Utamaduni wa Watanzania kudhani masuala ya siasa hayatuhusu utatugharimu sisi na vizazi vyetu

Utamaduni wa Watanzania kudhani masuala ya siasa hayatuhusu utatugharimu sisi na vizazi vyetu

Maendeleo ya vitu bila ya kuwepo kwa Haki, Uhuru na Demokrasia ni sawa na kazi bure, work done equal to zero!
Wananchi wengi zaidi waliopo kwenye hizo nchi hawana Uhuru Wala demokrasia, kwa kifupi ni kwamba hawafurahii maisha wakiwa kwenye hizo nchi zao. Karibia wananchi wote kabisa waliopo kwenye hizo nchi wamegeuzwa kuwa Mateka wa Watawala.

Utawala wa China ndio unaongoza duniani kwa Sasa kwa kunyonga Watu wengi zaidi nje ya mfumo wa kimahakama. Aidha, utawala wa Urusi pia unaongoza hapa dunianu kwa kuwafanyia uovu/uhalifu wananchi wake wasio na hatia ambao wanakosoa utawala. Idara ya Usalama wa taifa ya Urusi yaani KGB/FSB imekuwa ikitekeleza operesheni hatari Sana za udhalimu dhidi ya raia kwa kuwateka, kuwatesa, na kuwaua, kila siku raia wa Urusi wamekuwa wakiuawa kwa kuwekewa sumu na Mawakala wa Siri kutoka KGB/FSB.

But all in all, China kwa sasa ina sera mseto za itikadi ya siasa za ukomunisti, ujamaa, ubeoari, n.k.

Nini kinafanya TZ isi adopt sera mseto au za ubepari hivi sasa? Nyerere bado yupo kukataza hilo hivi sasa?
 
Watanganyika wamejenga dhana ya kutohoji wala kufuatilia masuala ya kisiasa na kudhani siasa haimunufaishi.

Mtu anaona kwakuwa anakula na kuishi mambo mengine sio ya muhimu, aani kwamba Katiba mpya sio suala linalotuhisu kwakuwa unaamka asbh unapata mkate basi.

Bandari zinauzwa
Serengeti unaenda kuchimbwa madini, kwa baadae Serengeti haitakuwepo, tupo kimya, Sasa vizazi vyetu vitakuta nini? Vitatuona tulikuwa wajinga kiasi gani?

Rushwa serikalini imekuwa kubwa, mali za umma zinauzwa.

Utekaji na mauaji
Tunaona kawaida Kwa kuwa hatujatekwa au kuuliwa sisi au ndugu wa karibu

Huduma mbovu za kijamii
Shule hazina walimu na madawati. Hospital hakuna madawa, watu hawana bima. Maji hakuna, umeme wa uhakika haupo.

Bunge limekuwa kama sehemu ya kuimba mapambio. Bunge limewekwa mfukoni. Bunge la wananchi linatunga sheria za kuwakandamiza wananchi, rejea mambo ya tozo n.k. Tuko kimya tu.

Tujifunze Kenya wao wale sio makondoo kama Watanganyika
Umesema ukweli kabisa! Sisi ni makondoo na mazombi! Tozo za kununua Esther! Halafu tuna mwenge, ndio tatizo!
 
Kumbe kubadilika inawezekana? Nini kinafanya TZ isibadilike au Nyerere bado anakataza mabadiliko? Point is, kuendelea kumlaumu mtu aliyeondoka madarakani over 30yrs ago kwa changamoto za sasa ni ufinyu wa mawazo.
Atalaumiwa kama muasisi wa hii mifumo ambayo ni rigid kimabadiliko, brain washing iliyofanyika kipindi chake ina athiri mpaka vizazi vya leo kimaamuzi, kiutawala, almost nyanja zote na hili alijua ila hakuweka mifumo ya ku counter hayo mazingira au haku set in motion kuondoa hizo effects.

But then lawama zote haziwez kuwa zake japokuwa yeye ndio source
So walimfuata
 
Nini kinafanya TZ isi adopt sera mseto au za ubepari hivi sasa? Nyerere bado yupo kukataza hilo hivi sasa?
One things. Fear of unknown. Lakini pia kuna tabaka au ombwe la viongozi ambao wanaogopa kuruhusu mabadiliko hayo kwa kuhofia vizazi vyao havito pata nafasi mbeleni or vitapotea

Matokeo yake imetengeneza vizazi vya hovyo, na sheria za hovyo( si zote)
 
Atalaumiwa kama muasisi wa hii mifumo ambayo ni rigid kimabadiliko, brain washing iliyofanyika kipindi chake ina athiri mpaka vizazi vya leo kimaamuzi, kiutawala, almost nyanja zote na hili alijua ila hakuweka mifumo ya ku counter hayo mazingira au haku set in motion kuondoa hizo effects.

But then lawama zote haziwez kuwa zake japokuwa yeye ndio source
So walimfuata

Ni sawa na kumlaumu babu yako kwa setbacks zako. Mzee wako kashindwa ku rectify na wewe umekuwa mtu mzima bado upo pale pale. Hapo tatizo ni wewe.

Kuna mambo alifanya yalikuwa sawa kwa muda na mazingira ya wakati huo, tatizo ni wale waliomfuata kubaki pale pale na hata kizazi cha sasa ni tatizo maana hakifanyi jitihada zozote kubadilika.

Hao Russia, China, Singapore, S. Korea wote walikua na hizi sera na umaskini kama wetu miaka ya uwani ila leo wapo mbali.

“If you are born poor, it's not your fault, but if you die poor it's your fault” Bill Gates Sr.
 
Nini kinafanya TZ isi adopt sera mseto au za ubepari hivi sasa? Nyerere bado yupo kukataza hilo hivi sasa?
Sababu ni Uhafidhina (Conservativeness) wa CCM. Ccm haitaki mabadiliko, waliopo huko wapo rigid na fikra mgando za "zidumu fikra za mwenyekiti."
 
Tusimlaumu sana Nyerere, tangu ameacha madaraka ni takribani miaka 44. Tangu amekufa ni miaka 25. Maana yake tangu ameacha utawala, waliozaliwa ni watu wazima na ndiyo wanayofanya yote haya tunayoona. Mali asili alizoacha ndiyo zinachezewa na kizazi hiki. Ndiyo kizazi kinachodanganywa na akina mwasambwa.
Sasa ni kazi kwenu vijana kubadiri Tanzania. Msikubali kudanganywa na Hawa wanaopewa nusu mkate.
Mkiambiwa andamana maisha magumu, mauaji na kutekwa, hakuna ajira, mnamuachia mbowe na wenzake.
Amka kijana, mabadiriko yanaanza na wewe

Watanganyika wamejenga dhana ya kutohoji wala kufuatilia masuala ya kisiasa na kudhani siasa haimunufaishi.

Mtu anaona kwakuwa anakula na kuishi mambo mengine sio ya muhimu, aani kwamba Katiba mpya sio suala linalotuhisu kwakuwa unaamka asbh unapata mkate basi.

Bandari zinauzwa
Serengeti unaenda kuchimbwa madini, kwa baadae Serengeti haitakuwepo, tupo kimya, Sasa vizazi vyetu vitakuta nini? Vitatuona tulikuwa wajinga kiasi gani?

Rushwa serikalini imekuwa kubwa, mali za umma zinauzwa.

Utekaji na mauaji
Tunaona kawaida Kwa kuwa hatujatekwa au kuuliwa sisi au ndugu wa karibu

Huduma mbovu za kijamii
Shule hazina walimu na madawati. Hospital hakuna madawa, watu hawana bima. Maji hakuna, umeme wa uhakika haupo.

Bunge limekuwa kama sehemu ya kuimba mapambio. Bunge limewekwa mfukoni. Bunge la wananchi linatunga sheria za kuwakandamiza wananchi, rejea mambo ya tozo n.k. Tuko kimya tu.

Tujifunze Kenya wao wale sio makondoo kama Watanganyika
Uchawi tu unakolezwa kila mwaka ili waendelee kuwa makondoo wa kuchinjwa kile kibatati kinachoitwa mwenge ni cha kupiga vita!!
 
Ni sawa na kumlaumu babu yako kwa setbacks zako. Mzee wako kashindwa ku rectify na wewe umekuwa mtu mzima bado upo pale pale. Hapo tatizo ni wewe.

Kuna mambo alifanya yalikuwa sawa kwa muda na mazingira ya wakati huo, tatizo ni wale waliomfuata kubaki pale pale na hata kizazi cha sasa ni tatizo maana hakifanyi jitihada zozote kubadilika.

Hao Russia, China, Singapore, S. Korea wote walikua na hizi sera na umaskini kama wetu miaka ya uwani ila leo wapo mbali.

“If you are born poor, it's not your fault, but if you die poor it's your fault” Bill Gates Sr.
Nyerere huwezi kumlaumu sana
Yeye alikuwa mchanga kwenye siasa na mifumo ya utawala
Hivyo kukosea ilikuwa laZima
Sasa sisi ndo tuyanyooshe mapungufu yake
 
Unategemea nini zaidi iwapo unaishi kwenye nchi ambayo biriani limetengewa hadi siku wanakuletea popote ule na mpishi wake? Kwamba kijana aliyeshiba biriani na kapewa na biriani jingine la kimwili atoke kupigana na polisi?
Kweli kabisa 😅😀
 
  • Kicheko
Reactions: Tsh
Tukijaribu TUNATEKWA, TUNAUWAWA we mwenzetu unaandika kutokea Kenya au upo humu humu.

Mchana chadema unavaa mboga mboga, usiku kilingeni unakuwa kamanda.
 
Kujumuisha kwamba wote hawaijui ni upotofu sana.Wewe ukiulizwa leo maswali ya darasa la tatu kutoka kwenye kitabu toleo la mwaka 1987 utakumbuka?
Na hakuna Nchi yeyote Duniani ambayo Wananchi wake wanaijua Katiba yao yote !
Kila mtu huwa anaijua Katiba katika vijisehemu vidogo vidogo vile vitakavyo mgusa kwenye mambo yake na harakati zake !

Hata hao wanasheria waliosomea Sheria mpaka waangalie kwenye Vitabu vyao vifungu vya Sheria kutoka kwenye kitabu cha Sheria Mama ambayo ndio inaitwa KATIBA !
Mwananchi wa kawaida ataijuaje Katiba yote ???!
Tusidanganyane Bandugu !!
 
Back
Top Bottom