Utapeli wa “Chumvi na Mafuta ya Upako” Wafichuliwa

Utapeli wa “Chumvi na Mafuta ya Upako” Wafichuliwa

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
1,679
Reaction score
2,123
Kabla ya kuufichua huo utapeli, hebu tuwasikilize kwanza hawa manabii feki:

Nabii XXL: Aisee, hizi sadaka tunazopata hazitoshi kununua ndege, na kutufanya tuishi maisha ya kifahari. Naomba tubuni mbinu ya kuongeza mapato.

Nabii X: Mi nafikiri wakati wa maombezi, tuwe tunawauzia watu chumvi, mafuta, maji na vitambaa, lakini tuwaambie kwamba vitu hivyo vina upako. Watanunua tu.

Nabii XXL: Mh, tukifanya hivyo kabla ya kuwaombea, watatugundua. Katika Biblia Yesu si alisema huduma za kuponya na kutenda miujiza hazipaswi kutolewa kwa malipo?

Nabii X: Mkuu, watu hawana muda wa kusoma Biblia, hawajui hilo Andiko. Nakwambia watanunua tu. Tena tukiwaambia mafuta na chumvi vimetoka Israeli, ndio kabisa, hata tukiwauzia kwa dola watanunua.

Nabii XXL: Hahaa, aisee we una akili. Hebu tuanze haraka kuifanyia kazi hiyo mbinu. Ndani ya mwaka mmoja tu, tutakuwa mabilionea.
================
Nyakati hizi za mwisho manabii wengi wa uongo wametokea na kuwadanganya wengi kama Maandiko yanenavyo(Mt24:11). Na watu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Maneno ya Mungu yako wazi lakini kwakuwa watu hawasomi Biblia wanadanganyika kirahisi.

Ni kweli katika Biblia mafuta na chumvi vimetajwa. Kwa mfano katika kitabu cha Yakobo 5:14 imeandikwa:"Mtu wa kwenu anaumwa? Na awaite wazee wa kanisa, nao watamuombea, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana." Andiko hili linaonyesha kuwa upako wa mafuta ni sehemu ya ibada na uponyaji wa kiroho.

Katika Marko 6:13 imeandikwa pia hivi – "Wakatoa pepo wengi, wakawapaka mafuta wengi waliokuwa wagonjwa, wakawaponya." Andiko hili linaonyesha pia jinsi Mitume walivyotumia mafuta kwa uponyaji.

LAKINI Maandiko hayo hayatuambii kwamba wagonjwa, wenye shida na wanaohitaji baraka wanapaswa kununua bidhaa hizo ili wapone au wabarikiwe. Kwahiyo wauzaji ni matapeli.

Katika Mathayo 10:8, tunasoma kuwa Yesu aliwapa wanafunzi wake mamlaka ya kuponya wagonjwa na kufukuza pepo, lakini aliwaonya wasifanye huduma hiyo kwa kudai malipo.

Mathayo 10:8 – "Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure."

Andiko hilo linaonyesha wazi kuwa karama za Mungu zinapaswa kutolewa bure.

Enyi mnaolifanya Jina la Mungu litukanwe kwa sababu mmewalaghai watu kuwa chumvi na mafuta mnayouza yana upako, kumbe uongo, nawasihi, popote pale mlipo ulimwenguni, badilikeni. La sivyo unabii huu utatimia kwenu:

Mathayo 7:22-23 – "Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu."
Matapeli.jpg
 
Kabla ya kuufichua huo utapeli, hebu tuwasikilize kwanza hawa manabii feki:

Nabii XXL: Aisee, hizi sadaka tunazopata hazitoshi kununua ndege, na kutufanya tuishi maisha ya kifahari. Naomba tubuni mbinu ya kuongeza mapato.

Nabii X: Mi nafikiri wakati wa maombezi, tuwe tunawauzia watu chumvi, mafuta, maji na vitambaa, lakini tuwaambie kwamba vitu hivyo vina upako. Watanunua tu.

Nabii XXL: Mh, tukifanya hivyo kabla ya kuwaombea, watatugundua. Katika Biblia Yesu si alisema huduma za kuponya na kutenda miujiza hazipaswi kutolewa kwa malipo?

Nabii X: Mkuu, watu hawana muda wa kusoma Biblia, hawajui hilo Andiko. Nakwambia watanunua tu. Tena tukiwaambia mafuta na chumvi vimetoka Israeli, ndio kabisa, hata tukiwauzia kwa dola watanunua.

Nabii XXL: Hahaa, aisee we una akili. Hebu tuanze haraka kuifanyia kazi hiyo mbinu. Ndani ya mwaka mmoja tu, tutakuwa mabilionea.
================
Nyakati hizi za mwisho manabii wengi wa uongo wametokea na kuwadanganya wengi kama Maandiko yanenavyo(Mt24:11). Na watu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Maneno ya Mungu yako wazi lakini kwakuwa watu hawasomi Biblia wanadanganyika kirahisi.

Ni kweli katika Biblia mafuta na chumvi vimetajwa. Kwa mfano katika kitabu cha Yakobo 5:14 imeandikwa:"Mtu wa kwenu anaumwa? Na awaite wazee wa kanisa, nao watamuombea, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana." Andiko hili linaonyesha kuwa upako wa mafuta ni sehemu ya ibada na uponyaji wa kiroho.

Katika Marko 6:13 imeandikwa pia hivi – "Wakatoa pepo wengi, wakawapaka mafuta wengi waliokuwa wagonjwa, wakawaponya." Andiko hili linaonyesha pia jinsi Mitume walivyotumia mafuta kwa uponyaji.

LAKINI Maandiko hayo hayatuambii kwamba wagonjwa, wenye shida na wanaohitaji baraka wanapaswa kununua bidhaa hizo ili wapone au wabarikiwe. Kwahiyo wauzaji ni matapeli.

Katika Mathayo 10:8, tunasoma kuwa Yesu aliwapa wanafunzi wake mamlaka ya kuponya wagonjwa na kufukuza pepo, lakini aliwaonya wasifanye huduma hiyo kwa kudai malipo.

Mathayo 10:8 – "Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure."
Biblia janjajanja sana..yaani kila mtu afufue wafu!!
Andiko hilo linaonyesha wazi kuwa karama za Mungu zinapaswa kutolewa bure.

Enyi mnaolifanya Jina la Mungu litukanwe kwa sababu mmewalaghai watu kuwa chumvi na mafuta mnayouza yana upako, kumbe uongo, nawasihi, popote pale mlipo ulimwenguni, badilikeni. La sivyo unabii huu utatimia kwenu:

Mathayo 7:22-23 – "Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu."
 
Biblia janjajanja sana..yaani kila mtu afufue wafu!!
Sio kila mtu afufue wafu. Andiko lile linasema waliopewa mamlaka yale ni Mitume 12. Baadaye Yesu aliwapa wengine 70. Halafu katika 1 Wakorintho 12:4-10, Paulo anaeleza kwamba kuna karama tofauti zinazotolewa na Roho Mtakatifu:
  • Karama ya imani
  • Karama ya kuponya
  • Karama ya kutenda miujiza
  • Karama ya unabii
  • Karama ya lugha
  • Karama ya kufasiri lugha nk
Roho Mtakatifu ndiye anayegawa karama hizo kwa kila mtu, kama yeye mwenyewe(Roho Mtakatifu) apendavyo. Kwa mantiki hiyo sio kila mtu atapewa karama ya kutenda miujiza au ya kufufua wafu.
 
Kabla ya kuufichua huo utapeli, hebu tuwasikilize kwanza hawa manabii feki:

Nabii XXL: Aisee, hizi sadaka tunazopata hazitoshi kununua ndege, na kutufanya tuishi maisha ya kifahari. Naomba tubuni mbinu ya kuongeza mapato.

Nabii X: Mi nafikiri wakati wa maombezi, tuwe tunawauzia watu chumvi, mafuta, maji na vitambaa, lakini tuwaambie kwamba vitu hivyo vina upako. Watanunua tu.

Nabii XXL: Mh, tukifanya hivyo kabla ya kuwaombea, watatugundua. Katika Biblia Yesu si alisema huduma za kuponya na kutenda miujiza hazipaswi kutolewa kwa malipo?

Nabii X: Mkuu, watu hawana muda wa kusoma Biblia, hawajui hilo Andiko. Nakwambia watanunua tu. Tena tukiwaambia mafuta na chumvi vimetoka Israeli, ndio kabisa, hata tukiwauzia kwa dola watanunua.

Nabii XXL: Hahaa, aisee we una akili. Hebu tuanze haraka kuifanyia kazi hiyo mbinu. Ndani ya mwaka mmoja tu, tutakuwa mabilionea.
================
Nyakati hizi za mwisho manabii wengi wa uongo wametokea na kuwadanganya wengi kama Maandiko yanenavyo(Mt24:11). Na watu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Maneno ya Mungu yako wazi lakini kwakuwa watu hawasomi Biblia wanadanganyika kirahisi.

Ni kweli katika Biblia mafuta na chumvi vimetajwa. Kwa mfano katika kitabu cha Yakobo 5:14 imeandikwa:"Mtu wa kwenu anaumwa? Na awaite wazee wa kanisa, nao watamuombea, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana." Andiko hili linaonyesha kuwa upako wa mafuta ni sehemu ya ibada na uponyaji wa kiroho.

Katika Marko 6:13 imeandikwa pia hivi – "Wakatoa pepo wengi, wakawapaka mafuta wengi waliokuwa wagonjwa, wakawaponya." Andiko hili linaonyesha pia jinsi Mitume walivyotumia mafuta kwa uponyaji.

LAKINI Maandiko hayo hayatuambii kwamba wagonjwa, wenye shida na wanaohitaji baraka wanapaswa kununua bidhaa hizo ili wapone au wabarikiwe. Kwahiyo wauzaji ni matapeli.

Katika Mathayo 10:8, tunasoma kuwa Yesu aliwapa wanafunzi wake mamlaka ya kuponya wagonjwa na kufukuza pepo, lakini aliwaonya wasifanye huduma hiyo kwa kudai malipo.

Mathayo 10:8 – "Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure."

Andiko hilo linaonyesha wazi kuwa karama za Mungu zinapaswa kutolewa bure.

Enyi mnaolifanya Jina la Mungu litukanwe kwa sababu mmewalaghai watu kuwa chumvi na mafuta mnayouza yana upako, kumbe uongo, nawasihi, popote pale mlipo ulimwenguni, badilikeni. La sivyo unabii huu utatimia kwenu:

Mathayo 7:22-23 – "Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu."
Hakuna Mtume aliyeuza mafuta – Mitume waliponya kwa jina la Yesu bila kuuza mafuta au chumvi (Matendo 3:6).
 
Nabii XXLL: Nataka kuacha kazi maana naona mshahara unanichelewesha kufika małengo yangu. Ngoja niende Nigeria nikirudi watu watanikoma, nitawapelekesha ile mbaya.
 
Siku hizi kuna viambata upako kama vile, mafuta, sidilia, chupi, Leso, udongo, maji etc, ndugu zetu wa upande huo mnapigwa kweli, huku kwetu siku hizi kuna waganga pia wauza mafuta lkn hiyo ni kazi yake binafsi hayauzwi msikitini na kugeuzwa sehemu ya ibada,, yani mtu ana ofisi yake somewhere, msikitini ni mchango wa kuendesha shughuli za pale msikitini tu kama maji, umeme , usafi. Na si kwamba kinapita kikapu cha mchango wa maji alafu baadae kipite kikapu cha umeme hiyo hapana,,, kikapu kinapita mara moja tu so kikipita kwa mara ya pili basi lazima yatoke maelezo marefu yenye sababu za msingi kwa nini kipite mara mbili,, kifupi upigaji huku amna, kwanza huyo mzee mandwanga akitoa buku lake atataka kulifatilia mpaka ajue limefanya kazi gani msikitini, seuse umtembezee kikapu marambili,, ila nyie wenzetu huko mchungaji akisema tu papai hili limetoka kwa yesu Israel basi litagombewa na kuuzwa hata milioni,, ila msikitini shehe akisema nimeoteshwa na mtume papai hili linauzwa elfu kumi kama hajachezea bakora huyo sijui,,, huo ndio utofauti wetu sie na nyie kila kitu ndio mchungaji.
 
Kabla ya kuufichua huo utapeli, hebu tuwasikilize kwanza hawa manabii feki:

Nabii XXL: Aisee, hizi sadaka tunazopata hazitoshi kununua ndege, na kutufanya tuishi maisha ya kifahari. Naomba tubuni mbinu ya kuongeza mapato.

Nabii X: Mi nafikiri wakati wa maombezi, tuwe tunawauzia watu chumvi, mafuta, maji na vitambaa, lakini tuwaambie kwamba vitu hivyo vina upako. Watanunua tu.

Nabii XXL: Mh, tukifanya hivyo kabla ya kuwaombea, watatugundua. Katika Biblia Yesu si alisema huduma za kuponya na kutenda miujiza hazipaswi kutolewa kwa malipo?

Nabii X: Mkuu, watu hawana muda wa kusoma Biblia, hawajui hilo Andiko. Nakwambia watanunua tu. Tena tukiwaambia mafuta na chumvi vimetoka Israeli, ndio kabisa, hata tukiwauzia kwa dola watanunua.

Nabii XXL: Hahaa, aisee we una akili. Hebu tuanze haraka kuifanyia kazi hiyo mbinu. Ndani ya mwaka mmoja tu, tutakuwa mabilionea.
================
Nyakati hizi za mwisho manabii wengi wa uongo wametokea na kuwadanganya wengi kama Maandiko yanenavyo(Mt24:11). Na watu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Maneno ya Mungu yako wazi lakini kwakuwa watu hawasomi Biblia wanadanganyika kirahisi.

Ni kweli katika Biblia mafuta na chumvi vimetajwa. Kwa mfano katika kitabu cha Yakobo 5:14 imeandikwa:"Mtu wa kwenu anaumwa? Na awaite wazee wa kanisa, nao watamuombea, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana." Andiko hili linaonyesha kuwa upako wa mafuta ni sehemu ya ibada na uponyaji wa kiroho.

Katika Marko 6:13 imeandikwa pia hivi – "Wakatoa pepo wengi, wakawapaka mafuta wengi waliokuwa wagonjwa, wakawaponya." Andiko hili linaonyesha pia jinsi Mitume walivyotumia mafuta kwa uponyaji.

LAKINI Maandiko hayo hayatuambii kwamba wagonjwa, wenye shida na wanaohitaji baraka wanapaswa kununua bidhaa hizo ili wapone au wabarikiwe. Kwahiyo wauzaji ni matapeli.

Katika Mathayo 10:8, tunasoma kuwa Yesu aliwapa wanafunzi wake mamlaka ya kuponya wagonjwa na kufukuza pepo, lakini aliwaonya wasifanye huduma hiyo kwa kudai malipo.

Mathayo 10:8 – "Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure."

Andiko hilo linaonyesha wazi kuwa karama za Mungu zinapaswa kutolewa bure.

Enyi mnaolifanya Jina la Mungu litukanwe kwa sababu mmewalaghai watu kuwa chumvi na mafuta mnayouza yana upako, kumbe uongo, nawasihi, popote pale mlipo ulimwenguni, badilikeni. La sivyo unabii huu utatimia kwenu:

Mathayo 7:22-23 – "Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu."
Yesu aliwafukuza wafanyabiashara hekaluni – Alisema, “Mnaifanya nyumba ya Baba yangu kuwa pango la wanyang'anyi” (Mathayo 21:13).
Hawa wauza chumvi na mafuta ya upako feki wanastahili kabisa kufanyiwa hivyo hivyo
 
Kabla ya kuufichua huo utapeli, hebu tuwasikilize kwanza hawa manabii feki:

Nabii XXL: Aisee, hizi sadaka tunazopata hazitoshi kununua ndege, na kutufanya tuishi maisha ya kifahari. Naomba tubuni mbinu ya kuongeza mapato.

Nabii X: Mi nafikiri wakati wa maombezi, tuwe tunawauzia watu chumvi, mafuta, maji na vitambaa, lakini tuwaambie kwamba vitu hivyo vina upako. Watanunua tu.

Nabii XXL: Mh, tukifanya hivyo kabla ya kuwaombea, watatugundua. Katika Biblia Yesu si alisema huduma za kuponya na kutenda miujiza hazipaswi kutolewa kwa malipo?

Nabii X: Mkuu, watu hawana muda wa kusoma Biblia, hawajui hilo Andiko. Nakwambia watanunua tu. Tena tukiwaambia mafuta na chumvi vimetoka Israeli, ndio kabisa, hata tukiwauzia kwa dola watanunua.

Nabii XXL: Hahaa, aisee we una akili. Hebu tuanze haraka kuifanyia kazi hiyo mbinu. Ndani ya mwaka mmoja tu, tutakuwa mabilionea.
================
Hayo mazungumzo umeyatoa wapi?
 
ila msikitini shehe akisema nimeoteshwa na mtume papai hili linauzwa elfu kumi kama hajachezea bakora huyo sijui,,,
Hahaa, umenivunja mbavu: "kama hajachezea bakora..."

Hata Yesu alipindua meza za waliokuwa wakifanya biashara hekaluni. Ni wakati mwafaka sasa wa kupindua meza za hao wauza viambata vya upako.
 
Back
Top Bottom