Utaratibu wa kodi baada ya kupokea mzigo Posta ukoje?

Utaratibu wa kodi baada ya kupokea mzigo Posta ukoje?

Ngumbaru

JF-Expert Member
Joined
Apr 24, 2018
Posts
495
Reaction score
677
Wakuu, wiki kadhaa zilizopita nilinunua kifaa kutoka nje ya nchi, nimetumiwa mzigo wangu kwa njia ya POSTA.
jana nimetumiwa sms kuwa kifaa changu kimefika, nimenunua kifaa kwa bei ya shilingi, aaah dola 100.
Sasa kabla sijaenda kuchukua kifaa changu nimefanya mawasiliano na mtoa huduma wa POSTA aliyenitumia sms. Mimi nipo nje ya mji, nilimuomba anisaidie kujua gharama za kodi ili nijue kiasi cha pesa nimachotakiwa kwenda nacho kabla sijafunga safari ya kufuata mzigo wangu.
Bila hiyana mtoa huduma amekubali.

MAJIBU SASA: Baada ya mtoa huduma wa POSTA kukubali kunisaidia kuuliza gharama za kodi ninazotakiwa kulipia, amekuja na jibu kwamba ninatakiwa kulipia pesa taslimu shilingi laki moja na thelathini (137000), hii ni pesa za Kitanzania.

Sasa hapa nimebaki najiuliza maswali, hivi ni kweli kitu nilichokinunua kwa dola 100 (sawa na shilingi za Kitanzania 272000) natakiwa kukilipia kodi ya shilingi za Kitanzania 137000?
Watanzania wenzangu, hivi hii ni kweli au kuna makosa sehemu?

Hivi ni kweli serikali yetu imewapa TRA mamlaka ya kututoza Watanzania kodi zaidi ya 50% ya bei tunayonunulia vitu.

Aione!
Chief-Mkwawa
 
Hii ndio Tanzania ninayoijua, yaani hapo ndio utaijua Tanzania vizuri.
Nashindwa kuelewa hii ni strategy gani ya ukataji kodi. Kama tungekuwa tunazalisha hapa nchini kifaa nilichokiagiza, ningeelewa kuwa wanataka kuinua uzalishaji wa ndani na kudhibiti ushindani wa kibiashara dhidi ya bidhaa za nje. Lakini kifaa nilichokiagiza hatuzalishi hapa Tanzania.
 
Kupokea mzigo wowote kupitia Posta ni sawa na kununua huo mzigo mara mbili ya bei uliyonunulia. Hizi tozo ziwe za Posta au bandarini, hazina tofauti na kuagiza gari iliyotumika kutoka nje ya nchi. Bei ni mara mbili hadi unapoimiliki.

Miaka ya 2000 mwanzoni mtu wangu wa karibu anayeishi nje ya nchi alihamasika kunitumia vifurishi vya zawadi kupitia Posta, Ilibidi nimzuie kutuma kitu chochote kupita Posta yetu hii kwa sababu ni kichaka cha upigaji kinachofanywa na watumishi wa Serikali bila hata kuona aibu.

Ni bora utumie western Union ujue kabisa unatakiwa kulipia malipo ghari kuliko kukutana na ujanja ujanja wa wale jamaa wa customs pale posta.
 
Kupokea mzigo wowote kupitia Posta ni sawa na kununua huo mzigo mara mbili ya bei uliyonunulia. Hizi tozo ziwe za Posta au bandarini, hazina tofauti na kuagiza gari iliyotumika kutoka nje ya nchi. Bei ni mara mbili hadi unapoimiliki.

Miaka ya 2000 mwanzoni mtu wangu wa karibu anayeishi nje ya nchi alihamasika kunitumia vifurishi vya zawadi kupitia Posta, Ilibidi nimzuie kutuma kitu chochote kupita Posta yetu hii kwa sababu ni kichaka cha upigaji kinachofanywa na watumishi wa Serikali bila hata kuona aibu.

Ni bora utumie western Union ujue kabisa unatakiwa kulipia malipo ghari kuliko kukutana na ujanja ujanja wa wale jamaa wa customs pale posta.
Ina maana utaratibu wa ulipaji kodi kwa vitu tunavyoagiza nje haupo wazi?
Kodi unayotakiwa kulipia inatajwa tu na TRA officer kulingana na mood yake ilivyo wakati unakutana naye?
 
Kwa
Wakuu, wiki kadhaa zilizopita nilinunua kifaa kutoka nje ya nchi, nimetumiwa mzigo wangu kwa njia ya POSTA.
jana nimetumiwa sms kuwa kifaa changu kimefika, nimenunua kifaa kwa bei ya shilingi, aaah dola 100.
Sasa kabla sijaenda kuchukua kifaa changu nimefanya mawasiliano na mtoa huduma wa POSTA aliyenitumia sms. Mimi nipo nje ya mji, nilimuomba anisaidie kujua gharama za kodi ili nijue kiasi cha pesa nimachotakiwa kwenda nacho kabla sijafunga safari ya kufuata mzigo wangu.
Bila hiyana mtoa huduma amekubali.

MAJIBU SASA: Baada ya mtoa huduma wa POSTA kukubali kunisaidia kuuliza gharama za kodi ninazotakiwa kulipia, amekuja na jibu kwamba ninatakiwa kulipia pesa taslimu shilingi laki moja na thelathini (137000), hii ni pesa za Kitanzania.

Sasa hapa nimebaki najiuliza maswali, hivi ni kweli kitu nilichokinunua kwa dola 100 (sawa na shilingi za Kitanzania 272000) natakiwa kukilipia kodi ya shilingi za Kitanzania 137000?
Watanzania wenzangu, hivi hii ni kweli au kuna makosa sehemu?

Hivi ni kweli serikali yetu imewapa TRA mamlaka ya kututoza Watanzania kodi zaidi ya 50% ya bei tunayonunulia vitu.

Aione!
Chief-Mkwawa
Kosa ni lako. Unatumiwa SMS ukafuate mzigo posta, unaanza kuwauliza kodi. Kwani POSTA ni watoza ushuru?
 
Exactly, ukitaka kujifunza wewe wape assignment ya kuhakikisha wanakukabidhi huo mzigo na gharama zote utalipia bila ubishi uone meno ya shetani.

Bills watakayokupa iweke hapa tuijadili.... Utashangaa!!.
 
Kwa

Kosa ni lako. Unatumiwa SMS ukafuate mzigo posta, unaanza kuwauliza kodi. Kwani POSTA ni watoza ushuru?
Mkuu, mbona ukisoma taratibu uzi wangu utaelewa sababu ya mimi kuuliza kabla sijakwenda.

Anyways, tufanye nimefunga safari nimeenda kufuata mzigo. Kumbuka nipo nje ya mji, sipo Dar es Salaam. Nafika Posta kwenye wallet yangu kuna 40000, nafika pale ninaambiwa nilipie kodi 60000. Unadhani itakuwa sawa mimi kurudi ninapoishi kufuata pesa iliyopungua kisha nifunge tena safari nikachukue mzigo wangu?
 
Exactly, ukitaka kujifunza wewe wape assignment ya kuhakikisha wanakukabidhi huo mzigo na gharama zote utalipia bila ubishi uone meno ya shetani.

Bills watakayokupa iweke hapa tuijadili.... Utashangaa!!.
Duuuh!
Mimi nilijua kodi haiwezi kuvuka 20% ya bei niliyonunulia kifaa.
Ndio maana nilivyokiona kifaa huko mtandaoni wala sikujiuliza mara mbili kulipia.
 
MAJIBU SASA: Baada ya mtoa huduma wa POSTA kukubali kunisaidia kuuliza gharama za kodi ninazotakiwa kulipia, amekuja na jibu kwamba ninatakiwa kulipia pesa taslimu shilingi laki moja na thelathini (137000), hii ni pesa za Kitanzania.

Sasa hapa nimebaki najiuliza maswali, hivi ni kweli kitu nilichokinunua kwa dola 100 (sawa na shilingi za Kitanzania 272000) natakiwa kukilipia kodi ya shilingi za Kitanzania 137000?
Watanzania wenzangu, hivi hii ni kweli au kuna makosa sehemu?
Ni kweli, Ukifika utapewa control number a utalipia.

Katika mwongozo wa kodi inaonesha ni kati ya asilimia 30% hadi 50% ya invoice value.
1730290936489.png
Hiyo huwa haikwepeki. Na wakati mwingine hujitokeza gharama ya kodi kuzidi gharama ya manunuzi + usafiri. Yaani kodi inakuwa ni zaidi ya asilimia 100%.

Hii imejitokeza kwangu mara kadhaa, Mwana JF mmoja alilazimika kuutelekeza mzigo( Huu ulitoka ebay). Naa mwana JF mwingine aliamua kulipia hivyo hivyo( Mzigo huu ulitoka aliexpress), hakika inaumiza sana.

Hata mimi binafsi nishawahi telekeza mzigo baadaya ya ghrama za kodi + clerance kufikia 550,000 wakati thamani ya bdhaa ununuzi + kusafirisha ilikuwa TZS 360,000
 
Ni kweli, Ukifika utapewa control number a utalipia.

Katika mwongozo wa kodi inaonesha ni kati ya asilimia 30% hadi 50% ya invoice value.

Hiyo huwa haikwepeki. Na wakati mwingine hujitokeza gharama ya kodi kuzidi gharama ya manunuzi + usafiri. Yaani kodi inakuwa ni zaidi ya asilimia 100%.

Hii imejitokeza kwangu mara kadhaa, Mwana JF mmoja alilazimika kuutelekeza mzigo( Huu ulitoka ebay). Naa mwana JF mwingine aliamua kulipia hivyo hivyo( Mzigo huu ulitoka aliexpress), hakika inaumiza sana.

Hata mimi binafsi nishawahi telekeza mzigo baadaya ya ghrama za kodi + clerance kufikia 550,000 wakati thamani ya bdhaa ununuzi + kusafirisha ilikuwa TZS 360,000
Hii ndo Tanzania mzeebaba, hapo bado haujasema. Hajakosea

Mimi huwa natumiwa parcels kutoka Czech zenye thamani ya dollars mfano 120 halafu huku nalipa tena dollars karibia nusu ya bei ya mzigo, nfo.hata kuagiza magari ipo hivyo. Hapo hamna rushwa mkuu. Ndo utaratibu wa kodi za Kiafrika.

Hapa chini nimekuwekea mfano wa kodi niliyolipa juzijuzi ya mzigo wenye thamani ya 500,000. Noma sana mkuu, tena bado unatakiwa ulipe hela ya wao posta kama 5,900 kutegemea na mzigo wako ndo under huko kwenye kodi sasa. Yupo sahihi. Hajakosea
Asanteni sana wakuu, itoshe kusema....
NIMEKOMA, SITORUDIA TENA HUU UJINGA!
 
Back
Top Bottom