Utetezi wa Sabaya: Amwangushia zigo Hayati Magufuli na kudai Gavana Luoga na Makamu wa Rais Dkt. Mpango walifahamu

Duh!! Mungu anamuona lakini!

Amejitetea kiume sana

Makamu wa Rais Dr Mpango na DC mstaafu Dr Kihongosi watakuwa mashahidi wake muhimu kama katiba inaruhusu.

Rais mstaafu Mkapa aliwahi kupanda kizimbani kumtetea Prof Mahalu pale Kisutu!
Sio fala huyo alichofanya yeye ameona jumba bovu mnamuangushia peke yake huku kina Makonda wanadunda tu mtaani na pengine anajua Makonda alifanya zaidi yake, Kama yeye tu ni mkuu wa wiliya asiye na mipaka kafanya hayo itakuwaje kwa naibu Rais Makonda? Ndio maana kaamua kutambaa na Makamu wa Rais kama mbwai na iwe mbwai
 
Vyote vinaendana, wewe huoni ajabu mwenyekiti wa chama kinachounda serikali, na ambaye ndiye Rais, anatajwa kuwaagiza wasaidizi wake wakawafanyie ujambazi wananchi waliompigia kura?!! Aibu tupu.
Unafikiri kama si katiba mbovu haya yangetokea? Na ujue hapo saa mbaya kafikishwa mahakaman ni kwa kutaka mama, mama asingetaka saa mbaya asingefikishwa popote...yote hayo ni katiba mbovu
 
Yan umewaza kama mimi...jamaa kaamua kuwa kama imeshakuwa mbaya basi acha iwe mbaya kabisa.
 
Kwa kifupi ana huo ushaidi kasema alipigiwa simu wakati ushaidi wa maandishi ndio unaitajika kwasababu order za serikali siyo kupigiwa simu ni maandishi
Kifungu kipi? Mbona kina nape iliwabidi waombe msamaha baada ya simu zao kudukuliwa? Mbona hayakutafutwa maandishi?
 
Kwa namna Sabaya anavyojitetea ni wazi wakimfunga wamemuonea na wakimwachia wanamuogopa...

Hii awamu inazidi kufeli kwa kila inalolifanya.

2025 Sina kura ya kuchezea.

tutaelewana tu.
 
Kwa hiyo kipi kikifanyika Ni Bora kwa mahakama wamfunge au wamwachie
 
Humjui Moses Mahuna?
 
Kwa maana nyingine amekiri kuhusika na hivyo asubiri kungininizwa tu. Hakuna mahakamanya kipumbavu ya kusikia mere stories za kuwasingizia rais au wengineo bila written proofs.

Angekuwa na akiri angejiuzuru baada ya kutumwa kinyume
Mbona mere narratives za mashahidi wa Jamhuri zimesikilizwa na mahakama hiyo hiyo?
 
Hawa mods wanaounganisha unganisha nyuzi za watu humu mbinguni wataenda kwa miguu.

Ila poa tu.
 
Duh!! Mungu anamuona lakini!

Amejitetea kiume sana

Makamu wa Rais Dr Mpango na DC mstaafu Dr Kihongosi watakuwa mashahidi wake muhimu kama katiba inaruhusu.

Rais mstaafu Mkapa aliwahi kupanda kizimbani kumtetea Prof Mahalu pale Kisutu!
Hakuna uwezekano wa kumsamisha Makamu wa Raisi Wala gavana kizimbani,hii kesi dogo ama ameishashinda,au mamlaka zinatengeneza mazingira ashinde,au dogo kachemka kuwataja hao wakubwa,sasa "the ginie is out of bottle"sasa itabidi dogo azimwe tu kiaina.
 
kama sio pompompo leo hii asingekuwa mahakamani. kuna CCM wangapi wameiba hela lakini wako salama tu kwenye serikali yao ya kifisadi
 
Sabaya amesema alipewa maafisa 4 alioambiwa akutane nao uwanja wa ndege. Maafisa hao walikuwa na nyaraka za opearation. Kwanini hilo linasahaulika? Kwanini kuna panics mtu akiamua kiweka stori sawa? Ina maana hakuna ambacho mahakama inaweza kuthibitisha kwa hayo yote aliyotaja Sabaya?
Huo ndio mfumo wa haki. Amekuwa muwazi. Hata kama atafungwa au atakufa, ameshaweka vizuri kuhusika kwakwe kwenye operation Arusha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…