Habari wana Jamiiforums. Ni matumaini yangu muwazima wa afya!
Naomba niende moja kwa moja kwenye mada, miaka ya hivi karibuni kutokana na ukuaji wa Teknolojia ya habari na Mawasiliano taarifa nyingi za mahusiano baina ya wanafunzi na walimu au hata watu wengine tu ambao si walimu zinafika mtandaoni na kutangazwa kwa wingi. Shukrani ziende kwenye Internet, hapo zamani kidogo wakati Teknolojia ipo duni habari hizi hazikuwa zikifikia masikio ya wengi sana japo zilifanyika.
Kwa bahati mbaya Utandawazi kwasasa uanawa-expose wanafunzi wa shule (wakiume na wakike) kwenye matukio mbalimbali ya video, picha, audio na vinginevyo ambavyo vipo juu ya umri wao na ni vitendo vihovu. Kuna nyimbo zinashushwa huko YouTube na maneno yake ni magumu, ya hovyo yaani yamejaa pornography ya maneno na matendo, sijajua kizazi hiki kitafichwaje au kitalimdwaje ila tupambane hivyo hivyo.
Kutokana na huu utandawazi vijana wadogo wanaanza mahusiano ya kimapenzi wakiwa wadogo na wana kasi za ajabu ajabu mno, kwasasa si ajabu binti wa form one kuwa na mahusiano na mtu ambaye ni kama baba yake kiumri na hapo tena ana boyfriend wake wa shuleni, mtaani n.k na wote anashiriki nao ngono.
Kuna scenario ya baba mmoja mtaani ambaye alitalakiana na mkewe miaka mingi iliyopita, mtoto wao mdogo kwa kipindi ambacho walikuwa wakitarakiana alikuwa na miaka saba. Mama mtu alipoondoka aliwaacha watoto watatu, wakike wawili na mmoja wa kiume. Sababu za kuachana kwao hazifahamiki (Si, issue yetu kujua wao ndio wanandoa), siku zimeenda mtoto wa kwanza wa huyu mzee alipofaulu na kuingia kidato cha tano alimuacha mdogo wake wa kike ambaye alikuwa akiendelea na Elimu ngazi ya O - level, mtoto wa kiume aliwahi kutoka nyumbani kwao na kuenda kuishi kwa shangazi yake miaka michache baada ya talaka ya wazazi wao.
Siku zimeenda mzee huyu alianza kuumwa mwishoe akafariki, mambo yameanza kusemwa kwamba mzee alikuwa akikaa na mtoto wake wa kike (wa O -level) kama mke wake, walikuwa wakishiriki ngono mara nyingi mno. Mtaani huyu dogo alionekana kama dogo aliyepinda sana nae alikuwa akikitembeza ki****e chake sana. Baba alikuwa mwathirika na dogo kaupata, na wote aliotembea nao huyu dogo wapo kwenye makadirio ya kuupata ugonjwa wa UKIMWI.
End of the story, inaweza onekana kama less traumatizing story kuisoma lakini worst truth ni kwamba hao wagonjwa wapya wa UKIMWI wapo mitaani na wao waambukiza wengine.
Vijana wa kiume na wakike wa miaka hii kwa asilimia kubwa wana akili za ajabu sana na wana mishawasha ya ngono ya hali ya juu mno, USITHUBUTU HATA SIKU MOJA KUJIHUSISHA KIMAPENZI NA WANAFUNZI, WAACHE FANYA MAMBO YAKO!
Hautaweza kujitetea mahakamani kwa kauli hizi "Alinitega yeye mwenyewe mwanzo", "Alianza kunizoea kilazima", "Alinifuata akiwa na khanga moja na kuivua na kuniambia nikikataa atapiga kelele kwa watu". Hawa madogo wa sasa asilimia kubwa ni fyatu wana tamaa ya mapenzi, waache wasome wamalize. Pambana na wakubwa wenzio.
Ikibidi fuata taratibu za ma Eunuchs