Utawezaje kutofautisha kati ya kutunza siri na kusema uongo?

Utawezaje kutofautisha kati ya kutunza siri na kusema uongo?

Lanlady

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2019
Posts
1,836
Reaction score
6,303
Wapo baadhi ya watu ambao hupenda kujua mambo yanayokuhusu au mambo asiyoyajua; na anatamani kuyajua ila hapaswi kuyajua kwa wakati huo.

Sasa ikiwa wewe ndiye unaulizwa kuhusu jambo au taarifa fulani unayoijua ila hupaswi kuisema kwa huyo anayekuuliza kwasababu ni SIRI; Je utamdanganya kwa kumpa majibu au taarifa ya uongo?

Nimeuliza swali hili kwasababu kuna watu wengi sana ili kuficha siri zao huamua kusema uongo. Mfano mtu ni mgonjwa ila hataki watu wajue, anaamua kusema kuwa yeye ni mzima tu..

Au mwingine ni mke wa mtu amepigwa na mmewe akavimba jicho akiulizwa anasema alijigonga mahali. Je hii ni sawa?
Kwa mtu kusema uongo ili kutunza siri?
 
Mfano umeona mtu anakimbizwa na mapanga ili auwawe mara akapita chumbani kwako akajificha ,wauwaji wakaja wakakukuta wewe,wakakuuliza ulimwona mtu fulani kapita hapa? utasema uwongo au ukweli?


Kwa mfano huo sio kila uwongo ni mbaya kuusema na sio kila ukweli ni mzuri kuusema
📌🔨
 
Mfano umeona mtu anakimbizwa na mapanga ili auwawe mara akapita chumbani kwako akajificha ,wauwaji wakaja wakakukuta wewe,wakakuuliza ulimwona mtu fulani kapita hapa? utasema uwongo au ukweli?


Kwa mfano huo sio kila uwongo ni mbaya kuusema na sio kila ukweli ni mzuri kuusema
📌🔨
Baada ya huu mchango basi mada hii ifungwe kabisa nahaya ndio majibu sahihi.
 
Back
Top Bottom