Lovelovie
JF-Expert Member
- Oct 2, 2021
- 12,582
- 26,053
Hilo ni yeye mwenyewe na dada zangu mim hapo nakaa pembeni kabisa.Vipi akiamua kutest mitambo yote miwili atapewa?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hilo ni yeye mwenyewe na dada zangu mim hapo nakaa pembeni kabisa.Vipi akiamua kutest mitambo yote miwili atapewa?
My name is Frank and the meaning of Frank is true 😂😂😂Hilo ni yeye mwenyewe na dada zangu mim hapo nakaa pembeni kabisa.
Lucha hatari sana anza na hiiUtajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 20.
Nilikuwa nina maswali kichwani mwangu zaidi ya elfu moja na ambayo hayakuwa na majibu.Iliwezekana vipi mwanamke ambaye hakuwahi kabisa kufika kwangu hata mara moja leo aje tena kwa hoja ya kwamba ameelekezwa kwa kuulizia ulizia?Je,alimuuliza nani huyo ambaye ananifahamu pale mwisho wa lami?Pili,inakuwaje Farah afanane kiasi kile na Zahra/Maya?,sawa yawezekana wangefanana kama ndugu wa tumbo moja,lakini je hadi mchoro mkononi?,kiukweli kwangu ilikuwa ni kama sinema ambayo sikuielewa hata kidogo.Kwakuwa Ally Mpemba amewahi kuniambia Farah ni dada yake,nilidhani uenda Farah na Maya wakawa ni mapacha kwasababu pia Ally aliniambia Maya/Zahra alikuwa ni dada yake pia.
Baada ya kuingia kwenye gari niliiwasha na kuanza kuiondoa taratibu kuelekea Magomeni.Sikutaka kabisa kukaa kimya,niliona niendelee kumdodosa Aunt Farah ili niweze kuufahamu ukweli!.
Mimi "Kwahiyo dada umekuja unaulizia?"
Farah "Mbona unakuwa na mashaka sana leo?,kwanini?"
Mimi "Hapana dada sina mashaka ila nauliza tu!"
Farah "Wewe hukuwahi kumwambia Ally unakaa Gongo la mboto mwisho wa lami?"
Mimi "nimewahi kumwambia lakini kaka Ally pia hajawahi kufika kwangu".
Farah "Nilipofika hapo mwisho wa lami nimeulizia nikaelekezwa"
Mimi "ooh sawa"
Kiukweli sikutaka kumbishia maana niliona uenda tungekwazana kwasababu sababu alizokuwa akinipa zilikuwa haziniingi akilini hata kidogo,nilijua kabisa alikuwa akinidanganya,pale mwisho wa lami mahali nilipokuwa nikikaa mimi kulikuwaga hakuna watu ninaofahamiana nao sana uenda jamaa mwenye duka pale nje,pia kwa mazingira yale isingekuwa rahisi mtu kumifahamu kwasababu nilikuwaga si mtu wa kujichanganya na ndiyo maana nikasema uenda ningekuwa maarufu pale mtaani hapo angenishawishi kwa ule uongo wake laki kiukweli sikukubaliana naye hata kidogo.Niliamua kukausha tu ili mambo mengine yaendelee maana niliona nikiendelea kulifuatilia hilo suala sana kiundani uenda ningeibua mambo mengine.
Mimi "Dada nikuulize swali?"
Farah "Karibu"
Mimi "Kwenu mmezaliwa wawili tu na Kaka Ally?"
Farah "Kwanini?"
Mimi "Nimeuliza tu maana mara zote nawaona nyie tu"
Farah "mmh! hapana tupo wengi"
Aliendelea "Wengine hawakai hapa Bongo"
Mimi "Kwahiyo kwa hapa Bongo upo wewe na kaka Ally tu!"
Farah "Hapana wapo wengine!"
Mimi "ooh sawa!"
Niliamua kukaa kimya sikutaka kabisa kuendelea kuuliza maswali mengi kwakuwa hata yeye pia niliona ananijibu kishingo upande hivyo nikaona nisiingie ndani sana ijapokuwa maswali nilikuwa nayo mengi sana.Sasa kichwani mwangu nilipanga ya kwamba,usiku wa siku hiyo nikamtazame vizuri Maya atakapokuwa akila chakula chake pale sebuleni ili kujiridhisha maana kiukweli walikuwa wakifanana kila kitu na Farah.
Baada ya kufika Magomeni kwenye nyumba ya Ally Mpemba,nilifungua geti na ile gari kuiingiza hadi ndani kwenye sehemu ya kuegeshea.Nilishuka kwenye gari nikaenda kumchukulia ndani funguo ya gari dada Farah ambaye wakati huo alikuwa nje akinisubiri.Baada ya kumpatia ule ufunguo akawa amechukua mkoba wake akatoa shilingi milioni 2 akanipatia.
Farah "Hela hizi hapa"
Mimi "Nashukuru dada"
Hakuchukua muda akaingia kwenye ile Range.Nilisogea nikamfungulia geti akawa ametoka na kuondoka.Sikutaka kabisa kupoteza muda hapo nyumbani niliondoka zangu hadi sokoni kwenda kununua mahitaji ya chakula cha Maya,niliwasha gari nikawa nimetoka zangu kuelekea soko la Ilala,kiukweli wakati huo nilikuwa nimenawiri sana na nilikuwa nanyuka pamba za ukweli,ulevi wangu mkubwa ulikuwa ni kupendeza kwa kuvaa vizuri.
Sasa kuna mahali nilifika nikapaki ile gari kisha nikashuka kuelekea sokoni kununua mahitaji,wakati nikiwa nanunua mahitaji kwa mama mmoja,ghafla nikasikia sauti ya mwanamke mmoja ambaye ilinifanya nikageuka kumtazama,hadi leo sijajua ni kitu gani kilitokea ila huwa najiuliza maswali mengi sana.
Huu ulimwengu hauko kama mnavyodhani ndugu zangu,kuna muda unaweza kuwaona watu wanapendeza na kuishi maisha bora ukadhani ni rahisi lakini si hivyo!,mimi baada ya kupitia mambo hayo machache ndiyo maana leo napambana kwa nguvu zangu kufa na kupona ili kujipatia riziki,sasa kuna watu nikiwaambia mimi ni naendesha bodaboda huwa hawaamini wanadhani natania,japokuwa pia najaribu kuwekeza kwenye kilimo lakini bodaboda hiyo hiyo ndiyo inanipatia pesa ya uwekezaji huo!.Niliamua kupambana na maisha yangu ya udundulizaji kwasababu hakuna maisha ambayo sijapitia,kila baya na jema nishaona,hivyo niliamua kutulia kujipambania,huko mbele mtaelewa vizuri ni kwanini leo naendesha bodaboda.
Sauti ya kike "Mama Eliya nikuletee?"
Mama Eliya "Leo sina hela mwaya!"
Huyo mama Eliya alikuwa ni mama ambaye nilikuwa nimesimama mbele yake nikuchukua kabeji,sasa wakati akiwa kwenye pilika pilika za kunirudishia chenji ndiyo nikawa nimesikia hiyo sauti ikimwambia hivyo,baada ya kumtazama yule mwanamke aliyemuita mama Eliya kiukweli nilibaki nikimtizama.Kiukweli baada ya yule mwanamke kumuita huyo mama niliyekuwa nikinunua mboga kwake nilijikuta tu nageuka kumtazama ni nani na nilipogeuka nilijikuta namtamani baada ya kumtazama,hakuwa mwanamke mbaya,alikuwa ni mwanamke mmoja wa kawaida ila alikuwa na umbo zuri sana.
Mimi "Anauza nini huyo?"
Mama Eliya "Anauza Juisi"
Mimi "Ni nzuri?"
Mama Eliya "Juisi yake huwa tamu kweli sema leo tu ndiyo hali ngumu ila ningechukua"
Mimi "Anauza bei gani?"
Mama Eliya "Anapima kwenye glasi shingi elfu moja"
Mimi "Mwambie akupe"
Mama Eliya "Ahsante mwanangu"
Aliendelea "Nitakunywa baadae "
Mimi "Mwambie aje akupe kabisa maana nyie huwa wajanja,nitakupa hela utaisunda huta nunua,nataka na yeye umuungishe kama mimi nilivyokuungisha"
Baada ya kumwambia hivyo yule mama muuzaji alianza kucheka sana.Nia yangu ilikuwa ni kwamba amuite yule mwanamke asogee kwa karibu nipate kumtazama vizuri maana alikuwa bize na juisi yake na kwangu isingekuwa rahisi kumsimamisha pale sokoni na kuanza kuzungumza nae kwasababu mara zote nimekuwa na aibu kusimama na mwanamke machoni pa watu.
Mama Eliya "Wala usijali baba namuungisha"
Aliendelea "Wewe Ray......Raaaaaay niletee juisi nimepewa ofa"
Baada ya kuita yule mwanamke alijongea taratibu hadi pale nilipokuwa nimesimama kwa mama Eliya.
Mama Eliya "Niwekee glasi moja nimepewa ofa na mwanangu"
Mimi "Mama wewe kunywa hadi utosheke sijakupa ofa yenye kikomo"
Mama Eliya "Mmh nashukuru baba"
Nilifahamu kabisa mama Eliya anaweza kuwa anauhitaji na pesa ndiyo maana ile ofa ni kama alitamani asinywe ili ile hela achukue,sasa mimi nilipanga kumpatia kiasi kidogo kitakachomsaidia.
Mimi "Jusi yako unatengeneza na nini?"
Muuza juisi "Ni mchanganyiko wa Embe,pasheni na parachichi"
Mimi "Ok"
Muuza juisi "Nichangie basi kaka"
Mimi "Haina shida wala usijali,nimepaki gari pale ng'ambo naomba twende ili ikiwezekana nitafute chombo uniwekee"
Muuza juisi "Ninazo chupa kaka"
Mimi "Mbona hapa sizioni?"
Muuza juisi "Kuna mahali nimeziweka nakimbilia mara moja"
Mimi "Ni safi?"
Muuza juisi "Ni safi kaka huwa naziosha na maji moto"
Aliendelea "Au kama hutoridhika basi unywee hapa kaka"
Mimi "Usijali nitanunua"
Basi baada ya mazungumzo mafupi nilimpatia yule mama noti ya shilingi elfu kumi kama malipo ya juisi na itakayobaki achukue yeye,kiukweli alinishukuru sana na nilimwambia wakati wote nitakapokuwa naenda hapo sokoni kununua bidhaa ningekuwa namtafuta yeye.
Niliondoka nikaongozana na yule dada muuza juisi kuelekea nilikokuwa nimepaki gari,mimi nilikuwa mbele na yeye alikuwa nyuma yangu huku mkononi akiwa ameshika galoni ya juisi na kapu la vikombe.Tulipofika nilifungua gari kisha nikamwambia animinie kwenye glasi ili ninywe kwanza niisikie radha yake.
Mimi "Ni tamu"
Mimi "Unaitwa nani?"
Muuza juisi "Naitwa Rehema"
Mimi "Unaishi wapi Rehema?"
Yeye "Naishi Ubungo msewe?"
Mimi "Ubungo msewe iko maeneo gani?"
Yeye "Pale pale Ubungo ni jirani na chuo kikuu"
Mimi "ooh,duuu mbona kama mbali?"
Yeye "Wala hata siyo mbali"
Mimi "Unaona siyo mbali kwasababu ushazoea"
Mimi "Kwahiyo kila siku unamaliza hiyo galoni?"
Yeye "Inategemea,kuna muda nauza hizi galoni hata tatu na kuna siku hata moja haiishi"
Mimi "Ok"
Mimi "Umeolewa?"
Yeye "Sijaolewa ila nina mtu wangu"
Mimi "Mnaishi wote?"
Yeye "Hapana,mi naishi kwa shangazi na yeye anaishi kwao!"
Mimi "Kwahiyo ndiyo umepanga aje awe mume wako?"
Yeye "Hayo sasa ni maajaliwa ya Mwenyezi Mungu"
Mimi "Kwenu anafahamika?"
Yeye "Anafahamika kwasababu ninaye mtoto wake!"
Mimi "Unaye mtoto wake kivipi?"
Yeye "Nimezaa naye "
Mimi "Mbona sasa mimi nakupenda Rehema"
Yeye "Kunipenda wala siyo dhambi kaka,dhambi ni kumtamani mke wa mtu"
Mimi "Mimi sijakutamani Ray mimi nakupenda"
Yeye "Toka lini mwanaume wa Dar akapenda mwanamke?,wewe sema umenitamani tu ili unipate umalize haja zako unikimbie,nyie wanaume hata sinaga hamu kabisa na nyie!"
Mimi "Hebu tuachane na mambo mengi Ray nipe namba yako ya simu nitakupigia"
Yeye "Simu yangu inasumbua betri nimeiacha nyumbani"
Mimi "Mimi nitakupataje ili tutafute mazingira mazuri tuzungumze"
Yeye "Mimi napatikana tu hapa hapa wewe ukija utamuuliza mama Eliya"
Mimi "Lakini umeelewa nilichokwambia Ray?"
Yeye "Lakini nishakwambia ninaye mtu wangu!"
Mimi "Kwani utamwambia?"
Yeye "Siyo hivyo,kumbuka penzi ni kama kikohozi huwa alijifichi!"
Aliendelea "Halafu unataka kuniambia wewe huna mtu?"
Mimi "Ningekuwa na mtu unadhani ningekusumbua?"
Yeye "Mimi nitajuaje!,nyie wanaume kwani mnaaminikaga?"
Mimi "Kwahiyo hata huyo jamaa yako pia humuamini?"
Yeye "Simuamini ndiyo,kwani anapokaa huko ninakuwa nae?"
Mimi "Siko kama unavyodhani Ray"
Yeye "Sawa,ushamaliza kuniongopea?,mi nataka niwahi kwenye biashara"
Mimi "Sikuongopei ila amini hivyo"
Yeye "Sawa ukiwa na shida basi utanitafuta napatikana hapa hapa sokoni"
Baada ya mazungumzo yale na yule mwanamke ambaye alionekana na msimamo,nilimpatia noti ya shilingi elfu kumi akawa anataka kunirudishia chenji nikamwambia hiyo nimempatia tu.
Yeye "Ahsante"
Yeye "Ila nimesahau kukuuliza jina lako!"
Mimi "Mimi naitwa Umughaka"
Yeye "Sawa nashukuru kukufahamu Umungaka"
Mimi "Siyo Umungaka,ni Umughaka!"
Yeye "ahahahaa nisamehe jamani unajina gumu,sijui kama nitaweza kulitamka"
Mimi "Kesho nitakuja kukucheki"
Yeye "Saa ngapi sasa ili niwe maeneo jirani?"
Mimi "Mida kama hii"
Yeye "Sawa,msalimie wifi "
Mimi "Wifi tena!"
Yeye "Utakubali sasa!?"
Aliendelea "Haya basi tutaonana!"
Yule mwanamke aliondoka huku namtazama namna alivyokuwa na nyama za kutosha,kiukweli alikuwa mwanamke fulani wa kawaida ila umbo lake halikuwa la kawaida,mara zote ugonjwa wangu kwa wanawake umekuwa ni uleule wa matako makubwa wastani na hips za kuzugia,mara zote huwa sihangaiki na sura kwasababu si sehemu ya hitaji langu kubwa kwa mwanamke,huwa naangalia vinavyo nihusu na visivyo nihusu naachana navyo.
Nilielewa ni kila mwanamke ukijaribu kumtongoza ni lazima akwambie anaye mtu wake ili kujipa thamani lakini mara zote huwa haiko hivyo,hata Rehema nilifahamu kabisa ili ajipe thamani ni lazima angeniambia anaye mtu ingawa nilipomtazama macho yake ilionekana kabisa anasema uongo.
Niliwasha mchuma nikaondoka zangu kuelekea Magomeni kupeleka zile bidhaa na baada ya kufika kama kawaida niliziweka pale mezani kisha nikafunga mlango nikaondoka zangu,sasa kwakuwa ilikuwa bado mapema,nilirudi hadi pale nilipokuwepo mwanzo kwa ajili ya kuendelea na makamuzi ya bia.Muda uliposogea niliamua kuondoka kuelekea magomeni ili kuweza kuufungua mlango wa Maya,nilipofika nilipaki lile gari kisha nikaingia ndani nikafungua mlango wa kwenye kile chumba cha Maya kisha nikauacha wazi nikatoka zangu nje.
Kwakuwa nilikuwa nimeshiba,niliingia kwenye ile gari nikafunga mlango nikawa nasubiri mida mida ifike ili niweze kumtazama Maya kwa uzuri ili kujiridhisha.Mpaka wakati huo sikuiona simu ya Ally Mpemba wala nini!,niliendelea kusubiri nikidhani angenipigia kama alivyokuwa ameniahidi lakini haikuwa hivyo.
Ilipofika mida ya saa 3 usiku nilianza kusikia yule kiumbe Maya akitafuna kile chakula chake kwa sauti kama mara zote ambavyo huwa akifanya.Nilifungua mlango wa gari taratibu kisha nikasogea hadi dirishani ambako kungeniwezesha kumtizama vizuri kwakuwa nilikuwa nimewasha taa na kufungua lile pazia.Nilisogea hadi pale dirishani kisha nikaanza kumtizama kwa makini sana,sasa wakati namtizama yeye alikuwa amenipa mgongo,nilijaribu kumuangalia kwa umakini mkubwa sana na kiukweli walifanana kila kitu na Faraha,kuanzia urefu hadi umbo,ile alama ya mkononi nilijaribu kuitazama lakini sikuweza kuiona kwakuwa muda wote mikono alikuwa ameshika chakula chake akiendelea kula,hivyo kufanya nisiweze kuitazama vizuri,sasa wakati nikiwa namtazama aligeuka ghafla kama mtu ambaye alihisi kitu akawa anaangaalia pale dirishani huku akiacha kutafuna kwa mshangao,nilisogea pembeni ili asinione,baada ya muda nilipochungulia pale sebuleni sikuweza kumuona tena akawa amendoka.Nilirudi zangu kwenye gari nikiwa najiuliza sana maswali mengi,kumbuka pamoja na mambo yote ikiwemo kulala na Maya lakini ni kiumbe ambaye sikupaswa kumzoea na hakuzoeleka.
Ilipofika mida ya saa 5 usiku nilisikia honi ikipigwa getini na ilikuwa ni honi ya lile gari alilokuwa amechukua Farah,niliondoka nikaenda kumfungulia geti kisha akawa ameingiza gari ndani.Aliposhuka kwenye ile gari akawa ameniambia anahitaji kuingia ndani kwenda kujisaidia.
Mimi "Habari za huko dada"
Farah "Nzuri,ndiyo narejea!"
Aliendelea "Nilidhani uenda nisingekukuta ila nimewasiliana na kaka Ally ameniambia upo"
Aliendelea "Ngoja nijisaidie kidogo nimebanwa"
Nilitaka kumzuia asiingie ndani lakini nilishindwa kumzuia kwasababu nilifahamu kabisa ni ndugu yake na Ally Mpemba pia walitoka kuongea muda si mrefu.Hapo awali Ally Mpemba aliwahi kuniambia sipaswi kabisa kumruhusu mtu yeyote kuingia ndani ya ile nyumba yake hata akiwa ndugu yake,kitu alichoniambia Ally Mpemba ambacho naweza kufanya ni kuruhusu ndugu zake tu kukalia kiti cha mbele kwenye gari aliyokuwa amenipatia kupigia misele lakini mtu mwingine hakuruhusiwa.
Sasa kabla hata sijamwambia chochote,nilishitukia kufungua mlango na kuingia ndani,kitu cha ajabu wakati Maya amemaliza kula nilikuwa bado sijasafisha pale sebuleni na mara zote huwa nasafisha asubuhi,sasa nilitaka kumwambia Farah atumie choo cha nje ili asingiingie ndani ambako kungeleta taharuki,niliingia ndani pale sebuleni lakini sikumuona Farah nikiamini uenda alikuwa ameingia chooni,nilianza kusafisha ile meza na pale chini kwa haraka,kabla hata sijamaliza nilimuona anafungua mlango wa chumba cha Ally na kutoka,kilichonishangaza zaidi ni kwamba ule mlango nilikuwa nimeufunga na funguo na funguo mara zote zilikuwa zinakaa kwenye kimeza cha luninga,nikajaribu kuzitazama funguo nikakuta zipo pale kwenye kimeza,sasa nikawa najiuliza ule mlango sikuufunga?,na kama nisingeufunga zile funguo zisingechomoka pale mlangoni!,na kwanini ameingia kwenye chumba cha Ally akashindwa kwenda chooni ambako vyoo vilikuwa vinajitegemea?.
Kiukweli hofu ilianza kuniingia na kwakuwa nilikuwa mtu mzima nilitambua fika yawezekana Farah hakuwa mtu wa kawaida.
Farah "Mimi nakwenda!"
Mimi "Sawa dada nikusindikize?"
Farah "Hapana"
Mimi "Sawa dada usiku mwema tutaonana kesho"
Farah "Panapo majaaliwa"
Baada ya kuondoka Farah kiukweli sikuelewa ile hali.
Itaendelea....................
LuchaUtajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 22
Aliendelea "Nakuuliza wewe,mbona upo kimya!?"
Mimi "Kaka kwani kuna nini?"
Ally Mpemba "Hujui ulichokifanya?"
Mimi "Kaka nipe nusu saa tuongee maana sipo salama kuzungumza!"
Baada ya kumwambia vile akawa amekata simu kwa jazba na kufyonza,nilitaka angalau nitoke nje niende hata kwenye gari nikazungumze na kaka Ally kwakuwa hadi muda huo sikuwa nimelielewa kosa langu hasa lilikuwa ni nini!.Niliamka nikaelekea kuoga kisha nikawa nimevaa vizuri nijiandae kutoka lakini Rehema nae akawa amesema nimsubiri akaoge kisha nimsindikize aondoke.Baada ya Rehema kumaliza kuoga alivaa nguo yake nzuri ya kitenge kisha tukawa tumetoka nje na kuondoka,sasa tulipofika kwenye gari,Rehema alishika kitasa cha mlango wa Mbele akawa amejiandaa kuufungua na kuingia ndani nilikumbuka maneno ya Ally Mpemba na nikamuwahi haraka nikawa nimemwambia asikae kiti cha mbele kwakuwa ni kibovu lakini ni kama hakunielewa na alidhani uenda ninamkataza kukaa mbele kwakuwa sitaki wanawake zangu wamuone.
Rehema "Wewe sema tu hutaki wanawake zako wanaione huna lolote"
Mimi "Kweli baby hicho kiti cha mbele huwa ni kibovu"
Rehema "Nshakwambia wewe sema hutaki wanawake zako wanione tu basi inatosha,mbona jana hukuniambia hivyo na tumekuja wote nikiwa nimekaa mbele! au kwasababu ilikuwa usiku ?"
Baada ya kuniambia jana usiku alikaa mbele ndipo nilizidi kuchanganyikiwa kabisa,sikutaka kumuonyesha nimeshituka ili asije kunishangaa,kiukweli hakuna siku niliyo ichukia pombe kama siku hiyo,kumbe baada ya kunywa bia kadhaa pale Tabata ukichanganya na kuchanganyikiwa kwa penzi jipya nikawa nimejisahau kabisa kwamba Ally Mpemba aliwahi kuniambia asije akatokea mtu yeyote akakaa kwenye siti ya mbele ya ile gari isipokuwa ndugu zake,sasa baada ya Rehema kuwa ameniambia vile ikabidi nimruhusu tu aendelee kukikalia kile kiti ili apunguze wivu kwakuwa kama ni kosa lilikuwa lishatokea.
Mimi "Basi baby kaa ili usinifikirie vibaya"
Rehema "Akuu wewe twende mi nitakaa nyuma nisije kukuletea shida kwa wanawake zako"
Mimi "Hapana baby kaa mbele twende maana ushanzaa nifikiria vibaya"
Baada ya kumbembeleza kidogo Rehema alifungua mlango wa mbele na kuingia ndani,niliwasha gari na kuondoka kuelekea Ubungo kumrudisha Rehema kwao;wakati tukiwa njiani nilikuwa nikimwambia kile kiti anakisikiaje ili kuendelea kutetea pointi yangu ya ubovu wa kiti asiendelee kunifikiria vibaya.
Mimi "Hausikii hicho kiti kama kinacheza?"
Rehema "Hapana,mbona mimi sisikiii?"
Mimi "Duuuu!..,nikishika kwa mfano breki mi naona kabisa kinaenda mbele na nikiachia kinakuwa kama kinarudi nyuma,wewe huwezi kuona "
Mimi "Nadhani baadae itanibidi niipeleke gereji warekebishe"
Maneno yote hayo ilikuwa ni kumfariji Rehema tu ili asinifikirie vibaya kuhusu maneno yangu yale ya uongo.Baada ya kumfikisha Rehema pale Ubungo nilimuachia na hela kiasi kwa ajili ya matumizi yake ya kawaida kisha nikaondoka zangu kuelekea Magomeni kwa Ally Mpemba.Nipofika nilifungua geti na kuiingiza ile gari ndani,nilishukaka nikaelekea kuufungua mlango na kuingia ndani ya nyumba.
Vile vyakula vya Maya vilikuwa pale sebuleni kama kawaida kwakuwa usiku ule hakuwa amekula na mimi sikutaka kabisa kuvitoa nikawa nimeacha palepale,nilikaa kwenye sofa pale sebuleni nikawa ninatafakari kwa kina jambo ambalo nilikuwa nimelifanya na kiukweli nilijuta sana na niliona kabisa naweza kukosana na Ally Mpemba hivi hivi!.Nijitahidi sana kuilazimisha furaha lakini moyoni mwangu tayari kulikuwa na majonzi makubwa mno.Baada ya masaa mawili kupita nikiwa naendelea kutafakari yaliyotokea,Ally Mpemba akanipigia simu tena na bado alionekana kukasirishwa na kukerwa kwa kile kitendo,kiukweli jamaa sikuwahi kumuona akiwa mkali kiasi kile.
Ally Mpemba "Nikwambia tangu mwanzo uwe makini lakini naona unataka kunitia kwenye umasikini,mimi siwezi kukubali kaka hiyo itakugharimu sana"
Mimi "Nisamehe sana kaka najuta kwa nilichokifanya"
Ally Mpemba "Mimi nikusamehe kama nani?,uliyemkosea yupo na ndiye mwenye mali unapaswa kumuomba msamaha"
Aliendelea "Umenikwaza sana Master pamoja na kukuamini lakini kumbe wataka kunirudisha kwenye umasikinik,aiseee wewe ni mtu mbaya sana"
Mimi "Kaka nilipitiwa tu nisamehe"
Ally Mpemba "Hebu kamuombe msamaha haraka kaka usije niletea matatizo!"
Kwakuwa nilifahamu kabisa kile kitendo nilichokuwa nimekifanya kilikuwa kimemkwaza Maya,moja kwa moja baada ya kuzungumza na Ally,nilichukua fungua nikausogelea mlango wa chumba cha Maya kisha nikaufungua na kuingia ndani,nilipoingia ndani sikutaka kabisa kuufunga ule mlango kwani niliogopa na nikaona ishu ikiwa ngumu basi mimi ni kutoka nduki!.
Nilipofika ndani nilianza kuongea kwa sauti ya upole na majuto ili kuonyesha nimefanya kosa na nalijutia.
Mimi "Nimekuja mbele yako Maya nakuomba unisamehe sitorudia tena!"
Mimi "Maya nakuomba unisikie na unisamehe kwa kitendo nilichokifanya na sitorudia tena"
Wakati naongea hivyo lile kabati ambalo ni kama mlango wa kuingilia kwenye lile shimo alimokuwa anakaa Maya lilikuwa limefungwa na ndipo nikaanza kusikia sauti za kilio cha kwikwi,kile kilio kilianza taratibu lakini kadiri dakika zilivyosogea ndipo nacho kilikuwa kikiongezeka.Mimi sikukata tamaa hata kidogo,niliendelea kumuomba msamaha lakini bado sikuona majibu.
Baada ya muda niliona ule mlango wa kabati ukifunguliwa na Maya akawa ametoka,kiukweli alikuwa amekasirika sana tofauti na mwanzo nilivyowahi kumuona,sikuwahi kumuona akiwa amejaa sumu kiasi kile huku machozi yakiwa yanamtoka,alisimama akawa ananiangalia huku akitetemeka kwa nguvu na kutoa sauti kama Nguruwe.Kile kitendo kiliniogopesha sana na nikaona naweza kupoteza maisha kimzaha mzaha,niliondoka kwenye kile chumba nikawa nimekimbilia sebuleni kwenye mlango wa kutokea nje,nilisimama pale mlangoni nikiendelea kuangalia hali itakuwaje na kama hali ingekuwa mbaya zaidi nilipanga kutoka nduki kuelekea nje.
Nikiwa nimesimama pale mlangoni Ally Mpemba akanipigia simu tena.
Ally Mpemba "Ushamuomba msamaha?"
Mimi "Ndiyo kaka nishamuomba msamaha lakini naona hajibu yupo kimya?"
Ally Mpemba "Yupoje?"
Mimi "Yupo vile vile tu kaka uchi"
Ally Mpemba "Nachotaka kufahamu yeye yupoje?,analia au anacheka?"
Mimi "Analia tu kaka na kutetemeka!"
Ally Mpemba "Hebu funga hiyo nyumba na uondoke haraka kuelekea Unguja,naomba ufanye haraka vinginevyo sitokuwa na huruma na wewe!"
Mimi "Kaka Unguja au Chumbe?"
Ally Mpemba "Usiendelee kupoteza muda hapo nimekwambia funga nyumba uondoke kwenda Unguja kwa Sheikh"
Mimi "Sawa kaka naondoka"
Ally Mpemba akawa amekata simu kwa jazba sana,Kiukweli jamaa alikuwa amechukia sana na ndipo sasa niliiona sura halisi ya Ally Mpemba akiwa amechukia namna anavyozungumza kwa ukali,mara zote nilikuwa nikimchukulia poa kumbe haikuwa kama nilivyodhani,niliondoka nikawa nimeenda kupanda daladala zilizokuwa zinaelekea posta maeneo ya bandari ili niwahi kuelekea Unguja kama alivyokuwa ameniambia Ally.Nilifanikiwa kuondoka mida ya saa 9 alasiri kuelekea Unguja ambapo baada ya kufikia kuna jamaa nilikuta ananisubiri na ndiye aliyeniepeleka hadi Chumbe kwa mzee yule ambaye nimewahi kwenda kwake nikiwa na Ally Mpemba.
Baada ya kufika pale hatukumkuta na jamaa yeye akawa ameniacha akaondoka,kuna mwanamke ambaye alikuwa mke wa mzee akawa amesema ametoka na hivyo ikabidi nimsubiri hadi arejee.Yule mzee alirejea saa 1 usiku na baada ya kufika tu swali lake la kwanza ilikuwa ni kwanini niko pale bila uwepo wa Ally Mpemba.
Mimi "kaka Ally ndiye kaniambia nije kwako"
Mzee "Mambo ni matamu ila mnashindwa kufanya utamu kuendelea kuuzuia utamu"
Aliendelea "watu wa bara mwatumia nguvu sana mahali isipohitajika!"
Mimi niliendelea kukaa kimya huku nikimsikiliza mzee akininanga kwa maneno ya kiswahili yasiyokuwa na chembe ya huruma.
Mzee "Mwenzio kajitahidi kutafuta mambo matamu nawe wataka mtia shubiri!"
Aliendelea "Haya wataka mie nikusaidie nini!"
Mimi "Kuna jambo limetokea mzee wangu ndipo baada ya kuwasiliana na Ally akaniambia nije kwako"
Mzee "Mie naelewa kila kitu weye ulichofanya,sasa hapa kwangu kuna mambo mawili,nsikize kwa makini,moja ni damu na mbili ni ufe wewe!"
Mimi "Sijakuelewa mzee tafadhali nieleweshe"
Mzee "Tangu lini watu wa bara mkaelewa!"
Aliendelea "Kuna mambo mawili weye uchague,moja utoe damu na mbili ufe weye!"
Mimi "Kufa hapana kwakweli,nitoe damu mzee wangu"
Mzee "Hupendi kufa na weye wafanya ujinga!"
Aliendelea "Haya nsikize kwa makini,huyo aliyesababisha haya inapaswa afe kwa kumwaga damu,sasa kuna dawa nitakupatia na nguo hivyo ukifika bara hakikisha unafanya kama nitakavyokueleza"
Mimi "Sawa mzee"
Usiku ule mzee alinichukua akawa amenipeleka kwenye nyumba moja ambayo hakukuwa na mtu ndani yake,tulivyofika hapo alichukua nguo ya ndani ya mwanamke (Chupi)ambayo ilikjwa mpya kabisa na ilikuwa ya rangi nyekundu,kisha akachukua kopo moja ambalo kulikuwa na unga fulani ambao sikuuelewa kisha akaniambia kwakuwa Mwanamke niliyekuwa naye usiku ndiye chanzo cha matazizo ni lazima yeye afe ili mimi nisalimike kwakuwa kosa lile halikuwa na mzaha hata kidogo,kimuonekano waweza kudhani kosa la kukaa siti ya mbele lilikuwa la kawaida kumbe haikuwa kama nilivyokuwa nimedhani.
Mzee "Shika hii!"
Niliichukua ile chupi nikawa nimeishika kama alivyokuwa amenitaka kufanya.
Mzee "Hii dawa utaipaka hivi,na ukishamaliza kuipaka utampelekea huyo mwanaizaya huu mzigo na uhakikishe anaupokea kwa mikono yake miwili usije mpa mtu mwingine kuipokea badala yake,ukifanya hivyo usije kunilaumu!"
Mimi "Sawa mzee"
Mzee "Hii chupi ataivaa na akishaivaa utanipa majibu"
Mimi "Sasa hawezi kuikataa?"
Mzee "Hawezi!,ukifika bara ingia duka lolote mnunulie chupi nyingine kama zawadi na umpelekee kwa pamoja ikiwemo na hii"
Mimi "Itamtosha kweli?"
Mzee "Hiki ndicho kipimo chake na hakikisha utakazonunua zilingane saizi na hii"
Mimi "Sawa ,nimekuelewa mzee"
Baada ya maelekezo yale mzee alinitaka niwe makini tena siku nyingine kwenye harakati kwasababu mambo huwa si mepesi kama nilivyodhani,nililala pale kwake na Asubuhi mida ya saa 2 niliodnoka kuelekea bandarini kwa ajili ya kuianza safari ya kuelekea Dar es salaam.
Nilipofika Dae es salaam nilielekea mitaa ya Kkoo kununua chupi nyingine kama zuga ili nije nimpelekee Rehema kama zawadi,chupi nilizonunua zilikuwa za rangi tofauti na zilikuwa jumla tano na hakukuwa na ugumu kwasababu nilipoingia kwenye lile duka nilimuonyesha ile chupi nyekundu na nikawa namwambia ni size ya mpenzi wangu hivyo anipatie size kama hiyo.
Itaendelea..................
Mfuate PM dada angu hana tatizo kabisa.
Aah kumbe haya sawaMy name is Frank and the meaning of Frank is true 😂😂😂
Thamin trakoo kwanza mengine huja badae.Hapana Manager huo ni mwili tu let's ameumia na akapata ulemavu hilo trako kama ulimpendea trako je upendo utakufa???
Mimi nathamini utu Kwanzaa
Hahahahaha haina shaka itakuwa tu. Weekend itakuwa ni next stepMfuate PM dada angu hana tatizo kabisa.
Sawa utaitumia card mambo yakiitika ili nishiriki kikamilifuHilo ni yeye mwenyewe na dada zangu mim hapo nakaa pembeni kabisa.
Hahahahaha Manager na wewe itabidi nifunge safari mpaka Mbeya sasa au yeye aje hapa DarThamin trakoo kwanza mengine huja badae.
Sawa utaitumia card mambo yakiitika ili nishiriki kikamilifu
Haya nasubiri cardH
Hii ni serious Mkuu. Itakuwa ya kijanja watu 15 tu.😊
Haya nasubiri card