Utengenezaji wa Sabuni za Aina Mbalimbali: Fahamu Mahitaji, Mchakato wa Uzalishaji na Masoko

Utengenezaji wa Sabuni za Aina Mbalimbali: Fahamu Mahitaji, Mchakato wa Uzalishaji na Masoko

Je inakuwa na ubora kama haya makampuni makubwa mana naona makampuni makubwa yanazidi kupeta sioni ushindani

Unajua haya wajasiriamali wadogo wanatengeneza sabuni zenye ubora sana. Tatizo ni Vifungashio wanavyotumia ni low quality haviwezi kupata soko supermarket. Ishu ukiwa na Vifungashio bora unaongeza thamani
 
Muzeiya karibu sana katika ukumbi wa ujasiliamali katika nyanja hiyo niko bomba ile mzuri waweza kinipata kwa {safariwafungo@yahoo.com} tuwasiliane tuweze fanya kazi mzee, na kwa wale wenye kutaka ku-invest in manufacturing industry and the like please let work together i have a huge exposure academically and in experience wise!
Wapi napata kemikali ya Salicylic Acid kwa hapa Dar?
 
Kwa ufupi mpendwa hapo juu amesaidia sana maelezo ila mimi ningependa kama upo dsm naweza kuja kukufundisha.0717539573 ila ukipata semina ya Dr.Lunyungu ni nzuri kwani hata mimi ni zao lake.
sabuni ya unga unaweza nifundisha na kunieleza upatikanaji wa raw material??
 
Habari

Kutokana na maombi ya wengi na umuhimu wa utengenezaji na matumizi ya sabuni za unga katika maisha ya kila siku ya mwanadamu, nimeona nitoe mafunzo ya jinsi ya utengenezaji wa sabuni za unga.

Kumekuwa na mafunzo mbali mbali yanayokuwa yanatolewa nchi nzima na watu mbalimbali ambao hufundisha utengenezaji wa sabuni za ungaambapo imekuwa ni vigumu kwa wajasiriamali wengi kuanzisha biashara zao kwa kuwa ni list ndefu ya malighafi nyingi wanafundishwa lazinma wazitumie ili kuweza kutengeneza sabuni hizo. Hiyo ni kwa kuwa wanaambiwa hivyo kwa kuwa wasambazaji hao wa malighafi ndio wanaotoa hayo ,afunzo. Hivyo ni faida kwao.

Natoa mafunzo ya jinsi ya kutengeneza sabuni za unga kwa kutumia malighafi tatu tu. Hivyo inakuwezesha kupata faida karibu mara mbili ya gharama ya uzalishaji. Mafunzo haya yanapatikana katika kitabu nilichokiandika kutokana na uzoefu wangu katika biashara hii kwa kuwa nilikuwa naifanya kabla sijaanzishabiashara nyingine ya kutengeneza mkaa wa kisasa. Bei ya kitabu ni sh. 20,000 ambapo nakutumia kitabu katika email kama attachment nae unanitumia pesa kwa mpesa ya namba hii 0758 308193. Ntakuunganisha na wasambazaji wa malighafi, vifungashio, kukupa mbinu za masoko, ntakuunnganisha na mwenye kiwanda cha sabuni za mche ukajifonee na ntakutumia mafunzo mengine free ambayo nimekuwa nikiyatoa kwa miaka kadhaa sasa.

Nipigie tuzungumze.
number yako ya simu tafadhali
 
Kipo kitabu cha mafunzo ya hizi sabuni za miche,unga,maji na bidhaa zingine na formula zote ni softcopy unaweza kutumiwa katika email au whatsapp kwa shilingi elfu 5 tu kipo vizuri.
 
Kuna hawa jamaa wa Tanzania Business Creation Company wanatoa semina kwa wajasiriamali wanaotaka kumiliki viwanda vidogo vidogo. Mafunzo wanayotoa ni pamoja na utengenezaji wa:
sabuni za kufulia na kuogea
sabuni za maji
shampoo za kila aina
dawa za viatu
bleaching agent
petrolleam jelly etc.

waweza wasiliana nao kwa simu 0715851665 / 0784851665 / 0765871665
Pia wanayo mitambo ambayo wanatengeneza wenyewe na kuiuza kwa ajili ya kutengenezea sabuni za miche. Wako Sinza Mori
Nimepiga hizo number ya tigo nimemuuliza naongea na kampuni ya Tanzania bussiness creation? akasema sio, number ya Voda nimepiga wanasema hiyo number haipo. Air tel haipatikani, ninashida na hiyo idea nataka kuonana na watu ain hiyo ili nipate msaada wao.
 
Nimepiga hizo number ya tigo nimemuuliza naongea na kampuni ya Tanzania bussiness creation? akasema sio, number ya Voda nimepiga wanasema hiyo number haipo. Air tel haipatikani, ninashida na hiyo idea nataka kuonana na watu ain hiyo ili nipate msaada wao
Jaribu SIDO

[emoji252] [emoji479]
 
Nimepiga hizo number ya tigo nimemuuliza naongea na kampuni ya Tanzania bussiness creation? akasema sio, number ya Voda nimepiga wanasema hiyo number haipo. Air tel haipatikani, ninashida na hiyo idea nataka kuonana na watu ain hiyo ili nipate msaada wao
Imekuwa muda kidogo, labda hawapo tena mkuu

Sent from my TECNO-J8 using Tapatalk
 
Karibuni katika uzi huu mpya wa kujifunza elimu mbali mbali juu ya utengenezaji wa losheni,cream na sabuni za:

1. Kung'arisha ngozi
2. Kuondoa chunusi harara mwilini
3. Kurekebisha ngozi
4. Kunawirisha ngozi.

Huu utakua ni uzi maalum wa kupeana maujuzi juu ya kutengeneza hivyo jamani mnaojua pls nawaomba muweke maujuzi yenu hapa hii ni fursa nzuri mnoo ya kujiajiri hata kujiingizia kipato pia.

Karibuni sana.
 
Malighafi na kazi zake:

[emoji843]Sulphonics Acid -inaongeza povu
[emoji843]Soda ash-inapunguza acid
[emoji843]Sless-hupunguza povu na kun'garisha
[emoji843]Perfume-kuleta harufu nzuri
[emoji843]Glycerin-kuleta umafuta na ulaini
[emoji843]Chumvi-kuleta uzito na kufanya bidhaa yako iishi kwa muda mrefu
[emoji843]Maji
[emoji843]Rangi-kuipa muonekano mzuri bidhaa yako
[emoji843]Kifaa kama ndoo au pipa
[emoji843]Mti au mwiko mkubwa
[emoji843]Gloves
[emoji843]Buti
[emoji843]Kifaa kitakachoziba pua na mdomo

[emoji841]VIPIMO[emoji841]
[emoji843]Sulphonic Acid vijiko 4 vya chakula
[emoji843]Soda ash vijiko 2 vya chakula
[emoji843]Maji lita4
[emoji843]Sless roho
[emoji843]Glycerin vijiko3 vya chakula
[emoji843]Rangi kijiko kimoja cha chai
[emoji843]Chumvi robo kilo

[emoji841]JINSI YA KUTENGENEZA[emoji841]
[emoji842]Andaa Malighafi zako zote na uhakikishe sehemu ni safi
[emoji842]Anza na sulphoic acid weka kwenye ndoo /pipa
[emoji842]Fuatia soda ash ila kabla haujaweka kwenye ndoo/pipa hakikisha wailoweka kwenye maji kidogo pembeni ikishakua uji ndio umimine kwenye ndoo/pipa
[emoji842]Koroga na mwiko au mti vichanganyike
[emoji842]Weka maji Lita 4 na ukoroge dk 10
[emoji842]Weka glycerine
[emoji842]Weka perfume
[emoji842]Weka rangi
[emoji842]Weka chumvi kwa kunyunyiza kidogo kidogo

Endelea kukoroga hadi bidhaa yako iwe nzito kama uji kwa dk 15. Hapo shampoo yako itakua tayari.

[emoji840]waweza ongeza vipimo vya Malighafi kutokana na wingi utakao

Shampoo yako ipo tayari kwa matumizi

Naomba maswali pale ambapo hamjaelewa

Ahsanteni
 
Back
Top Bottom