Utata wa Sheria na Kanuni hizi za Bunge la Katiba utazaa Katiba ya mtaa wa Lumumba

Utata wa Sheria na Kanuni hizi za Bunge la Katiba utazaa Katiba ya mtaa wa Lumumba

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2010
Posts
17,005
Reaction score
20,425
Wakuu nimekiwa kwenye lindi la msongo wa mawazo mazito juu ya upatikanaji wa katiba ya umma,

Utata wa sheria ya katiba mpya.

Kwenye tafsiri ya kiswahili inatafsiriwa hivi:

1. Tafsiri ya kifungu cha 25 (2)cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba juu ya Majukumu ya Bunge la Katiba Mpya inasema hivi: "Bunge Maalumu la Katiba litakuwa na jukumu la kuijadili rasimu ya Katiba na kuipitisha tu"

Sheria hii ya mabadiliko ya Katiba inalifunga Bunge Maalumu la Katiba kuishia katika kujadili na kupitisha rasimu hiyo bila kuondoa neno wala kuongeza neno litakalobadili maana ya neo hilo.

Vivyo hivyo Bunge la katiba litafanya kazi ya kuboresha masharti ya Katiba yaliyomo ndani ya rasimu ya Katiba pasipo kuweka masharti mapya ambayo kwa taathira yatabadili ama kufifisha masharti ya kikatiba yaliyomo kwenye Rasimu hii ya Katiba Mpya.


Lakini kwenye tafsiri ya sheria ile ya kiingereza kifungu hichohicho inatoa ruhusa kwa Bunge la katiba, kujadili, kuondoa kifungu, kutunga kifungu ama KUIONDOA/KUIFUTA kabisa rasimu ile ya Mzee Warioba ambayo ndio maoni ya umma na kuleta rasimu yao ya Lumumba,

Utata huo hauishii kwenye Sheria tu bali upo pia kwenye KANUNI za uendesha wa Bunge lenyewe la katiba,


Mathalani ukakasi wa kanuni ya 48 ya uendeshaji wa bunge la katiba unaosema kutakuwa na mambo ya faragha katika utungaji wa katiba hiyo,


Watanzania lazima tureje hata kwenye historia ya nchi yetu, Tujifunze huko ambapo tunaona wazi kuwa hata Lancaster House hapakuwa na faragha wakati Wazungu wakiandika katiba ya kwanza ya Tanganyika!

Katiba hutungwa na watu na bunge la katiba ni bunge la watu kwa niaba ya watanzania!

Watanzania tusimame tukatae uimla huu, sasa tuwaeleze hawa mabeberu wa ndani kuwa MAPINDUZI ya kiraia hayaepukiki ikiwa watafinyanga matakwa ya umma,

Jionee vifungu vyenye utata hapa chini.

Kwa mwendo huu katiba ni kiini macho chenya maslahi ya wavimbisha matumbo lakini si kwa maslahi ya nchi na watanzaia wenye dhamira ya kweli na nchi yao.


View attachment 141123View attachment 141124View attachment 141125View attachment 141126View attachment 141127View attachment 141128View attachment 141125View attachment 141129
 
Mkuu naona kama hakuna attachment/link au ndo simu inanisaliti?
 
Mkuu naona kama hakuna attachment/link au ndo simu inanisaliti?

Nimemtumia Max anisaidie kuziweka, naona yupo mbali kidogo, naomba kama upo Wasapu nitumie namba yako kwa pm nikutumie mkuu wangu,
 
vipi biashara yako ya vitabu na udhamini wa u.s aid unaendeleaje?.naona mbowe boss wako amepata zali la kushuglikia posho iongezwe japo ifikie laki 6 akulipe na wewe houseboy wake.
 
Kama watachakachua katiba mpya,basi nawaomba wapinzani ajenda kubwa ya uchaguzi ujao iwe ni kutengeneza KATIBA MPYA ya watanzania!
 
Nimemtumia Max anisaidie kuziweka, naona yupo mbali kidogo, naomba kama upo Wasapu nitumie namba yako kwa pm nikutumie mkuu wangu,

Wasapu ndo nini? Shule kitu mhimu sana. Kila wakati unakuja na ushuzi mtupu kama mwendawazimu mwenye makengeza Mbowe
 
Kwa mwendo huu katiba ni kiini macho chenya maslahi ya wavimbisha matumbo lakini si kwa maslahi ya nchi na watanzaia wenye dhamira ya kweli na nchi yao.


katiba 1.jpgkatiba2.jpgkatiba3.jpgkatiba4.jpgkatiba5.jpgkatiba6.jpgkatiba3.jpgkatiba8.jpg
 
vipi biashara yako ya vitabu na udhamini wa u.s aid unaendeleaje?.naona mbowe boss wako amepata zali la kushuglikia posho iongezwe japo ifikie laki 6 akulipe na wewe houseboy wake.
Mkuu, mjadala hauna uhusiano na ulichoandika kwa nini usifungue thread yako ili utoe haya unayosema kwa kujenga heshima yako na ya JF?

Mambo ya kutusi watu hadharani si mjadala wa hapa fungua thread
 
Nilivyokuwa nafahamu mimi (may be wrongly) Bunge la Katiba ni Supreme Council ambayo haifungwi na mipaka yoyote katika kuhoji na hata kurekebisha chochote kadiri itakavyoonekana inafaa. Tatizo ni "uhuni" wa CCM, otherwise ndivyo ilivyotakiwa kuwa.
 
Wakuu nimekiwa kwenye lindi la msongo wa mawazo mazito juu ya upatikanaji wa katiba ya umma,

kifungu hichohicho inatoa ruhusa kwa Bunge la katiba, kujadili, kuondoa kifungu, kutunga kifungu ama KUIONDOA/KUOFUTA kabisa rasimu ile ya Mzee Warioba ambayo ndio maoni ya umma na kuleta rasimu yao ya Lumumba,

Watanzania tusimame tukatae uimla huu, sasa tuwaeleze hawa mabeberu wa ndani kuwa MAPINDUZI ya kiraia hayaepukiki ikiwa watafinyanga matakwa ya umma.
Mkuu, Yeri, ulikuwa wapi nilipoupandisha uzi huu?, Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!
Chadema ndio tuliwategemea, hapa walifanya makosa, maji tumeisha yavulia nguo hatuna budi kuyaoga!.
Tafsiri sahihi ni ile ya Kiingereza, ukishauri Watanzania tusimame tukatae, tunahatari ya kukosa vyote!.

Namalizia kwa ule ule msisitizo wangu kwenye ile mada tuliyobishana sana humu na Mkuu Mzee Mwanakijiji, kuwa mimi nikisema Chadema imetuingiza chaka, yeye akiwatetea!, nasisitiza tena na tena, "Japo Watanzania walitaka "Katiba Bora!", lakini kitakachopatikana kwa mchakato huu ni "Bora Katiba!" nikasema "maji ukiisha yavulia nguo!", kwa misingi ya "if you can't get what you want (Katiba Bora", then take what you get "Bora Katiba" kwa msingi wa na "moja shika sii kumi nenda rudi!", kuliko kukosa yote tukarudia katiba ya zamani, nikawasisitiza watu humu, tukubali matokeo na kwenye kura ya maoni, tuipigie kura ya ndio hii "Katiba Mpya!".

Pasco.
 
Mkuu, Yeri, ulikuwa wapi nilipoupandisha uzi huu?, Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!
Chadema ndio tuliwategemea, hapa walifanya makosa, maji tumeisha yavulia nguo hatuna budi kuyaoga!.
Tafsiri sahihi ni ile ya Kiingereza, ukishauri Watanzania tusimame tukatae, tunahatari ya kukosa vyote!.

Namalizia kwa ule ule msisitizo wangu kwenye ile mada tuliyobishana sana humu na Mkuu Mzee Mwanakijiji, kuwa mimi nikisema Chadema imetuingiza chaka, yeye akiwatetea!, nasisitiza tena na tena, "Japo Watanzania walitaka "Katiba Bora!", lakini kitakachopatikana kwa mchakato huu ni "Bora Katiba!" nikasema "maji ukiisha yavulia nguo!", kwa misingi ya "if you can't get what you want (Katiba Bora", then take what you get "Bora Katiba" kwa msingi wa na "moja shika sii kumi nenda rudi!", kuliko kukosa yote tukarudia katiba ya zamani, nikawasisitiza watu humu, tukubali matokeo na kwenye kura ya maoni, tuipigie kura ya ndio hii "Katiba Mpya!".

Pasco.

Sikubaliani sana na dhana yako kuwa Chadema ilaumiwe katika hili, Katiba sio ya chadema wala ya ccm, Watanzania wote tubebe lawama kwakuruhusi siasa ziteke katiba hii
 
Ndio maana niliweka uzi hapa nikisema tunahitaji foreign experts kwani wataalamu wetu wa ndani wa sheria na mambo ya katiba wamepoteza "credibility".
 
Ndio maana niliweka uzi hapa nikisema tunahitaji foreign experts kwani wataalamu wetu wa ndani wa sheria na mambo ya katiba wamepoteza "credibility".

Najiuliza sana, hivi kwamfano kwenye hiyo Sheria ya mabadiliko ya katiba ambayo ilitungwa awali kabisa, wanasheria wetu mahiri na wazee wetu wote hawakuona kasoro hizo????
 
Najiuliza sana, hivi kwamfano kwenye hiyo Sheria ya mabadiliko ya katiba ambayo ilitungwa awali kabisa, wanasheria wetu mahiri na wazee wetu wote hawakuona kasoro hizo????

Tatizo hapa ni maslahi yao binafsi na ya makundi au taasisi wanazotoka!

Maslahi ya taifa hayana nafasi kwao!
 
Back
Top Bottom