Utata kifo cha Afisa Usalama Kijitonyama

Utata kifo cha Afisa Usalama Kijitonyama

Fred Katulanda

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2011
Posts
380
Reaction score
550
Utata umeibuka kuhusiana na kifo cha Ofisa Usalama wa Taifa, Peter Tyenyi, ambaye mwili wake umekutwa ndani ya kisima cha maji kilichopo eneo la ofisi za idara zilizopo Kijitonyama, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza kwa njia ya simu, msemaji wa familia ambaye ni kaka wa marehemu, John Tyenyi alisema mwili wa Peter (53) ulikutwa juzi ukiwa ndani ya kisima cha maji kilicho ndani ya eneo la Ofisi za Usalama wa Taifa, Kijitonyama baada ya kutoweka tangu Jumatatu ya Mei 27, alipoaga kwenda kazini.

"Peter alitoweka tangu Jumatatu alipoaga kwenda kazini. Mimi nimepigiwa simu jana saa tano asubuhi nikiwa Mombasa nchini Kenya kwamba amepatikana akiwa ndani ya shimo la maji," alisema John.

Baadhi ya ndugu zake waliozungumza kwa sharti la kutotajwa majina wakiwa msibani Kigamboni jijini Dar es Salaam, walisema kuwa baada ya ndugu yao kutoweka mkewe Joyce Mwakilama aliwataarifu na kuwasiliana na ofisi yake, lakini aliambiwa kuwa hata huko hayupo.

"Tuliwajulisha Usalama wa Taifa wakasema hata wao hawajui. Lakini jana (juzi) wakatupigia simu kuwa amekutwa kwenye kisima cha maji baada ya kutokea shida ya maji," alisema mmoja wa wanafamilia kwa sharti la kutotajwa jina na kuongeza:

"Walisema kuwa kisima hicho huwa kinalindwa, lakini tunashangaa ndugu yetu aliingiaje humo."

Ndugu mwingine alisema: "Awali tuliambiwa kuwa ndugu yetu yuko Muhimbili, tukaenda kuulizia tukamkosa. Baadaye tukaambiwa yuko hospitali ya Lugalo, huko tukamkuta ameshaandaliwa kwa mazishi. Tulipouliza tukaambiwa kibali cha kuzika kiko tayari na usafiri wa ndege uko tayari tujiandae kusafirisha."

Hata hivyo, msemaji wa familia John Tyeni alisema kuwa ndugu hao walipinga kuusafirisha mwili huo, hadi ufanyiwe uchunguzi (post mortem).

"Tulipokwenda hospitali tukakuta maofisa usalama wamemchukua OCD wa Wilaya ya Kinondoni Wilbrod Mutangungwa na askari wawili na kwenda kufanya post mortem. Yaani kulikuwa na ujanja ujanja unafanyika. Sisi tukamchukua Ofisa Upelelezi Mkoa wa Kinondoni, RCO Kimola na askari wawili na wapigapicha ndiyo tukafanya post mortem," alisema John.

Akizungumzia matokeo ya uchunguzi huo, John alisema kuwa watapewa matokeo hayo baada ya kutoka kwenye mazishi yatakayofanyika Musoma mjini mkoani Mara, baada ya kusafirishwa leo.

Hata hivyo alisema kuwa macho yake yalikuwa yametoka nje kwa sababu ya kujaa maji.

Baadhi ya ndugu wa marehemu walidai kuwa mwili wake ulikutwa ukiwa umetumbuliwa macho huku nguo na viatu vikiwa bado mwilini.
Akizungumzia kifo hicho, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela alikiri kutokea tukio hilo na kusema kuwa bado uchunguzi unaendelea.

"Ni kweli kuna ofisa usalama amefariki ndani ya kisima, lakini bado tunachunguza. Kwa sababu itabidi tupate taarifa ya daktari ndiyo tuunganishe na uchunguzi wetu," alisema Kenyela.

SOURCE: Kifo cha Ofisa Usalama chazua utata - Habari - mwananchi.co.tz

SERIAL DEATHS OF SPIES IS NOT SOMETHING UN-USUAL ,ITS ONLY THIS WEEK THAT WE LEARNED THAT IT WAS IMRAN KOMBE INFACT WHO ORDERED MORINGE SOKOINE"S PERSONAL BODYGUARDS TO HEAD TOWARD MONDULI INSTEAD OF ACCOMPANY HE FORMER PREMIER TO ROAD TRIP TO DAR......FEW PEOPLE KNOW THAT WHEN IMRAN WAS KILLED HIM AND HIS WIFE WERE ON THE WAY TO FLEE THE COUNTRY TO CANADA AFTER SMELT FISH....ON HIS ROLE AHEAD OF 1995 ELECTIONS...
.....THE THEN DEATH OF ANOTHER SPY THIS WEEK IN THERE COMPOUND ...IS NOT SOMETHING NEW...TWO YEARS AGO FORMER CHIEF JUSTICE BOARDGUARD WAS FOUND DEAD ..IN SUSPECTIVE ENVIRONMENT..IT WAS QUICK COVERED ....
WE DONT KNOW THE REASON FOR YET AGAIN THIS LATEST ONE....ONE THING IS WE ARE NOT SUPPOSED TO WASTE OUR VOICES SINCE IN SPY PROFFESSION THERE IS A PRICE TO PAY WHEN YOU ARE CONSIDERED A THREAT A TRAITOR ....WHO KNOWS ...MAY BE THIS IS A MESSAGE TO SPIES INVOLVED IN RECENT LEAKAGES .....,
COMING ACROSS ANY TOP SECRET IS ANOTHER REASON TO DIE ..PASSIONATELY IF YOU ARE CONSIDERED NOT STRONG ENOUGH TO KEEP SECRET....

THEY WERE SWORN TO DIE THESE KIND OF DEATHS ....SO FOR LOVED ONE BURY YOUR DEAD ..YOU HAVE NOTHING TO ASK !!!!! LIFE GOES ON!!
HIVI NDIVYO AFISA USALAMA WA TAIFA ALIVYOUWAWA KIKATILI NA KUZAMISHWA NDANI YA KISIMA CHA MAJI HUKO KIJITONYAMA...!!



Tuesday, June 4, 2013 | 12:18 PM






AFISA Usalama wa Taifa, Peter Patrick Tyenyi ,53, ambaye maiti yake ilikutwa Mei 27, mwaka huu katika kisima cha maji masafi kilichopo maeneo ya ofisini kwao, Kijitonyama Makumbusho jijini Dar, kifo chake kimetajwa kuwa ni cha kimafia.

Chanzo chetu makini ndani ya familia ya marehemu kimedai kuwa wao wanaamini kuwa ndugu yao hakufa kifo cha kawaida isipokuwa kuna mkono wa mtu.
Wanafamilia hao wanadai kuwa kifo hicho ni cha kimafia kwa sababu kisima kilichokutwa mwili huwa siyo rahisi mtu kuingia bila kuonekana.
Habari zinasema siku hiyo ya kutoweka kwake, asubuhi afisa huyo alitoka nyumbani kwake maeneo ya Kijitonyama akiwa na afya njema.
umafia.jpg

Kiliendelea kusema kwamba mara baada ya afisa huyo kufika ofisini, walikaa kikao cha kazini na mara baada ya kumalizika hakuonekana tena.
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa ofisa huyo alitafutwa kwa njia ya simu baada ya kutoonekana ofisini kwa saa kadhaa lakini zote zikawa hazipatikani.
Imeelezwa kuwa baadhi ya wafanyakazi wenzake waliingiwa na hofu kwa vile haikuwa kawaida yake kuondoka ofisini bila kuaga na hakuwa na tabia ya kuzima simu zake zote.
Habari zaidi zinaeleza kuwa kutoonekana kwa marehemu kwa saa kadhaa, kuliwafanya ndugu zake wapigiwe simu na maofisa wa idara ya usalama wa taifa kuulizwa na ikabidi wafike ofisini kwake ili kupata taarifa kamili.
UMAFIA3.jpg


Inasemekana kuwa mara baada ya ndugu hao kupewa taarifa hizo waliingiwa hofu, hali iliyowafanya waanze kutembelea baadhi ya hospitali za hapa Dar lakini hawakufanikiwa kupata taarifa zozote kuhusu ndugu yao huyo.
Wakati ndugu zake wanaendelea kumtafuta kwa siku za Jumanne na Jumatano, zikapatikana taarifa kuwa kuna mwili umeonekana katika kisima cha maji masafi kilichopo maeneo ya ofisini kwake.
Imedaiwa kuwa siku ya Alhamisi ambayo mwili ulionekana, maji yalikuwa yamekatika na mmoja wa wafanyakazi wa idara hiyo alikwenda kwenye kisima hicho ndipo alipouona mwili na kutoa taarifa kwa uongozi.
UMAFIA4.jpg


Imeelezwa kuwa baada ya uongozi kupata taarifa hizo, walienda kushuhudia na kuutambua kuwa ni wa Tyenyi.
Mwili huo ulikutwa ukiwa umeharibika na ulichukuliwa hadi Hospitali Kuu ya Jeshi la Wananchi Tanzania, Lugalo.
"Ndugu wa marehemu ilibidi wapewe taarifa ambapo walifika alipokua akifanyia kazi kisha kwenda Lugalo na kuutambua mwili," kilisema chanzo hicho.
Mwili huo ulifanyiwa uchunguzi (post mortem) na wanandugu waliruhusiwa kuuchukua tayari kwa mazishi.
Muda wote kabla mwili haujasafirishwa kwenda Musoma kwa mazishi, msiba ulikuwa kwa mdogo wake aitwaye Julius Patrick, Kigamboni.
Kwa mujibu wa familia kupitia kwa Julius, mwili ulisafirishwa kwa ndege Jumamosi asubuhi ya wiki iliyopita na kuzikwa siku hiyohiyo jioni lakini majibu ya uchunguzi hayajapatikana.
UMAFIA5.jpg

Marehemu ameacha watoto watatu na maofisa wa polisi wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo lakini wakasema msemaji ni mkuu wao, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, ACP Charles Kenyela.
UMAFIA6.jpg

ACP Kenyela alipopigiwa simu alithibitisha kutokea tukio hilo.
"Ni kweli mwili wa marehemu ulikutwa kwenye kisima chao lakini upelelezi bado unaendelea," alisema Kenyela.




Read more: HIVI NDIVYO AFISA USALAMA WA TAIFA ALIVYOUWAWA KIKATILI NA KUZAMISHWA NDANI YA KISIMA CHA MAJI HUKO KIJITONYAMA...!! - GUMZO LA JIJI
 
SERIAL DEATHS OF SPIES IS NOT SOMETHING UN-USUAL ,ITS ONLY THIS WEEK THAT WE LEARNED THAT IT WAS IMRAN KOMBE INFACT WHO ORDERED MORINGE SOKOINE"S PERSONAL BODYGUARDS TO HEAD TOWARD MONDULI INSTEAD OF ACCOMPANY HE FORMER PREMIER TO ROAD TRIP TO DAR......FEW PEOPLE KNOW THAT WHEN IMRAN WAS KILLED HIM AND HIS WIFE WERE ON THE WAY TO FLEE THE COUNTRY TO CANADA AFTER SMELT FISH....ON HIS ROLE AHEAD OF 1995 ELECTIONS...
.....THE THEN DEATH OF ANOTHER SPY THIS WEEK IN THERE COMPOUND ...IS NOT SOMETHING NEW...TWO YEARS AGO FORMER CHIEF JUSTICE BOARDGUARD WAS FOUND DEAD ..IN SUSPECTIVE ENVIRONMENT..IT WAS QUICK COVERED ....
WE DONT KNOW THE REASON FOR YET AGAIN THIS LATEST ONE....ONE THING IS WE ARE NOT SUPPOSED TO WASTE OUR VOICES SINCE IN SPY PROFFESSION THERE IS A PRICE TO PAY WHEN YOU ARE CONSIDERED A THREAT A TRAITOR ....WHO KNOWS ...MAY BE THIS IS A MESSAGE TO SPIES INVOLVED IN RECENT LEAKAGES .....,
COMING ACROSS ANY TOP SECRET IS ANOTHER REASON TO DIE ..PASSIONATELY IF YOU ARE CONSIDERED NOT STRONG ENOUGH TO KEEP SECRET....

THEY WERE SWORN TO DIE THESE KIND OF DEATHS ....SO FOR LOVED ONE BURY YOUR DEAD ..YOU HAVE NOTHING TO ASK !!!!! LIFE GOES ON!!


Utata umeibuka kuhusiana na kifo cha Ofisa Usalama wa Taifa, Peter Tyenyi, ambaye mwili wake umekutwa ndani ya kisima cha maji kilichopo eneo la ofisi za idara zilizopo Kijitonyama, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza kwa njia ya simu, msemaji wa familia ambaye ni kaka wa marehemu, John Tyenyi alisema mwili wa Peter (53) ulikutwa juzi ukiwa ndani ya kisima cha maji kilicho ndani ya eneo la Ofisi za Usalama wa Taifa, Kijitonyama baada ya kutoweka tangu Jumatatu ya Mei 27, alipoaga kwenda kazini.

“Peter alitoweka tangu Jumatatu alipoaga kwenda kazini. Mimi nimepigiwa simu jana saa tano asubuhi nikiwa Mombasa nchini Kenya kwamba amepatikana akiwa ndani ya shimo la maji,” alisema John.

Baadhi ya ndugu zake waliozungumza kwa sharti la kutotajwa majina wakiwa msibani Kigamboni jijini Dar es Salaam, walisema kuwa baada ya ndugu yao kutoweka mkewe Joyce Mwakilama aliwataarifu na kuwasiliana na ofisi yake, lakini aliambiwa kuwa hata huko hayupo.

“Tuliwajulisha Usalama wa Taifa wakasema hata wao hawajui. Lakini jana (juzi) wakatupigia simu kuwa amekutwa kwenye kisima cha maji baada ya kutokea shida ya maji,” alisema mmoja wa wanafamilia kwa sharti la kutotajwa jina na kuongeza:

“Walisema kuwa kisima hicho huwa kinalindwa, lakini tunashangaa ndugu yetu aliingiaje humo.”

Ndugu mwingine alisema: “Awali tuliambiwa kuwa ndugu yetu yuko Muhimbili, tukaenda kuulizia tukamkosa. Baadaye tukaambiwa yuko hospitali ya Lugalo, huko tukamkuta ameshaandaliwa kwa mazishi. Tulipouliza tukaambiwa kibali cha kuzika kiko tayari na usafiri wa ndege uko tayari tujiandae kusafirisha.”

Hata hivyo, msemaji wa familia John Tyeni alisema kuwa ndugu hao walipinga kuusafirisha mwili huo, hadi ufanyiwe uchunguzi (post mortem).

“Tulipokwenda hospitali tukakuta maofisa usalama wamemchukua OCD wa Wilaya ya Kinondoni Wilbrod Mutangungwa na askari wawili na kwenda kufanya post mortem. Yaani kulikuwa na ujanja ujanja unafanyika. Sisi tukamchukua Ofisa Upelelezi Mkoa wa Kinondoni, RCO Kimola na askari wawili na wapigapicha ndiyo tukafanya post mortem,” alisema John.

Akizungumzia matokeo ya uchunguzi huo, John alisema kuwa watapewa matokeo hayo baada ya kutoka kwenye mazishi yatakayofanyika Musoma mjini mkoani Mara, baada ya kusafirishwa leo.

Hata hivyo alisema kuwa macho yake yalikuwa yametoka nje kwa sababu ya kujaa maji.

Baadhi ya ndugu wa marehemu walidai kuwa mwili wake ulikutwa ukiwa umetumbuliwa macho huku nguo na viatu vikiwa bado mwilini.
 
Interesting kuna thread ilisema anaposafiri JK tega sikio kuna tukio

Huyo atakuwa walimpeleka quater guard au torture chamber ..kutakuwa kuna kosa alifanya ....la kiutendaji....huenda hawakuwa na nia afe ..labda gwaride likawa gumu!!
Nashangaa kwa nini wakakubali kuonesha amefia kisimani ...inaonekana sikuhizi TISS hakuna smooth operators ......la sivyo angetakiwa tu akutwe Mortuary...na msg tu kuwa aliokotwa barabarani ....
Taarifa kama hizi kwa kipindi hiki sio nzuri zinaleta tension bure bungeni ..... unless alikuwa anauza siri na wametaka kutuma message kwa waliokuwa wakimtuma na wengine wenye tabia kama zake
 
Huyo atakuwa walimpeleka quater guard au torture chamber ..kutakuwa kuna kosa alifanya ....la kiutendaji....huenda hawakuwa na nia afe ..labda gwaride likawa gumu!!
Nashangaa kwa nini wakakubali kuonesha amefia kisimani ...inaonekana sikuhizi TISS hakuna smooth operators ......la sivyo angetakiwa tu akutwe Mortuary...na msg tu kuwa aliokotwa barabarani ....
Taarifa kama hizi kwa kipindi hiki sio nzuri zinaleta tension bure bungeni ..... unless alikuwa anauza siri na wametaka kutuma message kwa waliokuwa wakimtuma na wengine wenye tabia kama zake
Mkuu kama siri ni shughuli za watawala wapuuzi apumnzike salama
 
Back
Top Bottom