Utajiri wa Magofu ya Rapta

Utajiri wa Magofu ya Rapta

Nikiwa kwenye usingizi mzito niliamshwa kwa
Kukanyagwa na safety boots maeneo ya mgongoni. Na safari hii tuliamshwa wote kwa pamoja na kupewa gloves tuvae na Kisha tukashikishwa vile vyuma (spammer) kwa ajili ya Lile zoezi la kukaza zile long bars na short bars.


Wakati huu mvua ilikua inanyesha kubwa mno na
Baridi lilikua kali sana, machozi yalinitoka baada ya
Kukumbuka maisha ya nyumbani especially baada
Ya kumkumbuka mama yangu kipenzi. Nilijiambia
Endapo nitafanikiwa kuponyoka eneo hilo, ningerudi Nyumbani Mara moja na nisinge jaribu tena ujinga ule.


Tuliendelea na zoezi la kukaza vyuma vilivyokua
Vimeshikiria kontena hizo. Lakini wakati huu kazi
Ilikua ngumu kutokana na hali ya bahari kuchafuka
Mvua na mawimbi makubwa. Meli ilikua inayumba kiasi kwamba mtu asingeweza kusimama straight lazima angedondoka tu. Ilikua ni mara yangu ya kwanza kushuhudia tukio mla aina hiyo.

Long-bar moja ilikua na urefu wa Zaidi ya futi15
Huku uzito wake ukiwa ni Zaidi ya kilo30's sasa
Kuinyanyua hii kufika urefu wa kontena mbili au tatu juu halikua swala dogo.Wengi waliishia kuzitupa Baharini kwa kuzidiwa na uzito wake wengine Zikiwapiga kichwani na kuumia vibaya.

Wengi waliumia kwakua hawakua na vitendea kazi
Rasmi kwa shughuli hiyo kama safety boots na kofia ngumu ( helmets).

Kwa mabaharia wenyewe walikua wamevalia full
PPE (personal protective equipment) yan walikua na Kofia ngumu, safety boots, safety belts Kwa baadhi Na overoll zenye reflector.


Kiukweli chuma cha meli ni kigumu tofauti na vyuma Vya kawaida tulivyo vizoea, nilipiigwa mguu wa kulia Chini ya goti nilijikuta nimekaa chini huku machozi Nikishindwa kabisa kuyazuia.

Baridi lilikua kali sana lakini mvua pia ilikua ikinyesha Cha ajabu kila mmoja wetu alitokwa na jasho kwa Zoezi lile. Nilikua mwepesi kwenye kuelewa Maelekezo yote, mfano ilikukaza vile vyuma tulikua Tunazungusha clockwise na kulegeza ilikuani Anticlockwise.


Kilichonishangaza kwenye meli ile ambacho nadhani Ni utaratibu wa meli zote, kulikua kuna daktari, askari na pia kulikua na mafundi wa umeme, mechanic na Taaluma nyingine nyingi.


Hivyo wale walioumia walipatiwa matibabu na
mtaalam wa afya alisisitiza tupewe vitendea kazi na tuwe kwenye full PPE.


Aiseee!!!! Siku ukiwa maeneo ya felly unaenda
Kigamboni na ukaona meli ya konten aina ingia kwa kusindikizwa na zile tag ndogo. Waheshimu sana Wale jamaa mule ndani ya zile meli wanafanyakazi Ngumu sana wanapokua deep
Sea.

Ubize ulikua wa hali ya juu kwa usiku ule, na hapo
Ndio niliona kazi ya zile radiocall ambazo niliwaona Nazo wale mabaharia tuliowafata kigamboni na Kwenda nao kijichi. Kwani kwa ukubwa wa meli ile Ilikua ngumu kuwasiliana kwa njia ya kawaida bali Radiocalls..


Baadae alitoka captain ambae alitoa amri kwa wote Ambao tulikua hatusiki na lashing (kazi ya kufunga na kufungua meli) tuache mara moja. Wale mabaharia waliokua wanatutumikisha walionekana Kuwa wapole sana, kwa haraka nikagundua captain Ni mtu anae ogopeka sana kwenye mambo yale ya Usafiri wa bahari.

Tuliludi kukaa eneo tulilopangiwa tokea mwanzo
Tunaingia ndani ya meli hiyo na wengi tulishukuru
Ujio wa captain yule kwani zoezi lile lilikua ni vita ya kupambana na dhoruba la baharini..

Tukiwa tumepumzika bwana mmoja alitupa story za Mambo ya bahari kwani alionekana kuwa mzoefu Japo kingereza chake kilikua kigumu kueleweka. Lakini point kubwa alikua anajaribu kutuelezwa Nguvu ya captain kwenye usafiri wa baharini.


Kwa maelezo yake ni kwamba captain ndio kiongozi Mkuu ndani ya meli, na mnapokua ndani ya meli Mabaharia hawaruhusiwi kusafiri na wanawake Isipokua captain anaweza akasafiri na familia yake. Ila mabaharia wa kawaida hawatakiwi kuwa na Wanawake na ndio maana wanapotia nanga popote Huwaza wanawake, hii hutokana na ukweli kwamba Wanasafiri umbali mrefu bila kuwaona kabisa wadada.


Alienda mbali Zaidi kwa kusema meli nyingi za karne Hii ya 21 unakuta ndani ya ile crew yao kunakua na Ma gay ata wawili. Hawa huwa ni chakula kwa wenzao, Na mabaharia wengi kazi zao hua ni za mikataba mifupi mifupi na popote pale mkataba utakapoishia basi utashuka kwenye chombo kisha watapanda wengine.


Story zilikua nyingi tulicheka kwa pamoja japo wengi Tulionekana kucheka kicheko cha uchungu
Uliosababishwa either na fatiki au mawazo ya kule
tunapoelekea.


Nikiwa ndani ya blanket nilikumbuka matukio mengi Ya ajabu niliyowahi kuyafanya kuanzia MAKOKO SEMINARY, KIZUKA SEKONDARI na kisha SENGEREMA SECONDARY. Niliamini hayo ndio yalikua malipo yangu kwa uhuni niliowahi kuufanya ambao Haukua na tija wala faida yoyote.


Nilimkumbuka Merry toka siku tunakutana maeneo Ya sengerema na kisha kumbukumbu ilinipeleka Mpaka siku tuna agana stand ya msamvu morogoro. Kisha masaa kadhaa mbele kupata taarifa ya kifo chake.


Niliingiza Mkono Mfukoni Na Kutoa Hereni zake
Ambazo aliziacha siku ile room tukiwa kwa ras, niliamini ile ilikua ni kumbukumbu tosha niliyoachiwa na merry ( kwa sasa hereni hizo anazivaa mke wangu japo sikuwahi kumpa uhalisia wa hereni hizo, hua anashangaa tu kwanini ni hereni flani local and cheap ila nazipenda sana)

kwa kipindi hiki nilitamani Second chance ya kuishi na wazazi wangu ili niwaonyeshe ni kwa namna gani nimebadilika.
Kiukweli kwa wakati huo nilikua naiangalia dunia
Kwa jicho linguine kabisa. Usiombe uwe kwenye
Situation kama hii kwani hutoona maana ya kuzaliwa kabisa.

Mpaka wakati huo sikuona tena thamani ya maisha yangu, nilimkumbuka mzee massawe ambae Mara Nyingi alikua mkali lakini bado kwa ukali wake Hakuacha kunilipia ada akisisitiza nisome.

Nilimkumbuka mama ambae alijitahidi kuhakikisha
Napata chakula hasa wakati ninapochelewa kurudi
Nyumbani huku mzee massawe akiacha taarifa
Nisipewe chakula niende nikale nilipovutia bangi
Zangu.




Nilikuja Kustuka Baada Ya Sauti Niliyoiskia kwambali ikiita "kunta! Kunta! Kunta! Hey little boy from Africa, good morning?"


Ilikua ni rafudhi ya kimexico hapo niligundua alikua
Ni yule Mzee mwenye pama. Ilikua ni asubuhi lakini Hatukuweza kuliona jua sijui ilikua ni mawingu au Bado hakuja pambazuka vizuri. Ile ya dhoruba la usiku hali ilikua imetulia Lile dhoruba la usiku lilipotea kabisa huwezi amini Kama usiku huo hatuku pumzika kwa kupambana na Upepo mkali.


Baada ya kuwa kumekucha vizuri walichukuliwa
Baadhi yetu kuelekea sehemu ambayo nadhani ndio Kulikua na jiko. Jamaa wale waliludi na chakula, Ilikua ni mikate pamoja na mapande makubwa ya samaki.I likua ngumu kutambua alikua ni samaki gani kwani yalikuani mapande makubwa usingeweza kuona ata miba ya samaki yule.


Tukiendelea na chai alikuja Miguel katika namna
Kama ana tuhesabu, hapo mwanzo tulikua 14 lakini Ata mimi nilistuka baada ya kuona tupo 12 pekee.
Miguel aliuliza wenzetu walipo lakini hakukua na
Mwenye majibu.


Ni yule jamaa ambae usiku alikua anatupa story za Mabaharia na maisha ya baharini kwa ujumla ndio Sikumuona wakati huo. Alionekana kuwa mzoefu Kidogo kwenye mambo ya bahari, nilimshuhudia Miguel akija na askaria mbao hapo mwanzo Sikufanikiwa kuwaona na sikujua askari hao walikua Wapi muda wote.


Nikawaida sana meli hizi za mizigo kutembea na
Askari ndani yake tena makomando kabisa kwani
Miaka hii kumekua na wimbi kubwa la shughuli za
kiharamia. Hasa kwa meli zinazokuja ukanda wetu huu wa Pwani ya Africa mashariki pia zina desturi hiyo. Kwani pwani ya somaria mpaka Mombasa inasifika pia kwa uwepo wa wazee wa kazi Yaani pilates.


Ndio maana meli inapotia nanga tu kwenye Bandari Ya dar es salaam utaona gari ya jeshi ya navy kigamboni itaenda kwenye meli husika.
Story zinasema jamaa wanaendaga kuchukua silaha za Askari ambao wanakuwepo kwenye meli hiyo.


Baada ya kushuka askari kwenye meli zinazoingia
Bandari ya dar es salaam anaefata anakua ni daktari Kwa ajili ya kuangalia afya za mabaharia na mwisho Kabisa ni afisa wa uhamiaji.

Nimetoa maelezo haya ilituone kwanini ndani ya
Meli hizi unakuta kuna makomando ndani yake.

Miguel alikuja na askari wale ambao walikua na
Mbwa watatu walioshiba lakini cha ajabu tokea
Tunapanda meli hiyo hatukusikia mlio au mbwa
akibweka. Ila baada ya mbwa wale kuja eneo ulilopo walianza kubweka huku wakiwa wameshikiliwa kwenye kamba.


Baada ya muda mbwa wale waliachiwa nakuanza kuzunguka Meli nzima especially maeneo yaliyokua yamejificha. Ilionekana wale mbwa ile ndio ilikua kazi yao yaan Kutafuta watu ambao walidhaniwa kuwa ni wazamiaji.


Hazikupita dakika 10 wale askari walikuja wakiwa
Wame wakamata jamaa wawili ambao Hatukuwafahamu kwa majina lakini mmoja wao
Alikua ni yule aliyekua anatupas tory usiku.
Miguel alitoa bastola kiunoni na kumshuti mmoja
Wao kifuani kisha ikatoka amri atupwe ndani ya maji.

Hapa sasa nilianza kuiona sura halisi ya Miguel
Alikua kijana mdogo lakini katili sana.


Mwingine aliyebaki alivunjwa mikono kuanzia maeneo ya Begani kwa vyuma vinavyojulikana kama twist lock na Kisha kutupwa baharini pia. Huyu yeye alitupwa mzima lakini mikono ilivunjwa so alikua ni wakufa tu kwani asingeweza kujitetea kwa namna yoyote.

Miguel: ofcourse I want to show you how cruel I am.

Aliongea maneno hayo tu na kuondoka bila kugeuka Nyuma huku akionekana amekasilika sana kwa Kitendo cha jamaa wale kujaribu kumtoroka.


Jambo lile lilituacha midomo wazi kwani
Hatukutegemea kama angefikia huko kwenye
kuuana. Kulikuana kimya cha takribani dakika 20,
watu wakionekana kutafakari kitendo kile kwani bila shaka wote tulijua tunapoenda ni kweli hakuna
Amani na tunaenda kufanya kazi ngumu.


Lakini hatukufikiri kama ata sisi hatuna thamani
Kiasi hicho. Mzee wangu wa ki Mexican alitoa pakiti Ya sigara iliyoandikwa CARIBE ambayo ilionekana ni sigara pendwa Sana kwa nchi za American ya kusini hususani Colombia, Peru, Chile na kwa uchache sana Cuba. Inazalishwa na COLTABACO huku piece moja ikifikia urefu wa Mpaka 82mm.


Alitoa pakiti hiyo akajaribu kuchungulia kama kuna
Chochote kimebaki hatimae alikuta sigara moja
Akaitoa na kisha kuiwasha. Alivuta kidogo na kunipa,


Sikua mtumiaji wa sigara lakini sikuona sababu ya
Kukataa kuvuta nilivuta kidogo na kumpatia jilani
Yangu mwingine. Sigara ile ilitembea kwa pafu moja mpaka pafu mbili Kwa kila mtu kati yetu wote 12 kisha ikamfikia tena Mzee yule m Mexicana. Ilipofika kwake alisimama Katikati yetu, kisha kwa lugha nisiyo itambua Aliongeamaneno ambayo baada ya kutafsiriwa hii Ndio ilikua maana yake.

"Tulikua 14 na sasa tupo12, sababu ya kupungua
Kwetu ni vifo ambavyo naweza sema wenzetu Wamejitakia . Sasa sigara hii imetuunganisha kuwa Kitu kimoja, hakuna asiyejua kuwa tunapoenda kuna Hari mbaya kuliko hapa. Labda kwa upande wa kunta Ye ni kipofu kabisa, kwa kumuona tu anahisi Tunapoenda ni sehem ya kupumzika na kushusha Shida zake. Kwa umri wangu huu nawaomba Tusijaribu kufanya lolote linalohusu kukimbia kwa Kufanya hivyo tutaisha, Miguel nimemjua miaka Mingi yeye ni Zaidi ya baba yake.

Likini kwa pamoja tuungane kumfariji kunta kinte
Kwani umri wake bado mdogo sana asipoteze Energy nyingi kwenye kulia usiku kucha bado ana Nafasi kubwa.


Alimaliza kwa kusema atakua mkali Kwa yoyote atakae onyesha kukata tamaa, kwani Mpaka wanaenda huko walisha kata tamaa ya Maisha ya mtaani hivyo ni Zaidi ya dhambi kukataTamaa mara mbili.


Wengi walimsikiliza kwa utulivu sana lakini kwa Upande wangu maneno yale yalinikumbusha mzee massawe ambae Mara nyingi nikiwa katika umri Mdogo aliniita mwanajeshi wake.

KWA AMBAO WATATAKA KUISOMA KWA HARAKA ZAIDI WA MUONE 0623329512 Whatsapp
 
Baada ya tukio lile wote tulipoa sana na hata wale ambao walionekana ni majasiri wa kule tunapoelekea walikua wapole zaidi. Baridi lilikua Kali sana huku kamvua karasha rasha kakiendelea, tulikaribiwa na meli ndogo ambayo kutokana na ukungu hatukuiona vizuri mpaka pale ilipotukaribia.

Ilikua ni meli ndogo ya rangi ya blue iliyojaa mabaharia weusi wenye miili mikubwa na ndevu nyingi. Kwa udogo wa meli ile tuliweza kuona mazingira yote ya ndani pasipo wao kutuona kabisa.

Kwa mara nyingine nilimuona McKenzie akitoka huku anaongea na radiocall, ni wazi alikua akiwasiliana na wale watu wa kwenye meli ile ndogo. Meli zile mbili zilisogeleana kwa ukaribu zaidi, ndani ya dakika chache tukasikia ngurumo.


Zilikua ni ngurumo za cranes (winchi) zilizokua kwenye meli yetu. Kitendo kilichokua kinafanyika pale kilikua kinaitwa TRANSHIPPING yaani baadhi ya mizigo ilikua inatolewa kwenye meli kubwa na kuhamishiwa meli ndogo.

Mizigo ile tulifanikiwa kugundua ilikua ni sukari, sukari hiyo ilikua ikitokea Brazil kwani kwa wakati huo, nadhani mpaka hivi sasa Brazil inashika namba 2 kama sio(1)moja kwa uzalishaji wa sukari Duniani. Ikizidiana takwimu na India kwa metrics tonnes chache sana.

Kwa namna nilivyokua nimekaa karibu na maeneo aliyokua amekaa McKenzie na kusikia mazungumzo yake kwenye radiocall niligundua sukari hiyo inaelekea (pwani ya Africa mashariki) Coast of East Africa.

Na ni wazi sukari hiyo ilikua ni ya magendo kwa namna walivyokua wakiwasiliana. Na hapo nikagundua kwanini sukari nyingi za magendo inchini hupatikana maeneo ya pwani hususani ukanda wa Tanga, Mombasa, bagamoyo, kilwa na sometimes Zanzibar.

Na mara nyingi sukari hizi zikikamatwa na taasisi kama KMKM au TRA, taasisi hizi hutangaza kama wamekamata shehena za sukari ambazo hazikua na vibali kutoka mamlaka ya chakula na dawa (TFDA) wala shirika la viwango (TBS).

Sukari hizi hutokea Brazil na baada ya kufika mikoa ya pwani huvikwa au hufanyiwa packaging mpya. Mara nyingi kwenye hizo packaging mpya wanatumia Brand za humu humu nchini kama vile kagera sugar au hata kilombero.

Aina hii ya smuggling ( biashara ya magendo) inasababishwa na sugar-gap kubwa iliyopo ndani ya nchi za Africa mashariki. Tunaposema sugar-gap yaani ni gap lililopo kati ya sukari inayozalishwa na mahitaji yenyewe halisi ya sukari ya majumbani na viwandani. Ambapo sukari inayozalishwa bado haikidhi mahitaji ya watu na viwanda kwa ukanda huu wa Africa mashariki.

Na hii ndio sababu kwanini tunaendelea ku import sukari mataifa mengine either kwa njia halali au ata smuggling. Mfano kwa Tanzania sugar-gap ilikua 350,000 metric tonnes kwa miaka ile ya 2012, kwa gap hili watu wa kucheza na fursa lazima walitumie effectively na hapa nilimuona McKenzie kama miongoni mwa wataalamu wa kucheza na fursa.

McKenzie alionekana kuijua vizuri Africa mashariki na watu wake pia ata hivyo alionekana kuwa mzoefu wa biashara zanazotumia bahari. Nilishangaa kwanini hakua captain wakati alionekana kuwa na mamlaka pia ndani ya meli ile.

Baada ya kuhamisha mizigo ile ya sukari, cranes zote ziliwekwa katika hali yake ya kawaida na ile meli ndogo ilikua ya kwanza kuondoka.

Mimi nilikua miongoni mwa watu wanaoshangaa sana kwani matukio mengi yalikua mapya kwangu. Hapo mwanzoni nilikua na kauoga ka kuangalia maji lakini mpaka wakati huo uoga ulikua umeisha kabisa.

Tuliendelea na safari mpaka mida ya usiku mnene tulipokaribia eneo moja ambalo lilikua na kisiwa tulichokiona kwa mbali sana. Kisiwa hicho kiliitwa FOCA ISLAND kwa mujibu wa wenyeji, kilikua kipo kaskazini mwa eneo moja linaitwa Piura huko Peru. Karibu kabisa na mkondo wa bahari wa Humboldt na ikweta.

Meli ilisimama kisiwani hapo kisha wachache tena wenye nguvu tulipelekwa engine room kwa ajili ya kufanya usafi. Kwa joto la mule ndani ya engine room wote tulivua nguo na kubaki boxer. Kazi ile haikua nyepesi sio tu sababu ya joto lakini pia jukumu lenyewe la kuhahakisha tunasafisha lilikua ni zoezi gumu.

Nilichowapendea wale jamaa wa meli ile ya panama walikua wanahakikisha tunapewa msosi mzito na mwingi kila baada ya kazi ngumu.

Hivyo baada ya zoezi lile ilikuja menu moja hatari sana kasoro maji ya kunywa ndio ilikua kipengere.

Basi tulishukia kisiwani pale tukiongozwa na Miguel ambaye safari hii alizidi kuonekana mwenye hasira zaidi ya zile za mbogo. Kutoka eneo tuliloshuka mita 100 mbele kulikua na helicopter iliyoandikwa Airbus H175 maandishi madogo kwa upande wa kulia.

Wakati nakiwa bado mdogo niliamini helicopter ina uwezo wa kubeba abiria kuanzia 2 mpaka 8, lakini tofauti na helicopter ile tuliyoikuta pale FOCA ISLAND ilionekana kua na uwezo wa kubeba mpaka abiria 20.

Na tulipoikaribia tulipelekwa kwa speed sana na wote tulipanda ndani ya helicopter ile, tukiwa ndani Miguel alifika na kutuhesabu kwa mara nyingine kisha akaondoka zake.

Apa chini nimeambatanisha baadhi ya dhana ambazo hutumiwa kwenye ufungaji wa containers

Lakini kwa watakao pata PDF nimejaribu kuzielezea pia View attachment 2616323
images%20(20).jpg
View attachment 2616322View attachment 2616324
 
Baada ya tukio lile wote tulipoa sana na hata wale ambao walionekana ni majasiri wa kule tunapoelekea walikua wapole zaidi. Baridi lilikua Kali sana huku kamvua karasha rasha kakiendelea, tulikaribiwa na meli ndogo ambayo kutokana na ukungu hatukuiona vizuri mpaka pale ilipotukaribia.

Ilikua ni meli ndogo ya rangi ya blue iliyojaa mabaharia weusi wenye miili mikubwa na ndevu nyingi. Kwa udogo wa meli ile tuliweza kuona mazingira yote ya ndani pasipo wao kutuona kabisa.

Kwa mara nyingine nilimuona McKenzie akitoka huku anaongea na radiocall, ni wazi alikua akiwasiliana na wale watu wa kwenye meli ile ndogo. Meli zile mbili zilisogeleana kwa ukaribu zaidi, ndani ya dakika chache tukasikia ngurumo.


Zilikua ni ngurumo za cranes (winchi) zilizokua kwenye meli yetu. Kitendo kilichokua kinafanyika pale kilikua kinaitwa TRANSHIPPING yaani baadhi ya mizigo ilikua inatolewa kwenye meli kubwa na kuhamishiwa meli ndogo.

Mizigo ile tulifanikiwa kugundua ilikua ni sukari, sukari hiyo ilikua ikitokea Brazil kwani kwa wakati huo, nadhani mpaka hivi sasa Brazil inashika namba 2 kama sio(1)moja kwa uzalishaji wa sukari Duniani. Ikizidiana takwimu na India kwa metrics tonnes chache sana.

Kwa namna nilivyokua nimekaa karibu na maeneo aliyokua amekaa McKenzie na kusikia mazungumzo yake kwenye radiocall niligundua sukari hiyo inaelekea (pwani ya Africa mashariki) Coast of East Africa.

Na ni wazi sukari hiyo ilikua ni ya magendo kwa namna walivyokua wakiwasiliana. Na hapo nikagundua kwanini sukari nyingi za magendo inchini hupatikana maeneo ya pwani hususani ukanda wa Tanga, Mombasa, bagamoyo, kilwa na sometimes Zanzibar.

Na mara nyingi sukari hizi zikikamatwa na taasisi kama KMKM au TRA, taasisi hizi hutangaza kama wamekamata shehena za sukari ambazo hazikua na vibali kutoka mamlaka ya chakula na dawa (TFDA) wala shirika la viwango (TBS).

Sukari hizi hutokea Brazil na baada ya kufika mikoa ya pwani huvikwa au hufanyiwa packaging mpya. Mara nyingi kwenye hizo packaging mpya wanatumia Brand za humu humu nchini kama vile kagera sugar au hata kilombero.

Aina hii ya smuggling ( biashara ya magendo) inasababishwa na sugar-gap kubwa iliyopo ndani ya nchi za Africa mashariki. Tunaposema sugar-gap yaani ni gap lililopo kati ya sukari inayozalishwa na mahitaji yenyewe halisi ya sukari ya majumbani na viwandani. Ambapo sukari inayozalishwa bado haikidhi mahitaji ya watu na viwanda kwa ukanda huu wa Africa mashariki.

Na hii ndio sababu kwanini tunaendelea ku import sukari mataifa mengine either kwa njia halali au ata smuggling. Mfano kwa Tanzania sugar-gap ilikua 350,000 metric tonnes kwa miaka ile ya 2012, kwa gap hili watu wa kucheza na fursa lazima walitumie effectively na hapa nilimuona McKenzie kama miongoni mwa wataalamu wa kucheza na fursa.

McKenzie alionekana kuijua vizuri Africa mashariki na watu wake pia ata hivyo alionekana kuwa mzoefu wa biashara zanazotumia bahari. Nilishangaa kwanini hakua captain wakati alionekana kuwa na mamlaka pia ndani ya meli ile.

Baada ya kuhamisha mizigo ile ya sukari, cranes zote ziliwekwa katika hali yake ya kawaida na ile meli ndogo ilikua ya kwanza kuondoka.

Mimi nilikua miongoni mwa watu wanaoshangaa sana kwani matukio mengi yalikua mapya kwangu. Hapo mwanzoni nilikua na kauoga ka kuangalia maji lakini mpaka wakati huo uoga ulikua umeisha kabisa.

Tuliendelea na safari mpaka mida ya usiku mnene tulipokaribia eneo moja ambalo lilikua na kisiwa tulichokiona kwa mbali sana. Kisiwa hicho kiliitwa FOCA ISLAND kwa mujibu wa wenyeji, kilikua kipo kaskazini mwa eneo moja linaitwa Piura huko Peru. Karibu kabisa na mkondo wa bahari wa Humboldt na ikweta.

Meli ilisimama kisiwani hapo kisha wachache tena wenye nguvu tulipelekwa engine room kwa ajili ya kufanya usafi. Kwa joto la mule ndani ya engine room wote tulivua nguo na kubaki boxer. Kazi ile haikua nyepesi sio tu sababu ya joto lakini pia jukumu lenyewe la kuhahakisha tunasafisha lilikua ni zoezi gumu.

Nilichowapendea wale jamaa wa meli ile ya panama walikua wanahakikisha tunapewa msosi mzito na mwingi kila baada ya kazi ngumu.

Hivyo baada ya zoezi lile ilikuja menu moja hatari sana kasoro maji ya kunywa ndio ilikua kipengere.

Basi tulishukia kisiwani pale tukiongozwa na Miguel ambaye safari hii alizidi kuonekana mwenye hasira zaidi ya zile za mbogo. Kutoka eneo tuliloshuka mita 100 mbele kulikua na helicopter iliyoandikwa Airbus H175 maandishi madogo kwa upande wa kulia.

Wakati nakiwa bado mdogo niliamini helicopter ina uwezo wa kubeba abiria kuanzia 2 mpaka 8, lakini tofauti na helicopter ile tuliyoikuta pale FOCA ISLAND ilionekana kua na uwezo wa kubeba mpaka abiria 20.

Na tulipoikaribia tulipelekwa kwa speed sana na wote tulipanda ndani ya helicopter ile, tukiwa ndani Miguel alifika na kutuhesabu kwa mara nyingine kisha akaondoka zake.

Apa chini nimeambatanisha baadhi ya dhana ambazo hutumiwa kwenye ufungaji wa containers

Lakini kwa watakao pata PDF nimejaribu kuzielezea pia View attachment 2616323View attachment 2616325View attachment 2616322View attachment 2616324
Upo vizuri sana mkuu
 
Ilituchukua zaidi ya masaa mawili tukiwa hewani na helicopter ile, kila mtu alitamani ile ndio iwe safari ya mwisho kwani walikua wamechoka sana huku wasijue mimi nilitokea Africa mashariki hivyo nilichoka zaidi yao.

Tukiwa ndani ya helicopter tulimkuta bwana mmoja wa kizungu aliyekua na kipara kisichoonyesha dalili ya nywele kabisa. Bwana yule alikua na hereni nyingi masikioni pamoja na vipini kwenye pua zote, alikua na tattoo mpaka kichwani muonekano uliompelekea kutisha kwa namna moja ama nyingine.

Alitukaribisha vizuri sana huku akitusisitiza tujiskie tupo nyumbani, kwa majina aliitwa Daniel. Alisema tukifika camp itakua nafasi yake ya kumjua kila mmoja wetu.


Daniel alionekana kua charming sana kwenye maongezi lakini kwa haraka haraka ukimuangalia usoni utasema jamaa anaweza kua roho mbaya sana na katili sana.

Muda wote tukiwa kwenye helicopter mzungu yule bwana Daniel alikua bize kutafuna majani kama mbuzi. Kwa wajuaji wa mambo niliopata kuwauliza walisema majani yale ndio mmea wa coca unaotumika kutengeneza madawa ya cocaine.

Inaaminika utaratibu au utamaduni wa kutafuna majani hayo ulianza zaidi ya miaka 3000 kabla ya kuja kristo. Sikushangaa sana kwani wakati nipo ENGARONI-ARUMERU nilipata kusikia kuwa binadamu hususani watu wa misri ya kale walianza kuvuta bangi zaidi ya miaka 10000 kabla ya kuja kristo.

Hivyo kwa story za utamaduni wa kutafuna majani hayo ya coca niliona ni sawa pia. inasemekana maeneo mengi ya American ya kusini mmea huu wa coca uliitwa divine plant na ulikua ni miongoni mwa accessories muhimu kwenye dini zao. Hivyo mababu wa huko waliutumia pia kwa sababu za kiroho (spiritual issues) na wapo ambao walitumia majani hayo ata kwa kutengeneza chai.

Ingredient kuu kwenye majani ya coca inaitwa Erythroxylum na Ndani ya mmea wa coca ukiachana na cocaine kuna zaidi ya alkaloids tofauti tofauti 14. tutatelezana kiundani alkaloids ni Nini.........

kinachotafutwa zaidi kwenye majani haya ya coca ni hiyo alkaloid, hivyo basi coca leaf iliyobora ni ile ambayo ndani yake kuna kiasi kikubwa cha cocaine alkaloids.

Best quality ya coca hulimwa maeneo ya higher altitudes na hii hupelekea coca inayopatikana nyanda za juu za safu ya milima ya andes kuwa bora kuliko zile za nyanda za chini. Hii husababishwa na ukweli kwamba coca ya kutoka higher altitudes inakua na cocaine alkaloids nyingi.

Alichokua anakifanya Daniel kiliitwa acullico, kitendo cha kutafuna majani hayo ya coca. Wengi hatafuna majani hayo either kwa ajili ya kuondoa uchovu, maumivu au hata njaa pia. Hivyo mmea huu wa coca umekua stimulant muhimu sana miongoni mwa watu wa America ya kusini.

Kwa kutafuna majani ya coca unakua umeimeza cocaine ikiwa kwenye basic form, hivyo ikifika tumboni hubadilishwa na kuwa hydrochloride........ Apo baade nitatoa maelezo zaidi,

Story hazikua nyingi kwani karibia wote tulikua hatujuani huku idadi kubwa ya watu hawakua waitokea America ya kusini hivyo mazingira yalikua ni mageni kwa ujumla.

Kwa makadilio safari ile ilituchukua umbali wa zaidi ya kilometers 700's. Na Hatimae tulitua ndani ya msitu mmoja mkubwa sana kandokando ya mto, mto ule ulijulikana kwa jina la haullaga.

Daniel ndio alikua mwenyeji wetu na ndio alianza kutoa maelezo yote yanayohusu geografia ya eneo hilo wakati tuna ingia ndani ya mashamba hayo.

Kulingana na maelezo ya Daniel, apo tulikua ndani ya jimbo moja maarufu kama Huánuco. mashamba hayo yalikua ndani ya bonde hilo la haullaga kwa miongo kadhaa. Lakini pia mto haullaga ni mto mdogo unaoenda kuungana na mto Maranon kisha Amazon.

Kwa miaka kadhaa nyuma mto haullaga uliitwa Gaullaga au Rio de Los motilones. Alimalizia kwa kusema kwakua hapo ndio makazi yetu mapya basi tutajua mengi sana kuhusu geografia nzima ya maeneo hayo. Tena tunaweza kuwa wenyeji kumzidi yeye.

Alimalizia kwa kusema around miaka ya 1930's, (UHV) maarafu kama upper haullaga Valley kwenda mpaka pembezoni mwa mto wenyewe haullaga Ndani ya jimbo hilo la Huánuco na San Martin ilikua sio rahisi kufikika.

Mara nyingi watu walitumia maboti kupitia mto au hata wengine walitumbea kufuata msitu kwa msitu kufika mahali apo. Na hiyo ndio asili au miongoni mwa sababu za kuanzishwa mashamba hayo kwa majimbo ya Huánuco.

Daniel alionekana mtu wa stories sana, na mara kwa mara aliongea pale tu alipoacha kutafuna majani yale ya coca.


Muda wote tukiwa tunatembea hatukubahatika kukutana na mtu yoyote mazingira yale.

Tulichokiona zaidi ni mashamba yaliyovutia na yaliyoonekana kua na matunzo ya hali ya juu. Mashamba hayo yalikua eneo la juu kutoka pale tulipokua kua.

Mita kama 30 mbele tuliona geti la mbao na askari wakiwa wamesimama eneo hilo, baada ya kusogelea geti hilo niligundua karibia askari wote waliokua pale walikua ni weusi kwa rangi.

Tulipita getini hapo bila kuongea na yoyote kwani ata Daniel mwenyewe sikuona akimsalimia yoyote miongoni mwao.

Ilionekana ni desturi ya maeneo yale kutokua na ukaribu na yoyote yule ambaye alikua ni askari.

Baada ya kuingia mazingira yale ya shambani nilishangaa kuona ni mazingira ambayo hayana tofauti na yale mazingira ya vijijini kabisa. Yaani kama nisingekua nimesafiri kwa ndege, bus na kisha meli ningesema pale tulikua tupo Moshi.

Nyumba zilikua za kawaida kabisa na nyingi zilijengwa kwa mtindo wa gharofo za mbao. Tuliendelea kutembea mpaka tulipofika eneo ambalo ndio lilikua ni special kwa ajili ya makazi ya wakulima.

Tulipofika eneo hilo kulikua na uwanja mkubwa zaidi ya uwanja wa mpira, chini ya uwanja huo kulikua na maturubai makubwa yaliyolazwa mpaka kujaa uwanja mzima.

Juu ya maturubai hayo makubwa yalianikwa majani mabichi, yaani kama ambavyo tunaanika mahindi au mazao mengine ndivyo ambavyo hawa jamaa walianika majani hayo.

NB: KWENYE PDF NDIO NIMEAMBATANISHA KWA WINGI KULIKO HUMU, KWA WATAKAO HITAJI PDF DOCUMENT ZA SIMULIZI NA KUSOMA KWA HARAKA 0623329512 WhatsApp
 
Ilituchukua zaidi ya masaa mawili tukiwa hewani na helicopter ile, kila mtu alitamani ile ndio iwe safari ya mwisho kwani walikua wamechoka sana huku wasijue mimi nilitokea Africa mashariki hivyo nilichoka zaidi yao.

Tukiwa ndani ya helicopter tulimkuta bwana mmoja wa kizungu aliyekua na kipara kisichoonyesha dalili ya nywele kabisa. Bwana yule alikua na hereni nyingi masikioni pamoja na vipini kwenye pua zote, alikua na tattoo mpaka kichwani muonekano uliompelekea kutisha kwa namna moja ama nyingine.

Alitukaribisha vizuri sana huku akitusisitiza tujiskie tupo nyumbani, kwa majina aliitwa Daniel. Alisema tukifika camp itakua nafasi yake ya kumjua kila mmoja wetu.


Daniel alionekana kua charming sana kwenye maongezi lakini kwa haraka haraka ukimuangalia usoni utasema jamaa anaweza kua roho mbaya sana na katili sana.

Muda wote tukiwa kwenye helicopter mzungu yule bwana Daniel alikua bize kutafuna majani kama mbuzi. Kwa wajuaji wa mambo niliopata kuwauliza walisema majani yale ndio mmea wa coca unaotumika kutengeneza madawa ya cocaine.

Inaaminika utaratibu au utamaduni wa kutafuna majani hayo ulianza zaidi ya miaka 3000 kabla ya kuja kristo. Sikushangaa sana kwani wakati nipo ENGARONI-ARUMERU nilipata kusikia kuwa binadamu hususani watu wa misri ya kale walianza kuvuta bangi zaidi ya miaka 10000 kabla ya kuja kristo.

Hivyo kwa story za utamaduni wa kutafuna majani hayo ya coca niliona ni sawa pia. inasemekana maeneo mengi ya American ya kusini mmea huu wa coca uliitwa divine plant na ulikua ni miongoni mwa accessories muhimu kwenye dini zao. Hivyo mababu wa huko waliutumia pia kwa sababu za kiroho (spiritual issues) na wapo ambao walitumia majani hayo ata kwa kutengeneza chai.

Ingredient kuu kwenye majani ya coca inaitwa Erythroxylum na Ndani ya mmea wa coca ukiachana na cocaine kuna zaidi ya alkaloids tofauti tofauti 14. tutatelezana kiundani alkaloids ni Nini.........

kinachotafutwa zaidi kwenye majani haya ya coca ni hiyo alkaloid, hivyo basi coca leaf iliyobora ni ile ambayo ndani yake kuna kiasi kikubwa cha cocaine alkaloids.

Best quality ya coca hulimwa maeneo ya higher altitudes na hii hupelekea coca inayopatikana nyanda za juu za safu ya milima ya andes kuwa bora kuliko zile za nyanda za chini. Hii husababishwa na ukweli kwamba coca ya kutoka higher altitudes inakua na cocaine alkaloids nyingi.

Alichokua anakifanya Daniel kiliitwa acullico, kitendo cha kutafuna majani hayo ya coca. Wengi hatafuna majani hayo either kwa ajili ya kuondoa uchovu, maumivu au hata njaa pia. Hivyo mmea huu wa coca umekua stimulant muhimu sana miongoni mwa watu wa America ya kusini.

Kwa kutafuna majani ya coca unakua umeimeza cocaine ikiwa kwenye basic form, hivyo ikifika tumboni hubadilishwa na kuwa hydrochloride........ Apo baade nitatoa maelezo zaidi,

Story hazikua nyingi kwani karibia wote tulikua hatujuani huku idadi kubwa ya watu hawakua waitokea America ya kusini hivyo mazingira yalikua ni mageni kwa ujumla.

Kwa makadilio safari ile ilituchukua umbali wa zaidi ya kilometers 700's. Na Hatimae tulitua ndani ya msitu mmoja mkubwa sana kandokando ya mto, mto ule ulijulikana kwa jina la haullaga.

Daniel ndio alikua mwenyeji wetu na ndio alianza kutoa maelezo yote yanayohusu geografia ya eneo hilo wakati tuna ingia ndani ya mashamba hayo.

Kulingana na maelezo ya Daniel, apo tulikua ndani ya jimbo moja maarufu kama Huánuco. mashamba hayo yalikua ndani ya bonde hilo la haullaga kwa miongo kadhaa. Lakini pia mto haullaga ni mto mdogo unaoenda kuungana na mto Maranon kisha Amazon.

Kwa miaka kadhaa nyuma mto haullaga uliitwa Gaullaga au Rio de Los motilones. Alimalizia kwa kusema kwakua hapo ndio makazi yetu mapya basi tutajua mengi sana kuhusu geografia nzima ya maeneo hayo. Tena tunaweza kuwa wenyeji kumzidi yeye.

Alimalizia kwa kusema around miaka ya 1930's, (UHV) maarafu kama upper haullaga Valley kwenda mpaka pembezoni mwa mto wenyewe haullaga Ndani ya jimbo hilo la Huánuco na San Martin ilikua sio rahisi kufikika.

Mara nyingi watu walitumia maboti kupitia mto au hata wengine walitumbea kufuata msitu kwa msitu kufika mahali apo. Na hiyo ndio asili au miongoni mwa sababu za kuanzishwa mashamba hayo kwa majimbo ya Huánuco.

Daniel alionekana mtu wa stories sana, na mara kwa mara aliongea pale tu alipoacha kutafuna majani yale ya coca.


Muda wote tukiwa tunatembea hatukubahatika kukutana na mtu yoyote mazingira yale.

Tulichokiona zaidi ni mashamba yaliyovutia na yaliyoonekana kua na matunzo ya hali ya juu. Mashamba hayo yalikua eneo la juu kutoka pale tulipokua kua.

Mita kama 30 mbele tuliona geti la mbao na askari wakiwa wamesimama eneo hilo, baada ya kusogelea geti hilo niligundua karibia askari wote waliokua pale walikua ni weusi kwa rangi.

Tulipita getini hapo bila kuongea na yoyote kwani ata Daniel mwenyewe sikuona akimsalimia yoyote miongoni mwao.

Ilionekana ni desturi ya maeneo yale kutokua na ukaribu na yoyote yule ambaye alikua ni askari.

Baada ya kuingia mazingira yale ya shambani nilishangaa kuona ni mazingira ambayo hayana tofauti na yale mazingira ya vijijini kabisa. Yaani kama nisingekua nimesafiri kwa ndege, bus na kisha meli ningesema pale tulikua tupo Moshi.

Nyumba zilikua za kawaida kabisa na nyingi zilijengwa kwa mtindo wa gharofo za mbao. Tuliendelea kutembea mpaka tulipofika eneo ambalo ndio lilikua ni special kwa ajili ya makazi ya wakulima.

Tulipofika eneo hilo kulikua na uwanja mkubwa zaidi ya uwanja wa mpira, chini ya uwanja huo kulikua na maturubai makubwa yaliyolazwa mpaka kujaa uwanja mzima.

Juu ya maturubai hayo makubwa yalianikwa majani mabichi, yaani kama ambavyo tunaanika mahindi au mazao mengine ndivyo ambavyo hawa jamaa walianika majani hayo.

NB: KWENYE PDF NDIO NIMEAMBATANISHA KWA WINGI KULIKO HUMU, KWA WATAKAO HITAJI PDF DOCUMENT ZA SIMULIZI NA KUSOMA KWA HARAKA 0623329512 WhatsApp
Mze baba uko vizuri story ni tamu sana [emoji120][emoji120]
 
Back
Top Bottom