afisa manispaa
Senior Member
- May 17, 2015
- 188
- 132
Shusha nondo ankoSio Gullaga boss, location yetu ilikua mto haullaga
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Shusha nondo ankoSio Gullaga boss, location yetu ilikua mto haullaga
Shusha nondo ankoMiaka ya nyuma sana hii haullaga iliitwa Gaullaga au Rio de Los motilones, tuwe wapole kunashughuli nyingi tutaziona ndani ya mto huu kuelekea Maranon na kisha Amazon.
Mkuu nitag na mm🤩Juu ya maturubai hayo makubwa yalianikwa majani mabichi, yaani kama ambavyo tunaanika mahindi au mazao mengine ndivyo ambavyo hawa jamaa walianika majani hayo.
Wote kwa pamoja tulikusanyika chini ya banda moja kubwa la mbao lililo funikwa na turubai kwa juu. Tukiwa hapa sasa nilimuona baba yake na Miguel akija eneo tulilo fikia.
Kwa mbali tuliona watu, watu walionekana kuwa wanatokea mashambani na walikua na mizigo mgongoni.
Mizigo ile ilikua ni aina ya viroba vikubwa, walielekea eneo lile la uwanja na kushusha mizigo ile na kisha kuendelea kuisambaza eneo zima.
Wote tuliowasili siku ile tulionekana kuwa wageni wa kile kilichokua kinaendelea eneo lile. Na yoyote angetambua hilo kwa namna ambavyo tulikua bize kushangaa shughuli hizo.
Daniel alikuja tena eneo hilo akiwa vijana wanne waliokua wamebeba maboxi makubwa lakini hayakua mazito kabisa kwa kuyaangalia tu.
Vijana wale walionekana wamechoka sana kwa kuwaangalia, suruali zoa hazikua na mikanda hawana mashati wakati huo wenye mashati mengi yalikua yametoboka au kuchanika kabisa.
Idadi kubwa ya wafanyakazi waliokua pale walikua ni weupe kwa muonekano. Na weusi niliowaona walikua na weusi ule wa design ya half-caste.
Kiukweli kila aliyekua eneo hilo alikua amechoka sana isipokua nafuu ilikua kwa viongozi ambao nao walionekana ni addicted pia kwenye matumizi ya unga.
Jamaa wale waliokua wamebeba maboxi walifika na kuacha chini maboxi kisha wakatokomea mashambani.
Niligundua eneo hilo halikua na utaratibu wa kusalimiana hovyohovyo. Utaongea na Mtu kama kuna sababu ya msingi la sivyo fanya majukumu yako mengine.
Hakukua na nafasi ya kupiga soga hovyohovyo muda mwingi waliutumia mashambani.
Kulikua na ulevi wa kipundukia pia, tulipofika hapo kulikua na kila dalili ya kuwepo kwa kila aina ya pombe.
Kwa muonekano wa wafanyakazi wale sikutaka kuamini kama wanalipwa kabisa. Mbaya zaidi walikuwepo mabinti ambao ilikua ngumu kujua kama ni wasichana au wazee.
Kama tunavyojua America ya kusini ilivyojaaliwa warembo lakini sio kwa warembo wale waliokua hoi wasingenivutia ata iweje.
Akati nipo kwenye mawazo ya kuwafikiria mabinti wale kwamba wasingenivutia kumbe kila mmoja wetu aliwaza hivyo.
Daniel aligundua hilo na akatukanusha kwa kusema pale ni kama bar au club, wakati unaingia bar utaona wanawake wote wabaya na hawatakuvutia. Lakini ukiwa kwenye bia ya sita au ya saba utaona walewale mabinti wameanza kuwa warembo.
Hivyo ata sisi baada ya mwezi tutaanza kuwa sumbua kwa kutaka kuchakata mbususu zao. Lakini Daniel alitukumbusha kuwa eneo hilo lina maambukizi makubwa ya ukimwi na waliouleta ni haohao tunao waona mabinti wabaya.
Na wengi walioupatia ukimwi hapo hawapo tayari kuondoka eneo hilo na watafia hapo na kuzikwa hapohapo.
Wakati tunaanza safari kule Cabo de la vela, hawa wafanyakazi wenzangu niliwaona wamechoka sana na ni kama watu wasio na matumaini ya kuishi. Lakini baada ya kufika hapa niliwaona kama watu wenye afya na nguvu zaidi.
Nilidhibitisha hili baada ya mkulima mmoja kupita na mwenzake huku wakiambiana kua wanaona nguvu mpya imeingia.
Baba yake na Miguel alisimama mbele yetu na kuanza kusoma majina, lakini kabla hajaanza,
BABA MIGUEL: mustapha!! I thought you dead at sea.
( Mustapha nilijua umefia baharini)
MIMI: no Dad I am still alive
( Hapana baba, Bado nipo hai)
BABA MIGUEL: shut the JamiiForums' Community Engagement Guidelines | Mwongozo wa Ushiriki kwenye Mijadala up, I'm not your dady
(Funga bakuri lako mi sio baba ako)
Wenzangu walicheka sana waliamini naanza kujipendekeza ili nisipitie ule msoto unaoonekana unaendelea eneo lile.
Baba Miguel aliamini mimi ni miongoni mwa wale waliotoroka kwa kua nilionekana kutoridhika kuwepo eneo lile.
Hapa tuligundua kuwa Miguel alitoa taarifa baada ya kuwaua jamaa wale waliokua wanajaribu kumtoroka.
Kila aliepita eneo lile alikua ana niangalia sana mimi kuliko wale wenzangu.
Baba Miguel aliendelea kuita majina kwa kutumia list yake ili kuhakikisha hakuna mtu yoyote alietoroka. Na ilikua ukiitwa jina unasogea mbele na kupewa blanket pamoja na gumboots.
Wote tulipewa vitu hivyo na zoezi liliishia pale, kulichofuata ni kuonyeshwa eneo ambalo tutalitumia kwa ajili ya kulala.
Nitafanya hivyo BossMkuu nitag na mm[emoji2956]
Tunasubiri kwa hamu kubwa huu uandishi ulotukukaKalii sanaa