Utetezi wa Sabaya: Amwangushia zigo Hayati Magufuli na kudai Gavana Luoga na Makamu wa Rais Dkt. Mpango walifahamu

Utetezi wa Sabaya: Amwangushia zigo Hayati Magufuli na kudai Gavana Luoga na Makamu wa Rais Dkt. Mpango walifahamu

Kwa hi
Hivi jamani kwa watumishi wa umma ,kile kipengele cha utafanya kazi yeyote utakayopangiwa na bosi wako huwa kina maana gani? Maana hapa sabaya akifungwa nyie mabosi msituone viburi tukigoma kufanya kazi mnazotutuma

Kwa uongozi was jpm ,je kuna MTU angeweza mbishia na akawa salama ? Hata huyo hakimu angeembiwa ahukumu kesi kadri mzee anavyotaka angekataa?

Kiufupi hapa sabaya anakosa alilotenda katika kutii mamlaka iliyomteua na ndo maana kwann hakushitakiwa enzi za jpm? Na je jpm angekuwa mzima angeshitakiwa?

KATIBA MPYA MUHIMU NDUGU ZANGU ,SIKU NIKAWA RAISI NIKAHITAJI KULA NYAMA ZA WATU MTAKOSA PA KUNIKAMATIA
Kwa hiyo wewe ni robot kwamba huwezi kupima kama uliloagizwa linavunja sheria au lah? Hakuna utetezi kama jambo ulilotenda linavunja sheria sababu kosa umetenda wewe. Kwa hiyo lazima ushirikishe ubongo ukiona huwezi unajiuzulu Kisha unavuka mpaka nchi jirani kuliko kadhia kama hizi.
Kumbuka mahakimu Wana Kinga ya kutoshitakiwa wakihukumu kinyume na sheria.
 
Wakili anae endesha kesi ya sabaya ana uwezo mdogo sanaa kisheria, yaan mpaka hapo kamtia hatiani mteja wake. Rasmi sabaya hachomoki sababu wakili uwezo mdogo. Hoja ilitakiwa Sabaya kuwapiga wale au kuiba vitu pale na uwezekano wa kutokuwepo kwenye eneo husika.
Jamaa kakiri kuwepo Arusha kwenye tukio.

Na wakili anatoka hapo anaomba fee!!!!

My God
 
Ole Sabaaya ameshapotoshwa na wanasheria wake,

1) Amri Kutoka Kwa Wakuu Wake (Order From Higher Personnel) sio utetezi wa jinai (Sio Criminal Defence). Ni Heri hata angejitetea alikua amelewa kupita kiasi kwasababu Ulevi (Intoxication) inaweza kutumika kama Criminal Defence.

Hakuna defence katika jinai ya Kutimiza Amri Ya Kiongozi Wa Juu (Order From Higher Personnel). Hii haipo kwenye Penal Code CAP 16 na hata kwa wanajeshi haipo kwenye Marshall Codes & Laws.

Ref: Nuremberg Trials and Nuremberg Codes.

Wanajeshi wa Nazi walitumia utetezi huo kujitoa katika hatia ya makosa ya jinai waliotenda dhidi ya binaadamu, walisema wao walitenda hayo mauwaji ila kwa kufuata na kutii amri za wakubwa zao. Ila mahakama ya kijeshi ya Nurenberg ilikataa utetezi huo kwa hoja moja kuu "UNAPOPEWA ORDER NA MKUU WAKO YA KUFANYA JAMBO LINALOKWENDA KINYUME NA SHERIA AU HAKI ZA BINAADAMU, UNA WAJIBU WA KUKATAA KUTII ORDER HIO".

2) Ushahidi wa kumtaja mtu kwamba amekupa maagizo fulani kisheria unahitaji "CORROBORATION" ya ushahidi wa ziada kutoka kwa huyo mtu alietajwa. Magufuli hawezi kupatikana kwaajili ya kutoa ushahidi wa ziada ku-support na ku-confirm ushahidi wa Ole Sabaaya.
Hakuna unachokijua mkuu, hapa Sabaya anachofanya ni kuweka matobo kwenye hoja ya kwanini alikwenda Arusha kufanya anachodai ni oparation wakati yeye ni mkuu wa Wilaya ya hai.Amabacho tu my opinion ndo hoja pekee iliyomkalia vibaya kwenye kesi hiyo!
 
Duh!! Mungu anamuona lakini!

Amejitetea kiume sana

Makamu wa Rais Dr Mpango na DC mstaafu Dr Kihongosi watakuwa mashahidi wake muhimu kama katiba inaruhusu.

Rais mstaafu Mkapa aliwahi kupanda kizimbani kumtetea Prof Mahalu pale Kisutu!
Serekali ya majambazi Raliye kuwa raisi mh.kichaa alikuwa jambazi
 
JELA MWAKA MMOJA KWA KOSA LA KUFANYA KAZI NJE YA KITUO CHA KAZI BAADA YA HAPO ANAKUWA HURU MWAKA MMOJA NI SAWA NA MIEZI SITA TU
Dada una mahaba sana na General Lengai Ole Sabaya. Makosa yake siyo ya hukumu ya muda mfupi hivyo. Ngoja tusubiri tuone hukumu yake. Kikubwa umeshaona kwamba hukumu inamhusu.
 
Hilo ni swali la msingi. Ule mchakato ulisitishwa utafikiri wakati unaanzwa tulilazimishwa.
Halafu umesitishwa watu kimyaaaa kama sio sisi.
Najiuliza, hata kama utaanzishwa tena kuna hakika gani wenye nguvu zao hawata sitisha tena.
 
Duh!! Mungu anamuona lakini!

Amejitetea kiume sana

Makamu wa Rais Dr Mpango na DC mstaafu Dr Kihongosi watakuwa mashahidi wake muhimu kama katiba inaruhusu.

Rais mstaafu Mkapa aliwahi kupanda kizimbani kumtetea Prof Mahalu pale Kisutu!
Mkapa hakuwa raisi lakini. Tusubiri hii movie tuone.
 
Kesi ni nzuri, kama hiyo mamlaka iliyomteua ndio iliyomtuma as they say "amri kutoka juu" wakijaga kututeka basi bado atakuwa na kesi ya ukatili alioufanya sababu ni kinyume na sheria na pia hao mabaunsa aliowakana itabidi wathibitishe kwamba kweli wapo ndani ya mfumo na sio wahuni wakuokota kama inavyodaiwa
Mpaka inaisha tutaona mengi ila hapa SABAYA hachomoi
 
Yaani ndugu yangu Sabaya kama DC wa Wilaya iliyopo mkoa wa Kilimanjaro unatoka Mkoa wa Kilimanjaro unakwenda mkoa mwingine ambao ni wa Arusha unafanya uliyoyafanya unaona uko sahihi!
 
Back
Top Bottom