Intelligence Justice
JF-Expert Member
- Oct 23, 2020
- 3,443
- 4,006
Wana jamvi,
Ni miongo kadhaa sasa kwa mjibu wa sheria kila anayepata ajali ili apokelewe na kutibiwa na hospitali/zahanati au vituo vya afya ni sharti mgonjwa awe na Fomu iliyotolewa na kituo cha polisi alikoenda au kupelekwa kabla.
Utaratibu huu umesababisha madhara makubwa ikiwemo vifo kutokana na kuchelewa kufika hospitalini au kukataliwa hospitalini kutokana na hofu ya kutibu mtu aliyehusika na matendo ya jinai kama ujambazi nk. Huu utaratibu unavunja haki za msingi za binadamu kuwa na haki ya kuishi.
Kwa maoni yangu, napendekeza kwa serikali kutengeneza utaratibu wa kwamba pindi polisi wakipata taarifa za ajali barabarani, nyumbani, ofisini au popote ambapo kuna majeruhi au vyovyote, basi jeshi la polisi liwape wanaohusika na masuala ya ajali kwenda na PF3 kwenye eneo la tukio ambako baada ya kufika afanye tathiminni haraka na kutoa hiyo hati ya matibabu ya kipolisi kuwahi kuokoa maisha kuliko ilivyo kwa sasa.
Mchango wenu wadau tafadhali
Ni miongo kadhaa sasa kwa mjibu wa sheria kila anayepata ajali ili apokelewe na kutibiwa na hospitali/zahanati au vituo vya afya ni sharti mgonjwa awe na Fomu iliyotolewa na kituo cha polisi alikoenda au kupelekwa kabla.
Utaratibu huu umesababisha madhara makubwa ikiwemo vifo kutokana na kuchelewa kufika hospitalini au kukataliwa hospitalini kutokana na hofu ya kutibu mtu aliyehusika na matendo ya jinai kama ujambazi nk. Huu utaratibu unavunja haki za msingi za binadamu kuwa na haki ya kuishi.
Kwa maoni yangu, napendekeza kwa serikali kutengeneza utaratibu wa kwamba pindi polisi wakipata taarifa za ajali barabarani, nyumbani, ofisini au popote ambapo kuna majeruhi au vyovyote, basi jeshi la polisi liwape wanaohusika na masuala ya ajali kwenda na PF3 kwenye eneo la tukio ambako baada ya kufika afanye tathiminni haraka na kutoa hiyo hati ya matibabu ya kipolisi kuwahi kuokoa maisha kuliko ilivyo kwa sasa.
Mchango wenu wadau tafadhali