Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Jamaa anakera sana, hata huku whatsup hadi leo hii bado hajamaliza. INaweza kupita hata wiki asitumie episode yoyote.Acha na nayo hatuitaki tena
mwamba kawapiga na kitu kizitoJamaa anakera sana, hata huku whatsup hadi leo hii bado hajamaliza. INaweza kupita hata wiki asitumie episode yoyote.
Kumbe ndio zake eeeh? Yaani mnalipa bado anajiskia anapotaka kuweka?Jamaa anakera sana, hata huku whatsup hadi leo hii bado hajamaliza. INaweza kupita hata wiki asitumie episode yoyote.
Leo nakomea hapaSEHEMU YA 04
Ras alikua anatumia nguvu kubwa kunishawishi kitu kilichofanya niamini kuna namna yeye atanufaika baada ya Mimi kuungana na McKenzie kwenye safari hiyo. Kwa maelezo ya Ras, kazi nitakayoenda kuifanya huko itakua ni kazi ya mkataba. hivyo nikiamaliza mkataba nitaweza kuludi tena bongo kuendelea na maisha yangu. Kwa Mara ya kwanza Ras aliniita jina langu MASSAWE huku akisisitiza kwamba nikiludi nitapata mrembo mwingine tena mzuri zaidi ya Merry kwani aliamini nilikua nampenda sana Merry.
Kutokana na ukweli kwamba toka nifike dar es salaam nilikua namtegemea Ras Kwa kila kitu sikuona haja ya kukataa kwani endapo ningemkatalia kuna uwezekano mkubwa asingeendelea kufanya shughuli zake na Mimi.
Kichwani nilikua najiambia kwamba nikiludi nitakuja kumfanyia mambo makubwa sana baba yangu na mama yangu. Mpaka wakati huo sikua na mawasiliano yoyote na familia yangu na sikua najua kama wananitafuta au wanaamini bado nipo shule. Maisha yangu yote yakusoma sikuwahi kutembelewa na mzazi ata siku moja nikiwa boarding school, hivyo niliamini mzee massawe hana taarifa yoyote kunihusu Mimi.
Nilimwambia Ras kama nipo tayari kwa safari lakini kwa sharti moja, endapo kuna baya lolote litanipata basi aitafute familia yangu. Nilimpa full physical address ya kuweza kumfikisha nyumbani Incase likitokea jambo lolote ambalo litahusu familia yangu.
Kiukweli ilikua ni safari ya nje ya nchi ambayo sikuifurahia wala sikuitarajia nilishangaa furaha aliyokua nayo Ras. Jioni ya siku hiyo tulitoka na kuelekea maeneo ya sinza ambako tulikula na kunywa, baadae tulielekea mitaa ya posta baada ya kukutana na wasichana wawili miongoni mwa wale ambao walikuwepo jana yake kwenye ile Houseparty kule kijichi.
Nililetewa yuleyule ambae alinipitisha rough road jana yake nilitamani kumkataa lakini ilionekana Ras aliongea nao mapema hivyo walijiandaa kwa ajili yetu.
Ugeni wa jiji ulinifanya niisiijue sehemu hiyo ni wapi zaidi ya kukalili kwamba tulikua posta lakini ilikua ni casino.
Ndani tulimkuta McKenzie nilianza kuhisi uwepo wake maeneo ya karibu kutokana na kaharufu ka cologne, baada ya kutulia na kumwangalia vizuri niligundua McKenzie ni zaidi ya baharia. Ras aliniambia hawa jamaa meli yao inapotia nanga bandarini hua wanapewa vibali vya dharula na wanatoka kufanya mambo yao ikiwepo shopping za misosi kama wana shortage ya chakula especially matunda.
Lakini pia kuna services kama kutoa uchafu wa vyakula na uchafu mwingine sio hilo tu pia wanafanya usafi kwenye vyumba vya engine na mengine mengi. Shipping agents ndio wanaratibu kila kitu na shughuli zote hizi hufanywa wakati meli inaendelea kupakua na kupakia container.
Wakati huu McKenzie alinipokea kwa furaha sana na hii ilionyesha tayar alikwisha wasiliana na Ras kuhusu maamuzi yangu. Baada ya kusalimiana na McKenzie nilitambulishwa kwa bwana mmoja mwenye asili ya kiarabu aliyekua amevaa suti aliyomkaa vizuri sana. Bwana huyu alijitambulisha kwa jina la ally, alikua mnene kiasi lakini sio muongeaji kabisa.
Kwa maelezo ya McKenzie, Ally ndio atahusika moja kwa moja na safari yangu. kwani kuanzia mchana wa siku hiyo alikua ananiandalia document zote na vibali muhimu kwa ajili ya safari yangu. Huyu Ally alionekana kuwa na connection kubwa sana lakini pia alikua na kiswahili safi kimenyooka vizuri.
Tulibadilishana namba za simu huku bwana Ally akisema kesho atanitafuta mapema kwa ajili ya maelekezo ya ziada kwenye safari yangu. Kisha ally na Ras waliondoka huku Ras akisisitiza kama hatoludi basi nisijali yule binti niliyekua naye atafanya mpango tutaludi home. Wakati huu Ras alinipa kadi ya bank kwa ajili ya shopping nikiwa nahisi kuna kitu cha kununua ili nijiandae na safari.
Kiukweli sikufurahia kuendelea kukaa pale casino kwani nilijiona watofauti sana na wale waliokuwepo pale hivyo nilimwambia binti tuondoke tuelekee sehemu ambayo nitapata maduka nifanye manunuzi.
Tulitoka posta kuelekea sehemu moja inaitwa morroco kisha tulikunja kulia na kupark sehemu inaitwa shoppers plaza. Binti aliniambia hapo naweza nanunua chochote hivyo tunaweza shuka, yeye alielekea juu akaingia duka limeandikwa touch SPA akaniacha pale nje nikitafakari nianzie wapi.
Sikuingia tena shopping zaidi niliamua kutoka nje kabisa ili kunyoosha miguu kwani nimetumia usafiri wa gari kwa siku nyingi mfululizo. Wakati natembea tembea mitaa ile niliskia mziki kwa mbali kidogo, siunajua watoto wa chuga kwa hip-hop kuna namna nilivutiwa na huo mziki.
Nilisogea mpaka kwenye geti moja na baada ya kuuliza niliambiwa hapo ni msasani club na humo ndani hua kuna shows za watu wanaopenda mziki huo. Nilipoteza mda mwingi eneo hilo kwa kuangalia vijana wakifanya battle na mengine mengi nilifurahi pia kuwaona wasanii kama nikki mbishi, one the incredible na wengine wengi.
Ila kiukweli sikua na amani ya moyo japo nilipoteza mawazo kidogo nikiwa eneo hilo. Niliamua kuludi eneo tulilopark gari ili kumchukua yule binti tuondoke nikapumzike sikuona haja ya kununua chochote. Baada ya kufika eneo lile sikumuona yule binti ikabidi niende lile duka aliloingia, nilikuta akiwa amemaliza huduma zake anajiandaa kuondoka.
Ndani ya lile duka sikuelewa ilikua saloon au kitu gani?? Lakini pia nilikuta mfilipino wa kike akiwa amevalia sare kama mmoja ya watoa huduma ndani ya eneo lile. Walinikaribisha kwa huduma ya massage na huduma nyingine kama kunyolewa nywele sehemu za siri na mengine mengi ila nilihisi wananizingua sikutarajia kama kunaweza kua na huduma ya hivyo kwenye ulimwengu huu.
Tulianza safari ya kuludi kijichi, lakini kutokana na sehemu tuliyokuwepo nilishindwa kutambua kijichi itakua upande gani hivyo yule binti ndie alikua dereva kutokana na uzoefu wake wa jiji.
Tukiwa njiani nilivunja ukimya na kuanza kumuuliza binti baadhi ya maswali kama jina lake na mahali penye anatoka. Anajishughulisha na nini ndani ya jiji hilo.
Alikua anaitwa mage, mwanafunzi ustawi wa jamii, mzaliwa wa dar es salaam na anaishi kimara. Alitabasamu kidogo akasema yeye ni mchaga mwenzangu, alijua mi ni mchaga kutokana na muonekano wangu pamoja na jina.
Ebwana eeeh tulianza kuponda kichaga japo yeye hakua vizuri kabisa ila alijitahidi ukilinganisha wa wengine. Ukaribu wetu ndani ya nusu saa uliongezeka mara dufu mpaka tunafika home tulikua kama wapenzi waliokutana zaidi ya miaka saba iliyopita.
Na usiku huo at least nili enjoy kwani tulipiga show kama wapenzi na sio mtu na mteja wake kama ilivyokua hapo awali.
Asubuhi simu ya kwanza ilikua ni ya ally akinielekeza niende kurasini kuchukua baadhi ya documents zilizokwisha kamilika. Na kwa maelezo ya ally ni kwamba jina ninalotumia kuanzia siku hiyo ni MUSTAPHA ABDUL-QADR MAKUNGU. Hivyo yoyote nitakae kutana nae nimwambie naitwa mustapha na maelezo mengine nitapewa baadae.
Nilimueleza mage kila kitu kuhusu wapi natakiwa kwenda Wakati huo lakini pia nilimueleza majina yangu mapya. Alicheka sana na akawa wakwanza kuniita mustapha, tulienda kurasini nikachukua document zote kisha tukaelekea mwenge kwenye ghetto la mage.
Nilishinda uko siku nzima, nilikula chakula kizuri na tuliongea mambo mengi sana na mage lakini kubwa ilikua ni kumsisitiza kama hana sababu ya msingi ya kufanya shughuli za umalaya aache mara moja.
Ras na mage ndio walinisindikiza siku ya safari yangu mpaka airport huku Ras akitumia uzoefu wake kwenye baadhi ya mambo. mfano kwenye kukaguliwa nyaraka sikua naelewa chochote ila yeye ndio alikua mbele kuhakikisha hakuna sehemu na kwama. Nilijikuta namkumbuka sana mama yangu, nilijiona ni mzambi na msaliti kwa wazazi wangu lakini sikua na namna zaidi ya kuongoza kwenye eneo la kusubiria ndege.
Alituchukua kama masaa matano (5) na dakika 27 kwa Emirates airlines kufika Dubai................
TUKUTANE BAADAE
.Tuliimaliza siku nzima tukiwa ndani ya maabara ile huku Catarina ambaye anaonekana kua ndio supervisor wa maabara hiyo alisisitiza kua nitakua bora kumzidi Javier. Alidai Javier ni mvivu sana, yupo makini kwenye misosi kuliko chochote.
Javier alikua akitabasamu kwa muda wote ambao Catarina akimsema, kwa maelezo ya Catarina ni kwamba Javier alikua mvivu sana linapokuja swala la kazi lakini alikua punctual sana wakati wa misosi.
Catarina alitumia muda huo kunionyesha sample za products zinazotolewa kwenye maabara hiyo. Kwenye ile meza kubwa kulikua na chombo ambacho ndani yake kulikua na sample kadhaa zimehifadhiwa.
Kwa maelezo ya Catarina, ni kwamba kwenye maabara hiyo wanatoa cocaine katika namna mbili tofauti tofauti ambazo ni:- cocaine hydrochloride na crack,
Cocaine hydrochloride ambayo ipo katika namnaa Fulani kama unga mweupe na matumizi yake yapo ya aina nyingi lakini njia pendwa ni kupitia injection (sindano) na snorting.
Crack hii ni namna nyingine ya mzigo unaozalishwa ndani ya maabara hii. Kwa muonekano inafanana na mapande ya chumvi ya mawe inapokua maabara, kawaida Ndani yake kuna mchanganyiko wa hydrochloride, ammonia au baking soda na maji.
Namna ya matumizi mara nyingi huvutwa kama kawaida. Huvutwa kwa kuchanganya na either bangi au sigara, mara nyingi huuzwa ikiwa kwenye solid state kisha mtumiaji anaenda kuisaga yeye mwenyewe kwa matumizi.
Sasa kulingana na wataalamu wa pharmacology cocaine hydrochloride na crack zote ni kitu kimoja ila kulingana na maabara hii kuna namna zimetenganishwa kama sample tofauti tofauti.
Kwenye zile sample zilipangwa kwa namna ya viwango vya quality lakini pia bei ya product inayozalishwa kwenye maabara hiyo.
Apa kwenye quality na bei hua tunaangalia ingredients (viungo) na level of purity (kiwango cha usafi) mzigo ukiwa na makapi mengi hupungua thamani pia.
Sasa kinacholeta makapi ni zile ingredients mfano nitroglycerin (gun powder) ambayo huwekwa kwa wingi kwenye Brown cocaine au Brown sugar kama wanavyoita watoto wa mjini, kiwango cha madhara kwa mtumiaji hutegemea na hizi ingredients pia.
Product ya kwanza iliitwa FISH SCALE COCAINE, hii ni pure cocaine ambayo purity level (viwango vya usafi) ni zaidi ya 90% yaani hakuna impurities kabisa kwenye mzigo huu na hii ndio cocaine ghali zaidi kwenye maabara hii. It is more powerful more expensive and harder to obtain hii yenyewe inang'aa sana kwa muonekano.
Product ya pili ilikua ni BROWN COCAINE ambayo ilikua ni mchanganyiko wa cocaine, amphetamine na nitroglycerin (gunpowder). Huu ni mchanganyo hatari zaidi kwani unaweza kupelekea mtumia kupatwa na madhara kama heart attack au stroke. Ile rangi wa Brown husababishwa na kuwepo kwa gunpowder kwenye mchanganyo huo.
Product ya tatu kuzalishwa kwenye maabara ile kulingana na maelezo ya Catarina ilikua ni CRACK COCAINES, hii kama nilivyoielezea hapo awali kama inafanana na crystals sometimes kama chumvi ya mawe.
Hii ndio low purity form of cocaine ( ina makapi mengi) viwango vya usafi ni sifuri kabisa kwani ndani yake kuna baking soda, maji na uchafu mwingine mwingi. Kawaida inakua na muonekano wa njano au brown inasemekana kua more addictive ukilinganisha na nyingine.
Catarina alinifundisha mambo mengi sikuile mwisho wa siku kichwa kilichoka sana kwani baada ya kugundua uwezo wangu alitaka tumalize ile orientation ndani ya siku moja.
Wakati naendelea na Catarina, Javier na Manuela walikua bize kusafisha baadhi ya apparatus kwani ilionekana siku inayofata kutakua na kazi kubwa. Nilichogundua kufanya kazi ndani ya ile maabara nilitakiwa nishukuru sana kwani hakukua na majukumu mazito ukilinganisha na wale wa mashambani.
Ila kuwepo maabara tatizo ni moja tu, kuwa teja ni kugusa hivyo nilidhamiria kuongea vizuri na Javier ili anielekeze ni kwa namna gani amefanikiwa katika hilo.
Tulitoka nje na Catarina kwa dhumuni la kunionyesha mazingira mengine ya nje ya jengo hilo la maabara. Nje hakukua na vitu vingi saaana zaidi ya sewage systems ambayo zilijengwa kwa mtindo wa kisasa zikitiririsha maji kwenye bonde hilo kuelekea mto haullaga.
Upande wa pili kuvuka sewage systems kulikua na jengo lingie refu lakini halikufikia lile la maabara kwa ukubwa. Jengo lile lilitumiwa kwa ajili ya packing ya mzigo uliokua tayari kusafirishwa, ni jengo ambalo lilikua na mfumo madhubuti wa umeme na hii ilimaanisha watu wa packing wakija hufanya kazi 24 hours.
Mazingira ya nje yalikua mazuri mno na nilivutiwa na kijani kibichi iliyotawalaa maeneo ya kuzunguka bonde lile. Kulikua na hewa safi na ya asili hakikaka taratibu nilijikuta nasahau dhiki za ile safari ya kufika hapo.
Nilimueleza Catarina hisia zangu juu ya uoto ule wa asili na hali ya hewa ya eneo lile. Catarina alitabasamu kwa muda kisha akaniambia kuwa miaka 10 nyuma eneo hilo lilikua bora kuliko hivi sasa.
Kwa maelezo ya Catarina ni kwamba maeneo ya kuzunguka bonde hilo kumekua na shughuli nyingi zinazopelekea (deforestation) ukataji wa miti. Hivyo hali ya hewa inabadilika taratibu sana tofauti na ilivyokua miaka ya nyuma. Aliendelea kusema kwamba wao ni miongoni mwa watu wanaopambana sana kuhakikisha mazingira ya eneo hilo yanatunzwa kwani wakulima wadogo wadogo ndio hufanya shughuli zao kienyeji bila kujali mazingira.
Kwa kuendelea kuchafua mazingira na kukata miti hovyo kungepelekea serikali ya Peru ku draw attention kwenye ukanda huo hivyo shughuli zao zingekua ngumu kuendelea.
Ilionekana wazi kuna viongozi wakubwa wa Peru na Bolivia wanajua au wanahusika na mashamba hayo ambayo yapo huko haullaga.
Nilimuuliza Catarina kuhusu soko la products zinazotolewa pale, bila kuchelewa alijibu kuwa wao hawahusiki kabisa na mambo ya soko kwani tayari kuna watu wa marketing ambao ndio wanajua kilakitu kuhusu soko.
Kikubwa anachojua yeye soko lao ni America ya kaskazini na ulaya na Asia wa uchache. Lakini pia alinionya kuendelea kuuliza maswali hovyo kama nitafanya hivyo kumuuliza kila mtu au kutaka kujua kila kitu kwa haraka naweza kuingia kwenye matatizo.
Bila shaka nilimuelewa Catarina anamaanisha nini, wakati wote huo nikiwa na Catarina alikua bize na sigara kwa kweli alikua mvutaji mkubwa. Nilihisi bado nahitaji kujua mengi kuhusu Catarina na Manuela nilikua kila nikimuangalia Catarina kuna kitu kinaniambia nahitaji kuendelea kuwa karibu zaid.
Sikuona haja ya kuendelea na maswali mengi zaidi kwani ata yeye alishanionya juu ya kuuliza maswali, ata hivyo kuuliza uliza maswali mengi haikua desturi yangu ila kuna muda nilitakiwa kufanya hivyo kutokana na ugeni wa mazingira hayo.
Baada ya muda alikuja bwana Javier akiwa na Manuela ambao wote kwa pamoja tuliungana kwenye meza moja iliyokua nje ya mazingira hayo na kuendelea na soga.
Wakati tunaendelea na stories, nilijiuliza ukiwa hapo mishahara tunalipwaje? Na matumizi tunafanyaje? Lakini baada ya kukumbuka onyo ya Catarina sikuona haja ya kuuliza hivyo nilitunza maswali yangu yote.
Niliamini Javier ndie mnyonge wangu ambae atajibu maswali yangu yote hapo baadae.
Nilijikuta nimekua na amani sana baada ya kuungana na kampani hiyo mpya kwenye maisha yangu. Javier alikua ana m-care sana Manuela ambaye mara zote nilipomuangalia usoni sura yake ilionekana wazi kama imebeba mengi mno.
Manuela alikua dhaifu mno kutokana na hali yake ya uteja, hauweza kufanya kazi yoyote ile iliyotumia nguvu hivyo Javier alipenda kuwa nae karibu na wanashirikiana mambo mengi.
Kwa haraka niligundua Catarina alikua na control kubwa kwenye maisha ya Manuela kwani yeye ndio aliamua ni muda gani wa Manuela wa sniff (kunusa cocaine) na ni kiasi gani ampe.
Kitendo cha Manuela kuwepo maabara pale ndio kilimpa favor ya kutumia high purity and expensive cocaine. Lakini kama angetumia aina nyingine ambazo zinakua contaminated kwa kiasi kikubwa asinge kua pale mpaka muda huo kwani alitumia kwa kiasi kikubwa sana.
Tukiwa pale tunaendelea na mazungumzo, niligundua kitu tofauti kutoka kwa Manuela kwani alikua kimya sana.
Alianza kutapika mfululizo huku akiwa anatokwa jasho jingi mno kiasi kwamba t-shirt yake yote ililowa. Aliporudi tulipokua tumeketi alionekana kutetemeka especially Upande wa mikono yote ilikua inatetemeka.
Catarina alinyanyuka na kuelekea Upande wa pili wa maabara hiyo na kuingia kwenye kamsitu kadogo jirani na maabara ile.
Javier alisema kinachomtokea Manuela ni arosto hivyo Catarina alikua anaenda kwenye ghetto lao kwa ajili ya kuchukulia unga ili arudi kwenye equilibrium. Catarina ndio alikua anajua dozi ya rafiki ake huyo na alifanya hivyo kwani angempa uhuru wa kutumia anavyotaka ingekua hatari.
Ingekua hatari sana kwakua upatikanaji wa dawa hizo kwa eneo hilo ulikua mrahisi sana hivyo ingeweza kumpelekea overdose na mpaka kufa.
Mabinti hawa wawili walikua wanaishi nyumba moja ambayo ilikua karibu kabisa na maabara hiyo pembezoni mwa mto. Nyumba ile ilijengwa kwa mbao lakini hii ya kwao ilikua tofauti na zile za kule kwetu tunapokaa mimi na bwana Javier.
Hii ilikua na viwango vya juu at least ukilinganisha na zote kwenye eneo hilo. Sababu kubwa ya umalidadi wa jengo hilo lililokua linakaliwa na Catarina na mwenzie emanuela, lilikua pia linatumiwa kama stores ya products zote zinazotokea maabara kwa ajili ya kusafirishwa.
Baada ya muda Catarina alirudi akiwa ameshika kitu mkononi na kumpatia Manuela, Manuela alipokea kwa pupa sana na kisha akatokomea upande mwingine kutoka pale tulipokua tumekaa.
Upande alioelekea ni ule upande uliokua na jengo la pili linalotumiwa na baadhi ya watu ambao huletwa apo kwa ajili ya packaging.
Watu wa packing wanakua wapo special na hufika apo baada ya kua maabara imekamilisha tayari mzigo. Na wao huandaa mzigo huo kwa ajili ya kusafirishwa, mara nyingi mzigo huo hupimwa kabla ya packaging na muhusika mkuu apa anakuaga Miguel pamoja na Daniel wao ndio huratibu mchakato huu.
Sababu ya kupimwa mzigo kabla ya packing ni kutafuta uhalisia wa kiwango kilichozalishwa kutoka maabara na mzigo uliosafirishwa kuwafikia watu wa marketing.
Kwa wastani ni kuwa kg 400 za majani ya koka (coca leaves) zinatumika kuzalisha kilo moja (1) ya coca paste na wakati huo huo inaweza kuzalisha kg 0.5 cocaine hydrochloride.
Mara nyingi wanaotumika kupack mzigo baada ya kua umepimwa wanakua ni wadada special ambao wapo kwa ajili ya kazi hiyo. Wadada hao hutokea jiji moja linaitwa Lima na wengine hutokea Arequipa.
Kwa stories za javier ni kwamba hao wadada wanakuaga ni warembo sana kwakua nipo hapo nitawaona siku mzigo ukiwa tayari.
Hivyo basi mara nyingi kama watu hao wa packing hawapo ndipo Manuela hupenda kulitumia eneo hilo tulivu kwa ajili ya shughuli zake za sniffing.
Bwana Javier ni moja ya watu waliofurahia uwezo wangu kwani ilionekana ninaenda kubeba majukumu mengi na kumpunguzia sehemu kubwa ya majukumu yake.
0623329512 Whatsapp
NB: Wanaoisomea kwa whatapp wapo mbele zaidi
(2000 wanalipia kwa simulizi yote)
Mwandish kanuna kisa tumemnyima aftatMwandishi katekwa!!![emoji17]
Siungi mkono kwamba anayetumia bange hawi romantic. Kila mtu na akili zake na hisia zake.Totally I agree with you, hii naisoma tu kama story ya kutunga inayoelimisha kwa sababu imeinclude baadhi ya matukio ya kweli ambayo yapo kwenye historia au hata ukigoogle yapo.
Mwandishi katumia usanii wa matukio hayo kama fursa ya kujipenyeza kwenye matukio yaliyokwisha tokea aonekane naye alikuwepo, Nice artistic trick.
It doesn't make sense ujuane na mtu for less than a week afu akupe connection abroad tena ya drugs, no thank you.
Vipi kama kuna majasusi wa Iran Tz, na wapo mitandao ya kijamii coz lazima jasusi aijue lugha ya sehemu husika, vipi wakikutana na simulizi ya kweli inayowaanika, mpaka dakika hii ushapotezwa kitambo.
(ukweli ni kwamba majasusi wanakutumia tu, mission ikikamilika huwa wanapoteza ushahidi)
Au tuseme mtandao wa Vikrea sijui Tondar, coz mitandao ya kigaidi haipotei huwa ina mute tu siku wanakutana na hii story kitatokea nini, ingekuwa story ni kweli mpaka dakika hii ushageuziwa kibla.
Afu ukisoma sehemu anazosimulia mapenzi au romance utagundua jamaa ni mpenzi wa tamthiliya za kihindi yaani anapita mulemule.
Pia amefeli kutunza uhusika kutoka muhuni mtukutu anayekula bange, mpaka kuwa softboy romantic anayelilia na mwanamke.
Naijua bange nimeivuta nimeacha miaka kadhaa iliyopita, kabla ya hapo nilikuwa mtoto wa mama baada ya kula kijiti nikawakauzu yaani mgumu simaanishi mgomvi, ila hata baada ya kuacha nimebaki kax mgumu vilevile, siamini kama naweza kulilia na mwanamke.... maisha, (kwa waliowahi kuvuta na kuacha hapa watanielewa)
Anyway story tamu hata mi naendelea kusoma, ila kusema ni ukweli BIG NO
Wapi nimetaja neno romantic, mwanaume kulialia ndo unaita romantic labda bwabwaSiungi mkono kwamba anayetumia bange hawi romantic. Kila mtu na akili zake na hisia zake.
Mpaka wiki iishe ndipo ataweka tena😳😳 eeh kumekucha bado tu
@grelishTHE WEALTH OF RAPTA RUINS
(Get Rich or Die Tryin)
Msimuliaji: LUDOVIC MASSAWE
PROLOGUE/DIBAJI
Mji wa rapta ni mji uliozama baharini kisiwani mafia kwa zaidi ya miaka 2000. Unaweza kua mji mgeni Kwa baadhi ya watu, lakini wengi mnaweza kua mmepata kuusikia uwepo wa mji huu wa kale pembezoni mwa pwani ya Africa mashariki. Wapo wanaodai mji huu unapatikana maeneo ya rufiji kwa sasa na wapo wanaodai mji huu unapatikana pembezoni mwa kisiwa cha mafia. Je, ni nani yupo sahihi?
Mji huu ulipata kuwepo mwanzoni mwa karne ya 1 na imepita zaidi ya miaka 1600 mpaka 2000 tangu kuwepo kwa mji huu. Unaaminika kuwa mji wa kwanza tajiri barani Africa na pia ni miongoni mwa miji kumi na tano inayopatikana chini ya maji. ukiacha miji kama vile Thonis-Heracleion na Alexandria iliyopo Egypt, Yonaguni Jima (Japan), Port Royal (Jamaica) Dwarka (India), Pavlopetri iliyopo south-western Greece, Villa Epecuen (Argentina) nk.
Tofauti na ilivyo kwa watanzania na wakazi wa Africa mashariki wakiwemo wana archeologia. Wengi wamechelewa kuzipata habari za mji huu, mimi nilizipata habari hizi nje kabisa ya ukanda huu. Nilizipata habari hizi nikiwa jiji la Tehran uko inchini Iran (uajemi ya kale) ndani ya maktaba ya taifa (National Library of the Islamic Republic of Iran) iliyoanzishwa mwaka 1937 ikiwa na zaidi ya items milion 15 ndani yake.
Wakati nafika Iran nilikua nikitokea nchini Colombia na Peru kwenye mashamba ya koka (coca plantations). kwa wasiojua koka leaf ndio mmea unaotumika kutengeneza madawa ya kulevya aina ya Cocaine kupitia mchakato mrefu. Na ugumu wa ku control uzalishaji wa cocaine unasababishwa au unatokana na kushindwa kuthibiti chemicals zinazotumitumika kwenye mchakato huo kwani ni chemicals za kawaida zinazotumiwa kila siku kwenye matumizi ya binadamu.
Mfano; ku process coca leaf kuwa coca paste mpaka kupata cocaine base na HCI zinatumika chemicals kama, Sulfuric Acid, Sodium Bicarbonate, Sodium Hydroxide, benzene, Potassium Permanganate, Dichromate, Ammonia Hydroxide, Sodium Hydroxide, Methyl Ethyl Ketone na kerosene. Tutajuzana mengi kuhusu cocaine hapo mbele tukiendelea na simulizi.
Sasa basi Niliwezaje kufika Colombia, Peru kisha Iran na miji mingine mikubwa duniani? Niliwezaje kuzisikia habari za mji wa rapta? nani alinipa habari hizi? na mji huu wa rapta una utajiri kiasi gan ndani yake? Nilifikaje rapta na kwa msaada wa technologia gan nilifanikisha zoezi langu? Kipi kilisababisha mji huu kuzama baharini?
Swali lingine la msingi, wageni wa kwanza wa pwani ya Africa mashariki walikua ni warumi na wachina kabla ya waarabu na waajemi, sasa imekuaje details za rapta zilizoandaliwa na warumi zikafika Iran (Persian gulf) zilifikaje huko?
Najua baada ya kutaja wachina wengi mtajiuliza maswali lakini msijali tutaona ushahidi wa uwepo wa wachina ndani ya mji wa rapta. 90% ya wachunguzi wa mji huu wanatumia taarifa za warumi zilizoandaliwa na Claudius Ptolemaeus (Claudio Ptolemy). Je wana fahamu kua details hizo kabla ya kuwafikia zilishatumiwa na waajemi wa kale Na kuna uwezekano taarifa hizo zilichakachuliwa!?
Je! Mzungu bwana Alan Sutton (mzamiaji) aliyegundua kuta za rapta akiwa kwenye helicopter hivi karibuni, ilikua ni bahati mbaya tu au na yeye ni moja ya wale treasure hunters ila hajaliweka hili wazi?
Ungana nami kwenye simulizi hii ya kuvutia ili kupata majibu ya maswali yote na kwa hakika utajifunza mambo mengi ndani yake.
SEHEMU YA 01
Mgomo sengerema secondary
Wakati unajiuliza Niliwezaje kufika Colombia, Peru na kisha Iran unatakiwa kujua safari yangu ya jasho na damu pamoja na misukosuko mingi ilianzia shule ya sekondari ya sengerema nikiwa kidato cha sita. Kwa waliopata kupita shule hii wanaweza kua mashihidi kwa namna shule hii ilivyokua ya kikomando yaan wenyewe tulikua tunaita late-summer boot camp.
Kwa haraka haraka tu ni shule aliyowahi kufundisha hayati magufuli kabla hajawa waziri na kisha raisi. Nadhani umeanza kupata picha ilikua shule ya aina gani, Ni shule ambayo kila mtu alikua jeuri kuanzia headmaster mpaka mpishi wa jikoni. Wakati nikiwa hapo tuliwahi kushuhudia kesi nyingi ngumu na za ajabu kama wanafunzi kukutwa na kombati za jeshi full set. Kuna mengi kuhusu sengerema ambayo hatuyajui nitawaeleza machache tu na ni kwa namna gani safari yangu ilianzia hapo.
Nilifika hapo kwa mbinde huku o'level nikitokea Ngerengere kizuka sekondari baada ya kufukuzwa MAKOKO SEMINARY, kiukweli nilikua mtoto mtukutu na jeuri ilifika hatua mzee wangu mzee MASSAWE alisema hizi tabia nimeridhi kutoka kwa babu yangu. Ambae alikimbia nchi baada ya kuhusika kwenye matukio mawili, lile la utekaji wa ndege ya ATC mwaka 1982 February kwa makusudi ya kushinikiza mwalimu ajiuzulu na lile jaribio la kuangusha serikali ya mwalimu Nyerere la mwaka 1980's. Babu Yangu alikua ni miongoni mwa wale maafisa wakuu waliosuka ule mpango, Tuachane na babu na tuludi zetu sengerema.
Tukio la mgomo ndio lililoanzisha safari yangu Na lilipangwa usiku baada ya mlo wa jioni, vidume baada ya kushiba dona maharage pamoja na nchima boyo akili zikatutuma tufanye mgomo usiku wa siku hiyo. Sababu za mgomo zilikuwepo japokua hazikua na mashiko sana naweza sema ni ujana tu ndio ulikua unatusumbua ukiongeza na zile bangi zakuvutia maporini (chaka).
Kama kawaida mzee baba siku hiyo ya mgomo niliwekwa kitengo cha TANESCO, yani niliambiwa ikifika saa 2 kamili usiku ni hakikishe shule nzima umeme umezima. Hii ilitokana na ujuzi wangu wa mambo ya electronics na wiring za ujanja ujanja za mabwenini especially bweni la kimweri na sokoine.
Basi ilipotimu saa 2 kamili nilihakikisha Giza limetanda shule nzima kasoro nyumba za walimu tu, na kazi yangu iliishia hapo na Majukumu mengine yaliyobaki yalikua kwa wenzangu wahamisishaji kuhakikisha kila mmoja anashiriki. Lakini pia kuna jamaa mmoja wa mwananyamala yeye alikua na dumu la petrol lita 5 sijui alilitolea wapi usiku ule huyu bwana kazi yake ilikua kuhakikisha moto unawaka maeneo yote yaliyopangwa kuchomwa.
Mpaka kufika saa nne usiku stationary ya mwalimu wetu siwezi kumtaja jina ilikua haitamaniki na baadhi ya walimu walikimbiza familia zao mjini. 90% ya wanafunzi tulikua michepuo ya sayansi yani PCM, PCB na combination nyingine hivyo tulikubaliana kutokugusa maabara wala library wala darasa, wachache sana walikua arts na cha ajabu kwenye hii shule watu wa arts walikua wamestaarabika ukilinganisha na sayansi.
Shule imejengwa mlimani kabisa kiasi kwamba ilipofika saa 4 na nusu usiku defender ilionekana ikipandisha na wote tukapotelea maporini. Jambo la kufurahisha ni kwamba askari hawakufanikiwa kukamata ata mwanafunzi mmoja kati ya wanafunzi 800. Wengi waliishia kulala kwenye miembe na majaruba ya mpunga kwa usiku huo kwani shule ilizungukwa na makachero wakutosha. Lakini massawe nikasema siwezi lala juu ya mti Kama tumbili, usiku ule ule nikaanza safari ya kuelekea mjini mitaa ya soko mjinga.
Pale mjini kuna binti alikua anasoma shule ya jilani inaitwa NTUNDURU alikua amepanga ghetto. Can you imagine! Shule ya boarding na bado amepanga mtaani! asee. Merry alikua ni hatari sana mnyaturu yule wa singida.
Mishale ya saa tano usiku nilikua mlangoni kwa merry nabisha hodi, baada ya dikaka 3 alifungua mlango nikaingia. Walikua wawili yeye na mwenzie anaitwa jane. Ndani kulikua na chupa za safari na mzinga mkubwa wa konyagi, nilipoingia nilihisi uwepo wa mwanaume mule ndani na baadae niliona funguo za sun LG na vipisi vya sigara. Ila sikujali sana nilijitupa kitandani nikapitiwa na usingizi mzito uliotokana na uchovu wa mgomo na mbio za kuwakimbia field Force.
Nilikuja kustuka saa kumi alfajiri na mlio wa pikipiki uliokua unamrudisha merry ambae alikuja yupo hoi na kwa haraka niligundua jane amebaki na yule kidume wa jana.
Merry akilewa bia hua zinashuka chini, waliosoma cuba wamenielewa hapa. Hivyo baada ya kuingia ndani hakutaka story zaidi ya kutupa nguo kwenye kila kona ya chumba hicho kama mwehu. Na mimi kutokana na nilikua namjua vizuri haikusumbua kujua anataka nini zaidi ya kuanza mtanange wa kukata na shoka uliochukua zaidi dakika 90 kama finally ya Argentina vs France kule Qatar.
Tulikuja kuamshwa na mwanga mkali wa jua la saa 4 asubuh uliokua unapita dirishani Huku merry akiwaza supu. Ilituchukua muda mfupi kujiandaa kwenda maeneo ya stendi kupata supu, nilishangaa baada ya kufika stendi nilikutana na wanafunzi wenzangu wakiwa na mabegi wengine ma tranka. Nilipowauliza walijibu shule imefungwa kwa muda wa week 3 na tutapewa utaratibu wa jinsi ya kurud tukiwa nyumbani. Hapo nilianza kuwaza namna ya kurud nyumbani huku mizigo yangu yote imebaki shule na hakuna mwanafunzi anaeruhusiwa kwenda tena shule kwa muda huo.
Basi bwana tulipata supu na mrembo merry kisha tukarud zetu ghetto kupumzika, nakumbuka ilikua siku ya alhamisi hivyo merry hakuenda shule kutokana na hangover na tulishinda ndani siku nzima mpaka kesho yake asubuhi.
Siku ya pili akili ilivurugika zaidi baada ya kupata habari kwenye vituo vya habari viwili tofauti kuhusu mgomo wa sengerema, kituo cha kwanza ni redio sengerema ilitangaza wanafunzi kumi na tisa (19) wamefukuzwa na wengine kusimamishwa masomo kwa muda usiojulikana. Hivyo hivyo kwa redio free Africa na gazeti la mwananchi, gazeti hili lilitoa majina ya waliofukuzwa na mimi nilikua jina la kwanza kwenye ile list.
Niliwaza namwambia nini mzee massawe ambae alichoshwa na tabia zangu.
Akili ikanituma kuangalia upande wa pili wa maisha na sio kukomaa na shule, niliamini siku Moja nikiludi home na pesa nyingi mzee massawe atanikubali sana jembe lake.
Baada ya kupata wazo la kutoendelea na shule nikaanza kuwaza natakiwa nianzie wapi kutafuta pesa. Apo apo akili ikaniambia dar ndio sehemu pekee naweza tengeneza pesa nyingi, lakin kwa bahati mbaya sikua mzoefu wa mji huo na wala sikutakiwa kufikia kwa ndugu yoyote na bado sina nauli ya kufika huko. Niliamini nikifika Mwanza kwenda dar itakua rahisi hivyo nikaanza mchakato wa kufika mwanza (nyegezi).
Nilimshirikisha merry kwa makusudi ili anisaidie nauli ya kufika nyegezi kwani kutoka sengerema hadi nyegezi ni kiasi cha shilingi 4000 tu. Na kwa maelezo ya merry aliniomba tufike stendi kuna mtu atampatia tukifika hapo.tukiwa stendi Merry alimfuata jamaa mmoja bonge hivi anadeal na tickets pale stendi, Kwa haraka niligundua huyo ndio sponsor waliekua nae jana. Sikujua waliongea nini na merry ila merry aliniambia tusubiri kuna coaster inatokea katolo ndio tutaenda nayo mwanza.
Haikuchukua muda mrefu ile coaster ilifika na walipanda abiria kadhaa kisha bonge akamwambia konda hawa ndio wadogo zangu wanaoenda nyegezi. na sisi tulipanda tukaanza safari, nilishangazwa na uwepo wa Merry kwenye safari sikujua na yeye anaelekea wapi kwani hakua na sababu ya kutoka sengerema siku hiyo kwani masomo kwa upande wake yalikua yanaendelea. Merry alikua mwanafunzi wa kidato cha nne NTUNDURU sekondari na ile siku tumeshinda ote ndani nilitumia fursa kumfundisha almost topics tatu za msingi.
Sasa tukiwa ndani ya coaster kuelekea nyegezi nilimuuliza kwanini na yeye ameamua kusafiri, majibu yake yalikua ni kwamba ana muda mrefu hajafika mjini mwanza hivyo alitaka kwenda kuosha macho kwa muda kisha baadae ataludi sengerema.
Nilipata nafasi ya kupiga stories na konda ndipo niligundua wametokea geita walipeleka msiba na hapo wanarudi dar es salaam. Niliamini safari yangu kufika Dar es Salaam imerahisishwa nachotakiwa ni kuwaza namna gani naweza kushawishi jamaa ili aniruhusu nisafiri nae.
Majadiliano na konda yalikua hivi.
Konda:"dogo! we ni mwanafunzi Nini? Jana tukiwa na msiba tulibeba madogo kama watatu hivi wakiwa na suruali nyeusi na tishet za bluu kama ulivyovaa wewe"
Merry alijibu fasta kama ameulizwa yeye.
Merry: ndio sisi ni wanafunzi, ila tumerudishwa nyumbani ghafla sababu ya mgomo wa juzi usiku.
(konda hakujua kama sengerema ni shule ya wavulana pekee)
Konda: kama wanafunzi wenyewe ndio nyinyi hiyo shule kazi ipo. Kwaiyo nyumbani ni wapi??
Nilitumia swali hilo kama fursa ya kufanikisha misheni yangu.
Mimi: home dar na hatujatumiwa nauli sijui tunafikaje?
Konda: we mtoto wa kiume jitahidi upambane.
Jibu lile lilinikatisha tamaa ya kuendelea na maongezi yale. Haikuchukua muda tulikua tumefika kivukoni busisi. Abiria wote tulishuka na kupanda kivuko, lakini nilifurahi baada ya kumuona konda anajisogeza kwa merry na kujiongeresha. nilijua kwa ujanja wa merry anaweza kufanikisha safari yangu kirahisi sana.
Baada ya kufika upande wa pili tulirudi ndani ya coaster na kuendelea na safari na wakati huu merry aliniambia ameshampanga konda hivyo tutafika wote dar es salaam.
Merry alikua binti mjanja sana na anamacho Fulani akikuangalia tu unajua atakua fundi, hahahahahaha kwa wale tuliopita sengerema miaka ile najua mtakua mnamkumbuka kwani alikua maarufu sana. Especially tukienda shuleni kwao kwa ajili ya michezo wengi walimtolea macho, nitakuja kueleza nilimpataje hapo baadae.
Baada ya kufika nyegezi tukijiandaa na safari ya kuanza kuitafuta dar es salaam nilishangaa konda aliniita na kunipa buku tano nikatafute msosi. Na kisha konda na merry walipotelea kusiko Julikana, Nilijua merry ameshafanya yake tayar niliishia kuitunza ile buku tano nikiamini itanisaidia mbele ya safari kwani sikua na chochote mfukoni.
Baada ya nusu saa merry na konda walirudi huku nikimuona merry na vifurushi vya kutosha bila shaka ilikua ni misosi na kimoyomoyo nikasema merry hajawahi kuniangusha ata siku moja. Tulikaa kwenye siti na kuendelea na safari Huku tukipiga msosi mzito nakumbuka ilikua ni Sato na chipsi kavu za kutosha.
Mimi: merry ulisema unaishia nyegezi vipi mbona unaendelea na safari?
Merry: sijawahi kufika Dar es Salaam, nadhani hii ni fursa ambayo sitakiwi kuichezea. Najua nipo na wewe hakuna kitachoharibika nitakaa week moja kisha nitarudi shule.
Daaaaah!!!!! Nilihisi mwili unakufa ganzi nilitaman kumwambia Mimi mwenyewe sina pa kufikia ila nikapiga moyo konde. tukaendelea na safari yetu huku stories zikiwa nyingi. Merry pekee ndio alikua na simu Mimi kilichokua mfukoni ni ile buku tano, kibiriti cha gesi na scientific calculator tu.
Baada ya safari ya muda mrefu wote tulipitiwa na usingizi, safari ile ni ya kutwa nzima kwani nakumbuka tuliingia morogoro usiku wa saa tano tena hiyo ilikua ni baada ya abiria kulalamikia speed ya gari ilikua kali mno. Tulipotoka moro baada ya kufika maeneo ya chalinze nilipitiwa tena na usingizi mzito. Nilikuja kushtuliwa na konda akidai alitusahau tumeshaingia mjini mda mrefu.
Konda: nyie mnashukia wapi tumeingia Dar es Salaam tayari. Lile swali lilikua gumu kwangu kwani sikua ata najua tunapoelekea baada ya kufika dar. Kwa Dar es Salaam nachojua ni ubungo tu hivyo nilimjibu tunashuka ubungo.
Konda: ubungo tumepita tayari sisi tunaelekea mbagara, shukeni hapa mrudi vertinary mkapande gari za ubungo.
Kiukweli sikumuelewa konda ata kidogo kila alichonambia kilikua kipya ila sikutaka kuonyesha kutokujua mbele ya Merry hivyo tulishuka. Tulishushwa eneo moja lina mataa na ilikua saa saba na nusu usiku, nikiwa sijui cha kufanya Merry alianza kulalamika maumivu makali ya tumbo. Nilijua tu itakua njaa kwani ni muda mrefu hatujapata chakula, baada ya kupepesa macho huku na kule niliona sehemu kwa mbaali kuna watu na mataa mengi yanawakawaka nikajua fika hapo patakua na bar hivyo hatuwez kosa msosi.
"Massawe hapa na kwenu kuna umbali gani?" Lilikua ni swali la Merry na mimi sikuona haja ya kuendelea kumficha ukweli, nilimueleza kila kitu kama nimeenda huko kutafuta maisha na nimeachana rasmi na masomo baada ya kufukuzwa shule na nilimueleza siwezi kurudi moshi kwa mzee massawe hatonielewa kabisa.
Kwa maumivu ya tumbo aliyokua anapitia Merry hakutaka kuendelea na mjadala nilimuona akiongoza kwenye lile eneo tuliloliona likiwa na watu wengi usiku ule. Baada ya kufika eneo Hilo niliona maandishi makubwa yakiwakawaka yameandikwa SUGAR REY. Ni dhahiri ilikua ni bar, nilishangazwa na mavazi ya wadada wa eneo hilo na sio mimi tu ata merry pia.
"Hhhmmm kweli hii ndio dar es salaam ninayoisikia kila siku" yalikua ni maneno ya Merry. Tukiwa bado tumeduwaa alikuja bodaboda
Bodaboda: vipi mnaenda?
Mimi: hapana tumefika bro.
Bodaboda: punguzeni kushangaa basi.
Tulisogea mpaka eneo lile nikiamini hatuwezi kukosa chakula ukizingatia nilikua bado na lile buku tano la konda.
Tulipofika tu merry alimfuata Binti mmoja aliekua amekaa pembeni akiwa kwenye pozi Kama anamsubiri mtu na waliongea baadae wakafatana sikujua wameenda wapi. Nilijisogeza kwa jamaa wa bodaboda wakiwa na makoti makubwa nikajiunga kupiga nao story huku nikimsubiri Merry.
Mimi: bro samahan hawa wadada mbona wapo wengi na wana mishe gani apa mbona wamevaa kiasala asala?
Bodaboda: hao wanajiuza mjomba. We mgeni nini?
Mimi: ndio mi mgeni.
Bodaboda aliniangalia tu na hakuendelea kuongea chochote Zaidi ya kuwafata abiria wawili waliokua mbele yake. Baada ya muda kidogo hivi nilimuona merry akiludi eneo nililokuwepo.
Mimi: merry punguza kujifanya unamjua kila mtu apa sio singida hii dar rafiki angu.
Merry: lile tumbo lilikua ni la siku zangu na sio njaa kama ulivyohisi hivyo nilienda kwa yule mdada kuona kama ata nipa msaada wowote si unajua sijatembea na chochote. Lakini pia nimemueleza changamoto niliyonayo kwamba hatuna pa kulala na ndio tumefika mjini.
Mimi: akasemaje?
Merry: kasema atanisaidia kwa leo sehemu ya kulala ila kuanzia kesho nitajua pa kwenda, lakini pia amenieleza kama sina ndugu kabisa atanionyesha kazi ya kufanya na tutakua tunachangia wote kulipa pango la nyumba hivyo mi nimeona niende nae tu.
Kiukweli sikutamani merry aondoke na yule dada lakini sikua na jinsi kwani hata hivyo sikua na sehemu yoyote ya kumpeleka. Merry alinikabidhi simu yake ili iwe rahisi kunipata siku inayofuata kwani alikua anajua sikua na simu. Tuliagana na merry na mimi nikabaki eneo hilo nikiwaza naelekea wapi kwa usiku huo wala sikutaka kujutia maamuzi yangu ata kidogo niliamini nipo sahihi kabisa.
Tunaendelea baadae usikae mbali.
View attachment 2583318
@grelish@grelish