Utajiri wa nchi ni akili za Watu sio rasilimali kama madini na nyinginezo

Utajiri wa nchi ni akili za Watu sio rasilimali kama madini na nyinginezo

Kwangu mimi tanzania ni Tajiri (rasilimali), lakini watanzania ni masikini. Hapa swali ni tufanyeje ili ku geuza utajiri wa nchi kuwa utajiri wa wananchi. Hapa ndio akili inapoingia.
Lakini pia hata kama ni masikini wa rasilimali ukiwa na akili unaweza ukajenga utajiri wa wananchi wako.
Hivyo cha msingi ni akili lakini utajiri wa rasilimali ukiwa na utajiri wa akili hukupaisha.

Akili hugeuza jangwa kuwa msitu.
Akili hugeuza jiwe kuwa dhahabu,
Akili hugeuza kinyago kuwa mnyama.
Akili hugeuza maji kuwa umeme,
Akili hugeuza pamba kuwa nguo.

Akili humfanya taifa kuvamia mataifa mengine na kuyadhibiti.

Huwezi kuwa na kuitwa Tajiri hata kama unarasilimali kama hauna AKILI.
Malighafi, na viumbe vya asili huitwa Rasilimali zikishapewa value na watu wenye Akili.

Hata Watu huitwa Rasilimali Watu ikiwa watakuwa Productive..

Wanaosema Afrika ni tajiri ni watu wasiofikiri au kutumia Akili vizuri Kwa sababu wanaangalia viumbe hai na viumbe visivyohai Ila Wazungu na mataifa Makubwa Afrika huichukulia masikini tuu Kwa sababu ya watu wake kuwa wajinga
 
Akili hugeuza jangwa kuwa msitu.
Akili hugeuza jiwe kuwa dhahabu...
Kwa ulimwengu wa sasa kuwa na rasilimali ni hatua kubwa kuelekea utajiri wa wananchi kama utatumia akili yako vizuri. Akili lazima ifanyie kazi kitu fulani kugeuza kuwa utajiri wa wananchi. Kwa Tanzania ni natural resources.
 
Kwa ulimwengu wa sasa kuwa na rasilimali ni hatua kubwa kuelekea utajiri wa wananchi kama utatumia akili yako vizuri. Akili lazima ifanyie kazi kitu fulani kugeuza kuwa utajiri wa wananchi. Kwa Tanzania ni natural resources.
Ndugu yangu huo ndiyo mtazamo wa zamani sana kuhusu swali la maendeleo ya binadamu yanaletwa na nini. Tazama historia ya dunia.

Kama huelewi basi jifunze, usibishe. Usipokubali kuwa kuna masuala huelewi huwezi kujifunza. Wala si lazima uelewe kila kitu ndiyo maana binadamu tunazidiana.
 
Mbaya zaidi waliopo juu kwenye uongozi wengi ni weupe mpaka huruma. Unajiuliza kama kiongozi wao yupo hivi wananchi watakuwaje. Tz haina huo utajiri katika nyanja zote iwe ni siasa, maofisini, michezo nk

Mbaya zaidi awamu ya 5 na 6 watu wanaotumia akili hawatakiwi

Mkuu hili tatizo la watu wenye uwezo mdogo kuwa viongozi ni la kihistoria. Wakati Nyerere anachukua nchi wasomi walikuwa ni wachache, hivyo watu wenye elimu kubwa wakawa wanajikita zaidi kwenye kazi za taaluma.

Matokeo yake wasio na elimu wakajikita kwenye siasa. Kidogo kidogo wasio na elimu wakaanza kuwa na maamuzi.

Wasomi walipoamua kuingia kwenye siasa wakakuta wameshachelewa maana wasio na elimu ni mabingwa wa fitina na zengwe.

Hii ndio sababu kwenye siasa zetu hasa ndani ya ccm mizengwe ni njia namba moja ya kupambana.
 
Nakubaliana na wewe 100% maana kuna nchi nimewahi kuishi miaka kadhaa na haina resources ata robo ya zetu ila ukitua tuu airport ndio utaelewa tunaishi dunia mbili tofauti na sio moja....
 
Picha linaanza wakoloni walivyokuja wakagawana maeneo, wazungu/waarabu 10 walimiliki kundi la mababu zetu kama 500 hivi na bado wanateswa balaa sasa kama ni watu timam si mngewaua tuu fasta... tatizo letu kubwa kabisa ni LOW IQ & SELFISHNESS..
 
Kulaumu viongozi ni sawa ila tatizo ni sisi, kwanza viongozi ni reflection ya watu wake maana hatukodi kutoka nje badi ni sisi wenyewe, kama kiongozi umemuweka madarakani lakini akizingua kumtoa huwezi sasa hapo alaumiwe nani kama sio wewe uliemchagua..
 
Yaani leo umegusa mfupa kabisa maana, nilikua nawaza kwa nini Israel ana export matunda mengi kuanzia marekani, south africa, uingereza na kusambaza grapes kwenye viwanda vya wine dunia nzima wakati ana ardhi ndogo lakini kaweza kuhimili kilimo cha umwagiliaji? Basi jibu ni akili
 
Nikawa nawaza kwa nini rafiki yangu mmoja wa German alinishauri ukitaka kuweka akiba kwa afrika usisumbuke na masoko ya hisa maana hayako stable wewe nunua gold kila mwaka weka, baada ya miaka kumi gold inakua imepanda maradufu na utapata faida kubwa kutokana na reserve ya dhahabu
 
Kwa ulimwengu wa sasa kuwa na rasilimali ni hatua kubwa kuelekea utajiri wa wananchi kama utatumia akili yako vizuri. Akili lazima ifanyie kazi kitu fulani kugeuza kuwa utajiri wa wananchi. Kwa Tanzania ni natural resources.

Ukishakuwa na akili inatosha.
Ili kitu kiwe Rasilimali lazima kipewe Value
 
💯
Ndio maana wachumi wanasema rasilimali muhimu ya kwanza ni rasilimali watu
Maana hata nchi mkiwa 61mil kama vichwan hamna kitu mtajikuta mnaongozwa na nchi yenye watu mil 10 tu
 
Yaani leo umegusa mfupa kabisa maana, nilikua nawaza kwa nini Israel ana export matunda mengi kuanzia marekani, south africa, uingereza na kusambaza grapes kwenye viwanda vya wine dunia nzima wakati ana ardhi ndogo lakini kaweza kuhimili kilimo cha umwagiliaji? Basi jibu ni akili

Ukikosa Akili umekosa kitu nyeti na muhimu sana
 
[mention]ROBERT HERIEL [/mention] taikoni leo umeongea issue kubwa sana kwa mfano hapo kwa TMA , wao walifold utabiri wao wakawapelekea wizara zote, hivo kila wizara wanatakiwa wajua wanajipanga vipi, kwa mfano nilitegemea wizara ya kilimo ihamasishe wakulima wasisahau kulima mazao yanayohimili ukame mazao kama viazi vitamu, muhogo, mtama( mweupe na mwekundu) , mahindi yanayochukua siku 90 kuiva, lakini pia wakati wa mavuno wahimize akiba maana wananchi ndio kama hao kama unavosema mtu mwenye akili timamu huwezi kula milo mitatu wakati hauna kazi ngumu za kutumia nguvu, basi tu
 
Kwahiyo Watanzania Wengi Hatuna Akili.?

Je hao Wachache Wenye akili wako wapi?
 
Kwahiyo Watanzania Wengi Hatuna Akili.?

Je hao Wachache Wenye akili wako wapi?

Sasa unaacha ku utilize rasimali ulizonazo unakwenda kutafuta mkopo wa bilioni kadhaa huku umekalia matrillion ya rasilimali, yaani unajua wenzako wanaokunzunguka wanahitaji chakula sana, unaacha kuwekeza kikwelikweli kwenye umwagiliaji wakati una vyanzo vya maji vya kutosha na wewe unasubiri mvua kama wao, hapo unakua na akili au mwendawazimu
 
Kwahiyo Watanzania Wengi Hatuna Akili.?

Je hao Wachache Wenye akili wako wapi?

Wewe umeambiwa kutakua na ukame na nishati kama umeme unategemea maji na kila mwaka unalia kuna ukame yaani haujaona vyanzo anuwai kama upepo, makaa ya mawe, gesi ukatumia kuzalisha umeme wa kukutosha na mwingine ukauza? Yaani kila mwaka unalia tatizo lilelile bado hata kama ni kiongozi useme una akili wakati kutatua changamoto umeshindwa miaka yote
 
Ukishakuwa na akili inatosha.
Ili kitu kiwe Rasilimali lazima kipewe Value
Tuna natural resources ambazo zina demand na kwa hiyo zina value na tunaweza kuziongezea value. Nisemacho ni kuwa kama tuna akili tutazifanyia kazi ili tujinufaishe.
Asiye kuwa na natural resources atatafuta mbinu nyingine.
 
UTAJIRI WA NCHI NI AKILI ZA WATU, SIO RASILIMALI KAMA MADINI N.K.

Anaandika, Robert Heriel.

Huwaga namshangaa mtu anayesema nchi yetu ni Tajiri. Kwa kweli sio tuu anachekesha Bali pia anaonyesha jinsi alivyokuwa mjinga na asiyeweza kufikiri sawia.

Kama nikiulizwa hivi leo sababu gani inatufanya Waafrika ikiwemo nchi yetu kuwa Masikini, basi jibu litakuwa ni kuwa Sisi tunaakili ndogo Kama sio kuwa hatuna Kabisa.

Taifa ili kiwe Tajiri linahitaji watu wenye akili zaidi kuliko Rasilimali. Utajiri ni Akili na sio wingi wa Rasilimali.
Kuna msemo usemao, penye miti hapana wajenzi.

Akili ndio inaweza kufanya madini kuwa Rasilimali Kwa kuipa Value. Madini kama madini hayajui kama yenyewe ni yathamani, Ila wenye akili ndio wanajua thamani ya madini hayo kutokana na matumizi waliyoyabuni kwayo.

Kidunia Bara la Afrika ndilo bara lenye malighafi nyingi kuliko bara lolote lile. Lakini watu wake wameshindwa kuzigeuza malighafi hizo kuwa Rasilimali Kwa kuzipa thamani.

Ukisikia mtu anakuambia Yeye ni Tajiri Kwa sababu nchi yake inamadini, maziwa na Mito, Ardhi yenye Rutuba, wanyama wa kuvutia, na mambo mengine lakini watu wake ni Hali zao za maisha ni duni jua mtu huyo hajui kufikiri vizuri, na pengine akawa mwendawazimu.

Nchi haiwezi kuwa Tajiri Kama ndani yake inawatu wajinga wengi. Watu wasio na akili wakiwa wengi ndivyo nchi inavyozidi kuwa Masikini.

Mtu asiye na akili Hana tofauti na mnyama wa porini, ni Sawa na tumbili au ngedere anayeishi msituni ananyeshewa mvua na kuchomwa na Jua lakini anashindwa kujenga nyumba hata ya mbao Kwa sababu ya upeo mdogo wa Akili.

Wazungu walivyotuita Waafrika manyani kuna watu walifikiri walimaanisha maumbile yetu yanafanana na nyani[emoji3][emoji3] Kama nawe ulifikiri hivyo basi nawe upo kundi la watu wajinga.

Wazungu walituita manyani mbali na ubaguzi wao lakini walituona akili zetu hazijaachana Sana na tumbili na nduguye ngedere.

Nyani au ngedere ukimpelekea Dhahabu au Almasi wala hataiona inatofauti na jiwe jingine. Kutokana na upeo mdogo wa Akili.

Sisi Watanzania wengi wetu tunaakili ndogo mno na hiyo ndio sababu Sisi sio matajiri. Na tutaendelea kuwa Vivi hivi Kwa Karne kadhaa zijazo.

Watanzania wengi ni Kama wanyama Kwa mambo mengi, kama unavyomuona ng'ombe basi ndivyo wengi wetu tulivyo.

Sio ajabu ukakuta watu kwenye makazi Yao kuna mavi au maji machafu waliyoyasababisha yamewazunguka, yananuka na nzi wamejaa lakini wao hawaoni Shida. Wanalala, wanakula hapohapo, na wanakunya na kukojoa hapohapo.

Hapo ati wanasubiri kiongozi aje awaambie wawe wasafi tena wengine ifikie hatua ya kupelekwa serikali za mitaa kisa anaambiwa asizibue chemba za mavi yake na familia yake, come on!

Sio ajabu jitu linakunya chooni labda cha umma alafu hali-flash uchafu wake. Hivi mtu huyo anatofauti ipi na Mnyama?

Mtu anajua kabisa ili aishi anatakiwa awe na chakula cha kutosha kinachomtosha yeye na familia yake, badala awe na ghala la kuhifadhi chakula kinachomtosha yeye na watoto wake angalau Kwa miaka miwili kulingana na Hali ya hewa.

Yeye anakula Kama mnyama asijue kesho atakula nini. Halafu ikifika kesho anaanza kumlalamikia mtu mwingine labda ni serikali au viongozi. Jamani hivi tunaakili kweli?

Tena wakati mwingine tunazidiwa akili hata na Wanyama.

Hakuna mnyama ambaye atazaa watoto ambao hawezi Kuwatunza. Hakuna na hajawahi kutokea. Mfano Kuku anaouwezo wa kutaga mayai hata Mia moja.

Lakini atataga mayai kumi (10-12) kulingana na uwezo wake wakuyaatamia, sio atage mayai 20 alafu wakati wa kuatamia mengine ashindwe kuyaatamia yajitokeze nje.

Kisha Kwa mayai 10-12 anaouwezo wa kuwachunga na kuwakuza watoto hao.

Halikadhalika na mbwa, ng"'ombe, mbuzi, Simba n.k.

Lakini Sisi unakuta mtu anazaa watoto nje ya uwezo wake wa Kuwatunza, labda watoto 10 alafu ananilaumu serikali kuwa gharama za Shule au hospitali ziondolewe.

Au anaomba msaada Kabisa wa kusaidiwa kulelewa watoto.

Hivi tumelogwa au ni kitu gani?

Mtu unajua kabisa miti ndio huleta hewa Safi, huleta mvua na kivuli kizuri, na Kupunguza joto la nchi. Alafu unakuta watu wamekata miti mtaa mzima ili wajenge nyumba.

Unashangaa mtaa mzima miti ipo 20 Kwa eneo la kilometa moja. Alafu muda huohuo unasikia mwehu akipiga kelele jamani joto Kali, jamani jua linawaka! Mara kiyama kinakaribia.

Kiama ya mavi. Ujinga na wehu wako ndio unaita Kiyama?

Utajiri WA nchi ni akili za watu na sio Rasilimali Kama madini.

Chakufanya;
I. Tujifunze kuwa na Akili ili tuwe nchi yetu itajirike.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Umemaliza kila kitu
 
Ndugu yangu huo ndiyo mtazamo wa zamani sana kuhusu swali la maendeleo ya binadamu yanaletwa na nini. Tazama historia ya dunia.

Kama huelewi basi jifunze, usibishe. Usipokubali kuwa kuna masuala huelewi huwezi kujifunza. Wala si lazima uelewe kila kitu ndiyo maana binadamu tunazidiana.
Ni muhimu kuangalia una nini wakati unatafuta maendeleo na kwa nchi kama tanzania natural resources ni muhimu. Hivyo hizo akili zinatakiwa zije na njia ya kuleta maendeleo kwa kutumia hizi resources.
 
Back
Top Bottom