Nafaka
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 12,154
- 31,246
Jaribu raid pia mkuu hata ukiipata supermarketHiyo hapana ktk maduka yetu huku ni hizo mbili RUNGU na HIT kukuta aina nyingine ni mpk uende Supermarket.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Jaribu raid pia mkuu hata ukiipata supermarketHiyo hapana ktk maduka yetu huku ni hizo mbili RUNGU na HIT kukuta aina nyingine ni mpk uende Supermarket.
😂😂😂😂Mweeeh! Dawa ya mbu 75k😳😳
Nyie maisha haya🙆🙆🙆
Naunga mkono hoja. Hii dawa nilianza kuishtukia muda. Bora na wewe umeliona hili. Dawa nzuri ya kupuliza ya mbu ni Rungu. HIT ni mtengenezaji ni MO?Hizi dawa zilikuwa vizuri miaka minne iliyopita ila hali ya sasa kwa kweli ni UTAPELI wa wazi.
1_ Haiui MBU kwa kiwango kinachopaswa yaani katika Mbu 50 watakufa watatu (3).
Yaan mpk mbu afe ni umloweshe na hiyo dawa ndio atakufa ila ukipuliza kama inavyoelekezwa upulize ktk mazingira ya eneo waliopo, hakika hatokufa Mbu hata mmoja, ukitaka mbu afe ni umshike umpulizie usoni.
2_ Hata Mbu kuzimia kidogo hakuna! Sana sana watajificha tu kwa muda wa lisaa limoja baada ya kupuliza ila watarudi na wakirudi wanarudi na NJAA ya kufa mtu. (Inawezekana hii Dawa ina wapa Appetite zaidi)
Si kwa HIT tu nimetumia dawa ya RUNGU pia haina matokeo mazuri ktk kuangamiza MBU.
Je wana JF mmekutana na hii changamoto?
Je mnapendekeza dawa ipi bora ya kuangamiza hawa viumbe?
NB: nimezungumzia kwa upande wa Mdudu aina ya MBU tu kwa kuwa ndio mdudu anayenisumbua mahala nilipo, hakuna Mende wala wadudu wengine, hivyo ufanisi wa dawa hii kwa kuua viumbe wengine sijaupima.
Nawasilisha.
Rungu kwa upande wangu haina matokeo au kuna RUNGU fake na OG?Naunga mkono hoja. Hii dawa nilianza kuishtukia muda. Bora na wewe umeliona hili. Dawa nzuri ya kupuliza ya mbu ni Rungu.
Tupo wengi..Nikajua peke yangu ndo naona hit na rungu hamna kitu kumbe tuko wengi
Ngoja nifatilie uzi nipate suluhisho jipya
Aisee. Rungu inaua mkuu zaidi ya HIT maradufu.Rungu kwa upande wangu haina matokeo au kuna RUNGU fake na OG?
Ntachukua RAID na Xpel. Nitaanza na moja kabla ya nyingineJaribu raid pia mkuu hata ukiipata supermarket
Weka mkato , ebu kwenye iyo figure.Nenda supermarket iliyo karibu yako,kanunue spray inaitwa SWASA inauzwa 75000/=....
utanishukuru baadae
Hapo ukwa 75k unapata dozi ngap za dawa ya mseto? Hahah😂😂😂😂
Mimi nilijua nimekosea kusoma ni 7,500/=, siwezi nunua dawa ya mbu ya 75K hao mbu wataona kama wanizike ama wanisafirishe...
Basi mie nauziwa fake nimetok kwenye RUNGU nikahamia HIT naona yale yale.Aisee. Rungu inaua mkuu zaidi ya HIT maradufu.
Debe 3 za mahindi hizooo [emoji23] [emoji23]nina mashaka sana kama atakua na hicho kiasi cha pesa mzee wangu [emoji23]
hataree sana 😂Debe 3 za mahindi hizooo [emoji23] [emoji23]
Rungu ni kali sana. Mimi ndiyo dawa ya mbu nayoiamini. Cha ajabu hata zile dawa za kuchoma za blue aka pellets siku hizi hazina ukali tena kama zamani.Basi mie nauziwa fake nimetok kwenye RUNGU nikahamia HIT naona yale yale.
Ipo..Hivi expel bado ipo?
Ulifanya mauwaji ya kimbari ya biodiversity mkuu [emoji23]miaka flani nyuma, kibanda hakijaisha vyema
niliziba madirisha, nilipiga chumbani, kwa kua inachoke nikatoka nje kwa mda wa dk 20
kurudi, nakuta mende, mijusi, nyoka wadogo, tandu, buibui, wote wamekufa wako pembeni
nilishangaa sana, ilihali lengo ilikua ni kuua mbu, nilishangaa pia kuona naishi na tandu chumbani [emoji28]
Ni kweli. Hili ni la siku nyingi sana. Sana sana unakuwa kama unawapulizia mbu perfume ili watoke out kuja kunyonya damu wakiwa wananukia vizuri. Vipi Expel siku hizi hamna? Jmabo jingine la kuzingatia ni kununua dawa kutoka vyanzo vinavyoaminika. Binadamu tumekuwa kama wanyama na tuko tayari kutengeneza dawa zenye madhara ili tu kupata fedha. Kama mchina mimi simwamini kabisa.Ni kama Air freshener.. tu
Tunaibiwa sana.
Mbona wadau wanazikandia hizo dawa za Rungu?Rungu ni kali sana. Mimi ndiyo dawa ya mbu nayoiamini. Cha ajabu hata zile dawa za kuchoma za blue aka pellets siku hizi hazina ukali tena kama zamani.
Kweli mkuu wanazimia tu halafu wanaamka. zamani ulikuwa unazoa/unafagia mbu kibao ukifukiza kwa dawa za kuchoma.Mbona wadau wanazikandia hizo dawa za Rungu?
Zile za kuchoma sas ndio huwa zinawazimisha.. Wanazimia kwa muda wakiamka wanarudi na Hasira na njaa.
Usiombe umeme ukatike maana feni inasaidia.
Dawa nyingi ni za kufukuza tu kaa muda yaan temporary solution.