UTETEZI WA LULU: Kanumba alitaka kunibaka...

UTETEZI WA LULU: Kanumba alitaka kunibaka...

Hapa kweli panahitaji ufafanunuzi zaidi!

ni kazi ya DPP kumtafuta yule dakitari atueleze vizuri kulikoni.....lol hizi ARVs na pombe kali wapi na wapi..........
 
Yaani Ruta ungekuwa ndiye Jaji ndiyo ingekuwa ile vodafasta ya Msomaji raia wa Raia Mwema hahahah...
 
lulu-top.jpg

Elizabeth Michael Kimemeta

attachment.php

Aliyekuwa nguli wa filamu nchini akimlea yule mthumiwa wa mauaji yake Elizabeth Michael Kimemeta


SDC11675.JPG


nFr43ZnXftQzcDHZdL6u+mJD7fm62qlgaDYWn4pXLyVblxrbF5MdZ5t7l1p65xo6FpJd43W1M03J0URiJBKdiCcmovGJUDTtD44GoIlwYDzgHwt4p8PQVMg3FQBn

Bw. Michael Edward Kimemeta - Baba Lulu


Mkakati wa Lulu kujitoa kwenye makucha ya hii dola kandamizi sasa umeanza kuchipuka pale ambapo mshitakiwa wa hii kesi ya mauaji alipokerwa pale mahakamani alipokuwa akisomewa mashtaka tajwa dhidi yake na hata kunyosha kidole na kutoa sahihisho ya kuwa umri wake ni miaka 17 na wala siyo 18.(Lulu alizaliwa tarehe 17 April 1995 katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.) Kwa kawaida kwenye kesi za mauaji mara ya kwanza husomwa katika mahakama ya hakimu mkaazi na mshitakiwa anayo haki ya kukaa kimya kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo lakini Lulu aliona aanze kuweka utetezi wake vyema hata katika hatua hiyo ya awali...............




Athari za kisheria za umri wa miaka 17
.

Umri huo unamweka Mwendazake -Steven Kanumba- ambaye ana umri wa miaka 28 katika khali mbaya ya kitabia na mwenendo kulingana na sheria ya makosa ya kijinai katika kujamiana pamoja na ya kuwa kwa vile yeye ni marehemu hawezi kushitakiwa nayo lakini yanapunguza makali ya Lulu kuwa na kesi tajwa ya kujibu.

Umri wa miaka 17 ni binti mtoto na wala siyo mtu mzima hivyo kuwa na mapenzi naye hata kama alipenda iwe hivyo unamgeuzia kibao mwendazake kuwa alikuwa anakusudia au alikuwa akimbaka Lulu na hivyo kuweka kesi ya mauaji kuwa na utetezi wa "self-defence" kwa maana ya kuwa Lulu alifanya yoyote yale yaliyo ndani ya uwezo wake kujitetea dhidi ya mwanaumme mtu mzima tena mwenye umri wa miaka 28 aliyekuwa anamkamia kumbaka.

Vilevile umri tajwa unamwondolea Lulu adhabu ya kifo endapo mahakama kuu itamtia hatiani kwenye makosa ya mauaji (very unlikely, though- uwezekano wa kumtia hatiani ni mdogo sana) na pia kumpa haki ya kuondolewa kwenye lupango ya watu wazima jambo ambalo polisi wetu wameendelea kukiuka haki zake kwa kumchanganya na lupango ya watu wazima. Utetezi wa kiawali wa Lulu unakuwa hauna mashiko pale Lulu atakapolalamikia ya kuwa polisi walimlazimisha kumshikilia kwenye lupango ya watu wazima na hivyo kumfanya aghafilike kiakili na hivyo kushindwa kutoa ushahidi sahihi na hivyo kuilazimu mahakama kuutupilia mbali ushahidi wa kiawali na hivyo kumruhusu autoe ushahidi mpya ambao ndiyo huu ninaouchambua na kuuwakilisha hivi sasa.

Lakini kubwa zaidi ni utetezi wa kimazingira ambao Lulu atautoa mahakamani wa ya kuwa yeye ni kinda wa chini ya miaka 18 na hivyo utamweka mwendazake katika mazingira ya kiubakaji au kukusudia kumbaka na hivyo utetezi wa self-defence kuwa na uzito wa kipekee.

Haya ni baadhi tu ya dondoo ambazo Lulu aweza kuzitumia katika kujinasua katika makucha tajwa:-


a) Mwendazake ndiye aliyemwita kuwa ana mazungumzo naye ya haraka usiku wa tukio juu ya tasnia ya filamu. Hivyo yeye Lulu hakuwa na makusudio ya kwenda kwa Kanumba kwa minajili ya kumwuuwa. Kumbuka DPP ni lazima athibitishe nia ya kuua ili mahakama imtie hatiani Lulu lakini kama ni kanumba ndiye aliyemwita mtuhumiwa nia ya Lulu kwenda kwa mwendazake kwa nia tajwa itaota mbawa kuwa isingewezakana kuwa vivyo kama DPP anavyodai.

b) Marafiki wa Lulu watathibitisha ya kuwa wao ndiyo waliokuwa wakimpigia simu na kutaka kujua alikuwa wapi na kwa nini amechelewa. Ushahidi huu wa kimazingira utazidi kubomoa hoja ya polisi ya kuwa Lulu alikwenda kwa mwendazake kwa nia ya kumtoa roho.

c) Lulu atathibitisha mahakamani ya kuwa kanumba siye mpenzi wake na kwa hivyo hoja ya DPP kuwa kulikuwa na ugomvi wa mapenzi kukosa mwelekeo.

d) Lulu atajenga hoja ya kuwa Kanumba alitaka kumbaka na yeye alitumia nguzu za mikono yake kujihami na kutokana na umri wa miaka 17 mahakama lazima ikubaliane naye ukizingatia mazingira yenyewe: Yawaje mtu mzima amkaribishe binti mdogo wa chini ya miaka 18 chumbani mwake kama lengo siyo kumbaka? Yawaje Kanumba akutwe hana nguo kwa maana ya kuwa yuko uchi wa mnyama na binti mdogo hivyo tena chumbani kwake? Kwa hiyo, hata kama lulu alitumia silaha iliyokuwemo chumbani kujilinda, mahakama itampa manufaa ya "benefit of doubt" na hivyo kuukubali utetezi wake. Lulu hakutumia silaha yoyote kulingana na ushahidi uliopo mikononi mwa DPP.

e) Lulu atadai kilichomwangusha Kanumba chini na kukosa fahamu hakina uhusiano na yeye bali ni matatizo yake ya kiafya na atatumia taarifa ya madaktari wa Muhimbili kuthibitisha ya kuwa kilichomtoa roho mwendazake ni mshtuko mkubwa katika ubongo wake (Brain concussion) ambao haukusababishwa na majeraha ya mwilini mwake ambayo hata hivyo hayapo. Mwendazake hakuwa na jeraha lolote kuonyesha lingeweza kumsababishia mshtuko tajwa.

f) Lulu atadai mahakamani ya kuwa hakuna ushahidi wowote ule wa kitaalamu ya kuwa marehemu alikufa kwa lolote jinginelo na inashangaza hata DPP kumfungulia kesi ya mauaji na hivyo kumbughudhi na kumdhaliliisha mbele ya jamii na hivyo kuiomba mahakama iangalie namna ya kumfidia dhidi ya kubambikiziwa kesi ambayo hata haipo au "malicious prosecution".

g) Lulu atarejea ushahidi wa ndugu wa marehemu aitwaye Seth ambaye alidai Lulu ana mazoea ya kwenda pale na ya kuwa hakuona kama kuna ubaya wowote kwa hiyo alimkaribisha na ya kuwa kaka yake ndiye aliyeanzisha zengwe pale aliposikia mlio wa simu ya Lulu na kuhisi ya kuwa Lulu alikuwa anapigiwa simu na mwanaumme mwingine. Hapa lengo litakuwa kuonyesha ya kuwa kama kuna ugomvi marehemu ndiye aliyeuanzisha kwa minajili ya kumbaka kwa kumzuia asiendelee na safari zake. Vile vile mdogo wa marehemu- Seth- aliona Lulu siyo mtu wa shari na ndiyo maana hakumzuia kuingia ndani kutokana na kuwa mtu wa amani na siyo wa hata kuweza kutishia maisha ya nduguye..........

h) Lulu atahoji kwa nguvu zote yawaje kwenye vielelezo vya DPP hakuonyesha afya ya mwendazake ilikuwaje kwa sababu ajuavyo yeye alikuwa akitumia madawa mengi sana kila siku madawa yanayosadikiwa kuwa ni ya kupunguza makali ya vvu yaani ARV na huku akiwa na tabia ya kunywa pombe kali sana kama Jack Daniel, Konyagi, Whisky, Ram n.k. Lulu atadai ya kuwa matumizi ya madawa tajwa na vinywaji vikali kwa wakati mmoja yalichangia katika kusitisha maisha ya mwendazake na wala siyo yeye. Pia ataikumbusha mahakama kuwa anashindwa kuelewa yule daktari wake hakushitakiwa kwa mauaji husika kwa kumpa mwendazake madawa tajwa bila ya vibali vya hospitali zenye mamlaka ya kufanya hivyo............

kwa ushahidi huu na mwingineo mwingi, hakuna Jaji ambaye atakubali kuchafua heshima yake kwenye jamii na kuhalalisha mabinti wadogo wafanyiwe unyama hata kama unyama huo unafanywa na aliyekuwa akijiita mwenyewe "mcheza filamu nambari moja hapa nchini".

Hivyo basi mahakama itaamua Lulu hana kesi ya kujibu na mwendazake ndiye aliyejenga mazingira kwa yote yaliyomkuta na hapaswi kumtupia lawama mtoto mdogo aliyechini ya miaka 18.......

FUNDISHO KWETU SOTE


Aidha ni jukumu la watu wazima kuwa mfano wa malezi ya watoto wadogo badala ya wao kuwarubuni na kuwafunza namna ya kuyaharibu maisha ya watoto hao kupitia makosa ya jinai ya ubakaji kwa kuwarubuni na kuwapa ajira njaa za hapa na pale.............


teeheeteehhhhh DADA HUYOOOOO ALIKWISHAAAAAAAAAAOLEWAAAAAAAAAAAAAAA DADA HUYOOOOOOOOOO ALIKWISHA OLEWAAAAAAAAAAAAAAA MAHARRIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII AMEPOKEAA NANIIIIIIIIIIII MAHARIIIIIIIIIIIIIIIII KAPOKEA NANIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII
SHAME ON HIM
 
Nimelazimika ku log in just to congratulate you my learnedbrother Rutashubanyuma! Hakika umechambua haswa shauri hili mwenye masikio naasikie na asiyetaka basi aache ila ukweli ndio huo.
Hapa kwakweli wapenda ndogo ndogo tuko hatwarini, kwaniSOSPA inatunyanyapaa vibaya japokuwa inasikitisha kwa ku focus jinsia moja!
 
Hizi sarakasi hadi lini?waachiwe mahakama wafanye kazi yao kwa uhuru.
 
Section 56(2)

Hizi sheria zinachanganya sana nafikiri issue si mtoto hebu tuangalie sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai(The Criminal procedure Act) kifungu cha 56 kifungu kidogo cha 2 (sect 56 subsection 2 of PCA) ninanukuu:

56. Special duties when interviewing children
(1) A police officer in charge of investigating an offence in respect of which a child is under restraint shall, forthwith after the child is placed under restraint, cause a parent or guardian of the child to be informed that he is under restraint and of the offence for which he is under restraint.
(2) In this section "child" means a person who has not attained the age of sixteen years.

Tuje kwenye tafsiri ya kisheria mtoto ni nani section 2 ninakuu:-

2. Interpretation according to PCA. Sect 2.
In this Act, unless the context requires otherwise–
"adult" means a person of or above the age of sixteen years;
"arrestable offence" means an offence for which a police officer may, in accordance with the First Schedule to this Act or under any written law for the time being in force, arrest without warrant;
"child" means a person who has not attained the age of sixteen;

Tuje kwenye sheria ya 'The children and young person act' sect 2 inatafsiri:-
"child" means a person under the age of twelve years
"young person" means a person who is twelve years of age or more but under the age of sixteen years.

Tuje kwenye sheria ya "The sexual offences special provision Act" Sect 2 inatafsiri:-
"girl" means a female person of the age of under eighteen years.
"woman" means any female person above the age of eighteen years; whether or not married;

Sasa ukiziangalia hizo tafsiri za kisheria utaona zinapingana namna ya kumuelezea mtoto kumbe basi ni sahihi kusema Lulu ni msichana yaani Girl au adult kuliko kusema mtoto kwa sababu Lulu teyari ana above 16 na less than 18 yaani ana 17yrs.
Lakini kwa Lulu umri si issue sana ya kujadili, issue ni ubakaji ambao hauzungumzii umri, kwani unaweza kumbaka hata mkeo, huyu binti ni mtoto mdogo.
 
Itapendeza sana kama Lulu atatoka kwani haiji akilini kwa binti huyu kufanya kosa hili. Nahisi yalikuwa ni matatizo ya kiafya kwa marehemu tu, iweje awe na uhusiano na watoto kimapenzi wakati ye mtu mzima, ameifundisha nini jamii yetu? Tukae mkao wa kula kushuhudia hukumu itakavyokuwa.
 
lulu-top.jpg

Elizabeth Michael Kimemeta

Mkakati wa Lulu kujitoa kenye makucha ya hii dola kandamizi sasa umeanza kuchipuka pale ambapo mshitakiwa wa hii kesi ya mauaji alipokerwa pale mahakamani alipokuwa akisomewa mashtaka tajwa dhidi yake na hata kunyosha kidole na kutoa sahihisho ya kuwa umri wake ni miaka 17 na wala siyo 18. Kwa kawaida kwenye kesi za mauaji mara ya kwanza husomwa katika mahakama ya hakimu mkaazi na mshitakiwa anayo haki ya kukaa kimya kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo lakni Lulu aliona aanze kuweka utetezi wake vyema hata katika hatua hiyo ya awali...............

Athari za kisheria za umri wa miaka 17
.

Umri huo unamweka Mwendazake -Steven Kanumba- ambaye ana umri wa miaka 28 katika khali mbaya ya kitabia na mwenendo kulingana na sheria ya makosa ya ki9jinai kujamiana pamojana yakuwa kwa vile yeye ni marehemu hawezi kushitakiwa nayo lakini yanapunguza makali ya Lulu kuwa na kesi ya kujibu tajwa.

Umri wa miaka 17 ni binti mtoto na wala siyo mtu mzima hivyo kuwa na mapenzi naye hata kama alipenda iwe hivyo unamgeuze mwendazake kuwa alikuwa anambaka Lulu na hivyo kuweka kesi ya mauaji kuwa na utetezi wa self-defence au Lulu alifanya yoyote yaliyo ndani ya uwezo wake kujitetea dhidi ya mwanaumme mtu mzima tena mwenye umri wa miaka 28 kutaka kumbaka.

Vilevile umri tajwa unamwondolea Lulu adhabu ya kifo endapo mahakama kuu itamtia hatiani kwenye makosa ya mauaji (very unlikely, though- uwezekano wa kutia hatiani ni mdogo sana)na pia kumpa haki ya kuondolewa kwenye lupango ya watu wazima jambo ambalo polisi wetu wameendelea kukiuka haki zake kwa kumchanganya na lupango ya watu wazima. utetezi wa kiawali wa Lulu unakuwa hauna mashiko pale Lulu atakapolalamikia ya kuwa polisi walimlazimisha kumshikilia kwenye lupango ya watu wazima na hivyo kumfanya aghafilike kiakili na hivyo kushindwa kutoa ushahidi sahihi na hivyo kuilazimu mahakama kuutupilia mbali ushahidi wa kiawali na hivyo kumruhusu autoe ushahidi mpya ambao ndiyo huu ninaouchambua hivi sasa.

Lakini kubwa zaidi ni utetezi wa kimazingira ambao Lulu atautoa mahakamani wa kinda wa chini ya miaka 18 utamweka mwendazake katika mazingira ya kiubakaji au kukusudia kumbaka na hivyo utetezi wa self-defence kuwa na uzito wa kipekee. haya ni baadhi tu ya dondoo ambazo Lulu aweza kuzitumia katika kujinasua katika makucha tajwa:-

a) Mwendazake ndiye aliyemwita kuwa ana mazungumzo naye ya haraka usiku wa tukio juu ya tansnia ya filamu. hivyo yeye Luou hakuwa na makusudio ya kwenda kwa kanumba kwa minajili ya kumwuuwa. kumbuka DPP ni lazima athibitishe nia ya kuua ili mahakama imtie hatiani Lulu lakini kama ni kanumba ndiye aliyemwita nia ya Lulu kwenda kwa mwendazake kwa nia tajwa itaoa mbawa kuwa isingewezakana kuwa kama DPP anavyodai.

b) Marafiki wa Lulu watathibitisha ya kuwa wao ndiyo waliokuwa wakimpigia simu na kutaka kujua alikuwa wapi na kwa nini amechelewa. Ushahidi huu wa kimazingira utazidi kubomoa hoja ya polisi ya kuwa Lulu alikwenda kwa mwendazake kwa nia ya kumtoa roho.

c) Lulu atathibitisha mahakamani ya kuwa kanumba siye mpenzi wake na kwa hivyo hoja ya DPP kuwa kulikuwa na ugomvi wa mapenzi kukosa mwelekeo.

d) Lulu atajenga hoja ya kuwa Kanumba alitaka kumbaka na yeye alitumia nguzu za mikono yake kujihami na kutokana na umri wa miaka 17 mahakama lazima ikubaliane naye ukizinatia mazingira yenyewe. Yawaje mtu mzima amkaribishe binti mdogo wa chini ya miak 17 chumbani mwake kama lengo siyo kumbaka? yawaje kanumba akutwe hana nguo yuko uchi wa mnyama na binti mdogo hivyo? Kwa hiyo ahata kama lulu alitumia silaha iliyokuwemo chumbani kujilinda mahakama itamp nufaa ya "benefit of doubt" na hivyo kuukubali utetezi wake.

e) Lulu atadai kilichomwangusha kanumba chini na kukosa fahamu hakina uhusiano na yeye bali ni matatizo yake ya kiafya na atatumia taarifa ya madaktari wa Muhimbili kuthibitisha ya kuwa kilichomtoa roho mwendazake ni mshtuko mkubwa katika ubongo wake ambao haukusababishwa na mahjeraha aya mwilini mwake ambayo hata hivyo hayapo. mwendazake hakuwa na jeraha lolote kuonyesha lingeweza kumsababishia mshtuko tajwa.

kw aushahidi huu na mwingineo mwingi, hakuna Jaji ambaye atakubali kuchafua heshima yake kwenye jamii na kuhalalisha mabinti wadogo wafanyiwe unyama hata kama unyama huo unafanywa na aliyekuwa mcheza failamu nambari moja hapa nchini. Hivyo basi mahakama itaamua Lulu hana kesi ya kujibu na mwndazake ndiye aliyejenga mazingira kwa yote yaliyomkua na hapaswi kumtupia lawama mtoto mdogo aliyechini ya miaka 18.. Aidha ni jukumu la watu wazima kuwa mfano wa malezi ya watoto wadogo badala ya wao kuwarubuni na kuwafunza namna ya kuyaharibu masiha ya watoto hao kupitia makosa na jinai ya ubakaji.

Utetezi wa kubakwa utafunika suala la mahusiano yao? hasa ile simu ya mwanaume mwingine kupigwa na Lulu kutoka kwenda kuipokea nje? Vipi hapo? Mdogo wake Kanu aliyekuwepo katika eneo la tukio ana ushadidi huu. Je unafutika kwa utetezi wa ubakaji?
 
sipendi Lulu aishie jela lakini kwa uongo huu wa kusema alitaka kubakwa namwombea Mungu afungwe maisha.
 
Hongera wana JF kwa uchambuzi wa sheria mbalimbali juu ya umri wa mtuhumiwa Lulu,Lakini kwa mawazo yangu nadhani Lulu anakabiliwa na kesi ya mauaji.
Among the available defences for murder cases, rape is not one of them!!!

Hata hivyo si rahisi kama watu wengi wanavyodhani, kuwa Lulu ana hatia ya kesi hiyo.
It must be proved beyond any reasonable doubt that its Lulu who in fact caused the death of Kanumba by doing any culpable act with an intention of causing the death of the deceased( This intentio is known as MALICE AFORETHOUGHT).
Nawasilisha tafadhari,
KISHOKA.
 
kwa mzaha mzaha wa aina hii sote tunapswa kuwa lupango......kwa maana soe ni wahuni na tuna mafaulo yetu kibao..........acha kumnyanyapaa dogodogo...anahitaji sisi wakubwa zake tumwelekeze lipi litamfaa maishani mwake........

Wewe ndiyo unajua hilo leo? Tuache wanasheria wafanye kazi yao, tusianze kuhukumu kabla, AKUTWE NA HATIA AU ASIKUTWE NA HATIA, AWE AMA ASIWE MTOTO, LULU ANA MAMBO YA KIUTU UZIMA...KALE SIYO "KATOTO LUTASHUBANYUMA KANABEBA WAZEE KUZIDI WEWE"
 
tabia yake haihalalishi abakwe...............kwa hiyo hoja zako Alien 1-9 zinapoteza mwelekeo. Hoja no. 10 ya kuwa mahakama itazingatia mob-justice....................sioni hata umuhimu wa kujibu kwa sababu that is the last thing the court wants to entertain....................pitia polepole hoja zangu utagundua Lulu has no case to answwer ila DPP anafanyakazi kwa mashinikizo ya mob-justice na wala siyo kwa kuongozwa na sheria au ushahidi alionao mikononi mwake..........

Hii kesi kama lulu asipotendewa haki tuko tayari wanaharakati kuichukua na kuutangazia ulimwengu mzima kwamba Tanzania si mahali salama kwa watoto kutokana na vitendo vya ubakaji kwa watu wenye nafasi kuchukua advantage ya umaarufu wao kuwaabuse watoto under the govt watch
 
Back
Top Bottom