Utapeli wa Dawa ya 'HIT' katika kuua Mbu

Utapeli wa Dawa ya 'HIT' katika kuua Mbu

Hizi dawa zilikuwa vizuri miaka minne iliyopita ila hali ya sasa kwa kweli ni UTAPELI wa wazi.

1_ Haiui MBU kwa kiwango kinachopaswa yaani katika Mbu 50 watakufa watatu (3).

Yaan mpk mbu afe ni umloweshe na hiyo dawa ndio atakufa ila ukipuliza kama inavyoelekezwa upulize ktk mazingira ya eneo waliopo, hakika hatokufa Mbu hata mmoja, ukitaka mbu afe ni umshike umpulizie usoni.

2_ Hata Mbu kuzimia kidogo hakuna! Sana sana watajificha tu kwa muda wa lisaa limoja baada ya kupuliza ila watarudi na wakirudi wanarudi na NJAA ya kufa mtu. (Inawezekana hii Dawa ina wapa Appetite zaidi)

Si kwa HIT tu nimetumia dawa ya RUNGU pia haina matokeo mazuri ktk kuangamiza MBU.

Je wana JF mmekutana na hii changamoto?

Je mnapendekeza dawa ipi bora ya kuangamiza hawa viumbe?

NB: nimezungumzia kwa upande wa Mdudu aina ya MBU tu kwa kuwa ndio mdudu anayenisumbua mahala nilipo, hakuna Mende wala wadudu wengine, hivyo ufanisi wa dawa hii kwa kuua viumbe wengine sijaupima.

Nawasilisha.
Naunga mkono hoja. Hii dawa nilianza kuishtukia muda. Bora na wewe umeliona hili. Dawa nzuri ya kupuliza ya mbu ni Rungu. HIT ni mtengenezaji ni MO?
 
miaka flani nyuma, kibanda hakijaisha vyema
niliziba madirisha, nilipiga chumbani, kwa kua inachoke nikatoka nje kwa mda wa dk 20

kurudi, nakuta mende, mijusi, nyoka wadogo, tandu, buibui, wote wamekufa wako pembeni
nilishangaa sana, ilihali lengo ilikua ni kuua mbu, nilishangaa pia kuona naishi na tandu chumbani [emoji28]
Ulifanya mauwaji ya kimbari ya biodiversity mkuu [emoji23]
 
Ni kama Air freshener.. tu

Tunaibiwa sana.
Ni kweli. Hili ni la siku nyingi sana. Sana sana unakuwa kama unawapulizia mbu perfume ili watoke out kuja kunyonya damu wakiwa wananukia vizuri. Vipi Expel siku hizi hamna? Jmabo jingine la kuzingatia ni kununua dawa kutoka vyanzo vinavyoaminika. Binadamu tumekuwa kama wanyama na tuko tayari kutengeneza dawa zenye madhara ili tu kupata fedha. Kama mchina mimi simwamini kabisa.
 
Rungu ni kali sana. Mimi ndiyo dawa ya mbu nayoiamini. Cha ajabu hata zile dawa za kuchoma za blue aka pellets siku hizi hazina ukali tena kama zamani.
Mbona wadau wanazikandia hizo dawa za Rungu?

Zile za kuchoma sas ndio huwa zinawazimisha.. Wanazimia kwa muda wakiamka wanarudi na Hasira na njaa.

Usiombe umeme ukatike maana feni inasaidia.

Dawa nyingi ni za kufukuza tu kaa muda yaan temporary solution.
 
Mbu wame evolve na kuweza kutengeneza usugu dhidi ya hizi dawa. Inatakiwa kununu dawa ya aina tofauti ili kupata matokeo chanya, jaribu kumtumia Ile dawa ya kuchoma inakua kwenye package ya silver .
 
Mbona wadau wanazikandia hizo dawa za Rungu?

Zile za kuchoma sas ndio huwa zinawazimisha.. Wanazimia kwa muda wakiamka wanarudi na Hasira na njaa.

Usiombe umeme ukatike maana feni inasaidia.

Dawa nyingi ni za kufukuza tu kaa muda yaan temporary solution.
Kweli mkuu wanazimia tu halafu wanaamka. zamani ulikuwa unazoa/unafagia mbu kibao ukifukiza kwa dawa za kuchoma.
 
Back
Top Bottom