikumbuka zile moment tukiwa haullaga namna gani alikua anapata shida kuhusiana na jambo ambalo javier aliliita ni arosto ya fish scale Cocaine aliyokuwa akipewa na Catarina.
Lakini binafsi nikiwa haullaga sikuwahi kumshuhudia kwa macho yangu aki sniff kwani alikua akienda kwenye jengo la pili pembeni ya maabara ambapo lilikua linatumika kufungashia mzigo pindi unapokamilika.

Shahzad alinitahadharisha niache kuendelea kuuliza maswala ya methylphenidate kwani kwa siku hiyo yeye hakutakiwa kuwepo hapo kwa muda mrefu kwani ataondoka.

Na aliniomba tukimaliza pale tufuatane kama nitakubaliana nae ili akanikutanishe na baadhi ya watu ambao anafikiria watakua na msaada kwa namna moja ama nyingine juu ya jambo letu.

Sikutaka kujibu moja kwa moja kwani niikumbuka kauli au masharti ya fatemeh kwamba sikutakiwa kwenda popote pale bila idhini yake wala siku takiwa kukutana na yeyeto bila idhini yake.

Lakini nilimuambia shahzad kwamba tutaenda wote kwakua ameshatangulia kusema watu tutaokutana nao watakua na msaada kwenye project yetu.
 
3/4 umesimulia habari za Cocaine na Arosto
🫢🫢🫢[emoji848][emoji848]
Kwenye utangulizi nilishaweka bayana kwamba ukiacha habari za rapta pia kwa sehemu kubwa nitaelezea masuala yanayohusu cocaine hydrochloride.

Nadhani kwa episodes za mbele hutoona habari yoyote inayohusu cocaine, hapa tulipo hatujafika ata nusu ya simulizi hivyo basi ni sehemu pekee utayoweza kuziona habari zinazohusu cocaine.

Huko mbele tutacheza na bahari, fukwe za pwani ya Africa mashariki pamoja na mali kale zilizoachwa kwenye maeneo husika.
 
Story inapoteza mvuto,yaani mwanzo mwisho madawa simama kwenye point mzee,story kama picha la kihindi unazunguuka inaboa mno
 
Kwa siku ile naweza kukili kuwa hatukuzungumza chochote kuhusu mji wa kale wa rapta na hii ilitokana na mimi mwenyewe baada ya kuleta stories za methylphenidate.

Hivyo basi tulitumia mda mrefu sana katika kueleweshana ni namna gani dawa hiyo hufanya kazi lakini pia namna gani dawa hiyo inavyotumiwa bila kusahau outcomes zake baada ya matumizi.

Mimi binafsi niliondoka hapo na assignment moja kichwani kwangu, nilitakiwa kujua ni kwanini fatemeh anatumia dawa hizo za methylphenidate na kama kweli anatumia ina maana na yeye anashida hiyo ya ADHD.

Je! Wakati tupo haullaga alikua anatumia dozi hiyo au ilikuaje.

Kwakua tayari nilishakubaliana na shahzad kuhusu kwenda nae eneo analotakiwa kwenda siku hiyo, shahzad alisema sikuhiyo alitakiwa kuhudhuria clinic ya moyo na ni kawaida yake kila unapofika muda huo kuhudhuria uko.

Mara nyingi shahzad akiwa anatoka basi anatoka na mjukuu wake kwani ndiye alikua nae karibu mda mwingi sana.

Dereva alikuja na tukiwa watatu tuliingia kwenye gari kuelekea maeneo yaliyokua na clinic ambayo shahzad anahudhuria.

Clinic ile ilikua inaitwa Arrhythmia Clinic na tulipofika tu pale shahzad alimtafuta daktari wake ambae ndio humtibu mara zote. Dr Saeed ndio jina la daktari huyo ambae mara zote anafuatilia kwa karibu matibabu ya mkongwe huyu.

Tukiwa eneo la wazi kwenye viti ambavyo wagonjwa na waliowasindikiza wagonjwa hukaa nilivunja ukimya kwa mjukuu wa shahzad ambae alikua anazungumza kingereza pia ukiacha ile lugha yao ambayo sikua na mpango wa kuijua kabisa.

Kwa muonekano tu ni kwamba dogo alikua talkative sana lakini kuna namna alikua ananiogopa hivyo hakuwa akinesemesha kabisa.

Kitu cha kwanza kabisa nilimuuliza kama anasoma na akajibu yupo college, wenzetu bwana yaani mtu ana umri mdogo lakini kwenye masuala ya shule unakuta amepiga hatua nyingi sana.

Kwa umri wa mjukuu wa shahzad kibongobongo angetakiwa kuwa kama sio form two basi form three lakini kwa kule kwao eti tayari mtu yupo college ni jambo la kufurahisha sana.

Wakati naendelea kupiga stories na mjukuu yule wa shahzad nyuma yangu alikuja mtu na kukaa karibu yetu japo sio karibu sana lakini mtu yule nilijaribu kumfananisha na Mohamed yule mlinzi kwenye lile jengo lenye apartments anazoishi fatemeh.

Lakini niliamini hawezi kuwa yeye itakua nimemfananisha tena ukilinganisha na muda niliokutana nae siku ile ilikua usiku sana hivyo kuna uwezekano mkubwa asiwe yeye.

Apa sasa ndio niligundua kama dogo yule mjukuu wa shahzad alikua muongeaji yaani alikua anaongea yeye tu.

Ni kama alikua anasubiri nilianzishe, kwani muda wote alikua kimya lakini baada ya mimi kumuuliza tu kuhusu shule basi yalikuja majibu mengi na ya ziada pia.

Baada ya takribani dakika 40 mzee wetu shahzad alitoka kwa daktari na hapo alisema tuelekee msikitini kwanza kisha mizunguko mingine itafuata.

Kwa sasa nilikua tayari nimeanza kuwa vizuri kwenye sarah kwani nilikua na uwezo wa kufanya kila kitu bila kutazamia kwa yeyote. Kilichokua kinanishinda ilikua ni kutamka maneno yale ya kiarabu pekee.

Uzuri pekee wa mji wa Tehran ni kwamba misikiti haipo mbali sana yaani karibia kwenye kila mtaa kuna msikiti na una jaa.

Kama kawaida yangu nikiingia msikitini huwa natafuta safu au mstari wa nyuma kabisa kwani au backbench kama ilivyozoeleka mashuleni. Sababu ya kukaa mstari wa nyuma ni kujiepusha mambo madogo madogo kama vile kuambiwa usome dua na mambo mengine ya kufanana na hayo.
Sasa nikiwa bado nipo kwenye mkao wa sala, kuna ule mkao wa kukalia miguu mara nyingi tunawaona sana watoto wa madrasa wakipenda sana kukaa pozi hilo.

Chini ya miguu yangu niliona karatasi ndogo ya rangi ya njano yaani karatasi ile ilikaa katikati ya miguu yangu. Baada ya kumaliza sarah niliichukua na kuingalia kwani wakati nafika hapo haikuwepo eneo lile.

Watu walikua tayar wameanza kutoka msikitini muda huo karatasi ilikua na maandishi lakini baada ya kuichunguza maandishi yale yalikua ni ya kingereza.

Japo muandishi alionekana ni mzoefu wa kuandika lugha kama kiarabu hivi na niligundua hilo kupitia herufi zake mbaya za kiingereza ni wazi hakua mzoefu kuandika alphabet za kingereza.
Ludovic, keep listening to tara sikujua muandishi ni nani! Na hayo ndiyo maandishi niliyoyakuta kwenye karatasi hiyo.

Baada ya kuona jina langu nilijua moja kwa moja karatasi ile ilikua pale kwa niaba yangu na sio mtu mwingine.

Sasa Ludovic ndio mimi mwenyewe ila huyu Tara sikuwahi kumjua wala kumsikia hapo kabla. Mjukuu wa shahzad alinikuta bado nikiwa na karatasi ile na akaichukua kwani alishaanza kunizoea na aliona ana nimudu tayari kwa dakika zile chache tulizokaa pale.

Dogo aliuliza Ludovic ni nani baada ya kusoma karatasi ile na mimi nilimjibu simjui kwani karatasi hiyo niliikuta pale pale chini.



Sasa tukiwa nje bwana niliona ile gari yetu ambayo Mara nyingi ndio ilikua inatubeba mimi na fatemeh ilikua imeegeshwa maeneo ya parking ya msikiti.

Apo nilijua tu gari ile ipo pale kwa ajili yangu hivyo ile safari tena ambayo shahzad aliniambia kuna watu wanaweza kua na msaada kwenye jambo letu niliona kabisa haiwezi kuwepo tena.

Nilichofanya ni kumwambia shahzad kuwa nimepata dharula na natakiwa kwenda nyumbani kwani gari iliyokuwa mbele yetu ilikua pale kwa ajili yangu.

Shahzad alijibu kuwa aina shida tuonane siku inayofuata kwani yeye bado anaendelea na mizunguko yake ya sikuhiyo.



Baada ya kuikaribia gari mlango ulifunguka na nilipoingia nilimkuta fatemeh kanuna vibaya sana kwani hakuitikia ata Salam yangu.

Gari iliondoka eneo la parking na kuelekea nyumbani lakini wakati wote huo nilijaribu kujichekesha tukiwa njiani lakini wapi fatemeh alikua amevimba na ni wazi alikua anajaribu kuji control mpaka tufike home ndipo aniwashie moto.

Mpaka wakati huo nilishajua kosa langu kubwa nililolifanya kwani alishanionya hapo awali kwamba sitakiwi kwenda popote wala kukutana na yeyeto bila idhini yake.

Bilashaka fatemeh hua anabadilika sana linapokuja swala linalohitaji seriousness, anakua kiumbe mwengine kabisa yaani huwezi jua kama ndio yule kibonde wangu ninaemshika karibu kila sehemu ya mwili wake.
Hii gari ambayo tunatumia mara nyingi mimi na fatemeh huyu dereva wake anatembega mwendo wa hovyo sana. Kwani ukiangalia umbali wa kule tulipokuwepo mpaka kufika nyumbani hapo tungetumia usafiri wa kawaida basi tungetumia mda mrefu sana kufika hapo.

Lakini kwa kutumia gari hiyo ilikua ni kama kugusa tu tayari tumeliona jengo lile ambalo lilikua na apartments tuliyokua tunaishi mimi na fatemeh kwa muda huo.

Muda wote huo fatemeh hakuwa amenisemesha kabisa mpaka Tunaingia kwenye lifti na kisha tunafika floor ambayo ndio ilikua sehemu tunayoishi.

Tuliingia ndani moja kwa moja, na baada tu ya kuingia ndani fatemeh alifunga mlango huku yeye akibaki kasimama pale pale mlangoni wakati huo mi nilielekea kwenye sofa.

FATEMEH: " Ludovic, do you remember the last time you asked me to come here, what did I tell you?

(" Ludovic unakumbuka mara ya mwisho umeniomba kufuatana na mimi uje uku nilikwambia nini")

Lilikua ni swali kutoka kwa fatemeh huku uso ukiwa serious sana yaani serious kupitiliza siku zote alizowahi kuwa serious.

MIMI: You told me not to meet anyone without your permission
( Uliniambia nisikutane na yoyote pasipo idhini yako)

"Unataka nikwambie kwa namna gani ili uamini kama haupo safe, sitaki kushuhudia kifo chako ukiwa huku ni bora ukafie kwenu ukifa huku mimi nakupeleka wapi."

Ulikua unamlalamikia Javier ana maneno ya kibaguzi lakini kiukweli wewe mwenyewe ndie anaesababisha maneno hayo.

Unafikiri mimi nakufikiriaje kama nimeshakwisha kukupa maelekezo na wewe bado unaenda kinyume.

Nilimuonea huruma fatemeh kwani alikua anaongea kwa hasira sana na kwa Wakati mmoja akijaribu kupishana au kudhibiti mihemko aliyokua nayo wakati huo.

Ni sawa na kusema ni kama kulikua na nafsi mbili kwenye mwili wa fatemeh kwani alionekana kabisa kuna nafsi nyingine anayoshindana nayo ipo ndani yake ambayo ilikua na maamuzi mabaya juu yangu.

Baada ya fatemeh kuona kama anashindwa kabisa kudhibiti kile kilichopo ndani yake aliamua kuondoka akaelekea chumbani kwake.

Binafsi niliona si busara kuendelea kukaa kimya ilihali tayari nimemkosea mtu ambae ni rafiki mzuri na ana ni treat vizuri toka nimeanza kuishi nae.

Hivyo niliamua kwenda kwenda chumbani kwake kwa lengo la kuomba msamaha kwa yale yaliyotokea siku hiyo huku nikijaribu kuwaza kwamba haitakiwi jambo lile kujirudia tena.
 
Niliingia ndani ya chumba ambacho fatemeh alikua analala na nilimkuta yupo bize sana kwenye tarakirishi yake. Yaani huwezi jua kama ndio yule aliyekua ananiwakia dakika chache zilizopita kwa jinsi alivyokua apo.

Ubize huo wa fatemeh uliambatana na lugha ya ki mandarin aliyoiongea utafikiri ni mzawa kabisa kwenye lugha hiyo.

Kwa wasiojua mandarin ni lugha inayozungumza na watu wenye asili ya uchina na ni lugha ya pili kwa kuzungumzwa na watu wengi duniani baada ya lugha ya kingereza.

Inaaminika mpaka sasa ulimwenguni lugha ya mandarin inazungumzwa na watu takribani 1.1 billion ( watu zaidi billion moja nukta moja).

Wakati huo lugha ya kingereza ikizungumzwa na watu wapatao au zaidi ya watu billion 1.4+ duniani kote mpaka hivi sasa.

Mpaka wakati huo tangu nianze kukaa na fatemeh nimemshuhudia akizungumza lugha nyingi sana na karibua lugha zote kubwa Duniani alizizungumza vizuri sana.

Uwezo mkubwa wa kuzungumzwa lugha zinazozungumzwa na watu wengi duniani ni moja ya kigezo kikubwa kinachomfanya mtu kuwa jasusi kokote kule duniani.

Mfano tu huwezi kuwa jasusi wa idara ya usalama wa taifa TISS na ukaenda kutengeneza spy ring huko Burundi na usijue kuzungumza kifaransa. Hivyo ni moja ya sifa ya wafanyakazi wa idara hizi za inteligensia kujua lugha kubwa za duniani kote.

Kwakua nchi inakua kisiasa na kidiplomasia kilasiku bila kusahau muingiliano na mataifa mengine basi kuna haja ya kuwa na watu au na maafisa wanaozungumza lugha nyingi kubwa Duniani.

Na hiki kinatakiwa kuwa kama kigezo namba moja wakati wa ku recruit vijana wa kazi ukiachana na vigezo vingine ambavyo hutumika kwenye huu ulimwengu wa kisasa wa kiinteligensia.

Nasema ulimwengu wa kisasa kwakua hapo zamani kama nchi tulijikita kwenye traditional procedures za kudahili vijana kwenye idara hizi nyeti. Yaani idara ilikalia kuangalia vijana kutoka kwenye makambi ya jeshi polisi na vyuoni.

Lakini dunia ilipofikia sasa kulingana na level ya technology kuna mambo mengi ambayo yanataka utashi wa TEHAMA ilikua jasusi au shushushu wa viwango vya kisasa.
Tuachane na zile nadharia za kwamba ili uwe afisa wa idara hiyo basi uwe unatokea chama fulani au familia fulani. hapana!!! kwa ulimwengu huu wa kisasa tunatakiwa kuangalia uzalendo wa mtu na sio politics za mtu.

Vigezo vya afisa wa kisasa sio connection tena kama ilivyokua hapo awali bali wenzetu wanaangalia exposure aliyonayo mtu, wanaangalia uwezo wa kiakili ( intelligence) pamoja na uzalendo bila kusahau uwezo wake kwenye technology za mawasiliano.

Ebu tuhame uku turudi zetu kwa fatemeh, hua najitahidi sana nisiguse maeneo ya huku lakini najikuta nimefika tu from no where.

Sasa basi fatemeh alikua anazungumza lugha nyingi sana zikiwemo lugha zile za mandarin, kiingereza, kifaransa, kihispania, kiarabu, kirusi na lugha hizi ni zile alizozingumza kwa ufasaha bila kusuasua.
Binafsi niliuona ni uwezo wa ajabu alionao mwanadada huyo wa kuzungumza lugha zote hizo huku mzee baba nikizungumza lugha tatu tu ambazo ni kichaga, kiswahili na kiingereza cha PCM.

Napenda kusema au kutumia neno kingereza cha PCM nadhani wote tunakijua kingereza cha PCM jinsi kilivyo. Ni kingereza fulani hivi hakina mambo mengi, habari za grammar sahau kabisa na terminology nyingi ni za ki fizikia, hesabu na chemistry.

Basi bwana nilijisogeza na kukaa kwenye kitanda cha fatemeh yeye akiwa bize kwenye maongezi ambayo sikuweza kuelewa chochote kinachozungumzwa.

Alitumia muda mrefu sana kwenye maongezi yale mpaka pale nilipokuja kustuka ananiambia niende nikalale kwani muda umeenda sana. Ila kiukweli toka nimefika pale Mara nyingi nalala na fatemeh japo sio kwa kudhamiria inatokea tu accidentally na tunalala wote hivyo niliamini ameanza kuzoea kulala na mimi ila alikua mgumu kuliweka wazi jambo hilo.

Nilimueleza fatemeh kwamba kwa siku hiyo sidhani kama nitaweza kupata usingizi pasipo kujua mambo baadhi ambayo nilimuomba anielezee kama hatojali.

Jambo la kwanza nilimuomba anielezee kwanini anatumia dozi ya methylphenidate, kama ni mgonjwa nilihitaji anielezee ugonjwa alionao kwani tunaishi pamoja sasa japo itakua ni muda mfupi ni vyema nikajua baadhi ya changamoto zake.

Nilimueleza au nilimuomba aniambie tu na aachane na slogan yake ya privacy is power don't overshare nime i bold na kuipa rangi hiyo sentence nikimaanisha itafakari kwanza itakusaidia sana baadae.

Sio kila mtu anapaswa kujua kila kitu kuhusu wewe na sio kila mtu anapaswa kujua unapitia nyakati zipi aidha ziwe ni za heri au Shari.

Wanasaikolojia wanasema kuelezea tatizo au changamoto zako kwa mtu zaidi ya mmoja apo hautafuti solution bali unatafuta attention.

So take care broh!!!!!!!

Fatemeh aliniangalia kwa muda kisha akaniuliza nimewahi kuisikia wapi dawa ile mpaka nataka kujua yeye anachangamoto zipi.

Nilimjibu kuwa dawa ile nimeikuta kwa shahzad na alishanieleza kila kitu kuhusu dawa hiyo hivyo nilichotaka kujua ni kwamba yeye anaitumia kwa manufaa gani je! Ni mgonjwa au kuna matumizi mengine yanayohusiana na dawa hiyo.

Kwa mujibu wa fatemeh ni kwamba dawa ile ya methylphenidate ilikua na matumizi rasmi makuu mawili,

Kwanza kabisa methylphenidate ilitumika kutibu tatizo moja kubwa sana linalotambulika kama narcolepsy.

NARCOLEPSY ni ugonjwa unaosababisha mtu kushindwa kujizuia kulala, yaani mtu anakua analala muda wote na sehemu yoyote ile haijalishi ni muda gani na ni sehemu gani.

Wakati kwa kawaida binadamu hupendelea kulala nyakati za usiku basi wagonjwa wa narcolepsy hali kwao ni tofauti kabisa na sisi wengine.

Mara nyingi watu hawa hupotelea usingizini mahali popote pale na hii huwasababishia matatizo mengi sana, imagine ni dereva ukikutana na foleni ya dakika 2 tu basi umepotela usingizi.

Wagonjwa wa narcolepsy watu wengi hudhania ni swala la ulevi au kukesha, hapana huu ni ugnjwa na upo kabisa kama umewahi kukaa na mtu ambaye akitulia kwa dakika mbili anasinzia unaweza kunielewa ninachosema.

Mfano mkubwa wa wagonjwa hawa tunawakuta makazini na mashuleni ambamo tulipita miaka hiyo ya nyuma.

Unakuta mwanafunzi mwenzako karibia kwenye kila somo yeye hulala tu tena mbaya zaidi wengine mpaka paledi wakati wa national anthem (hahaha ahahahahah ahah)
tulikua nae mmoja primary siwezi kumtaja kwa jina jamaa alikua analala sometimes mpaka chooni akienda long-call.

Sasa kwa mujibu wa fatemeh ni kwamba methylphenidate ilitibu au ili tumiwa sana na wale waliokua wanasumbuliwa na ugonjwa huo wa narcolepsy.

Apa niliona kumbe shahzad na yeye hakua anajua mambo mengi kwani hakunieleza chochote kuhusu ugonjwa huo wa narcolepsy.

Fatemeh alisema tatizo lingine linalofanya watu watumie methylphenidate ni lile linalojulikana kama ADHD ( Attention-Deficit Hyperactivity Disorder).

Na alidai yeye mwenyewe alikua anasumbuliwa na tatizo hilo kwa miaka mingi hivyo nikimuona na methylphenidate basi sababu ni tatizo hilo.

Aliongezea tena kwa kusema mara kadhaa anapotumia dozi hiyo mwili hupitia changamoto za hapa na pale ambazo amezizoea pia.
Mfano kutapika, na kichefuchefu joto la mwili kuongezeka pamoja na viungo kuuma. Alidai pia wakati yupo haullaga Catarina alikua anachukulia hali hiyo kama ni arosto na ilipelekea kuwa anapewa cocaine kwa vipindi maalum ili kuithibiti arosto hiyo.

Sababu ya Catarina kuichukulia hali hiyo ni kama arosto ni kwa sababu Catarina hakuwahi kujua kama Manuela au fatemeh kwa sasa kama alikua na tatizo hilo la ADHD.

Kwa maelezo ya fatemeh mara zote alizopewa cocaine alienda kujifungia kwenye jumba lile la wale wanaotumia kufanyia packing ya mzigo pindi unapokamilika.

Fatemeh alifika hapo kwa kujifanya mlaibu wa madawa hayo ili tu kufanikisha misheni yake huku akitumia uzaifu wa Catarina wa kupenda kusagana na wanawake wenzie.
Tunamkumbuka Dan?!!!!!

Dan yule bwana mwenye tattoo mwili mzima mpaka kichwani na muda mwingi alipenda kutafuna majani ya coca.

Basi Dan ndio aliyetumiwa kuhakikisha Manuela au fatemeh anaingia haullaga tena kitengo kile cha maabara. Na hii ilikua ni baada ya majasusi wa MOIS kugundua kuwa Javier alikimbilia huko kama mafichoni.

Manuela alifika hapo haullaga kama muhalifu aliyetokea spain baada ya kukamatwa na kilo 4 za cocaine kwenye begi lake. Baada ya kutoroshwa na maofisa wa nchi hiyo waliona mahala pekee anapoweza kukaa kutokana na hali yake ni haullaga valley.


Basi kwa kumtumia Dan ambae baada alimshirikisha baba yake na Miguel waliingia kwenye mtego huo na kumtambulisha Manuela kama mfanyakazi mwingine ambae atashirikiana na Catarina kwenye maabara hiyo.

Na wakati Manuela au fatemeh anaenda kwenye maabara hiyo tayari alikua na profile yote ya Catarina. Alijua Catarina alikua akifanya kazi na Juan Carlos ila baada Ya kutiwa mbaloni kwa muuza mihadarati huyo Catarina ndipo akatimkia haullaga.

Lengo la MOIS kumtumia fatemeh ilikua ni kuangalia kwa namna gani wanaweza kumfikia Javier, na hivyo basi fatemeh akatolewa Cerro de Pasco alikokua kwenye misheni mama aliyompeleka huko na kisha akapelekwa haullaga kama emergency.

Misheni mama iliyompeleka fatemeh kwenye nchi ya Peru ilikua kitu kinachoitwa INDUSTRIAL ESPIONAGE.
Mataifa makubwa ya ulaya na marekani yamejitahidi sana kuwekeza kwa namna nyingi ndani ya nchi ya Peru kwenye sekta ya viwanda. ( Tutalizungumzia wakati mwingine)

MOIS waliona misheni ya haullaga ni kama misheni ya dharula na hii ilitokana baada ya wao kugundua uwepo wa Javier na washirika wake kwenye mashamba hayo.

Wakati fatemeh au manuela anafika hapo mtihani wa kwanza ulikua ni kum win Catarina na jambo hili halikua gumu kabisa kwani alitumia siku chache sana kumteka kimapenzi mwanadada huyo.

Mtihani wa pili na mgumu ulikua ni kuhakikisha anatengeneza ukaribu na Javier kwa namna yoyote bila Javier kumjua yeye ni nani na anatokea wapi.


Kwani javier angejua kuwa Manuela mi mtu wa Iran lazima ingempa ukakasi na angetaka kumchunguza vizuri mwanadada huyo.

Hivyo Manuela kwa ufanisi mkubwa alifanikiwa kuuficha utamaduni wake wa asili wa Iran tena ukilinganisha na uraia pacha wa Javier ilikua ngumu kumgundua Manuel kama alitokea Iran.

Baada ya Manuela kufanikiwa kumteka Catarina aliyefuata apo alitakiwa kuwa Javier na huu ndio ulikua mtihani mgumu. Kwani kama mbinu zote zingeshindikana basi mwisho kabisa alitakiwa atumie kitu kinachitwa HONEY TRAP.

Honey trap jina lingine huitwa sexpionage au Honeypot, kama una demu ambaye ni spy basi kwenye hii mbinu mademu wengi ambao ni ma spy huliwa tunda kimasihala.

Na hulazimika kufanya hivyo ili tu kupata taarifa walizokusudia kuzipata, ni mbinu anayotumiwa sana au mara nyingi na majasusi wa KGB baadae tutaingalia KGB kwa uchache.

Lakini pia tutaangalia hiyo mbinu ya sexpionage kwa uchache hapo baadae.
 
Back
Top Bottom