Utata wa mpaka wa ziwa Nyasa: Google map wako sahihi kwa 100%, serikali ya Tanzania msipotoshe na kutisha watu

Utata wa mpaka wa ziwa Nyasa: Google map wako sahihi kwa 100%, serikali ya Tanzania msipotoshe na kutisha watu

Unajua kwamba OAU walikubaliana kuwa mipaka ya kikoloni ndio iendelee kutumika baada ya uhuru?

Yani unataka kusema kwamba nchi za Afrika tuna busara sana kwahiyo tuanze kuchora upya mipaka. Unazijua akili za Mwafrika kweli mkuu?

Yani turudie kuchora, Uganda wapendekeze kupata Kagera salient, Kenya wapendekeze kupata mlima Kilimanjaro pale ambapo ramani ilipindishwa ili mlima uwe Tanzania, Zanzibar wadai pwani ya bara maana kuna Sultan aliwahi sema anaimiliki na akiwapa Wajerumani sijui, Tanzania tudai sehemu ya Masai Mara ya Kenya ili Wamasai wote wawe Tanzania, Kenya wapendekeze waongezewe sehemu ya ziwa Victoria wawe nayo nyingi maana Tanzania imechukua kipande kikubwa zaidi, Burundi nao waombe sehemu kubwa zaidi ya ziwa Tanganyika. Hapo ni sisi tu, bado sehemu nyingine za Afrika.

Kiuhalisia ukisoma Helligoland treaty na mkataba mwingine, hakuna ushahidi unaoonyesha Tanzania tunamiliki nusu ya ziwa Nyasa. Hata Wajerumani waliokuwa wanatawaka Tanganyika ramani yao inaonyesha Nyasa nzima ni ya Malawi.

Sisi Tanzania tunakuwa na claim kuwa wazungu walikubaliana kama kuna chanzo cha maji mpakani basi kigawanywe kila nchi inayopakana ipate kiasi chake. But that wasn't the case kwa ziwa Nyasa. Tukienda mahakama ya usuluhishi, zikaletwa mikataba na mashahidi wakoloni Tanzania tunashindwa asubuhi na mapema kabisa.
Kuna jamii na makabila yapo upande wa tanzania yalikuwa yanatumia ziwa nyasa kuvua zaidi ya miaka 1000+ kabla hata ya ukoloni leo unawaambia wasitumie kwa sababu ziwa ni la nchi ya malawi unadhani ina-make sense
 
Naamini huyu mpemba atakuwa ametumwa kupima upepo,namshukuru Mungu ameshauona upepo Upo vipi..
 
Ukweli usemwe na sio kupotoshwa.
Ziwa Nyasa ni mali ya Malawi kisheria, Tanzania mpaka leo tunaendelea kudai haki ya kudhurumiwa kupata sehemu ya ziwa. Hicho ndio google map wamefanya.
Wewe ndiyo ulikuwa unapinga serikali isisitishe mkataba wa songas eeeh ok
 
Wakati wa masika tenende yote Ile inafurika maji hadi inakuwa ngumu kupita kwenda Ipinda na kyela...maji yoote yanakwenda Sumbi...halafu mpemba mmoja anakuja kusema maji yakishaingia kwa Sumbi...yanakuwa siyo yetu tena,yanakuwa ya Malawi..
 
Hili jambo litaleta shida huko mbeleni. JPM angekuwa mtu sahihi wa kulimaliza.
Hakuna shida yoyote ...mpaka wakusadikika utakuwa huo wa mabeberu na mpaka halisi utakuwa katikati ya ziwa over ....wala msiwe na wasiwasi wowote kwenye jambo hilo
 
You are an asshole, wewe umezaliwa, hukuijua google, umeanza kuijua google, kuanzia 2000+, lakini upo hapa kutetea usahihi w google map, software ambayo haikuwepo miaka ya 60!,
Sheria za kimataifa, mipaka kwenye maji upo Kati Kati! It's a universal law!
Na logic ni ndogo tu, pwani za mito, maziwa, bahari hahaha, kwa kumongonyoa udongo, ukisema mpaka wa Malawi upo mwanzo wa ziwa kwa upande wa Tz, ipo siku Mbeya yote itakuwa Malawi! Maana mpaka huhama,unatumia vigezo gani kusema google ipo sahihi, google imetengenezwa na watu, sio bible, data ilizonazo,zimewekwa na watu,
Ur so fucking stupid, this is very treasonous! You must be hanged
UMEMALIZA KILA KITU 🫡🤝
 
Serikali ya Tanzania imetoa tamko la marufuku ya kuzuia matumizi ya google map yenye kuonyesha mpaka wa Tanzania na Malawi kwenye ziwa Nyasa ulipo kutumika kufundishia mashuleni. Kwenye ramani hiyo ya google inaonyesha mpaka wa kisheria uko pwani ya Ziwa Nyasa upande wa Tanzania na hapo hapo kuonyesha mpaka ambao Tanzania inadai ambao uko katikati ya Ziwa Nyasa. Kimsingi google map wako sahihi kwa 100%. Huo ndio ukweli ambao umekuwepo siku zote kabla hata ya kupata Uhuru na baada ya kupata uhuru.

Mpaka leo hii Tanzania tunadai kupata haki ya kumiliki karibu nusu ya Ziwa Nyasa lakini hiyo haiondoi ukweli kuwa Malawi bado wana umiliki wa Ziwa Nyasa lote katika mpaka wake na Tanzania. Ni ukweli mchungu dhidi ya Tanzania na ukweli usio wa haki. Lakini ndio ukweli halisi. Tuna haki ya kudai ubadilishwe lakini hatuna haki ya kuupotosha.

Zama za kuwadanganya watu kielimu na kuwatisha wasijifunze kujua nini dunia inasema na kutambua (tofauti na vile walivyoaminishwa awali) kuhusu jeografia, historia na sayansi zimepitwa na wakati.

Kulingana na ramani uliyoiweka ndugu Zanzibar-ASP, ninkwamba ziwa hilo limegusa nchi tatu, Malawi, Mozambique na Tanzania.

Kulingana na ramani hiyo, kwenye nchi za Malawi na Tanzania, mpaka umepita kwenye ufukwe upande wa TZ. Lakini unapoambaa na mpaka huo mpaka nchini Mozambique, unagundua kwamba mpaka unarudi katikati ya ziwa, hapo mimi ndio sijaelewa aisee!!

Kwamba, kati ya Malawi na TZ mpaka upo ufukweni kwetu, ila kati ya Malawi na Mozambique mpaka upo katikati ya ziwa, inakuwaje hapo?

Pia ukiangalia mipaka kwenye maziwa mengine yanayounganisha nchi na nchi, mipaka inakuwa katikati ya ziwa!

Sasa kwanini kipande cha Tanzania na Malawi mpaka uwe ufukweni TZ ila kipande cha Malawi na Mozambique mpaka uwe katikati kama maziwa mengine?
 
Mtu sahihi alikuwa Nyerere (kwa sababu alikuwa na ushawishi), na labda Kikwete (alikuwa ni mwanadiplomasia mzuri), tofauti na hapo tupate rais mwenye kujua sheria za kimataifa vizuri (hapa nadhani Lissu atatufaa zaidi). Magufuli angeishia kutumia nguvu (jeshi), Ziwa tungelipata lakini tungeshindwa kulitumia, lingeishia kuwa kambi ya wanajeshi wa majini.
Huyo Kikwete alishindwa vibaya mno alichofanya ni kumtishia Joyce Banda kwamba atapeleja jeshi
 
sheria za UN zinatamka wazi, mipaka ya kikoloni ya kisheria ndio mipaka rasmi baada ya uhuru. Mpaka wa kikoloni unatamka wazi kuwa Ziwa Nyasa lote ni mali ya Malawi
Naomba vifungu viwili tuu sehemu ilipoandikwa lake nyasa ni mali halali ya wamalawi
 
Serikali ya Tanzania imetoa tamko la marufuku ya kuzuia matumizi ya google map yenye kuonyesha mpaka wa Tanzania na Malawi kwenye ziwa Nyasa ulipo kutumika kufundishia mashuleni. Kwenye ramani hiyo ya google inaonyesha mpaka wa kisheria uko pwani ya Ziwa Nyasa upande wa Tanzania na hapo hapo kuonyesha mpaka ambao Tanzania inadai ambao uko katikati ya Ziwa Nyasa. Kimsingi google map wako sahihi kwa 100%. Huo ndio ukweli ambao umekuwepo siku zote kabla hata ya kupata Uhuru na baada ya kupata uhuru.

Mpaka leo hii Tanzania tunadai kupata haki ya kumiliki karibu nusu ya Ziwa Nyasa lakini hiyo haiondoi ukweli kuwa Malawi bado wana umiliki wa Ziwa Nyasa lote katika mpaka wake na Tanzania. Ni ukweli mchungu dhidi ya Tanzania na ukweli usio wa haki. Lakini ndio ukweli halisi. Tuna haki ya kudai ubadilishwe lakini hatuna haki ya kuupotosha.

Zama za kuwadanganya watu kielimu na kuwatisha wasijifunze kujua nini dunia inasema na kutambua (tofauti na vile walivyoaminishwa awali) kuhusu jeografia, historia na sayansi zimepitwa na wakati.
Angalau kuwa mzalendo; yanapotokea masuala ya kitaifa huwa haifai kuegemea upande wa pili.
Tupambane kwa jasho na damu tunufaike na ziwa nyasa, mipaka iliwekwa na mkoloni wala muafrika hakuweka mipaka.
Babu zetu walinufaika na ziwa nyasa miaka nenda rudi, iweje mkoloni atugawe?
Afrika mashariki yote Tanzania inanufaika na ziwa Victoria, Ziwa Tanganyika, Ziwa Nyasa na mito kama kagera na mto ruvuma ambayo imegawa Nchi, pamoja na hivyo tunanufaika na bahari pia.

Kumiliki nusu ya ziwa ni muhimu sana kwa masuala ya usalama wa nchi, leo ww unaleta ujinga wa kutetea malawi, WHY??
Wewe na Wamalawi acheni ubinafsi
 
Wewe ni under 18,ramani zote za vitabu vya zamani zinaonyesha mpaka upo kati kati ya ziwa lakini Kuna version mpya ya vitabu kuanzia miaka ya 2000 viliteta shida
 
Serikali ya Tanzania imetoa tamko la marufuku ya kuzuia matumizi ya google map yenye kuonyesha mpaka wa Tanzania na Malawi kwenye ziwa Nyasa ulipo kutumika kufundishia mashuleni. Kwenye ramani hiyo ya google inaonyesha mpaka wa kisheria uko pwani ya Ziwa Nyasa upande wa Tanzania na hapo hapo kuonyesha mpaka ambao Tanzania inadai ambao uko katikati ya Ziwa Nyasa. Kimsingi google map wako sahihi kwa 100%. Huo ndio ukweli ambao umekuwepo siku zote kabla hata ya kupata Uhuru na baada ya kupata uhuru.

Mpaka leo hii Tanzania tunadai kupata haki ya kumiliki karibu nusu ya Ziwa Nyasa lakini hiyo haiondoi ukweli kuwa Malawi bado wana umiliki wa Ziwa Nyasa lote katika mpaka wake na Tanzania. Ni ukweli mchungu dhidi ya Tanzania na ukweli usio wa haki. Lakini ndio ukweli halisi. Tuna haki ya kudai ubadilishwe lakini hatuna haki ya kuupotosha.

Zama za kuwadanganya watu kielimu na kuwatisha wasijifunze kujua nini dunia inasema na kutambua (tofauti na vile walivyoaminishwa awali) kuhusu jeografia, historia na sayansi zimepitwa na wakati.
Angalia mambo ya fursa na mipaka ya nyumba yako au familia yako,haya mambo ya kumsaidia Hangaya haya tusaidii chochote
 
Back
Top Bottom