Utapeli wa “Chumvi na Mafuta ya Upako” Wafichuliwa

Utapeli wa “Chumvi na Mafuta ya Upako” Wafichuliwa

Kabla ya kuufichua huo utapeli, hebu tuwasikilize kwanza hawa manabii feki:

Nabii XXL: Aisee, hizi sadaka tunazopata hazitoshi kununua ndege, na kutufanya tuishi maisha ya kifahari. Naomba tubuni mbinu ya kuongeza mapato.

Nabii X: Mi nafikiri wakati wa maombezi, tuwe tunawauzia watu chumvi, mafuta, maji na vitambaa, lakini tuwaambie kwamba vitu hivyo vina upako. Watanunua tu.

Nabii XXL: Mh, tukifanya hivyo kabla ya kuwaombea, watatugundua. Katika Biblia Yesu si alisema huduma za kuponya na kutenda miujiza hazipaswi kutolewa kwa malipo?

Nabii X: Mkuu, watu hawana muda wa kusoma Biblia, hawajui hilo Andiko. Nakwambia watanunua tu. Tena tukiwaambia mafuta na chumvi vimetoka Israeli, ndio kabisa, hata tukiwauzia kwa dola watanunua.

Nabii XXL: Hahaa, aisee we una akili. Hebu tuanze haraka kuifanyia kazi hiyo mbinu. Ndani ya mwaka mmoja tu, tutakuwa mabilionea.
================
Nyakati hizi za mwisho manabii wengi wa uongo wametokea na kuwadanganya wengi kama Maandiko yanenavyo(Mt24:11). Na watu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Maneno ya Mungu yako wazi lakini kwakuwa watu hawasomi Biblia wanadanganyika kirahisi.

Ni kweli katika Biblia mafuta na chumvi vimetajwa. Kwa mfano katika kitabu cha Yakobo 5:14 imeandikwa:"Mtu wa kwenu anaumwa? Na awaite wazee wa kanisa, nao watamuombea, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana." Andiko hili linaonyesha kuwa upako wa mafuta ni sehemu ya ibada na uponyaji wa kiroho.

Katika Marko 6:13 imeandikwa pia hivi – "Wakatoa pepo wengi, wakawapaka mafuta wengi waliokuwa wagonjwa, wakawaponya." Andiko hili linaonyesha pia jinsi Mitume walivyotumia mafuta kwa uponyaji.

LAKINI Maandiko hayo hayatuambii kwamba wagonjwa, wenye shida na wanaohitaji baraka wanapaswa kununua bidhaa hizo ili wapone au wabarikiwe. Kwahiyo wauzaji ni matapeli.

Katika Mathayo 10:8, tunasoma kuwa Yesu aliwapa wanafunzi wake mamlaka ya kuponya wagonjwa na kufukuza pepo, lakini aliwaonya wasifanye huduma hiyo kwa kudai malipo.

Mathayo 10:8 – "Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure."

Andiko hilo linaonyesha wazi kuwa karama za Mungu zinapaswa kutolewa bure.

Enyi mnaolifanya Jina la Mungu litukanwe kwa sababu mmewalaghai watu kuwa chumvi na mafuta mnayouza yana upako, kumbe uongo, nawasihi, popote pale mlipo ulimwenguni, badilikeni. La sivyo unabii huu utatimia kwenu:

Mathayo 7:22-23 – "Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu."
Manabii wauza chumvi, Paulo anawaambia katika Wafilipi 3:19:
"Mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, na utukufu wao ni aibu yao; wanafikiri mambo ya dunia."
 
Kabla ya kuufichua huo utapeli, hebu tuwasikilize kwanza hawa manabii feki:

Nabii XXL: Aisee, hizi sadaka tunazopata hazitoshi kununua ndege, na kutufanya tuishi maisha ya kifahari. Naomba tubuni mbinu ya kuongeza mapato.

Nabii X: Mi nafikiri wakati wa maombezi, tuwe tunawauzia watu chumvi, mafuta, maji na vitambaa, lakini tuwaambie kwamba vitu hivyo vina upako. Watanunua tu.

Nabii XXL: Mh, tukifanya hivyo kabla ya kuwaombea, watatugundua. Katika Biblia Yesu si alisema huduma za kuponya na kutenda miujiza hazipaswi kutolewa kwa malipo?

Nabii X: Mkuu, watu hawana muda wa kusoma Biblia, hawajui hilo Andiko. Nakwambia watanunua tu. Tena tukiwaambia mafuta na chumvi vimetoka Israeli, ndio kabisa, hata tukiwauzia kwa dola watanunua.

Nabii XXL: Hahaa, aisee we una akili. Hebu tuanze haraka kuifanyia kazi hiyo mbinu. Ndani ya mwaka mmoja tu, tutakuwa mabilionea.
================
Nyakati hizi za mwisho manabii wengi wa uongo wametokea na kuwadanganya wengi kama Maandiko yanenavyo(Mt24:11). Na watu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Maneno ya Mungu yako wazi lakini kwakuwa watu hawasomi Biblia wanadanganyika kirahisi.

Ni kweli katika Biblia mafuta na chumvi vimetajwa. Kwa mfano katika kitabu cha Yakobo 5:14 imeandikwa:"Mtu wa kwenu anaumwa? Na awaite wazee wa kanisa, nao watamuombea, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana." Andiko hili linaonyesha kuwa upako wa mafuta ni sehemu ya ibada na uponyaji wa kiroho.

Katika Marko 6:13 imeandikwa pia hivi – "Wakatoa pepo wengi, wakawapaka mafuta wengi waliokuwa wagonjwa, wakawaponya." Andiko hili linaonyesha pia jinsi Mitume walivyotumia mafuta kwa uponyaji.

LAKINI Maandiko hayo hayatuambii kwamba wagonjwa, wenye shida na wanaohitaji baraka wanapaswa kununua bidhaa hizo ili wapone au wabarikiwe. Kwahiyo wauzaji ni matapeli.

Katika Mathayo 10:8, tunasoma kuwa Yesu aliwapa wanafunzi wake mamlaka ya kuponya wagonjwa na kufukuza pepo, lakini aliwaonya wasifanye huduma hiyo kwa kudai malipo.

Mathayo 10:8 – "Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure."

Andiko hilo linaonyesha wazi kuwa karama za Mungu zinapaswa kutolewa bure.

Enyi mnaolifanya Jina la Mungu litukanwe kwa sababu mmewalaghai watu kuwa chumvi na mafuta mnayouza yana upako, kumbe uongo, nawasihi, popote pale mlipo ulimwenguni, badilikeni. La sivyo unabii huu utatimia kwenu:

Mathayo 7:22-23 – "Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu."
Nilienda mahali nikakuta mtu anawaonyesha kwa furaha wenzake, kichupa kidogo alichonunua kwa bei mbaya. Nafikiri kilichomvuta kukinunua kichupa kile ni kwamba aliambiwa kina mafuta ya mizeituni. Sasa kwakuwa alisoma kwenye Biblia kwamba Yesu alikuwa akienda kusali katika mlima wa mizeituni aliamini mafuta hayo lazima yana upako. Lakini si ajabu kilichokuwemo kwenye hicho kichupa sio mafuta, bali ni maji yaliyotiwa rangi😀

Kwani wanaoenda kwenye mikutano ya manabii wa uongo, wakiambiwa wanunue mafuta ya mizeituni, nani anahangaika kwenda kuyapima maabara ili ahakikishe kuwa ni mafuta au ni maji. Hivi ndivyo watu wanavyopigwa mchana kweupe.
 
Kabla ya kuufichua huo utapeli, hebu tuwasikilize kwanza hawa manabii feki:

Nabii XXL: Aisee, hizi sadaka tunazopata hazitoshi kununua ndege, na kutufanya tuishi maisha ya kifahari. Naomba tubuni mbinu ya kuongeza mapato.

Nabii X: Mi nafikiri wakati wa maombezi, tuwe tunawauzia watu chumvi, mafuta, maji na vitambaa, lakini tuwaambie kwamba vitu hivyo vina upako. Watanunua tu.

Nabii XXL: Mh, tukifanya hivyo kabla ya kuwaombea, watatugundua. Katika Biblia Yesu si alisema huduma za kuponya na kutenda miujiza hazipaswi kutolewa kwa malipo?

Nabii X: Mkuu, watu hawana muda wa kusoma Biblia, hawajui hilo Andiko. Nakwambia watanunua tu. Tena tukiwaambia mafuta na chumvi vimetoka Israeli, ndio kabisa, hata tukiwauzia kwa dola watanunua.

Nabii XXL: Hahaa, aisee we una akili. Hebu tuanze haraka kuifanyia kazi hiyo mbinu. Ndani ya mwaka mmoja tu, tutakuwa mabilionea.
================
Nyakati hizi za mwisho manabii wengi wa uongo wametokea na kuwadanganya wengi kama Maandiko yanenavyo(Mt24:11). Na watu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Maneno ya Mungu yako wazi lakini kwakuwa watu hawasomi Biblia wanadanganyika kirahisi.

Ni kweli katika Biblia mafuta na chumvi vimetajwa. Kwa mfano katika kitabu cha Yakobo 5:14 imeandikwa:"Mtu wa kwenu anaumwa? Na awaite wazee wa kanisa, nao watamuombea, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana." Andiko hili linaonyesha kuwa upako wa mafuta ni sehemu ya ibada na uponyaji wa kiroho.

Katika Marko 6:13 imeandikwa pia hivi – "Wakatoa pepo wengi, wakawapaka mafuta wengi waliokuwa wagonjwa, wakawaponya." Andiko hili linaonyesha pia jinsi Mitume walivyotumia mafuta kwa uponyaji.

LAKINI Maandiko hayo hayatuambii kwamba wagonjwa, wenye shida na wanaohitaji baraka wanapaswa kununua bidhaa hizo ili wapone au wabarikiwe. Kwahiyo wauzaji ni matapeli.

Katika Mathayo 10:8, tunasoma kuwa Yesu aliwapa wanafunzi wake mamlaka ya kuponya wagonjwa na kufukuza pepo, lakini aliwaonya wasifanye huduma hiyo kwa kudai malipo.

Mathayo 10:8 – "Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure."

Andiko hilo linaonyesha wazi kuwa karama za Mungu zinapaswa kutolewa bure.

Enyi mnaolifanya Jina la Mungu litukanwe kwa sababu mmewalaghai watu kuwa chumvi na mafuta mnayouza yana upako, kumbe uongo, nawasihi, popote pale mlipo ulimwenguni, badilikeni. La sivyo unabii huu utatimia kwenu:

Mathayo 7:22-23 – "Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu."
Kuna nabii fulani alivyojua watu wameishtukia chumvi ya kununua, akawa anagawa bure chumvi. Lakini saa ya maombezi anawaambia watu watoe sadaka ya kujimaliza. Mtu anayetoa pesa ndefu ndo anaombewa kwa kuwekewa mikono.

Soma Biblia yote hautaona Mitume wakitoza pesa kabla ya kuwaombea wagonjwa. Tushtuke jamani
 
Sio kila mtu afufue wafu. Andiko lile linasema waliopewa mamlaka yale ni Mitume 12. Baadaye Yesu aliwapa wengine 70. Halafu katika 1 Wakorintho 12:4-10, Paulo anaeleza kwamba kuna karama tofauti zinazotolewa na Roho Mtakatifu:
  • Karama ya imani
  • Karama ya kuponya
  • Karama ya kutenda miujiza
  • Karama ya unabii
  • Karama ya lugha
  • Karama ya kufasiri lugha nk
Roho Mtakatifu ndiye anayegawa karama hizo kwa kila mtu, kama yeye mwenyewe(Roho Mtakatifu) apendavyo. Kwa mantiki hiyo sio kila mtu atapewa karama ya kutenda miujiza au ya kufufua wafu.
Paulo ni nani bwana wewe,mhuni mmoja tu hivi!!..yesu anahubiri hamtaki,anaondoka eti kamtokea akienda damascus,akampa utume
 
Sio kila mtu afufue wafu. Andiko lile linasema waliopewa mamlaka yale ni Mitume 12. Baadaye Yesu aliwapa wengine 70. Halafu katika 1 Wakorintho 12:4-10, Paulo anaeleza kwamba kuna karama tofauti zinazotolewa na Roho Mtakatifu:
  • Karama ya imani
  • Karama ya kuponya
  • Karama ya kutenda miujiza
  • Karama ya unabii
  • Karama ya lugha
  • Karama ya kufasiri lugha nk
Roho Mtakatifu ndiye anayegawa karama hizo kwa kila mtu, kama yeye mwenyewe(Roho Mtakatifu) apendavyo. Kwa mantiki hiyo sio kila mtu atapewa karama ya kutenda miujiza au ya kufufua wafu.
Paulo ni nani? je amemzidi YESU
 
Kabla ya kuufichua huo utapeli, hebu tuwasikilize kwanza hawa manabii feki:

Nabii XXL: Aisee, hizi sadaka tunazopata hazitoshi kununua ndege, na kutufanya tuishi maisha ya kifahari. Naomba tubuni mbinu ya kuongeza mapato.

Nabii X: Mi nafikiri wakati wa maombezi, tuwe tunawauzia watu chumvi, mafuta, maji na vitambaa, lakini tuwaambie kwamba vitu hivyo vina upako. Watanunua tu.

Nabii XXL: Mh, tukifanya hivyo kabla ya kuwaombea, watatugundua. Katika Biblia Yesu si alisema huduma za kuponya na kutenda miujiza hazipaswi kutolewa kwa malipo?

Nabii X: Mkuu, watu hawana muda wa kusoma Biblia, hawajui hilo Andiko. Nakwambia watanunua tu. Tena tukiwaambia mafuta na chumvi vimetoka Israeli, ndio kabisa, hata tukiwauzia kwa dola watanunua.

Nabii XXL: Hahaa, aisee we una akili. Hebu tuanze haraka kuifanyia kazi hiyo mbinu. Ndani ya mwaka mmoja tu, tutakuwa mabilionea.
================
Nyakati hizi za mwisho manabii wengi wa uongo wametokea na kuwadanganya wengi kama Maandiko yanenavyo(Mt24:11). Na watu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Maneno ya Mungu yako wazi lakini kwakuwa watu hawasomi Biblia wanadanganyika kirahisi.

Ni kweli katika Biblia mafuta na chumvi vimetajwa. Kwa mfano katika kitabu cha Yakobo 5:14 imeandikwa:"Mtu wa kwenu anaumwa? Na awaite wazee wa kanisa, nao watamuombea, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana." Andiko hili linaonyesha kuwa upako wa mafuta ni sehemu ya ibada na uponyaji wa kiroho.

Katika Marko 6:13 imeandikwa pia hivi – "Wakatoa pepo wengi, wakawapaka mafuta wengi waliokuwa wagonjwa, wakawaponya." Andiko hili linaonyesha pia jinsi Mitume walivyotumia mafuta kwa uponyaji.

LAKINI Maandiko hayo hayatuambii kwamba wagonjwa, wenye shida na wanaohitaji baraka wanapaswa kununua bidhaa hizo ili wapone au wabarikiwe. Kwahiyo wauzaji ni matapeli.

Katika Mathayo 10:8, tunasoma kuwa Yesu aliwapa wanafunzi wake mamlaka ya kuponya wagonjwa na kufukuza pepo, lakini aliwaonya wasifanye huduma hiyo kwa kudai malipo.

Mathayo 10:8 – "Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure."

Andiko hilo linaonyesha wazi kuwa karama za Mungu zinapaswa kutolewa bure.

Enyi mnaolifanya Jina la Mungu litukanwe kwa sababu mmewalaghai watu kuwa chumvi na mafuta mnayouza yana upako, kumbe uongo, nawasihi, popote pale mlipo ulimwenguni, badilikeni. La sivyo unabii huu utatimia kwenu:

Mathayo 7:22-23 – "Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu."
Maisha magumu na watu wanataka kutakata kwa namna yoyote ile. Sasa huku kwenye imani wameona watu weusi wengi hawana uwezo wa kuchambua mambo na kuhoji. Wanapigwa wengi sana.
 
Paulo ni nani bwana wewe,mhuni mmoja tu hivi!!..yesu anahubiri hamtaki,anaondoka eti kamtokea akienda damascus,akampa utume
Kabla Paulo hajaokoka alikuwa akiitwa Sauli. Ni kweli Sauli alikuwa zaidi ya mhuni. Lakini Yesu alimbadilisha na kumtumia kuhubiri Injili na kutenda miujiza ya kupita kawaida, lakini HAKUUZA CHUMVI WALA MAFUTA kabla ya kuwaombea wagonjwa na wenye shida.
 
Dini ni UTAPELI.
Dini sio utapeli. Utapeli ni kuwaambia wagonjwa kwamba wakitaka kupona wanunue kwanza chumvi na mafuta ya upako. Yesu aliponya watu bure (free of charge).

Mathayo 9:35 (NEN)​

Yesu akazunguka katika miji yote na vijiji vyote, akifundisha katika masinagogi yao, akihubiri Habari Njema za ufalme, na akiponya kila ugonjwa na kila aina ya maradhi.
 
Paulo ni nani? je amemzidi YESU
Jibu hili hapa:
Warumi 1:1-17 BHN
Kutoka kwangu mimi Paulo, mtumishi wa Kristo Yesu, na mtume niliyeteuliwa na kuitwa kwa ajili ya kuhubiri Habari Njema ya Mungu. Hapo kale, Mungu aliwaahidi watu hii Habari Njema kwa njia ya manabii wake katika Maandiko Matakatifu. Hii Habari Njema inamhusu Mwana wa Mungu, Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kuhusu ubinadamu wake, alikuwa mzawa wa Daudi; kuhusu utakatifu wake wa kimungu, alithibitishwa kwa uwezo mkuu kwamba ni Mwana wa Mungu kwa kufufuliwa kutoka kwa wafu. Kwa njia yake, mimi nimepewa neema ya kuwa mtume, ili kwa ajili yake niwaongoze watu wa mataifa yote wapate kuamini na kutii...
 
Ukristo sio dini.
Dini ni biashara ,ukiona Ukristo umefanywa dini basi Kuna biashara ndani yake

Ukristo ni wokovu wa MUNGU kumtafuta mwanadamu aliyepotea dhambini

Dini ni njia , mishemishe, mbilingembilinge,harakati ,utapeli wa mwanadamu kutafuta pesa na ku manipulate watu kupitia jina la Mungu
 
Dini ni biashara ,ukiona Ukristo umefanywa dini basi Kuna biashara ndani yake

Ukristo ni wokovu wa MUNGU kumtafuta mwanadamu aliyepotea dhambini

Dini ni njia , mishemishe, mbilingembilinge,harakati ,utapeli wa mwanadamu kutafuta pesa na ku manipulate watu kupitia jina la Mungu
Duh! Umechanganya masomo... lakini
Dini iliyo safi na isiyo na hitilafu mbele ya Mungu Baba ni hii: Kuwasaidia yatima na wajane katika shida zao, na kujilinda mwenyewe usichafuliwe na ulimwengu huu.(Yakobo 1:27 BHN)
 
Duh! Umechanganya masomo... lakini
Dini iliyo safi na isiyo na hitilafu mbele ya Mungu Baba ni hii: Kuwasaidia yatima na wajane katika shida zao, na kujilinda mwenyewe usichafuliwe na ulimwengu huu.(Yakobo 1:27 BHN)
Dini iliyotajwa hapa sio hizi dini zenu mnazoita Leo

Kasome tafsiri mbalimbali utajua sio hizi dini zenu
 
Back
Top Bottom