UTEUZI: Rais Samia afanya teuzi za Wakurugenzi Watendaji wa Hospitali ya Muhimbili na JKCI

mwanamwana

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2011
Posts
1,309
Reaction score
4,798
UTEUZI: Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Prof. Mohamed Yakubi Janabi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Muhimbili.

Prof. Janabi alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)
Prof. Janabi anachukua nafasi ya Prof. Lawrence Maseru ambaye amestaafu.

Aidha Rais Samia amemteua Dkt. Peter R. Kisenge kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete.

Dkt. Kisenge anachukua nafasi ya Prof. Janabi.

Kabla ya uteuzi, Dkt. Kisenge alikuwa Mkurugenzi wa Tafiti na Mafunzo wa (JKCI).



Pia, soma: Rais Samia Suluhu Hassan afanya uteuzi wake wa kwanza Ikulu. Gerson Msigwa atolewa Ikulu, Dotto James ahamishwa. TPA, TCRA na TRA zapata wakuu wapya
 
Hongera kwa Prof. Janabi ana moral authority. Sio mchoyo nina jifunza mengi mfumo wa maisha kwa magonjwa yasioambukiza kwa kuishi ushauri na elimu yake ya Bure tv na mitandaoni. Wasomi wengine jifunzeni kutoa huduma ya ziada.
 
Hizo nafasi sio za kufanya uteuzi wangeweka tu ajira portal watu waende dodoma 😂
 
Prof Janabi kateuliwa kuwa mkurugenzi Mtendaji hospital ya Taifa Muhimbili, kabla ya uteuzi alikua ni mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya moyo ya Jakaya kikwete.



Aliekuwa Mtendaji Mtendaji wa hospital ya Taifa Muhimbili prof mseru amestaafu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…