Utajiri wa ushirikina una masharti magumu sana

Utajiri wa ushirikina una masharti magumu sana

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Bwa Uyoga alikua mfanyabiashara wa kawaida lakini huku Kwamtogole tulimuona wa mboga saba, alikua na usafiri wa IST na mke wake hakupanda basi kwenda sokoni. Watoto walisoma English Medium.

Katika kupambana na maisha alikutana na fundi aliyemuahidi utajiri wake utaongezeka akifuata masharti yake. Sharti la kwanza ni kuwa mwanaune wa kwanza kulala na binti yake mkubwa na la pili ni kutokulala na mke wake usiku. Uyoga alianza kufanya mapenzi na binti yake, utajiri ulianza kumiminika na mke alinunuliwa Mercedes Benz Sport Car. Sifahamu kama mama alifahamu au la.

Kule ofisini oder ziliongezeka mpaka ilibidi atatute sehemu kubwa ya kuweka ofisi na kuanza kuajiri vijana wasomi wa kusaidia kuendesha biashara. Katika wasomi wakiajiriwa kulikua na kijana mhasibu, alijipenda sana, alikua nadhifu muda wote.

Mhasibu alikaa sana bench tangu amalize chuo kwahiyo ile kazi kwake ilikua life line, alifanya kazi mpaka saa mbili usiku siku nyingine mradi alikwenda nyumbani aliacha hesabu zime balance. Uyoga. alimpenda sana mhasibu, hata mikutano yake mingine ya kibiashara alimuomba amuakilishe kama mikutano inaingiliana.

Kule nyumbani binti wa Uyoga alikamata ujauzito. Uyoga hajui afanye nini, akiwa Mzee wa heshima katika jamii. Alimuita Mhasibu na kumuweka kikao ofisini kwake. Alimuambia unaoa mwezi ujao, unamuoa binti yangu na harusi yote nitaigharamia mimi. Mhasibu alipewa ghorofa la kuanzia maisha gari na mtaji wa biashara kwa masharti pia awe mhasibu wa Uyoga kwa siku hata mbili kwa wiki.

Harusi ilikua kubwa sana, ndugu wa mhasibu walisafiri kutoka kijijini kwa usafiri wa ndege na walifikia hotelini.. Baada ya harusi mhasibu anagundua yaliyomo yamo mkewe ni mjamzito tena mimba karibu miezi mitatu. Ndipo alipofahamu kuwa hakuna free lunch mjini. Alilea mimba mpaka inakua na mtoto anazaliwa.

Mtoto alizaliwa na matatizo ya kiafya kutokana na muingiliano wa genes. Uyoga aliwasaidia wanandoa wapya kutafuta matibabu nje ya nchi ikiwemo Afrika ya Kusini na India. Watoto waliofuata walikua ni wa mhasibu.
 
Stori kama hii nilikutana nayo Arusha kuna Mfanya biashara alikuwa anakula binti yake na mkewe anakula kisamvu tu labda awe anataka kupata mtoto. Utajiri una mengi sana ndani yake hasa hawa matajiri wa kuibuka bika kuhangaika miaka nenda rudi
Kuna wengine wanaambiwa wawaingilie watoto wao wa kiume. Unakuta mtoto wa kiume ana hasira na baba yake na anaweza kumtoa roho.
 
Story zako huwa nazipenda ni chai fukani hivi amazing fupifupi,hazichoshi kusoma,ziko kwenye mtiririko lakini zinafundisha sana, ubarikiwe sana.
Mkuu unadhani chai basi, binafsi namfahamu mtu anakula binti na mama mkwe, binti hajui ila mama mkwe hapindui kwa jamaa..
 
Back
Top Bottom